Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumia Kila Siku ya Maisha Yako kwa Utukufu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • Neno la Mungu linaeleza waziwazi mambo ambayo Yehova anatutarajia tutimize. (Kum. 10:12, 13) Mambo kadhaa yameorodheshwa kwenye sanduku lenye kichwa “Mambo Ambayo Mungu Anataka Tufanye,” kwenye ukurasa wa 22. Mambo hayo yote ambayo Mungu anataka tutimize ni ya maana. Tunaweza kuamua jinsi gani jambo la kutanguliza ikiwa tuna mambo mawili au zaidi ya kufanya?

      Tunatanguliza utumishi wetu mtakatifu, unaotia ndani kujifunza Biblia, sala, mikutano ya Kikristo, na huduma. (Mt. 6:33; Yoh. 4:34; 1 Pet. 2:9) Lakini hatuwezi kufanya mambo ya kiroho siku nzima. Tunahitaji pia kufanya mambo mengine kama vile kazi, kusoma, na shughuli mbalimbali za nyumbani. Hata hivyo, tunajitahidi kabisa kupanga kazi na shughuli zetu nyingine kwa njia ya kwamba hazivurugi utumishi wetu mtakatifu, kama vile kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Kwa mfano, tunapopanga kwenda likizo, tunahakikisha kwamba hatukosi ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la pekee na la mzunguko, au kusanyiko la wilaya. Wakati mwingine, tunaweza kuunganisha shughuli zetu pamoja. Kwa mfano, tunaweza kuamua kusafisha Jumba la Ufalme tukiwa familia au kutumia wakati wa chakula cha mchana kazini au shuleni kuwahubiria wafanyakazi au wanafunzi wenzetu. Kwa kweli, tunapohitaji kufanya uamuzi wowote maishani—kama vile kutafuta kazi, kuchagua shule, au kuchagua marafiki—tungependa maamuzi yetu yote yategemee jambo muhimu zaidi katika maisha yetu—yaani, kumwabudu Yehova, Baba yetu mwenye upendo.—Mhu. 12:13.

  • Tumia Kila Siku ya Maisha Yako kwa Utukufu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 22]

      Mambo Ambayo Mungu Anataka Tufanye

      • Kusali kwa kawaida.—Rom. 12:12.

      • Kusoma na kujifunza Biblia, na kutumia tunayojifunza.—Zab. 1:2; 1 Tim. 4:15.

      • Kumwabudu Yehova kutanikoni.—Zab. 35:18; Ebr. 10:24, 25.

      • Kuiandalia familia mahitaji ya kimwili, ya kiroho, na ya kihisia.—1 Tim. 5:8.

      • Kuhubiri habari njema ya Ufalme, na kufanya wanafunzi.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

      • Kutunza afya yetu kimwili, kiroho, na kihisia, na pia kuwa na tafrija inayofaa.—Marko 6:31; 2 Kor. 7:1; 1 Tim. 4:8, 16.

      • Kutimiza madaraka yetu kutanikoni.—Mdo. 20:28; 1 Tim. 3:1.

      • Kutunza nyumba yetu na Jumba la Ufalme.—1 Kor. 10:32.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki