-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hotuba za Biblia zilizorekodiwa zilikuwa na sehemu ya maana pia wakati wa miaka ya 1930 na mapema katika miaka ya 1940. Katika 1934 baadhi ya Mashahidi walianza kuchukua kinanda kinachobebeka walipoenda kutoa ushahidi. Mashine hiyo ilikuwa nzito kidogo, kwa hiyo wangeiweka katika gari lao au waiache mahali panapofaa hadi walipopata watu waliotaka kusikiliza hotuba ya Biblia iliyorekodiwa. Kisha, katika 1937, utumizi wa kinanda kinachobebeka kwenye milango ulianzishwa. Utaratibu ulikuwa rahisi: Baada ya Shahidi kusema kwamba alikuwa na ujumbe wa maana wa Biblia, angeweka sindano juu ya rekodi na kuiacha izungumze. Kasper Keim, painia Mjerumani aliyetumikia katika Uholanzi, alishukuru sana kwa “Haruni” wake, kama vile alivyoita kinanda hicho, kwa sababu aliona vigumu kutoa ushahidi katika Kiholanzi. (Linganisha Kutoka 4:14-16.) Kwa sababu ya udadisi, nyakati nyingine familia nzimanzima zingesikiliza rekodi hizo.
Kufikia 1940, zaidi ya vinanda 40,000 vilikuwa vikitumiwa. Mwaka huo aina mpya ya kinanda kilichokuwa wima kilichobuniwa na kuundwa na Mashahidi, kilitokezwa na kilitumiwa hususa katika mabara ya Amerika. Kilichochea udadisi mkubwa hata zaidi kwa sababu wenye nyumba hawangeweza kuona rekodi yenyewe ilipokuwa ikichezwa. Kila rekodi ilikuwa na mwendo wa mara 78 kwa dakika na ilikuwa na urefu wa dakika nne na nusu. Vichwa vilikuwa vifupi na vya moja kwa moja: “Ufalme,” “Sala,” “Njia Inayoenda Kwenye Uhai,” “Utatu,” “Purgatori,” “Sababu Kwa Nini Makasisi Hupinga Kweli.” Hotuba tofauti zaidi ya 90 zilirekodiwa; rekodi zaidi ya milioni zilitumiwa. Utoaji ulikuwa waziwazi na rahisi kuelewa. Wenye nyumba wengi walisikiliza kwa uthamini; wachache waliitikia kwa jeuri. Lakini ushahidi wenye matokeo na wenye kupatana ulikuwa ukitolewa.
-
-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufikia 1933 walikuwa wakitumia mashine zenye nguvu za kurekodia ili kucheza mirekodio ya moja kwa moja ya hotuba za Biblia hadharani. Ndugu Smets na Poelmans walibeba vifaa vyao kwa baiskeli ya miguu mitatu na kusimama kando yayo huku likitoa ujumbe kwa sauti katika sehemu za soko na karibu na makanisa katika Liège, Ubelgiji. Mara nyingi walifanya hivyo kwa muda wa saa kumi kila siku. Kwa kuwa watu katika Jamaika wangekusanyika upesi waliposikia muziki, kwa hiyo akina ndugu huko walicheza muziki kwanza. Umati mkubwa ulipomiminika kutoka mashambani hadi kwenye barabara kuu ili kuona yale yaliyokuwa yakiendelea, wangewapata Mashahidi wa Yehova wakitoa ujumbe wa Ufalme.
Vifaa vingine vya kurekodia viliwekwa katika magari na mashua, vikuza-sauti vikiwa juu yazo ili sauti iende mbali zaidi. Bert na Vi Horton, katika Australia, waliendesha gari lenye honi kubwa juu yayo iliyoandikwa maneno “Ujumbe wa Ufalme.” Mwaka mmoja walifanya karibu kila barabara katika Melbourne ijae sauti ya kufunuliwa kwa dini bandia kwa njia yenye kuchochea na maelezo yenye kuchangamsha moyo ya baraka za Ufalme wa Mungu. Wakati wa miaka hiyo Claude Goodman alikuwa akipainia katika India. Utumizi wa gari la kuvumisha habari, lenye rekodi katika lugha za wenyeji, kulimwezesha kufikia watu wengi katika mabaraza, bustanini, kando ya barabara—mahali popote ambapo watu wangeweza kupatikana.
Wakati ndugu katika Lebanoni walipoegesha gari la kuvumisha habari kwenye kilima na wakatangaza mihadhara, sauti hiyo ilienda hadi kwenye mabonde. Nyakati nyingi watu walio vijijini wangeogopa kwa sababu hawangeweza kuona chanzo cha sauti huku wakifikiri kwamba Mungu alikuwa akizungumza nao kutoka mbinguni!
Hata hivyo, kulikuwa na nyakati ambapo ndugu waliona wasiwasi. Katika pindi moja, katika Siria, padri wa kijiji aliacha chakula chake mezani, akachukua fimbo yake kubwa ya kutembelea, na kukimbia nje hadi kwenye umati uliokuwa umekusanyika kusikiliza hotuba ya Biblia iliyotolewa kutoka kwa gari la kuvumisha habari. Huku akitikisa fimbo yake kwa hasira na kupiga kelele, aliamuru: “Komeni! Ninawaamuru nyinyi mkome!” Lakini ndugu waling’amua kwamba si kila mtu aliyekubaliana naye; kuna wale waliotaka kusikia. Upesi, baadhi ya watu katika umati walimwinua padri juujuu na kumbeba hadi nyumbani mwake, ambamo walimweka tena kwenye meza ya chakula! Kujapokuwa upinzani wa makasisi, Mashahidi walihakikisha kwamba watu walikuwa na fursa ya kusikiliza.
-