-
Ule Uasi-imani Mkubwa WasitawiMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Lakini mara mitume walipokufa, taraja la Kikristo la kuwapo kwa Kristo na kuja kwa Ufalme wake lilififia. Kwa nini?
Sababu moja ilikuwa kuchafuliwa kiroho kulikosababishwa na fundisho la Kigiriki la kutokufa kwa nafsi. Kwa kadiri lilivyotia mizizi miongoni mwa Wakristo, tumaini la mileani liliachiliwa hatua kwa hatua. Kwa nini? The New International Dictionary of New Testament Theology chaeleza hivi: “Fundisho la kutokufa kwa nafsi liliingia kuchukua mahali pa eskatolojia [fundisho juu ya “Mambo ya Mwisho”] ya AJ [Agano Jipya] pamoja na tumaini layo la ufufuo wa wafu na uumbaji upya (Ufu. 21 mistari inayofuata), hivi kwamba nafsi hupokea hukumu baada ya kifo na hufikia paradiso ambayo sasa hufikiriwa kuwa ya ulimwengu mwingine.” Yaani, Wakristo waasi-imani walifikiri kwamba nafsi iliendelea kuwa hai baada ya mwili kufa na kwamba kwa hiyo baraka za Utawala wa Mileani wa Kristo lazima ziwe zahusiana na makao ya roho. Hivyo walihamisha Paradiso kutoka duniani hadi mbinguni, ambako, wao waliamini, ndiko nafsi iliyookolewa huenda wakati wa kufa. Basi, hakukuwa na uhitaji wa kuwa macho kutazamia kuwapo kwa Kristo na kuja kwa Ufalme wake, kwa kuwa wakati wa kufa wote walitumaini kujiunga na Kristo mbinguni.g
-
-
Ule Uasi-imani Mkubwa WasitawiMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mwanafalsafa Mgiriki Plato (aliyezaliwa kama 428 K.W.K.) hakuwa na njia ya kujua kwamba hatimaye mafundisho yake yangepata njia ya kuingia ndani ya Ukristo ulioasi imani. Mambo makuu ambayo Plato aliuchangia “Ukristo” yalihusu mafundisho ya Utatu na kutokufa kwa nafsi.
-
-
Ule Uasi-imani Mkubwa WasitawiMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kuhusu fundisho la nafsi isiyoweza kufa, “New Catholic Encyclopedia” yasema: “Dhana ya Kikristo ya nafsi ya kiroho iliyoumbwa na Mungu na kutiwa katika mwili wakati wa mtungo wa mimba ili kufanyiza mwanadamu kuwa kitu kizima kilicho hai ni tunda la usitawi wa muda mrefu wa falsafa ya Kikristo. Ni kupitia Origen tu [aliyekufa kama 254 W.K.] katika Mashariki na Mt. Augustine [aliyekufa 430 W.K.] katika Magharibi kwamba nafsi ikathibitishwa kuwa namna ya kiroho na dhana ya kifalsafa iliyofanyizwa kutoka asili yayo. . . . Fundisho lake [la Augustine] . . . lilikuwa na mambo mengi (kutia na makosa fulanifulani) kutokana na mawazo mapya ya Plato.”—Buku la 13, kurasa 452, 454.
-