Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Lile “Hekalu” na Yule “Mkuu” Leo
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
    • 12. Kwa nini twapaswa kuthamini kazi ya watiwa-mafuta?

      12 Kila mmoja wetu aweza kujiuliza, ‘Je, ninathamini kielelezo kilichowekwa na watiwa-mafuta kwa miaka mingi ya utumishi wao mwaminifu? Je, ninaiga imani yao?’ Ni vizuri kwa wale wa umati mkubwa kukumbuka kwamba hawatakuwa na watiwa-mafuta sikuzote hapa duniani. Yehova alisema hivi kuhusu makuhani katika ono la Ezekieli: “Wala hamtawapa milki [ya nchi] iwayo yote katika Israeli; mimi ni milki yao.” (Ezekieli 44:28) Vivyo hivyo, watiwa-mafuta hawana sehemu yoyote yenye kudumu milele hapa duniani. Wao wana urithi wa kimbingu, na wale wa umati mkubwa huliona kuwa pendeleo kuwaunga mkono na kuwatia moyo wakiwa wangali hapa duniani.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 1:3, 4.

  • Lile “Hekalu” na Yule “Mkuu” Leo
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
    • 15. (a) Ono la Ezekieli hutufafanuliaje uhusiano uliopo baina ya wazee ambao ni wa umati mkubwa na jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta? (b) Wazee watiwa-mafuta wamechukua uongozi upi katika tengenezo la Mungu la kidunia?

      15 Lakini je, ni uhusiano gani uliopo baina ya jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta na wanaume wazee hao ambao, wakiwa sehemu ya umati mkubwa, wanatumikia katika vyeo vya usimamizi? Ono la Ezekieli ladokeza kwamba fungu la wazee hao walio washiriki wa umati mkubwa ni la chini na la kuunga mkono, huku watiwa-mafuta wakichukua uongozi wa kiroho. Jinsi gani? Kumbuka, makuhani katika ono hilo walipewa daraka la kufundisha watu mambo ya kiroho. Pia waliambiwa watumikie wakiwa mahakimu katika kesi za kisheria. Kwa kuongezea, Walawi walipewa kazi ya kuwa “wasimamizi” katika malango ya hekalu. (Ezekieli 44:11, 23, 24) Kwa wazi, mkuu huyo alipaswa kujitiisha kwa utumishi wa kiroho na uongozi wa hao makuhani. Basi, inafaa kwamba katika nyakati za kisasa watiwa-mafuta wamechukua uongozi katika ibada safi. Kwa mfano, washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova wamechaguliwa kutoka miongoni mwao. Wazee hao waaminifu, watiwa-mafuta, wamekuwa wakiizoeza kwa makumi ya miaka jamii ya mkuu huyo inayokua. Washiriki hao wa Baraza Linaloongoza wanawatayarisha wale wanaotazamia kuwa washiriki wa jamii hii kwa ajili ya siku watakapoachiwa mamlaka kamili ya madaraka yao katika ulimwengu mpya wa Mungu unaokuja.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki