-
Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
-
-
6. Yehova alikuwaje mwaminifu kwa kusudi lake na kwa jina lake?
6 Kwa kuwa yeye ni mwaminifu kwa kusudi lake na kwa maana ya jina lake, Yehova alijifanya kuwa Nabii na Mwokozi.a Alimwambia Shetani hivi: “Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamke na kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye atakuponda kichwa nawe utamtia jeraha kwenye kisigino.” (Mwanzo 3:15) Kupitia Uzao wa “mwanamke” wake, au sehemu ya mbinguni ya tengenezo lake, Yehova angejibu dai la Shetani na kuwapa wazao wa Adamu tumaini la kupata ukombozi na uzima.—Waroma 5:21; Wagalatia 4:26, 31.
-
-
Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
-
-
9. Yehova alifunuaje hatua kwa hatua siri takatifu ya mapenzi yake?
9 Kupitia maagano mbalimbali yaliyofuatana, Yehova alifunua hatua kwa hatua jinsi ambavyo kusudi lake kuhusiana na Uzao ulioahidiwa huko Edeni lingetimizwa. Agano lake na Abrahamu lilifunua kwamba Uzao ulioahidiwa ungekuja duniani katika ukoo wa Abrahamu, na kupitia Uzao huo “mataifa yote ya dunia” yangejibariki. Agano hilo pia lilidokeza kwamba wengine wangeshirikiana na sehemu ya msingi ya uzao huo. (Mwanzo 22:17, 18) Agano la Sheria lililofanywa pamoja na taifa la Israeli la asili lilifunua kusudi la Yehova la kuwa na “ufalme wa makuhani.” (Kutoka 19:5, 6) Agano lililofanywa pamoja na Daudi lilionyesha kwamba Uzao huo ungekuwa Kichwa cha Ufalme mpaka wakati usio na kipimo. (2 Samweli 7:12, 13; Zaburi 89:3, 4) Baada ya agano la Sheria kuwaongoza Wayahudi kwa Masihi, Yehova alifunua mambo mengine kuhusu utimizo wa kusudi lake. (Wagalatia 3:19, 24) Wanadamu ambao wangeshirikiana na sehemu ya msingi ya uzao ndio wangefanyiza “ufalme wa makuhani” uliotabiriwa, nao wangeingizwa katika “agano jipya” wakiwa “Israeli” jipya, taifa la kiroho.—Yeremia 31:31-34; Waebrania 8:7-9.c
10, 11. (a) Yehova alifunuaje Uzao uliotabiriwa? (b) Kwa nini Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu alikuja duniani?
10 Kupatana na usimamizi wa kusudi la Mungu, wakati ulifika ili Uzao uliotabiriwa utokee duniani. Yehova alimtuma malaika Gabrieli amwambie Maria kwamba angemzaa mwana ambaye angeitwa Yesu. Malaika huyo alimwambia Maria hivi: “Huyo atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi; na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (Luka 1:32, 33) Hivyo, Uzao ulioahidiwa ulitambulishwa waziwazi.—Wagalatia 3:16; 4:4.
-