Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kundi Moja, Mchungaji Mmoja
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • 10, 11. (a) Tumeona maneno ya Yesu yakitimizwa kwa njia gani yenye kutia nguvu imani? (b) Ni swali gani linalotokea kuhusu kondoo wengine?

      10 Yesu alisema kuhusu “kondoo wengine,” ambao hawangekuwa katika “zizi” la “kundi dogo” la wafuasi wake watiwa-mafuta. (Yoh. 10:16; Luka 12:32) Alisema hivi: “Hao pia nitawaleta, nao wataisikiliza sauti yangu, nao watakuwa kundi moja, mchungaji mmoja.” Imani yetu imetiwa nguvu kama nini kuona maneno hayo yakitimizwa! Vikundi viwili vya watu vimeunganishwa pamoja, yaani, kikundi kidogo cha watiwa-mafuta na umati mkubwa wa kondoo wengine. (Soma Zekaria 8:23.) Ingawa kondoo wengine hawatumiki kwa njia ya mfano katika ua wa ndani wa hekalu la kiroho, wanatumika katika ua wa nje wa hekalu hilo.

  • Kundi Moja, Mchungaji Mmoja
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • “Nao Watakuwa Watu Wangu”

      17, 18. Unabii ulio katika Ezekieli 37:26, 27 umetimizwa jinsi gani?

      17 Yehova alitabiri hivi kuhusu umoja wa watu wake: “Nitafanya agano la amani pamoja nao; watakuwa na agano lenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo. Nami nitawaweka na kuwazidisha na kuweka patakatifu pangu katikati yao mpaka wakati usio na kipimo. Na maskani yangu kwa kweli itakuwa juu yao, nami hakika nitakuwa Mungu wao, na wao wenyewe watakuwa watu wangu.”—Eze. 37:26, 27.

      18 Watu wote wa Mungu wana pendeleo la kufaidika kutokana na utimizo wa ahadi hiyo nzuri ajabu, agano hilo linalowaletea Wakristo amani. Ndiyo, Yehova amewahakikishia watumishi wote wanaomtii kwamba watapata amani. Matunda ya roho yake yanaonekana wazi kati yao. Patakatifu pake, ambapo panafananisha ibada safi ya Wakristo, pako katikati yao. Kwa kweli, wamekuwa watu wake, kwa sababu wameacha ibada ya sanamu ya kila namna, nao wanamwabudu Yehova akiwa Mungu wa pekee wa kweli.

      19, 20. Ni nani wanaohesabiwa kati ya wale ambao Yehova anawaita “watu wangu,” na ni nini kinachowezekana kupitia agano jipya?

      19 Tumesisimuka kama nini kuona vikundi hivyo viwili vikiunganishwa katika nyakati zetu! Ingawa washiriki wa umati mkubwa ambao unaendelea kuongezeka hawana tumaini la kwenda mbinguni, wanathamini pendeleo la kushirikiana na wale walio na tumaini hilo. Wameshikamana na Israeli wa Mungu. Kwa kufanya hivyo, wanahesabiwa kati ya wale ambao Yehova anawaita “watu wangu.” Wanatimiza unabii huu: “Mataifa mengi yatajiunga na Yehova siku hiyo, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa katikati yako.”—Zek. 2:11; 8:21; soma Isaya 65:22; Ufunuo 21:3, 4.

      20 Yehova ametumia agano jipya kutimiza mambo hayo yote. Mamilioni ya wageni wa kiroho wamejiunga na taifa linalokubaliwa na Yehova. (Mika 4:1-5) Wameazimia kuendelea kulishika agano hilo kwa kukubali maandalizi ya agano hilo na kutii matakwa yake. (Isa. 56:6, 7) Wanapofanya hivyo, wao pamoja na Israeli wa Mungu, wanafurahia baraka kubwa ya kuendelea kuwa na amani. Na ufurahie baraka hiyo sasa na kwa umilele wote!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki