Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuchoka Lakini Si Kuchoka Kabisa
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Agosti 15
    • 1, 2. (a) Ni mwaliko gani wenye kuvutia unaotolewa kwa wote wanaotaka kufuata ibada safi? (b) Ni nini kinachoweza kuhatarisha sana hali yetu ya kiroho?

      TUKIWA wanafunzi wa Yesu tunaufahamu vizuri mwaliko wake wenye kuvutia: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha ninyi. . . . Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mathayo 11:28-30) Pia Wakristo wanapewa “majira ya kuburudisha . . . kutoka kwa uso wa Yehova.” (Matendo 3:19) Bila shaka, umejionea mwenyewe matokeo yenye kuburudisha ya kujifunza kweli za Biblia, kuwa na tumaini zuri la wakati ujao, na kutumia kanuni za Yehova katika maisha yako.

      2 Hata hivyo, waabudu fulani wa Yehova hupatwa na uchovu wa kihisia-moyo pindi kwa pindi. Nyakati nyingine, vipindi hivyo vya kuvunjika moyo huwa vifupi. Wakati mwingine vinaweza kudumu kwa muda mrefu. Baada ya muda, huenda wengine wakahisi kwamba madaraka yao ya Kikristo yamekuwa mzigo mzito badala ya mzigo wenye kuburudisha kama alivyoahidi Yesu. Maoni hayo yasiyofaa yanaweza kuhatarisha sana uhusiano wa Mkristo pamoja na Yehova.

  • Kuchoka Lakini Si Kuchoka Kabisa
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Agosti 15
    • Ukristo Haukandamizi

      5. Ni jambo gani kuhusu kuwa mwanafunzi Mkristo linaloonekana kuwa lenye kupingana?

      5 Ni kweli kwamba kuwa Mkristo hutaka mtu ajitahidi sana. (Luka 13:24) Hata Yesu alisema: “Yeyote yule asiyeuchukua mti wake wa mateso na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.” (Luka 14:27) Yakichukuliwa kijuujuu tu, huenda maneno hayo yakaonekana kuwa yanapingana na taarifa ya Yesu kuhusu mzigo wake mwepesi na wenye kuburudisha, lakini sivyo.

      6, 7. Kwa nini tunaweza kusema kwamba namna yetu ya ibada haichoshi?

      6 Ingawa kazi ngumu na inayohitaji jitihada huuchosha mwili, inaweza kuwa yenye kuridhisha na kuburudisha inapofanywa kwa kusudi zuri. (Mhubiri 3:13, 22) Na kusudi lililo bora zaidi ni kuwaeleza majirani wetu kweli nzuri za Biblia. Pia jitihada yetu ya kuishi kupatana na viwango vya juu vya maadili vya Mungu huwa si kitu inapolinganishwa na manufaa tunayopata. (Methali 2:10-20) Hata tunaponyanyaswa, tunaona hilo kuwa pendeleo kuteseka kwa ajili ya Ufalme wa Mungu.—1 Petro 4:14.

      7 Kwa kweli mzigo wa Yesu ni wenye kuburudisha, hasa unapolinganishwa na giza la kiroho la wale walio chini ya nira ya dini ya uwongo. Mungu ana upendo mwororo kutuelekea naye hadai mambo tusiyoweza kutimiza. ‘Amri za Yehova si mzigo mzito.’ (1 Yohana 5:3) Ukristo wa kweli, kama unavyoonyeshwa katika Maandiko, si wenye kukandamiza. Ni wazi kwamba, namna yetu ya ibada haisababishi uchovu na kuvunjika moyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki