Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 15-17. Toa mfano unaoonyesha jinsi Yesu alivyotumia maneno “hata zaidi” alipokuwa akifundisha kweli zenye kuchochea mioyo kumhusu Baba yake.

      15 Pia, Yesu alitumia hoja zenye kusadikisha na zinazopatana na akili alipokuwa akifundisha kweli zenye kuchochea mioyo kumhusu Baba yake. Mara nyingi alifanya hivyo kwa kutumia maneno “hata zaidi” kuwasaidia wasikilizaji wake wasadiki zaidi kweli wanayoifahamu. Njia hiyo ya kutoa hoja kwa kulinganisha mambo inaweza kuchochea sana. Acheni tuchunguze mifano miwili tu.

      16 Alipokuwa akijibu ombi la wanafunzi wake la kuwafundisha kusali, Yesu alieleza jinsi wazazi wa kibinadamu wasio wakamilifu wanavyowapa watoto wao “zawadi zilizo njema.” Kisha akasema: “Ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!” (Luka 11:1-13) Yesu alitoa hoja yake kwa kulinganisha mambo. Ikiwa wazazi wenye dhambi wanawatimizia watoto wao mahitaji yao, Baba yetu wa mbinguni ambaye ni mkamilifu na mwadilifu katika mambo yote atawapa hata zaidi roho takatifu waabudu wake washikamanifu wanaomwomba kwa unyenyekevu!

      17 Yesu alitumia njia kama hiyo alipotoa mashauri yenye hekima kuhusu jinsi ya kushughulika na mahangaiko. Alisema: “Kunguru hawapandi mbegu wala hawavuni, nao hawana bohari wala ghala, na bado Mungu huwalisha. Ninyi ni wenye thamani kama nini kuliko ndege? Angalieni jinsi mayungiyungi hukua; hayo hayafanyi kazi wala hayasokoti . . . Ikiwa, basi, Mungu huvika hivyo mimea iliyo shambani ambayo leo ipo na kesho hutupwa ndani ya jiko, basi atawavika ninyi hata zaidi, ninyi wenye imani kidogo!” (Luka 12:24, 27, 28) Ikiwa Yehova anatunza ndege na maua, atawatunza hata zaidi wanadamu wanaompenda na kumwabudu! Bila shaka, kwa kutumia njia hiyo yenye kuchochea fikira, Yesu alifikia mioyo ya wasikilizaji wake.

  • “Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 20, 21. (a) Tunaweza kutumia jinsi gani maneno “hata zaidi” ili kukazia sifa na njia za Yehova? (b) Tutazungumzia nini katika sura inayofuata?

      20 Tunapofundisha, iwe katika huduma ya shambani au kutanikoni, sisi pia tunaweza kulinganisha mambo kwa kutumia maneno “hata zaidi” ili kukazia sifa na njia za Yehova. Kwa mfano, tunapoonyesha kwamba fundisho la moto wa mateso linamvunjia Yehova heshima, tunaweza kusema: “Ni baba gani mwenye upendo anayeweza kumwadhibu mtoto wake kwa kuushika mkono wa mtoto wake na kuuweka motoni? Basi, wazo la moto wa mateso linamchukiza hata zaidi Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo!” (Yeremia 7:31) Ili tumhakikishie mwamini mwenzetu aliyeshuka moyo kwamba Yehova anampenda, tunaweza kusema: “Ikiwa Yehova anamwona shomoro mdogo kuwa mwenye thamani, basi anamjali na kumpenda hata zaidi kila mmoja wa waabudu wake walio duniani, kutia ndani wewe!” (Mathayo 10:29-31) Hoja kama hizo zinaweza kutusaidia kufikia mioyo ya wengine.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki