Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Faraja ya Kweli Inaweza Kupatikana Wapi?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Mei 1
    • Msaada Wakati wa Mateso Makali

      15. (a) Wakristo wamekabili magumu gani zamani na wakati huu? (b) Kwa nini wale wanaotoa kitia-moyo huenda nyakati nyingine wakahitaji kutiwa moyo?

      15 Wote waliojitoa kwa Yehova na walio waaminifu kwake watanyanyaswa kwa njia fulani. (2 Timotheo 3:12) Hata hivyo, Wakristo wengi wamepatwa na mateso makali sana. Wakati wetu, baadhi yao wameshambuliwa na watu wenye ghasia na kupelekwa kwenye kambi za mateso, magereza, kambi za kazi ngumu, ambako wametendwa kinyama. Serikali nyingine zimewatesa au kuruhusu watu fulani wasiotii sheria wawatende Wakristo kwa jeuri pasipo kuwaadhibu.

  • Faraja ya Kweli Inaweza Kupatikana Wapi?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Mei 1
    • 16. Daudi alipata msaada gani alipokabili magumu?

      16 Mfalme Sauli alipotaka kumwua Daudi, Daudi alimwendea Mungu ili kupata msaada: “Ee Mungu, uyasikie maombi yangu,” aliomba. “Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako.” (Zaburi 54:2, 4; 57:1) Je, Daudi alipata msaada? Ndiyo. Pindi hiyo, Yehova alimtuma nabii Gadi na kuhani Abiathari kumpa Daudi mwongozo, na Yonathani, mwana wa Sauli, amwimarishe mwanamume huyo kijana. (1 Samweli 22:1, 5; 23:9-13, 16-18) Yehova aliwaruhusu pia Wafilisti kushambulia nchi hiyo, hivyo alimkengeusha Sauli asimfuate Daudi.—1 Samweli 23:27, 28.

      17. Yesu alipata wapi msaada alipokabili mateso makali?

      17 Yesu Kristo mwenyewe aliteswa vikali alipokaribia kufa. Alijua kabisa matokeo ambayo mwenendo wake ungeleta kwa jina la Baba yake wa mbinguni na wakati ujao wa wanadamu wote. Alisali kwa bidii, hata ‘aliingia katika maumivu makali.’ Mungu alihakikisha kwamba Yesu alipata msaada aliohitaji wakati huo mgumu.—Luka 22:41-44.

      18. Mungu aliwapa Wakristo wa mapema walioteswa vikali faraja gani?

      18 Baada ya kutaniko la karne ya kwanza kuanzishwa, Wakristo waliteswa vikali sana hivi kwamba wote walitawanyika, na mitume peke yao ndio waliobaki Yerusalemu. Wanaume na wanawake waliburutwa kutoka katika nyumba zao. Mungu aliwafariji jinsi gani? Aliwahakikishia kupitia Neno lake kwamba walikuwa na “miliki bora na yenye kudumu,” yaani, urithi wa milele wa mbinguni pamoja na Kristo. (Waebrania 10:34; Waefeso 1:18-20) Walipoendelea kuhubiri, waliona uthibitisho kwamba roho ya Mungu ilikuwa pamoja nao, na yale waliyojionea yaliwapa sababu nyingine ya kufurahi.—Mathayo 5:11, 12; Matendo 8:1-40.

      19. Ingawa Paulo aliteswa vikali, alihisije kuhusu faraja ambayo Mungu hutoa?

      19 Hatimaye, Sauli (Paulo), aliyekuwa mtesi mkali, aliteswa pia kwa sababu alikuwa amegeuka na kuwa Mkristo. Kwenye kisiwa cha Saiprasi, kulikuwa na mlozi aliyejaribu kumzuia Paulo asiendelee na huduma yake kwa kutumia ulaghai na udanganyifu. Huko Galatia, watu walimpiga Paulo kwa mawe na kumwacha wakiwazia alikuwa amekufa. (Matendo 13:8-10; 14:19) Huko Makedonia alipigwa kwa fito. (Matendo 16:22, 23) Baada ya kushambuliwa na watu wenye ghasia huko Efeso aliandika hivi: “Tulikuwa chini ya mkazo mkali mno upitao nguvu yetu, hivi kwamba tulikuwa bila hakika kabisa hata juu ya uhai wetu. Kwa kweli, tulihisi ndani yetu wenyewe kwamba tulikuwa tumeipokea hukumu ya kifo.” (2 Wakorintho 1:8, 9) Lakini katika barua hiyohiyo, Paulo aliandika maneno yenye kufariji yaliyonukuliwa katika fungu la 2 la makala hii.—2 Wakorintho 1:3, 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki