Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Furahia Neno la Mungu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Soma Biblia Kila Siku

      Mtunga-zaburi alisema hivi kuhusu mtu anayesoma Neno la Mungu kila siku: “Kila alitendalo litafanikiwa.” (Zab. 1:3) Ndiyo, japo hatujakamilika, japo tunaishi katika mfumo mwovu wa mambo wa Shetani, na japo jitihada za Ibilisi za kutuangamiza, kusoma na kuyatumia kwa ukawaida yaliyomo katika Neno la Mungu kutafanya tufanikiwe katika mambo yote yanayohusu uhusiano wetu na Yehova.

      Kwa sababu tumekazwa sana na mfumo huu, tunaweza kuimarishwa tukichukua hata dakika chache muhimu kila siku kujifunza mawazo ya Muumba. Wengine ambao walifungwa gerezani kwa sababu ya imani yao waliweza kupata tu mstari mmoja-mmoja wa Biblia ulionukuliwa katika magazeti ya habari. Walikata manukuu hayo, wakayashika akilini, na kuyatafakari. Yehova alibariki jitihada zao kwa sababu walifanya kadiri hali zao zilivyoruhusu ili kujua Neno la Mungu. (Mt. 5:3) Lakini, wengi wetu wana uhuru mkubwa zaidi. Tusifikirie kwamba tutatimiza maajabu kwa kusoma haraka-haraka mstari fulani wa Biblia mara moja kwa siku. Lakini tutabarikiwa tukirekebisha hali yetu ili jambo la kwanza liwe ni kusoma sehemu fulani ya Biblia kila siku, kuitafakari, na kuitumia maishani.

      Hata mipango bora inaweza kuvurugika. Mipango yetu inapovurugwa, tutangulize mambo muhimu zaidi. Kwa mfano, hatuwezi kukataa kimakusudi kunywa maji kwa siku moja au mbili. Basi hata hali gani itukie katika maisha yetu ya kila siku, na tuchukue muda fulani wa kujiburudisha kwa maji ya kweli.—Mdo. 17:11.

  • Furahia Neno la Mungu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • SOMA BIBLIA KILA SIKU KWA MAFANIKIO

      Sehemu kubwa ya elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inakazia programu ya kusoma Biblia. Tunakuhimiza ushiriki.

      Sehemu ndogo ya Biblia inapangwa kwa ajili ya usomaji wa kibinafsi na kwa ajili ya mazungumzo katika shule kila juma. Hiyo itakufanya umalize Biblia nzima hatua kwa hatua.

      Ili ufanye kusoma Biblia kila siku kuwe sehemu ya maisha yako, tenga wakati wa kawaida wa kuisoma—labda mapema asubuhi, wakati wa mchana, wakati wa mlo wa jioni, au kabla ya kulala. Kusoma tu sehemu fupi-fupi wakati unaposhtukia kwamba una nafasi hakutafanya uisome kwa ukawaida.

      Ikiwa wewe ni mzazi, onyesha kwamba unajali kwa kuwasaidia watu wa familia yako wakuze kawaida nzuri ya usomaji. Kusoma Biblia mkiwa familia kunaweza kutia moyo wengine katika familia wasome Biblia kila siku kibinafsi.

      Unahitaji kujitia nidhamu ili kusoma Biblia kila siku. Mtu hazaliwi na tamaa hiyo. Unahitaji ‘kufanyiza hamu sana’ ya Neno la Mungu. (1 Pet. 2:2) Unapokuza zoea hilo, hamu yako ya kiroho itakua. Kisha huenda ukaona kwamba unaweza kupanua usomaji wako kwa kufanya miradi maalumu ya kusoma na kujifunza Biblia, ili uzidi kufahamu na kuthamini utajiri mwingi wa kiroho ambao Yehova ametuandalia.

      Unaposoma Biblia, tumia wakati kutafakari maana ya mambo unayosoma—yanakuambia nini juu ya Yehova, yanaweza kuleta faida gani maishani mwako, na unaweza kuyatumiaje kuwasaidia wengine.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki