Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—II
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
    • 40:3–47:12—Hekalu la maono ya Ezekieli linafananisha nini? Kwa kweli, hekalu hilo kubwa sana ambalo Ezekieli anaona katika maono halikujengwa kamwe. Linafananisha Hekalu la kiroho la Mungu—mpango wake ulio kama hekalu kwa ajili ya ibada safi katika siku zetu. (Ezekieli 40:2; Mika 4:1; Waebrania 8:2; 9:23, 24) Maono ya hekalu yanatimizwa katika “siku za mwisho” wakati ambapo ukuhani unasifishwa. (2 Timotheo 3:1; Ezekieli 44:10-16; Malaki 3:1-3) Hata hivyo, utimizo wa mwisho wa maono hayo utakuwa katika Paradiso. Hekalu la maono ya Ezekieli liliwapa Wayahudi waliohamishwa ahadi ya kwamba ibada safi itarudishwa na kwamba kila familia ya Kiyahudi itapata urithi wake katika nchi.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—II
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
    • 43:13-20—Madhabahu ambayo Ezekieli aliona katika maono inafananisha nini? Madhabahu hiyo inafananisha mapenzi ya Mungu kuhusiana na dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo. Kwa sababu ya uandalizi huo, watiwa-mafuta wanatangazwa kuwa waadilifu, nao “umati mkubwa” una msimamo safi machoni pa Mungu. (Ufunuo 7:9-14; Waroma 5:1, 2) Labda hiyo ndiyo sababu “bahari ya kuyeyushwa” ya hekalu la Sulemani, yaani, beseni kubwa la maji ambalo makuhani walitumia kuoga, haiko katika hekalu hilo la maono.—1 Wafalme 7:23-26.

      44:10-16—Ni nani wanaofananishwa na jamii ya kikuhani? Jamii ya kikuhani ilionyesha kimbele kikundi cha Wakristo watiwa-mafuta katika siku zetu. Walisafishwa mnamo 1918 Yehova alipoketi “kama msafishaji na mtakasaji” katika hekalu la kiroho. (Malaki 3:1-5) Wale waliokuwa safi au waliotubu wangedumisha pendeleo lao la utumishi. Baada ya hilo, walihitaji kujitahidi sana kuendelea kujitunza “bila doa kutokana na ulimwengu,” na hivyo kuuwekea mfano “umati mkubwa,” unaofananishwa na makabila yasiyo ya kikuhani.—Yakobo 1:27; Ufunuo 7:9, 10.

      45:1; 47:13–48:29—“Nchi” na kugawanywa kwa nchi kunafananisha nini? Nchi inafananisha eneo la utendaji la watu wa Mungu. Haidhuru anaishi wapi, mwabudu wa Yehova yumo katika nchi iliyorudishwa mradi tu anaunga mkono ibada ya kweli. Kugawanywa kwa nchi kutatimizwa mara ya mwisho katika ulimwengu mpya wakati kila mtu mwaminifu atakapopewa urithi wake.—Isaya 65:17, 21.

      Ezekieli 45:7, 16—Ni nini kinachoonyeshwa na mchango ambao watu wanatoa kwa ajili ya jamii ya kikuhani na kwa mkuu? Katika hekalu la kiroho, hilo hasa linaonyesha utegemezo wa kiroho, yaani, kutoa msaada na kuonyesha roho ya ushirikiano.

      47:1-5—Ni nini kinachofananishwa na maji ya mto ambao Ezekieli anaona katika maono? Maji hayo yanafananisha uandalizi wa Yehova kwa ajili ya uzima, kutia ndani dhabihu ya fidia ya Kristo Yesu na ujuzi juu ya Mungu unaopatikana katika Biblia. (Yeremia 2:13; Yohana 4:7-26; Waefeso 5:25-27) Kina cha mto huo kinazidi kuongezeka ili wapya wanaokubali ibada ya kweli wapate nafasi humo. (Isaya 60:22) Maji ya uzima ya mto huo yatatiririka kwa nguvu zaidi wakati wa ile Miaka Elfu, nayo yatatia ndani uelewaji zaidi unaotegemea vile “vitabu vya kukunja” vitakavyofunguliwa wakati huo.—Ufunuo 20:12; 22:1, 2.

      47:12—Miti ya matunda inafananisha nini? Miti hiyo ya mfano inafananisha maandalizi ya kiroho ya Mungu ya kuwarudisha wanadamu kwenye ukamilifu.

      48:15-19, 30-35—Jiji katika maono ya Ezekieli linafananisha nini? Jiji la “Yehova-Shama” liko katika nchi “najisi,” na hilo linaonyesha kwamba linafananisha jambo fulani la kidunia. Inaelekea kwamba jiji hilo linafananisha usimamizi wa kidunia ambao unawafaidi wote watakaofanyiza “dunia mpya” yenye uadilifu. (2 Petro 3:13) Kuwa na malango kila upande kunaonyesha kwamba linaweza kuingiwa kwa urahisi. Waangalizi miongoni mwa watu wa Mungu wanapaswa kuwa wenye kufikika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki