Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Simameni, Mkauone Wokovu wa Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 1
    • 9, 10. (a) Yehova aliusaidiaje ufalme wa Yuda kushinda jeshi kubwa la maadui? (b) Ni lazima Wakristo waendelee kufanya nini leo?

      9 Wakati wa dhiki kubwa inayokuja itakayofikia upeo katika Har-Magedoni, Kristo atapambana na uovu wote. Lakini kama vile makabila mawili ya ufalme wa Yuda hayakuhitaji kupigana maelfu ya miaka iliyopita, wafuasi wake hawatahitaji kupigana. Vita ilikuwa ya Yehova, naye aliwapa ushindi. Simulizi hilo lasema hivi: “BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa. Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe. Hata Yuda walipofika mnara wa kulindia wa jangwani, wakalitazama hilo jeshi; nao, angalia, walikuwa maiti walioanguka nchi, wala hapana aliyeokoka.”—2 Mambo ya Nyakati 20:22-24.

      10 Ilitukia tu kama Yehova alivyotabiri: “Hamtahitaji kupigana vita.” (2 Mambo ya Nyakati 20:17) Wakristo watafuata kielelezo hichohicho Yesu Kristo atakapowasili “kukamilisha ushindi wake.” Lakini kwa sasa wanaendelea kupambana na uovu si kwa kutumia silaha za kimwili bali za kiroho. Na hivyo ‘wanafuliza kushinda lililo ovu kwa lililo jema.’—Waroma 6:13; 12:17-21; 13:12; 2 Wakorintho 10:3-5.

  • Simameni, Mkauone Wokovu wa Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 1
    • Watumishi wa Mungu Watatendaje?

      14. Ni mambo gani matatu ambayo watu wa Mungu watafanya watakaposhambuliwa?

      14 Watumishi wa Mungu wanatazamiwa kufanya nini watakaposhambuliwa? Kwa mara nyingine tena, taifa la Mungu katika siku za Yehoshafati liliweka kielelezo cha kuigwa. Ona kwamba watu wa taifa hilo waliamriwa wafanye mambo haya matatu: (1) wajipange, (2) wasimame, na (3) wauone wokovu wa Yehova. Watu wa Mungu leo watatendaje kulingana na maneno hayo?—2 Mambo ya Nyakati 20:17.

      15. Watu wa Yehova watajipanga katika maana gani?

      15 Wajipange: Watu wa Mungu wataendelea kudumisha msimamo wao wa kuunga mkono kwa bidii Ufalme wa Mungu bila kuyumbayumba. Wataendelea kudumisha msimamo wao wa Kikristo wa kutokuwamo. Watakuwa ‘imara na wasioondoleka’ wanapomtumikia Yehova kwa uaminifu, na wataendelea kumsifu Yehova hadharani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo. (1 Wakorintho 15:58; Zaburi 118:28, 29) Hakuna mkazo wowote sasa wala wakati ujao utakaowafanya waache msimamo wao unaokubaliwa na Mungu.

      16. Watumishi wa Yehova watasimama katika maana gani?

      16 Wasimame: Watumishi wa Yehova hawatajaribu kujiokoa bali watamtumaini Yehova kwa moyo wao wote. Ni yeye tu anayeweza kuwaokoa watumishi wake kutokana na msukosuko wa ulimwengu, na anaahidi kufanya hivyo. (Isaya 43:10, 11; 54:15; Maombolezo 3:26) Kumtumaini Yehova kunatia ndani kutumaini tengenezo lake linaloonekana leo ambalo amekuwa akitumia kwa miaka mingi ili kutimiza makusudi yake. Wakati huo, kuliko wakati mwingine wowote, Wakristo wa kweli watahitaji kuwatumaini waabudu wenzao ambao wamepewa mamlaka ya kuongoza na Yehova na Mfalme wake anayetawala. Wanaume hao waaminifu watawaongoza watu wa Mungu. Kupuuza mwelekezo wao kunaweza kuleta msiba.—Mathayo 24:45-47; Waebrania 13:7, 17.

      17. Kwa nini watumishi waaminifu wa Mungu watauona wokovu wa Yehova?

      17 Waone wokovu wa Yehova: Wote watakaodumisha ushikamanifu wao wa Kikristo na kumtumaini Yehova ili awakomboe watapata thawabu ya wokovu. Watatangaza kuja kwa siku ya hukumu ya Yehova kwa kadiri wawezavyo hadi saa ya mwisho. Ni lazima viumbe wote wajue kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli na kwamba ana watumishi waaminifu duniani. Hakutakuwa tena na suala la muda mrefu kuhusu haki ya Yehova ya kuwa mwenye enzi kuu.—Ezekieli 33:33; 36:23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki