Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Kuzunguka tufe lote, watu wa Yehova wakiwa mmoja mmoja na wakiwa kundi, wamepatwa na magumu mengi, mikazo, na minyanyaso, inayofanana na ile aliyoieleza mtume Paulo katika kutoa ithibati ya huduma yake. (2 Wakorintho 11:23-28) Mashahidi wa Yehova wamehitaji “nguvu zinazopita zilizo za kawaida,” ili wavumilie, hasa katika sehemu za vita na jeuri. (2 Wakorintho 4:7, NW) Lakini hata katika hali zenye kujaribu zaidi Mashahidi waaminifu wameweza kusema kama alivyosema Paulo: “Bwana alisimama karibu na mimi na akatia nguvu ndani ya mimi, kwamba kupitia mimi kuhubiri kupate kutimizwa kikamili.” (2 Timotheo 4:17, NW) Ndiyo, Yesu alishinda kwa niaba yao. Naye ataendelea kwenda akishinda kwa niaba yetu, maadamu sisi tunaazimia kukamilisha ushindi wetu wa imani.—1 Yohana 5:4.

      8, 9. (a) Ni ushindi gani ambao kundi la Mashahidi wa Yehova la pote katika tufe limeshiriki? (b) Ni wapi ambako ukuzi wa Mashahidi wa Yehova umekuwa wenye kutokeza kweli kweli?

      8 Kundi la Mashahidi wa Yehova la pote katika tufe limeshiriki ushindi mwingi chini ya mwongozo wa Mfalme walo mwenye kushinda. Kwa kutokeza sana, yeye aliwapa himaya hawa Wanafunzi wa Biblia wasipatwe na utowesho katika 1918, wakati wao wenyewe ‘waliposhindwa’ kwa muda na tengenezo la Shetani la kisiasa. Hata hivyo, katika 1919, alivunja mapingo ya gereza awaache huru, kisha akawahuisha ili wapige mbiu ya habari njema “mpaka kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Ufunuo 13:7; Matendo 1:8, NW.

      9 Kabla na wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, yale Mataifa Mhimili ya kidikteta yalijaribu kufutilia mbali Mashahidi wa Yehova katika mabara mengi ambako viongozi wa kidini, hasa mapadri wa Roma Katoliki, walitoa uungaji-mkono wa waziwazi au usio wa waziwazi kwa madikteta waonezi. Lakini Mashahidi 71,509 waliokuwa wakihubiri wakati vita ilipoanza katika 1939 wakawa 141,606 kufikia mwisho wayo katika 1945, hata ingawa zaidi ya 10,000 walikuwa wametumia miaka mirefu katika magereza na kambi za mateso, na 2,000 hivi walikuwa wameuawa.

  • Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 92]

      Yule Mfalme Apanda kwa Ushindi

      Katika Miaka ya 1930 na 1940, maadui wenye kujikaza walijaribu kufanya ionekane kwamba huduma ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa haramu, yenye uhalifu, au hata yenye kufitini serikali. (Zaburi 94:20) Katika mwaka 1936 pekee, kulikuwako kutiwa mbaroni kulikorekodiwa 1,149 katika United States. Mashahidi walipiga vita ya kesi za kisheria mwendo wote kufikia ile Mahakama Kuu Zaidi Sana, na ufuatao ni baadhi ya ushindi wao mbalimbali wenye kutokeza.

      Katika Mei 3, 1943, Mahakama Kuu Zaidi Sana katika kesi ya Murdock v. Pennsylvania iliamua kwamba Mashahidi hawakuhitaji leseni ili waangushe vitabu kwa pesa. Siku iyo hiyo, ule uamuzi katika kesi ya Martin v. City of Struthers ulishikilia kwamba si kinyume cha sheria kupiga kengele ya mlango wakati wa kushiriki kugawa karatasi na vitu vingine vya kuvumisha habari.

      Katika Juni 14, 1943, Mahakama Kuu Zaidi Sana iliamua katika kesi ya Taylor v. Mississippi kwamba Mashahidi hawakutia moyo utovu wa ushikamanifu kwa serikali kwa kuhubiri kwao. Siku iyo hiyo, katika kesi ya West Virginia State Board of Education v. Barnette, Mahakama hiyo ilishikilia kwamba baraza la shule halikuwa na haki ya kufukuza kutoka shuleni watoto wa Mashahidi wa Yehova waliokataa kusalimu bendera. Kesho yake yenyewe, Mahakama Kuu ya Australia iliyojaa iliondoa marufuku ambayo nchi hiyo iliwekea Mashahidi wa Yehova, hiyo ikitangazwa kuwa “isiyo ya haki, bila sababu nzuri na yenye uonevu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki