-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
‘Mana Iliyofichwa na Kijiwe cha Mviringo Cheupe’
17. Ni thawabu gani inayongojea Wakristo wapakwa-mafuta ‘wanaoshinda,’ na ni nini ambacho Wakristo katika Pargamamu walihitaji kushinda?
17 Thawabu tukufu inawangojea wote ambao hutii shauri la Yesu, linalotolewa kwa mwelekezo wa roho takatifu ya Yehova. Sikiliza! “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye anashinda mimi nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa kijiwe cha mviringo cheupe, na juu ya kijiwe cha mviringo cheupe jina mpya lililoandikwa ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.” (Ufunuo 2:17, NW)
-
-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
20, 21. (a) Ni nini inayofananishwa na kuwapa Wakristo wapakwa-mafuta kijiwe cha mviringo cheupe? (b) Kwa kuwa kuna vijiwe vya mviringo vyeupe 144,000 tu, ni tumaini gani ulilo nalo ule umati mkubwa?
20 Hawa pia wanapokea “kijiwe cha mviringo cheupe.” Katika mahakama za Kiroma vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa katika kupitisha hukumu.b Kijiwe cha mviringo cheupe kilimaanisha ondoleo la hatia, hali kijiwe cha mviringo cheusi kilimaanisha hukumu ya laana, mara nyingi ni ya kifo. Kwa kuwapa Wakristo katika Pargamamu “kijiwe cha mviringo cheupe” Yesu angeonyesha kwamba yeye anawahukumu wao kuwa wasio na hatia, wenye kutakata, na walio safi. Lakini maneno ya Yesu huenda yakawa na maana zaidi. Katika nyakati za Kiroma, vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa pia kuwa tikiti za kupata ruhusa ya kuingia kwenye matukio ya maana. Kwa hiyo kijiwe cha mviringo cheupe huenda kikaonyesha kitu fulani cha pekee sana kwa Mkristo mpakwa-mafuta mwenye kushinda—kuruhusiwa kwake kuingia mahali penye heshima katika mbingu kwenye arusi ya Mwana-Kondoo. Ni vijiwe vya mviringo vyeupe kama hivyo 144,000 tu vinavyoandaliwa.—Ufunuo 14:1; 19:7-9.
21 Je! hii inamaanisha kwamba wewe umeachwa bila kufikiriwa ikiwa wewe ni mmoja wa waabudu waandamani wa ule umati mkubwa? Sivyo hata kidogo! Ingawa hupokei kile kijiwe cha mviringo cheupe cha ruhusa ya kuingia mbinguni, huenda wewe, ukivumilia, ukatoka katika dhiki kubwa uwe na sehemu katika kazi yenye kujaa furaha ya kurudisha Paradiso duniani. Watakaoshiriki pamoja nawe kazi hiyo ni waaminifu watakaofufuliwa wa tangu nyakati za kabla ya Ukristo na wale wa kondoo wengine ambao huenda wakawa walikufa hivi majuzi zaidi. Mwishowe, wafu wengine wote waliokombolewa watapendelewa wawe na ufufuo kwenye uhai katika dunia paradiso.—Zaburi 45:16; Yohana 10:16; Ufunuo 7:9, 14.
22, 23. Ni nini maana ya lile jina lililoandikwa juu ya kijiwe cha mviringo cheupe wanalopewa Wakristo wapakwa-mafuta, na hilo lapasa liandae kitia-moyo gani?
22 Ni nini lile jina jipya lenye kuandikwa juu ya kile kijiwe cha mviringo cheupe? Jina ni njia ya kutambulisha mtu na kumtofautisha huyo na wengine. Hawa Wakristo wapakwa-mafuta wanapokea kile kijiwe cha mviringo cheupe baada ya wao kumaliza mwendo wao wa kidunia wakiwa washindi. Kwa wazi, basi, lile jina juu ya kijiwe cha mviringo cheupe linahusiana na pendeleo lao la kuwa wameunganishwa na Yesu mbinguni—cheo cha ukaribu zaidi sana cha utumishi wa kifalme kinachopasa kuthaminiwa kabisa kabisa na kufurahiwa na wale tu wanaorithi Ufalme wa kimbingu. Kwa sababu hiyo, ni jina au mtajo wa ofisi, “ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.”—Linga Ufunuo 3:12.
-
-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 45]
Kijiwe cha mviringo cheupe ni kwa ajili ya wale wanaoruhusiwa kuingia kwenye ndoa ya Mwana-Kondoo
-