Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa nini wengine hunitenga?
    Amkeni!—2007 | Julai
    • ◼ Panuka. (2 Wakorintho 6:11-13) Chukua hatua ya kwanza kufahamiana na watu. Ni kweli kwamba inaweza kuwa vigumu kufanya hivyo. Liz, mwenye umri wa miaka 19, anasema: “Mtu anaweza kuona haya kuzungumza na kikundi cha watu, lakini ukimsalimu mmoja wao, mara moja unakuwa sehemu ya kikundi hicho.” (Ona sanduku “Mapendekezo ya Jinsi ya Kuanzisha Mazungumzo.”) Badala ya kulalamika kwamba unatengwa, hakikisha wewe humtengi yeyote, kama vile watu wenye umri mkubwa. “Nilipokuwa na umri wa miaka 10 au 11,” anakumbuka kijana anayeitwa Cori, “nilikuwa na rafiki mwenye umri mkubwa. Tulikuwa na uhusiano wa karibu, ingawa umri wetu ulikuwa umetofautiana sana.”

      Fikiria watu wawili katika kutaniko lako wenye umri mkubwa ambao ungependa kufahamiana nao vizuri zaidi.

      ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

      ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

      Kwenye mkutano unaofuata, mbona usizungumze na mmoja kati ya watu uliowaandika hapo juu. Anzisha mazungumzo naye. Mwulize jinsi alivyoanza kujifunza Biblia. Kadiri unavyofahamiana zaidi na watu katika “ushirika mzima wa akina ndugu,” ndivyo utakavyopunguza hisia za upweke.—1 Petro 2:17.

  • Kwa nini wengine hunitenga?
    Amkeni!—2007 | Julai
    • ◼ Wafikirie wengine. (1 Wakorintho 10:24) Biblia inasema tunapaswa ‘twendelee kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yetu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’ (Wafilipi 2:4) Ni kweli, unapohisi kwamba wengine wanakutenga, ni rahisi kuhuzunika. Hata hivyo, badala ya kukata tamaa, kwa nini usimfanyie mtu mwenye uhitaji jambo fulani? Huenda ukaanzisha urafiki kwa njia hiyo!

      Mfikirie mtu fulani, labda katika familia au kutaniko lenu, ambaye anaweza kufurahia kushirikiana nawe au kupata msaada wako. Andika jina la mtu huyo hapa chini, na ufafanue jinsi unavyoweza kumsaidia.

      ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

      Unapowafikiria wengine badala ya kujifikiria tu na kuwafanyia mambo, huwezi kujihisi mpweke. Kufanya hivyo kunaweza kukufanya uwe na mtazamo mzuri na mwelekeo unaofaa, na hivyo kukufanya uwe rafiki anayefaa. Methali 11:25 inasema: “Anayenywesha wengine kwa ukarimu yeye mwenyewe pia atanyweshwa kwa ukarimu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki