-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Nyimbo za Sifa
14. (a) Wale viumbe hai wanne na wazee 24 wanatendaje kwa kuitikia kutwaa kwa Yesu hati-kunjo? (b) Ile habari ambayo Yohana anapokea kuhusu wale wazee 24 inathibitishaje utambulisho na cheo chao?
14 Wale wengine mbele ya kiti cha ufalme cha Yehova wanatendaje kwa kuitikia? “Na wakati alipotwaa ile hati-kunjo, wale viumbe hai wanne na wale wazee ishirini na wanne walianguka chini mbele ya Mwana-Kondoo, kila mmoja akiwa na kinubi na mabakuli ya dhahabu yaliyokuwa yamejaa uvumba, na huo uvumba humaanisha sala za watakatifu.” (Ufunuo 5:8, NW) Kama wale viumbe hai wanne wa kikerubi mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu, wazee 24 wanainamia Yesu katika kukiri mamlaka yake. Lakini hao wazee wako peke yao katika kuwa na vinubi na mabakuli ya uvumba.a Na wao peke yao sasa waimba wimbo mpya. (Ufunuo 5:9) Hivyo wanafanana na wale 144,000 wa “Israeli wa Mungu” watakatifu, ambao pia wanabeba vinubi na kuimba wimbo mpya. (Wagalatia 6:16; Wakolosai 1:12; Ufunuo 7:3-8; 14:1-4) Na zaidi, wale wazee 24 wanaonyeshwa wakitimiza utendaji wa kikuhani wa kimbingu, uliofananishwa na ule wa makuhani katika Israeli wa kale ambao walimchomea Yehova uvumba katika ile tabenakulo—utendaji ambao ulikwisha wakati Yehova alipoioondolea mbali ile Sheria ya Musa, akiigongomelea penye nguzo ya mateso ya Yesu. (Wakolosai 2:14) Tunakata neno gani kutokana na haya yote? Kwamba hapa wale washindi wapakwa-mafuta wanaonekana wakiwa katika mgawo wao wa mwisho kabisa wakiwa ‘makuhani wa Mungu na wa Kristo, wakitawala wakiwa wafalme pamoja naye kwa miaka elfu.’—Ufunuo 20:6, NW.
15. (a) Katika Israeli, ni nani pekee aliyependelewa kuingia ndani ya Patakatifu Zaidi Sana pa ile tabenakulo? (b) Ni kwa nini ilikuwa ni uhai au kifo kwamba kuhani mkuu achome uvumba mbele ya kuingia ndani ya Patakatifu Zaidi Sana?
15 Katika Israeli wa kale, kuhani mkuu pekee ndiye aliyeruhusiwa kuingia Patakatifu Zaidi Sana mbele za kuwapo kwa ufananisho kwa Yehova. Kwake yeye, kupeleka uvumba kulikuwa ni uhai au kifo. Sheria ya Yehova ilisema: “Ni lazima [Haruni] achukue kishika-moto kilichojaa makaa-mawe yenye kuwaka moto kutoka madhabahu mbele za Yehova, na mavungu mawili ya mikono yake yakiwa yamejaa uvumba mzuri uliotiwa manukato, na yeye lazima avilete ndani ya pazia. Ni lazima pia atie uvumba juu ya moto mbele za Yehova, na wingu la uvumba lazima litande juu ya funiko la Arka, lililo juu ya Agano, ili asije akafa.” (Walawi 16:12, 13, NW) Haikuwezekana kuhani mkuu apenye kwa kufaulu ndani ya Patakatifu Zaidi Sana isipokuwa yeye alichoma uvumba.
16. (a) Katika mfumo wa mambo wa Kikristo, ni nani wanaopenya ndani ya Patakatifu Zaidi Sana palipofananishwa? (b) Ni kwa nini Wakristo wapakwa-mafuta sharti ‘wachome uvumba’?
16 Katika mfumo wa mambo wa Kikristo, anayepata kuingia Patakatifu Zaidi Sana palipofananishwa, mahali pa kuwapo kwa Yehova katika mbingu, si Kuhani Mkuu tu aliyefananishwa, yaani, Yesu Kristo, bali hatimaye kila mmoja wa makuhani wa chini 144,000 pia hupata kupaingia. (Waebrania 10:19-23) Mwingio ndani wa hapa Patakatifu Zaidi Sana hauwezekani kwa makuhani hawa, kama wanavyowakilishwa hapa na wale wazee 24, isipokuwa wao ‘wachome uvumba,’ yaani, watoe sala na dua kwa Yehova kwa kuendelea.—Waebrania 5:7; Yuda 20, 21; linga Zaburi 141:2.
-
-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
19. (a) Ni baraka gani ambazo Israeli wa kimnofu walishindwa kupata kwa sababu ya kutoaminika kwao? (b) Taifa jipya la Yehova linapata kufurahia baraka gani?
19 Wakati Yehova alipofanyiza Waisraeli wa kale kuwa taifa huko nyuma katika siku za Musa, yeye alifanya agano pamoja nao na akaahidi kwamba ikiwa wao wangebaki wakiwa waaminifu kwa agano hilo, wao wangekuwa ufalme wa makuhani mbele zake. (Kutoka 19:5, 6) Waisraeli hawakuwa waaminifu na kwa hiyo hawakupata kamwe utimizo wa ahadi hiyo. Kwa upande mwingine, taifa jipya, lililofanyizwa kwa thamani ya agano jipya lenye kupatanishwa na Yesu, limebaki likiwa jaminifu. Basi washiriki walo wanapata kutawala juu ya dunia wakiwa wafalme na pia wanatumikia wakiwa makuhani, wakisaidia wale wenye mioyo inayofaa miongoni mwa aina ya binadamu wapatanishwe kwa Yehova. (Wakolosai 1:20) Ni kama vile ule wimbo mpya unavyoonyesha hilo: “Na wewe ulifanya wao kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao wanapaswa kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:10, NW) Hao wazee 24 wana shangwe kama nini katika kuimba huu wimbo mpya wa sifa kwa Yesu Kristo aliyetukuzwa!
-
-
“Ni Nani Ambaye Anastahili Kufungua Hati-Kunjo?”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 86]
-