Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya Petro
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • Katika barua yake ya pili, iliyoandikwa muda mfupi tu baada ya ile ya kwanza, Petro anawatia moyo waamini wenzake wakazie uangalifu neno la Mungu na anawaonya kuhusu kuja kwa siku ya Yehova.

  • Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya Petro
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • “SIKU YA YEHOVA ITAKUJA”

      (2 Pet. 1:1–3:18)

      Petro anaandika hivi: “Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” Kukazia uangalifu neno la unabii kunaweza kutulinda tusidanganywe na “walimu wa uwongo” na watu wengine wapotovu.—2 Pet. 1:21; 2:1-3.

      Petro anaonya hivi: “Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki na dhihaka zao.” Lakini “siku ya Yehova itakuja kama mwizi.” Petro anamalizia barua yake kwa kutoa mashauri mazuri kwa wale ‘wanaongojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova.’—2 Pet. 3:3, 10-12.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      1:19—Ni nani aliye “nyota ya mchana,” anachomoza wakati gani, na tunajua jinsi gani kwamba jambo hilo tayari limetukia? “Nyota ya mchana” ni Yesu Kristo akiwa katika mamlaka ya Ufalme. (Ufu. 22:16) Katika mwaka wa 1914, Yesu alichomoza mbele ya uumbaji wote akiwa Mfalme wa Kimasihi, na hivyo kutangaza mapambazuko ya siku mpya. Kugeuka sura kulionyesha kimbele utukufu wa Yesu na mamlaka ya Ufalme, na hivyo kukazia kwamba neno la Mungu la kinabii linategemeka. Kukazia uangalifu neno hilo kunatia mwangaza katika mioyo yetu, na hivyo tunajua kwamba Nyota ya Mchana amechomoza.

      2:4—“Tartaro” ni nini, na malaika waasi walitupwa humo wakati gani? Tartaro ni hali kama ya gereza ambamo ni viumbe wa roho tu wanazuiliwa, bali si wanadamu. Ni hali ya giza tititi la akili kuhusiana na makusudi matukufu ya Mungu. Wale walio katika Tartaro hawana tumaini lolote la wakati ujao. Mungu aliwatupa malaika waasi ndani ya Tartaro katika siku za Noa, na watabaki katika hali hiyo ya kushushwa mpaka watakapoharibiwa.

      3:17—Petro alimaanisha nini alipotaja ‘ujuzi wa kimbele’? Petro alikuwa akizungumza kuhusu ujuzi wa kimbele wa matukio ya wakati ujao, ambao yeye na waandikaji wengine wa Biblia walipewa kwa mwongozo wa roho ya Mungu. Kwa kuwa ujuzi huo haukuwa na mipaka, Wakristo wa mapema waliokuwa nao hawakujua mambo yote kuhusu matukio ya wakati ujao. Walijua tu mambo ya jumla ambayo yalitarajiwa.

      Mambo Tunayojifunza:

      1:2, 5-7. Zaidi ya kutusaidia kuongeza “ujuzi sahihi juu ya Mungu na Yesu,” kujitahidi sana kusitawisha sifa kama vile imani, uvumilivu, na ujitoaji-kimungu kunaweza ‘kutuzuia kuwa ama wasiotenda au wasiozaa matunda’ kuhusiana na ujuzi huo.—2 Pet. 1:8.

      1:12-15. Ili tubaki tukiwa ‘tumewekwa imara katika kweli,’ kila mara tunahitaji vikumbusho, kama vile tunavyopokea kupitia mikutano yetu ya kutaniko, funzo la kibinafsi, na usomaji wa Biblia.

      2:2. Tunapaswa kuwa waangalifu ili mwenendo wetu usimletee suto Yehova na tengenezo lake.—Rom. 2:24.

      2:4-9. Kwa sababu ya mambo ambayo alifanya wakati uliopita, tunaweza kuwa na uhakika wa kwamba “Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa watu wenye ujitoaji-kimungu kutoka katika jaribu, lakini kuwaweka akiba watu wasio waadilifu kwa ajili ya ile siku ya hukumu ili wakatiliwe mbali.”

      2:10-13. Ingawa “watukufu,” yaani, wazee Wakristo, wana kasoro na huenda nyakati nyingine wakakosea, hatupaswi kuwatukana.—Ebr. 13:7, 17.

      3:2-4, 12. Kukazia karibu akilini “maneno yaliyosemwa hapo zamani na manabii watakatifu na amri ya Bwana na Mwokozi” kutatusaidia kukumbuka kwamba siku ya Yehova imekaribia sana.

      3:11-14. Tukiwa watu ambao ‘wanangojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova,’ ni lazima (1) ‘tuwe watakatifu katika mwenendo,’ tukidumisha usafi wa kimwili, kiakili, kiadili, na kiroho; (2) tuwe na matendo mengi ya “ujitoaji-kimungu,” kama yale yanayohusiana na kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi; (3) tuwe na mwenendo na utu ‘usio na doa,’ usiochafuliwa na ulimwengu; (4) tuwe “bila dosari,” kwa kufanya mambo yote kwa nia nzuri; na (5) tuwe “katika amani”—amani pamoja na Mungu, pamoja na ndugu zetu Wakristo, na pamoja na wanadamu wenzetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki