-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Peru
Jorge ni painia wa kawaida naye hufanya kazi ya uchoraji. Alimhubiria mchoraji mwingine aitwaye Hubert, aliyekubali kujifunza Biblia. Licha ya upinzani mkali kutoka kwa familia, marafiki, na majirani, Hubert alimaliza kujifunza kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele katika muda wa miezi sita tu. Katika sala zake, alimwomba Yehova asaidie familia yao kujifunza kweli. Alishangaa na kufurahi wakati kaka yake Jhon alipoanza kujifunza na kuhudhuria mikutano. Juma lililofuata, Cesar, shemeji yake alianza kujifunza pia. Na ingawa mke wake alimpinga mwanzoni, yeye pia alianza kujifunza. Baadaye, Reynaldo aliyesomea shule moja na Hubert, alitaka kujifunza. Kwa sababu ya upinzani mkali alilazimika kujifunzia nyumbani kwa Hubert. Muda mfupi baadaye, Milton, ndugu mdogo wa Hubert, alianza kujifunza. Baada ya kujifunza mara moja tu, Milton aliwahubiria wanafunzi wawili, Darwin na Christian, ambao alisoma nao shuleni na wakaanza kujifunza na kuhudhuria mikutano. Hubert ana kaka wengine wawili, Ronald na Martin. Ronald alihudhuria funzo la Hubert akiwa na orodha ndefu ya maswali ya Biblia. Jorge alimweleza kuwa atajibiwa maswali hayo yote akijifunza Biblia, naye akakubali. Martin naye alianza kujifunza na binti zake wawili wakajiunga naye. Hubert na Jhon walibatizwa kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Ukombozi Unakaribia!” Habari za karibuni zinaonyesha kwamba watu 18 wamejifunza kumhusu Yehova kwa sababu ya ule ushahidi wa kwanza uliotolewa na Jorge.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 57]
Hubert, Jorge, na Jhon
-