Msaada wa Kielimu wa Namna ya Kuishi
Mwalimu wa shule katika Zimbabwe, Afrika, alitaja kwamba kwenye Chuo cha Nyatsime, ambapo yeye hufunza, somo la “Elimu ya Namna ya Kuishi” hufunzwa. Yeye alifafanua matatizo ya familia aliyokuwa amepata na kukiri kwamba alikuwa amehitaji msaada wa kuyatatua.
Akielezea kilichotokea baada ya ndoa yake mwenyewe, yeye alisema: “Matatizo yalianza mara moja na kufanya tuamue kutengana katika Novemba 1989.” Kulikuwa pia na matatizo mengine. Yeye aliandika hivi: “Mimi ni mwana wa kwanza wa mama yangu, ambaye alikuwa mke wa kwanza wa baba yangu. Nilipokuwa kwenye mwaka wa pili wa programu yangu ya mazoezi ya kuwa mwalimu, baba yangu alikufa, ikanibidi kutunza ndugu na dada zangu wadogo 16.”
Funzo la Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova lilimsaidia mwalimu huyo kutatua matatizo yake ya familia. Yeye na mke wake wamerudiana na wana furaha. Yeye aliandika: “Mke wangu nami tumejifunza kupitia magumu tuliyojionea kwamba jitihada za mwanadamu za kutatua matatizo yake bila kumtegemea Mungu ni ubatili.” Ingawa hivyo, namna gani kuhusu kusaidia wanafunzi wake kutatua matatizo yao?
“Nilipendekeza kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi kwa mwalimu mkuu wa shule yetu na walimu wengine kuwa hicho ni kitabu cha mafunzo kifaacho,” akaandika. “Wote walikubali, na shule ikanipa agizo la vitabu 56, ambavyo nimevileta shuleni.”
Twaamini kwamba wewe pia utanufaika sana kutokana na kitabu hiki ambacho ni msaada wa kielimu chenye picha za kuvutia na kurasa 320. Ikiwa ungependa kupata nakala yacho au ungependa kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa kutumia anwani ihusuyo kwenye ukurasa 5.