Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unapenda Neno la Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • 18. Taja kielelezo cha mtu ambaye alistahi Neno la Mungu katika nyakati hizi.

      18 Watumishi wengi waaminifu wa Yehova katika nyakati hizi vilevile wameiga jinsi Yesu alivyopenda Neno la Mungu. Mapema katika karne hii, kijana mmoja alipokea Biblia kutoka kwa rafikiye mmoja. Kijana huyo akaeleza matokeo ya zawadi hiyo aliyoithamini: “Nikaazimia maishani kusoma sehemu fulani ya Biblia kila siku.” Kijana huyo ni Frederick Franz, na upendo wake kwa Biblia ulifanya afurahie maisha marefu na yenye mafanikio katika utumishi wa Yehova. Yeye anakumbukwa kwa upendo kuwa mwenye uwezo wa kunukuu sura nzima-nzima za Biblia kutoka akilini.

      19. Wengine huweka ratiba gani ya kusoma Biblia kila juma kwa ajili ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi?

      19 Mashahidi wa Yehova hukazia sana kusoma Biblia kwa ukawaida. Kila juma, wanapotayarisha mojawapo ya mikutano yao ya Kikristo, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, wao husoma sura kadhaa za Biblia. Mambo makuu ya sehemu wanayosoma katika usomaji wa Biblia huzungumziwa kwenye mkutano huo. Mashahidi wengine hupendelea kugawanya usomaji wa Biblia wa juma katika sehemu saba ndogondogo na kusoma sehemu moja kila siku. Wasomapo, wao hutafakari habari hiyo. Inapowezekana, wao hufanya utafiti wa ziada wakitumia vichapo vinavyotegemea Biblia.

      20. Ni nini kinachohitajika ili kupata wakati wa kusoma Biblia kwa ukawaida?

      20 Huenda ukahitaji ‘kununua wakati’ kutoka kwenye utendaji mwingine ili usome Biblia kwa ukawaida. (Waefeso 5:16) Na utapata manufaa nyingi kushinda dhabihu zozote utakazofanya. Kadiri ukuzavyo tabia ya kusoma Biblia kila siku, ndivyo utakavyozidi kupenda Neno la Mungu. Muda usio mrefu, utasukumwa kusema kama mtunga-zaburi: “Sheria yako naipenda mno ajabu, ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.” (Zaburi 119:97) Mtazamo kama huo unanufaisha sana sasa na katika wakati ujao, kama makala ifuatayo itakavyoonyesha.

  • Unapenda Neno la Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • 12. Hezekia angeweza kuepuka kuyarudia makosa ya babake kwa kufanya nini?

      12 Hatimaye, Ahazi akafa na Hezekia akawa mfalme akiwa na umri wa miaka 25. (2 Mambo ya Nyakati 29:1) Japo alikuwa angali kijana kwa kadiri, hiyo haikumzuia asiwe mfalme mwenye mafanikio. Badala ya kuiga mwenendo wa babake asiye mwaminifu, yeye alishikamana na Sheria ya Yehova. Hiyo ilitia ndani amri ya kipekee kwa wafalme: “[Mfalme] aketipo juu ya kiti cha ufalme wake, ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi; na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha BWANA, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii.” (Kumbukumbu la Torati 17:18, 19) Kwa kusoma Neno la Mungu kila siku, Hezekia angejifunza kumcha Yehova na kuepuka kuyarudia makosa ya babake ambaye hakumcha Mungu.

      13. Mkristo anawezaje kuwa na hakika kwamba kwa njia ya kiroho, kila alitendalo litafanikiwa?

      13 Si wafalme wa Israeli tu waliotiwa moyo kufikiria Neno la Mungu daima, bali pia Waisraeli wote wenye kumcha Mungu walitakiwa wafanye hivyo. Zaburi ya kwanza yafafanua mtu mwenye furaha kwelikweli kuwa yule ambaye “sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku.” (Zaburi 1:1, 2) Mtunga-zaburi asema hivi juu ya mtu kama huyo: “Kila alitendalo litafanikiwa.” (Zaburi 1:3) Kwa kutofautisha, Biblia yasema hivi kumhusu mtu ambaye hana imani katika Yehova Mungu: “Yeye ni mtu wa kusitasita kuamua, asiye imara katika njia zake zote.” (Yakobo 1:8) Sisi sote twataka kuwa wenye furaha na wenye mafanikio. Kusoma Biblia kwa ukawaida na kwa njia ya maana kwaweza kuchangia furaha yetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki