-
Réunion2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
MSAADA KUTOKA UFARANSA
Ofisi ya tawi ya Ufaransa, iliyosimamia kazi wakati huo, iliwaomba wahubiri wenye ustadi wahamie Réunion. Familia ya Pégoud—André, Jeannine, na Christian, mwana wao mwenye umri wa miaka sita—pamoja na Noémie Duray, mtu wa jamaa yao, walikubali mwito huo. Waliwasili Januari 1961. Noémie, ambaye pia huitwa Mimi, alitumika akiwa painia wa pekee kwa miaka miwili kabla ya kurudi Ufaransa.
Muda si mrefu, walipata watu wengi wenye kupendezwa na hata walifanya mikutano kwenye chumba chao hotelini katika jiji kuu la Saint-Denis. Mara tu familia hiyo ilipohamia nyumba nyingine, walianza kufanya mikutano huko.
-
-
Réunion2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 224]
Noémie Duray, Jeannine Pégoud, na mwanawe, Christian, wakielekea Réunion mnamo 1961
-