Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Yeye anawasifu, akisema: “Mimi najua matendo yako—tazama! mimi nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, ambao hakuna mmoja awezaye kufunga—kwamba wewe una nguvu chache, na wewe ulishika neno langu na hukuthibitika kuwa bandia kwa jina langu.” (Ufunuo 3:8, NW) Kundi limekuwa lenye kutenda, nao mlango umefunguliwa mbele yalo—bila shaka mlango wa nafasi ya utumishi wa kihuduma. (Linga 1 Wakorintho 16:9; 2 Wakorintho 2:12.) Kwa hiyo, Yesu analitia moyo kundi litumie kwa faida kamili ile nafasi ya kuhubiri. Wao wamevumilia na kuonyesha kwamba wana nguvu za kutosha, kwa msaada wa roho ya Mungu, kuendelea kufanya “matendo” zaidi katika utumishi wa Yehova. (2 Wakorintho 12:10; Zekaria 4:6) Wametii amri za Yesu nao hawakumkana Kristo ama kwa neno ama kwa tendo.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao hudai kuwa Wayahudi wa kiroho, waliongoza kwa hila watawala wakandamize Wakristo wa kweli. Hata hivyo, hao walijaribu sana ‘kushika neno la uvumilivu wa Yesu’; kwa sababu hiyo, kwa msaada wa kiroho, “nguvu chache” zenye maana, waliokoka na wakaamshwa waingie kupitia mlango ambao sasa ulifunguliwa mbele yao. Katika njia gani?

      “Mlango Uliofunguliwa”

      18. Ni kuweka rasmi gani alikofanya Yesu katika 1919, na hivyo mwekwa alikuwaje kama mtumishi wa nyumba mwaminifu wa Hezekia?

      18 Katika 1919 Yesu alitimiza ahadi yake na kukitambua kile kikosi kidogo cha Wakristo wapakwa-mafuta cha kweli kuwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wake. (Mathayo 24:45-47) Hao waliingia ndani ya pendeleo linalofanana na lile alilofurahia Eliakimu mtumishi wa nyumba mwaminifu katika wakati wa Hezekia.d Yehova alisema hivi kwa habari ya Eliakimu: “Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.” Eliakimu alibeba begani madaraka mazito kwa ajili ya Hezekia, yule mwana wa kifalme wa Daudi. Hali moja na hiyo leo, jamii ya Yohana ya wapakwa-mafuta imewekelewa begani mwayo “ufunguo wa nyumba ya Daudi” katika maana ya kwamba wameaminishwa masilahi ya kidunia ya Ufalme wa Kimesiya. Yehova ameimarisha watumishi wake kwa ajili ya pendeleo hili, akiongezea nguvu chache zao kuwa nishati yenye msukumo inayotosha kwa ushuhuda mkubwa wa tufe lote.—Isaya 22:20, 22; 40:29.

      19. Jamii ya Yohana ilishughulikiaje madaraka ambayo ilipewa na Yesu katika 1919, kukiwa na tokeo gani?

      19 Tangu 1919 na kuendelea mabaki ya wapakwa-mafuta, wakifuata kielelezo cha Yesu, walianzisha kampeni yenye bidii ya kutangaza kotekote habari njema za Ufalme. (Mathayo 4:17; Warumi 10:18) Kama tokeo, wengine wa lile sinagogi la Shetani la ki-siku-hizi, Jumuiya ya Wakristo, walijia baki hili la wapakwa-mafuta, wakatubu na ‘wakainama,’ wakikiri mamlaka ya mtumwa huyo. Wao vilevile walikuja kutumikia Yehova katika muungano na wale wazee-wazee wa jamii ya Yohana. Hilo liliendelea mpaka hesabu kamili ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu wakakusanywa. Kufuatia hili, “umati mkubwa . . . kutoka mataifa yote” umekuja ‘ukainamia’ mtumwa mpakwa-mafuta. (Ufunuo 7:3, 4, 9, NW) Pamoja, mtumwa huyu na huu umati mkubwa wanatumikia wakiwa kundi moja la Mashahidi wa Yehova.

      20. Ni kwa nini hasa leo lazima Mashahidi wa Yehova wawe thabiti katika imani na watendaji katika utumishi wa Mungu?

      20 Wakiwa na umoja kama wale Wakristo katika Filadelfia katika kifungo cha shauku halisi ya kidugu, Mashahidi wa Yehova leo wanathamini kwamba kazi yao ya kuhubiri lazima ifanywe kwa hima. Upesi, ile dhiki kubwa itavua pazia la ulimwengu mbovu wa Shetani. Wakati huo, kila mmoja wetu na apatikane akiwa mwenye nguvu katika imani na akitenda katika utumishi wa Mungu, ili majina yetu yasifutwe kutoka kitabu cha uhai cha Yehova. (Ufunuo 7:14) Acheni tulichukue kwa uzito sana onyo ambalo Yesu alilipa kundi katika Filadelfia ili tuweze kushikilia kwa imara mapendeleo yetu ya utumishi na kufikilia thawabu ya uhai wa milele.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • b Gazeti Mnara wa Mlinzi linalotangazwa na jamii ya Yohana, limeendelea kukazia umuhimu wa kutwaa nafasi hii na kushiriki kikamilifu kadiri iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri; mathalani, ona makala “Wote na Wautangaze Utukufu wa Yehova” na “Sauti Yao Ilifika Katika Dunia Yote” katika toleo la Januari 1, 2004. Katika toleo la Juni 1, 2004, katika makala “Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa,” mkazo uliwekwa juu ya kuingia “mlango uliofunguliwa” ndani ya utumishi wa wakati wote. Kulikuwako kilele cha mapainia 1,093,552 walioripoti utumishi kama huo katika pindi ya mwezi mmoja katika 2005.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Chati katika ukurasa wa 64]

      Katika 1919 yule Mfalme anayetawala Yesu alifungua mlango wa nafasi kwa utumishi wa Kikristo. Nambari yenye kuongezeka ya Wakristo waliojitoa wametumia kwa faida nafasi hiyo.

      Mabara Wakristo Wahubiri

      Yaliyofikiwa Walioshiriki wa Wakati

      Mwaka kwa Kuhubiri Katika Kuhubirie Wotef

      1918 14 3,868 591

      1928 32 23,988 1,883

      1938 52 47,143 4,112

      1948 96 230,532 8,994

      1958 175 717,088 23,772

      1968 200 1,155,826 63,871

      1978 205 2,086,698 115,389

      1988 212 3,430,926 455,561

      1998 233 5,544,059 698,781

      2005 235 6,390,022 843,234

      [Maelezo ya Chini]

      e Tarakimu zilizo juu ni wastani wa kila mwezi.

      f Tarakimu zilizo juu ni wastani wa kila mwezi.

      [Picha katika ukurasa wa 65]

      Utendaji wa Mashahidi wa Yehova unatolewa kwa moyo mzima wote. Mathalani, fikiria zile saa ambazo wametumia katika kuhubiri na kufundisha na ile hesabu kubwa mno ya mafunzo ya Biblia bila malipo ambayo wameongoza katika nyumba za watu.

      Saa Zilizotumiwa Mafunzo ya Biblia

      Kuhubiri Yaliyoongozwa

      Mwaka (Jumla ya Mwaka) (Wastani wa Mwezi)

      1918 19,116 Hayakurekodiwa

      1928 2,866,164 Hayakurekodiwa

      1938 10,572,086 Hayakurekodiwa

      1948 49,832,205 130,281

      1958 110,390,944 508,320

      1968 208,666,762 977,503

      1978 307,272,262 1,257,084

      1988 785,521,697 3,237,160

      1998 1,186,666,708 4,302,852

      2005 1,278,235,504 6,061,534

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki