-
Iga Subira ya YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
-
-
Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake, kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Petro 3:8, 9)
-
-
Iga Subira ya YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
-
-
6. Hatupaswi kukata kauli gani kumhusu Mungu, na kwa nini?
6 Ni kweli kwamba si rahisi kungojea kitu ambacho mtu anataka sana. (Methali 13:12) Hivyo, watu wanapokosa kutimiza ahadi zao haraka, wengine wanaweza kukata kauli kwamba hawataki kuzitimiza. Tukiwa na maoni hayo kumhusu Mungu, basi tutakuwa tumekosa hekima sana! Tukielewa vibaya subira ya Mungu kwa kuona kwamba amekawia, baada ya muda tunaweza kuanza kuwa na shaka, tuvunjike moyo, na kulegea kiroho. Hata tunaweza kupotoshwa na watu ambao Petro alikuwa amewaonya Wakristo wajihadhari nao, yaani, wadhihaki, wale wasio na imani. Watu hao husema hivi kwa dhihaka: “Huku kuwapo kwake kulikoahidiwa kuko wapi? Kwani, tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji.”—2 Petro 3:4.
-