-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
7, 8. (a) Kuna miaka gani miwili ‘ya nia njema’? (b) ‘Siku za kisasi’ cha Yehova ni zipi?
7 Kuna wakati hususa uliowekwa ili habari njema zihubiriwe. Yesu na wafuasi wake walipewa utume wa “kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa [“mwaka wa nia njema,” “NW”], na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao.” (Isaya 61:2) Mwaka ni muda mrefu, lakini una mwanzo na mwisho. “Mwaka wa nia njema” wa Yehova ni kile kipindi ambacho yeye huwapa watu watiifu nafasi ya kuitikia anapowatangazia uhuru.
8 Katika karne ya kwanza, mwaka wa nia njema kwa taifa la Kiyahudi ulianza mwaka wa 29 W.K. Yesu alipoanza huduma yake ya kidunia. Aliwaambia Wayahudi hivi: “Tubuni, nyinyi watu, kwa maana ufalme wa mbingu umekaribia.” (Mathayo 4:17) Mwaka huo wa nia njema uliendelea hadi “siku ya kisasi” cha Yehova, ambayo ilifikia upeo mwaka wa 70 W.K. Yehova aliporuhusu majeshi ya Roma yaharibu Yerusalemu na hekalu lake. (Mathayo 24:3-22)
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.
11. Ni nani katika karne ya kwanza waliokuwa na sababu nzuri ya kumsifu Yehova kuhusu tendo lake kubwa?
11 Katika karne ya kwanza, hata Wayahudi waliokubali kufunguliwa watoke katika kifungo cha dini ya uwongo walimsifu Mungu kwa tendo kubwa alilowafanyia. Badala ya roho yao iliyoshuka, wakawa na “vazi la sifa” walipokombolewa kutoka katika taifa lililokufa kiroho. Badiliko hilo liliwapata kwanza wanafunzi wa Yesu walipoacha kuombolezea kifo chake wakaanza kushangilia wakati Bwana wao aliyefufuliwa alipowatia mafuta kwa roho takatifu. Upesi baada ya hapo, badiliko kama hilo lilipata kila mmoja wa watu watiifu 3,000 walioitikia na kubatizwa kwenye Pentekoste ya 33 W.K. baada ya kuhubiriwa na Wakristo hao waliotiwa mafuta karibuni. (Matendo 2:41) Ilikuwa vizuri kama nini kuwa na uhakika wa kupata baraka ya Yehova! Badala ya ‘kulilia Sayuni,’ walipokea roho takatifu wakaburudishwa na “mafuta ya furaha,” yanayofananisha furaha nyingi ya wale wanaobarikiwa sana na Yehova.—Waebrania 1:9.
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
6. Ni nani waliopata kitulizo kwa kusikia habari njema zilizohubiriwa nyakati za kale, na namna gani leo?
6 Ujumbe wa Isaya uliopuliziwa uliwaletea kitulizo Wayahudi wenye toba kule Babiloni. Siku za Yesu na wanafunzi wake, ujumbe huo uliwapa kitulizo Wayahudi waliokuwa wamevunjwa moyo na uovu uliokuwa katika Israeli na kunyong’onyea katika utekwa wa mapokeo ya uongo ya Dini ya Kiyahudi ya karne ya kwanza. (Mathayo 15:3-6)
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15 Mwaka wa 33 W.K., wanafunzi wa Yesu walihuzunika sana alipokamatwa, akajaribiwa, na kuuawa. (Mathayo 26:31) Hata hivyo, maoni yao yalibadilika alipowatokea baada ya kufufuliwa kwake. Kisha roho takatifu ilipomiminwa juu yao, walijishughulisha na kazi ya kuzihubiri habari njema, “katika Yerusalemu na pia katika Yudea yote na Samaria na hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8) Hivyo walianza kurudisha ibada safi.
-