Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yohana Aona Yesu Aliyetukuzwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 5

      Yohana Aona Yesu Aliyetukuzwa

      Njozi ya 1—Ufunuo 1:10–3:22

      Habari: Yesu hukagua Israeli wa kiroho duniani na hutoa kitia-moyo kichangamfu

      Wakati wa utimizo: Sehemu hii ya siku ya Bwana hutandaa kutoka 1914 na mpaka yule wa mwisho wa wapakwa-mafuta waaminifu anapokufa na kufufuliwa

      1. Ile njozi ya kwanza inatolewaje, na Yohana alionyeshaje wakati wa utumizi halisi wayo?

      NJOZI ya kwanza katika kitabu cha Ufunuo inaanza na sura ya 1, mstari wa 10. Njozi hii, kama zile nyinginezo katika Ufunuo, imetangulizwa na tangazo kwamba Yohana anasikia au anaona kitu fulani kisicho cha kawaida. (Ufunuo 1:10, 12; 4:1; 6:1) Njozi hii ya kwanza inatolewa katika muundo wa karne ya kwanza ambao katika huo jumbe zinaelekezwa kwenye makundi saba yaliyokuwapo wakati mmoja na Yohana. Lakini Yohana anaonyesha wakati wa utumizi halisi wayo anaposema: “Kwa kuvuviwa mimi nilikuja kuwa katika ile siku ya Bwana.” (Ufunuo 1:10a, NW) “Siku” hii inakuwa wakati gani? Je! matukio yenye kutazamisha ya nyakati hizi zenye msukosuko yana uhusiano wowote nayo? Ikiwa ndivyo, imetupasa tutoe uangalifu sana kwenye unabii huo, kuwa unaathiri maisha zetu zenyewe—hata kuokolewa kwetu.—1 Wathesalonike 5:20, 21.

      Katika Siku ya Bwana

      2. Ile siku ya Bwana inaanza lini, na inamalizika lini?

      2 Hii inaweka utimizo wa Ufunuo katika muundo gani wa wakati? Basi, siku ya Bwana ni nini? Mtume Paulo anairejezea kuwa wakati wa hukumu na wa utimizo wa ahadi za kimungu. (1 Wakorintho 1:8; 2 Wakorintho 1:14; Wafilipi 1:6, 10; 2:16) Inapowasili “siku” hiyo, makusudi yenye utukufu ya Yehova yanasonga kwa kuendelea na kwa ushindi wenye shangwe kuelekea upeo wayo. “Siku” hiyo inaanza kwa kuvikwa Yesu taji kuwa Mfalme wa kimbingu. Hata baada ya Yesu kutekeleza hukumu juu ya ulimwengu wa Shetani, ile siku ya Bwana inaendelea, na kurudishwa kwa Paradiso na ukamilifu wa aina ya binadamu, mpaka mwishowe Yesu ‘anakabidhi ufalme kwa Mungu na Baba yake.’—1 Wakorintho 15:24-26, NW; Ufunuo 6:1, 2.

      3. (a) Unabii wa Danieli wa “nyakati saba” unatusaidiaje tuone wakati siku ya Bwana inapoanza? (b) Ni matukio gani duniani yanayothibitisha mwaka wa 1914 kuwa ndio mwanzo wa siku ya Bwana?

      3 Utimizo wa unabii mwingine wa Biblia husaidia sisi tuone wakati siku ya Bwana inapoanza. Mathalani, Danieli alieleza kukatwa mpaka chini kwa utawala katika ukoo wa Mfalme Daudi; baada ya “nyakati saba” ingejulikana “ya kwamba Aliye Juu Zaidi Sana ndiye Mtawala katika ufalme wa aina ya binadamu, na ya kwamba kwa mmoja ambaye yeye hutaka huutoa huo.” (Danieli 4:23, 24, 31, 32, NW) Utimizo mkubwa wa unabii huo ulianza wakati wa kuharibiwa kwa ufalme wa Yuda, jambo ambalo ithibati ya Biblia inaonyesha kwamba lilikuwa limekamilishwa kufikia Oktoba 607 K.W.K. Ufunuo 12:6, 14 huonyesha kwamba nyakati 3 1/2 hujumlika kuwa siku 1,260; kwa hiyo, nyakati saba (mara mbili za nambari hiyo) lazima ziwe siku 2,520. Tukihesabu “siku moja kwa mwaka mmoja,” tunawasili kwenye miaka 2,520 kuwa ndio urefu wa zile “nyakati saba.” (Ezekieli 4:6) Kwa hiyo, Kristo Yesu alianza utawala wake wa kimbingu katika sehemu ya mwisho ya 1914. Ule mpasuko wa vita ya ulimwengu ya kwanza katika mwaka huo ulitia alama “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu” ambayo yameendelea kusumbua aina ya binadamu. Tangu 1914, jinsi matukio katika dunia hii yenye kutiwa madoa ya damu yamethibitisha mwaka huo kwa njia yenye kutokeza kuwa ndio mwanzo wa ile “siku” ya kuwapo kwa Yesu!—Mathayo 24:3-14, NW.a

      4. (a) Maneno ya Ufunuo yenyewe yanaonyesha nini kwa habari ya wakati ambao ile njozi ya kwanza inatimizwa? (b) Utimizo wa ile njozi ya kwanza unamalizika lini?

      4 Kwa sababu hiyo, njozi hii ya kwanza na shauri iliyo nalo ni kwa ajili ya siku ya Bwana, kuanzia 1914 na kuendelea. Kipimo hiki cha wakati huungwa mkono na uhakika wa kwamba, baadaye katika Ufunuo, maandishi yanaeleza kutekelezwa kwa hukumu ya Mungu ya uadilifu na ya kweli—matukio ambayo katika hayo Bwana Yesu anatimiza sehemu yenye kutokeza. (Ufunuo 11:18; 16:15; 17:1; 19:2, 11) Ikiwa utimizo wa hiyo njozi ya kwanza ulianza katika 1914, unamalizika wakati gani? Kama zinavyoonyesha zile jumbe, lile tengenezo linalopelekewa ni kundi la wapakwa-mafuta la Mungu lililopo duniani. Basi, utimizo wa hii njozi ya kwanza unamalizika wakati mshiriki mwaminifu wa mwisho wa kundi hilo lililopakwa mafuta anapokufa na kuinuliwa kwenye uhai wa kimbingu. Hata hivyo, ile Siku ya Bwana, ikiwa na mibaraka kwa kondoo wengine wa kidunia, huendelea mpaka mwisho wa Utawala wa Yesu Kristo wa Mileani.—Yohana 10:16; Ufunuo 20:4, 5.

      5. (a) Sauti inamwagiza Yohana afanye nini? (b) Kwa nini mahali yalipokuwa “yale makundi saba” palifaa kuyapelekea ile hati-kunjo?

      5 Katika hii njozi ya kwanza, kabla ya Yohana kuona kitu chochote, yeye anasikia kitu fulani: “Na mimi nikasikia nyuma yangu sauti yenye nguvu kama ile ya tarumbeta, ikisema: ‘Unachoona andika katika hati-kunjo na kuipeleka kwenye makundi saba, katika Efeso na katika Smirna na katika Pargamamu na katika Thiatira na katika Sardisi na katika Filadelfia na katika Laodikia.’” (Ufunuo 1:10b, 11) Sauti yenye mamlaka na yenye kuamrisha kama ya tarumbeta, inamwambia Yohana aandikie “makundi saba.” Yeye atapokea mfululizo wa jumbe na kutangaza vitu atakavyoona na kusikia. Angalia kwamba yale makundi yanayotajwa hapa yalikuwako kikweli katika siku ya Yohana. Yote yalikuwa katika Esia Ndogo, ng’ambo tu ya bahari kutoka Patmosi. Yalikuwa yenye kuwasilikana kwa urahisi yenyewe kwa yenyewe kwa njia ya barabara bora zaidi za Kiroma zilizokuwako katika eneo hilo. Mjumbe hangalipata shida ya kupeleka hati-kunjo kutoka kundi moja kwenda lifuatalo. Makundi saba haya yangelingana na sehemu ya mzunguko wa ki-siku-hizi wa Mashahidi wa Yehova.

      6. (a) Ni nini linalomaanishwa na “vitu vilivyopo”? (b) Kwa nini sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba hali katika kundi la Wakristo wapakwa-mafuta leo lazima ziwe zinafanana na zile za siku ya Yohana?

      6 Mwingi wa unabii katika Ufunuo ungetimizwa baada ya wakati wa Yohana. Ulirejezea “vitu ambavyo vitatukia baada ya hivi.” Lakini shauri kwa yale makundi saba linashughulika na “vitu vilivyopo,” hali ambazo zilikuwamo kweli kweli katika hayo makundi saba wakati ule. Jumbe hizo zilikuwa misaada yenye thamani kwa wazee waaminifu waliowekwa rasmi katika makundi hayo saba, vilevile makundi mengine yote ya Wakristo wapakwa-mafuta ya wakati huo.b Kwa kuwa ile njozi ina utumizi mkuu katika siku ya Bwana, yale anayosema Yesu yanatoa onyo kwamba hali kama hizo zingetarajiwa ziweko katika kundi la Wakristo wapakwa-mafuta la siku yetu wenyewe.—Ufunuo 1:10, 19.

      7. Yohana anaona nani katika hii njozi ya kwanza, na kwa nini ni jambo la maana sana na lenye kusisimua kwetu sisi leo?

      7 Katika hii njozi ya kwanza Yohana anamwona Bwana Yesu Kristo mwenye kung’aa katika utukufu Wake wa kimbingu. Ni jambo gani lingekuwa lenye kufaa zaidi ya hilo kwa kitabu cha unabii unaohusu ile siku kubwa ya huyu Bwana ambaye amepewa utume na mbingu? Na ni jambo gani lingekuwa la maana zaidi ya hilo kwetu sisi, tunaoishi katika kipindi hicho cha wakati na tunaotoa utii wa uangalifu kwa kila amri yake? Na zaidi, inasisimua kama nini kwa wategemezaji wa enzi kuu ya Yehova kuhakikishiwa kwamba ile Mbegu ya Kimesiya, ikiisha kuvumilia mitihani na minyanyaso yote iliyoletwa na Shetani na ikiisha taabishwa na kifo chenye maumivu makali wakati ‘kisigino’ Chake kilipochubuliwa karibu miaka 2,000 iliyopita, sasa anaishi katika mbingu, akiwa amevikwa uwezo alete kusudi tukufu la Mungu kwenye ukamilisho walo wenye ushindi wa shangwe!—Mwanzo 3:15, NW.

      8. Yesu yu chonjo kuchukua hatua gani sasa?

      8 Ni wazi kwamba sasa Yesu yu chonjo, tayari kuchukua hatua akiwa Mfalme mtawazwa. Yeye amewekwa rasmi kuwa Mtekelezaji Mkuu wa Yehova afikilize hukumu za mwisho za Yehova dhidi ya huu mfumo wa mambo wa kale ulio mbovu, na mungu wao wa kiibilisi, Shetani. Pia yupo karibu ahukumu wale wa kundi lake la wapakwa-mafuta na ule umati mkubwa wa washiriki wenzao, vilevile kuhukumu ulimwengu.—Ufunuo 7:4, 9; Matendo 17:31.

      9. (a) Yohana anaelezeaje Yesu Kristo aliyetukuzwa akiwa katikati ya vile vinara vya taa vya dhahabu? (b) Ni nini linaloonyeshwa na mazingira yaliyo kama hekalu na lile vazi analovaa Yesu? (c) Ni nini linalomaanishwa na mshipi wake wa dhahabu?

      9 Wakati wa mvumo wa sauti kubwa Yohana ageuka, na hiki ndicho anachoona: “Na mimi niligeuka nione ile sauti ambayo ilikuwa ikisema na mimi, na, nikiisha kugeuka, mimi niliona vinara vya taa saba vya dhahabu.” (Ufunuo 1:12, NW) Baadaye, Yohana anajifunza kinachofananishwa na hivyo vinara vya taa saba. Lakini ni mtu aliye katikati ya hivyo vinara vya taa saba anayevuta jicho lake. Alikuwako “katikati ya vinara vya taa mtu fulani kama mwana wa binadamu, amevaa vazi ambalo lilifika chini kwenye nyayo, na amefungwa kwenye matiti kwa mshipi wa dhahabu.” (Ufunuo 1:13, NW) Yesu “mwana wa binadamu,” hapa anajileta mwenyewe mbele ya Yohana, shahidi ambaye ameshikwa na hofu ya staha, akiwa umbo tukufu, lenye mwako. Anatokea akiwa na utukufu wenye kumetameta miongoni mwa vinara vya taa vya dhahabu vyenye mwali wa moto. Mazingira haya yaliyo kama hekalu yanatia katika akili za Yohana uhakika wa kwamba Yesu yupo akiwa katika cheo cha Kuhani Mkuu wa Yehova, akiwa na nguvu za kuhukumu. (Waebrania 4:14; 7:21-25) Vazi lake refu, lenye kuvutia linapatana na cheo chake cha kikuhani. Kama makuhani wakuu wa kale wa Kiyahudi, yeye anavalia mshipi—mshipi wa dhahabu juu ya matiti yake ambapo unafunika moyo wake. Hilo linamaanisha kwamba yeye atatekeleza kwa moyo utume wake wa kimungu aliopokea kutoka kwa Yehova Mungu.—Kutoka 28:8, 30; Waebrania 8:1, 2.

      10. (a) Ni nini linaloonyeshwa na nywele nyeupe kama theluji na macho yenye moto ya Yesu? (b) Ni nini maana ya nyayo za Yesu zikiwa kama shaba inayowaka?

      10 Elezeo la Yohana linaendelea: “Zaidi ya hilo, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, kama theluji, na macho yake kama mwali wa moto.” (Ufunuo 1:14, NW) Nywele zake nyeupe kama theluji huonyesha hekima kwa sababu ya urefu wa maisha. (Linga Mithali 16:31.) Na macho yake yenye moto huonyesha kwamba yu chapuchapu, yu chonjo, anapochunguza-chunguza, anapotahini au anapoonyesha ghadhabu. Hata nyayo za Yesu zavuta fikira za Yohana: “Na nyayo zake zilikuwa kama shaba safi inapowaka katika tanuri; na sauti yake ilikuwa kama mvumo wa maji mengi.” (Ufunuo 1:15, NW) Katika njozi hii, nyayo za Yesu ni kama shaba, yenye kuwaka, nyangavu—na kwa kumfaa hivyo mmoja anayetembea kwa bidii na akiwa na msimamo mzuri katika kuwapo kwa Yehova Mungu. Zaidi ya hilo, ingawa katika Biblia mara nyingi vitu vya kimungu hufananishwa na dhahabu, vivyo hivyo vitu vya kibinadamu vinawakilishwa na shaba.c Basi nyayo za Yesu zenye kuwaka kama shaba safi hutukumbusha sisi jinsi nyayo zake zilivyokuwa “zenye uzuri” alipoitembea dunia akihubiri habari njema.—Isaya 52:7; Warumi 10:15, NW.

      11. (a) Nyayo za Yesu zenye utukufu zinatukumbusha sisi nini? (b) Ni nini linaloonyeshwa na uhakika wa kwamba sauti ya Yesu “ilikuwa kama mvumo wa maji mengi”?

      11 Kweli kweli, akiwa binadamu mkamilifu, Yesu alikuwa na mng’ao ulioonekana wazi kwa malaika na wanadamu. (Yohana 1:14) Nyayo zake zenye utukufu pia hutukumbusha sisi kwamba yeye anakanyaga ardhi takatifu katika tengenezo la Yehova, ambamo yeye ndiye Kuhani Mkuu. (Linga Kutoka 3:5.) Zaidi ya hilo, sauti yake hutoa mwangwi ikinguruma kama anguko kubwa mno la poromoko la maji. Inavutia sana, na kutia hofu ya staha, kama imfaavyo mmoja ambaye anaitwa rasmi Neno la Mungu, mmoja ambaye anakuja “kuhukumu dunia inayokaliwa katika uadilifu.”—Matendo 17:31, NW; Yohana 1:1.

      12. Ni nini maana ya ule “upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili”?

      12 “Na katika mkono wake wa kulia alikuwa na nyota saba na katika kinywa chake upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili ulitokeza, na wajihi wake ulikuwa kama jua wakati linapong’aa katika nguvu zalo. Na mimi nilipoona yeye, mimi nilianguka kama mfu kwenye nyayo zake.” (Ufunuo 1:16, 17a, NW) Baadaye kidogo, Yesu mwenyewe anaeleza maana ya hizo nyota saba. Lakini ebu angalia kinachotokeza katika mdomo wake: “Upanga mkali, mrefu na wenye makali mawili.” Ni sura yenye kufaa kama nini! Kwa maana Yesu ndiye aliyewekwa rasmi atamke hukumu za mwisho za Yehova dhidi ya adui Zake. Matamko yenye kukata maneno kutoka kinywa chake hutokeza kufishwa kwa waovu wote.—Ufunuo 19:13, 15.

      13. (a) Wajihi wa Yesu, mwangavu na wenye kuangaza hutukumbusha sisi nini? (b) Tunapata chapa gani yote kutokana na elezeo la Yohana juu ya Yesu?

      13 Wajihi wa Yesu ulio mwangavu, wenye kuangaza hutukumbusha sisi kwamba uso wa Musa ulitokeza miale yenye kuangaza Yehova alipokuwa amezungumza naye juu ya Mlima Sinai. (Kutoka 34:29, 30) Kumbuka, pia, kwamba wakati Yesu alipogeuka sura mbele ya mitume wake watatu karibu miaka 2,000 iliyopita, “uso wake uliangaza kama jua, na mavazi yake ya nje yakawa maangavu kama nuru.” (Mathayo 17:2, NW) Sasa, katika mwakilisho wa kinjozi wa Yesu katika kipindi cha hii siku ya Bwana, hali kadhalika uso wake unarudisha ubora wenye kung’aa wa mmoja ambaye amekuwa katika kuwapo kwa Yehova. (2 Wakorintho 3:18) Kwa kweli, chapa yote inayopelekwa na njozi ya Yohana ni ile ya mng’ao wa utukufu. Kutoka nywele nyeupe kama theluji, macho yenye kutoa mwali wa moto, na wajihi wenye kung’aa mpaka chini kwenye nyayo zenye mwako, ni njozi yenye ubora unaopita wote ya Mmoja ambaye sasa hukaa “katika nuru isiyoweza kukaribiwa.” (1 Timotheo 6:16) Uhalisi wa tamasha hii ni dhahiri sana! Yohana aliyeshikwa mno na hofu ya staha alitendaje? Mtume huyo anatuambia hivi: “Na mimi nilipoona yeye, mimi nilianguka kama mfu kwenye nyayo zake.”—Ufunuo 1:17, NW.

      14. Imetupasa kuathiriwaje wakati tunaposoma njozi ya Yohana juu ya Yesu aliyetukuzwa?

      14 Leo, yale maelezo yenye kupendeza ya njozi ya Yohana yenye habari nyingi yanajaza watu wa Mungu uthamini wa kuhisi moyoni. Tayari, sisi tumekwisha pita zaidi ya miaka 90 ya ile siku ya Bwana, ambayo katika hiyo ile njozi inaendelea kuwa na utimizo wayo wenye kusisimua. Kwetu sisi utawala wa Ufalme wa Yesu ni uhakika uliopo, ulio hai, si tumaini la wakati ujao. Kwa sababu hiyo, inatufaa sisi tulio raia washikamanifu wa Ufalme huo tuzidi kutazama kwa kustaajabu yale ambayo Yohana anaelezea katika njozi hii ya kwanza na kusikiliza kwa utii yale maneno ya Yesu Kristo aliyetukuzwa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kwa elezo refu zaidi, ona kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kurasa 88-92, 215-218, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

      b Katika karne ya kwanza, kundi lilipopokea barua kutoka kwa mtume, ilikuwa desturi kuzungusha barua hiyo kwa makundi mengine ili yote yaweze kunufaika na shauri.—Linga Wakolosai 4:16.

      c Mapambo ya ndani na samani za hekalu la Solomoni yalikuwa yenye kufanyizwa kwa dhahabu au yalifunikwa nayo, lakini shaba ilitumiwa katika kutolea ua vifaa.—1 Wafalme 6:19-23, 28-35; 7:15, 16, 27, 30, 38-50; 8:64.

  • Yohana Aona Yesu Aliyetukuzwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 23]

      Masalio ya uchimbuzi wa vitu vya kale ya majiji ambako yale makundi saba yalikuwa yanathibitisha maandishi ya Biblia. Ni huku Wakristo wa karne ya kwanza walikopokea jumbe zenye kutia moyo za Yesu ambazo leo zinaaamsha kundi la ulimwenguni pote

      PARGAMAMU

      SMIRNA

      THIATIRA

      SARDISI

      EFESO

      FILADELFIA

      LAODIKIA

  • Kufungua Kufuli ya Siri Takatifu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 6

      Kufungua Kufuli ya Siri Takatifu

      1. Imetupasa sisi tutendeje kwa ile picha yenye kuwaka iliyorekodiwa kwenye Ufunuo 1:10-17?

      ILE njozi ya Yesu aliyetukuzwa ni yenye kutia hofu ya staha kweli kweli! Bila shaka, kama sisi tungalikuwa watazamaji kule pamoja na mtume Yohana, sisi pia tungalishindwa na utukufu huo wenye kung’aa, tukisujudu kama alivyofanya. (Ufunuo 1:10-17) Njozi hii bora kuliko zote iliyovuviwa imehifadhiwa ili itwamshe sisi kwenye tendo leo. Kama Yohana, inatupasa tuonyeshe uthamini wa unyenyekevu kwa yote ambayo njozi hii inamaanisha. Sikuzote sisi na tuwe na staha yenye kicho kwa ajili ya cheo cha Yesu akiwa Mfalme mtawazwa, Kuhani Mkuu, na Hakimu.—Wafilipi 2:5-11.

      “Wa Kwanza na wa Mwisho”

      2. (a) Yesu anajitokeza kwa mtajo gani wa cheo? (b) Ni jambo gani linalomaanishwa wakati Yehova anaposema: “Mimi ndiye wa kwanza na wa mwisho”? (c) Kutaja Yesu kuwa “wa Kwanza na wa Mwisho” kunavuta fikira kwenye jambo gani?

      2 Hata hivyo, hofu yetu haipasi kuwa woga wa kufisha. Yesu alimtuliza Yohana, kama vile mtume huyo anavyosimulia yanayofuata: “Na yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu mimi na akasema: ‘Usiwe mwenye hofu. Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho, na yeye aliye hai.’” (Ufunuo 1:17b, 18a, NW) Katika Isaya 44:6, NW, kwa kufaa Yehova anakieleza cheo chake kuwa ndiye Mungu mweza yote mmoja tu na wa pekee, akisema: “Mimi ndiye wa kwanza na wa mwisho, na mbali na mimi hakuna Mungu.”a Yesu anapojitokeza mwenyewe kwa mtajo wa cheo “wa Kwanza na wa Mwisho,” yeye hadai kuwa yu sawa na Yehova, yule Muumba Mtukufu. Yeye anatumia mtajo wa cheo aliopewa kwa kufaa na Mungu. Katika Isaya, Yehova alikuwa akitoa taarifa kuhusu cheo Chake kisicho na kifani akiwa ndiye Mungu wa kweli. Yeye ni Mungu milele, na mbali na yeye hakuna Mungu kweli kweli. (1 Timotheo 1:17) Katika Ufunuo, Yesu anazungumza juu ya mtajo wake wa cheo ambao amepewa, akivuta fikira kwenye ufufuo wake usio na kifani.

      3. (a) Ni katika njia gani Yesu alikuwa “wa Kwanza na wa Mwisho”? (b) Ni jambo gani linalomaanishwa na Yesu kuwa na “funguo za kifo na za Hadesi”?

      3 Yesu alikuwa kweli kweli ndiye binadamu “wa Kwanza” kufufuliwa kwenye uhai wa roho usioweza kufa. (Wakolosai 1:18) Na zaidi, yeye ndiye “wa Mwisho” kufufuliwa hivyo na Yehova binafsi. Hivyo, yeye anakuwa ‘aliye hai, ambaye anaishi milele na milele.’ Yeye anajifurahisha kutokufa. Katika jambo hili, yeye ni kama Baba yake asiyeweza kufa, ambaye anaitwa “Mungu aliye hai.” (Ufunuo 7:2; Zaburi 42:2) Kwa wengine wote wa ubinadamu, Yesu mwenyewe ndiye ‘ufufuo na uhai.’ (Yohana 11:25, NW) Kupatana na hili, yeye anasema kwa Yohana hivi: “Mimi nilipata kuwa mfu, lakini, tazama! mimi ninaishi milele na milele, na mimi nina funguo za kifo na za Hadesi.” (Ufunuo 1:18b, NW) Yehova amempa yeye mamlaka ya kufufua wafu. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaweza kusema kwamba yeye ana funguo za kufungua kufuli za malango kwa ajili ya wale ambao wamefungwa na kifo na Hadesi (jumla ya makaburi).—Linga Mathayo 16:18.

      4. Ni amri gani ambayo Yesu anarudia, na kwa manufaa ya nani?

      4 Hapa Yesu anarudia amri yake ya kuiandika njozi, akimwambia Yohana hivi: “Andika vitu ulivyoona, na vitu vilivyopo na ambavyo vitatukia baada ya hivi.” (Ufunuo 1:19, NW) Ni vitu gani vyenye kusisimua ambavyo bado Yohana atajulisha kwa kutufundisha sisi?

      Zile Nyota na Vile Vinara vya Taa

      5. Yesu anaelezaje “zile nyota saba” na “vile vinara vya taa saba”?

      5 Yohana amemwona Yesu akiwa katikati ya vinara vya taa saba vya dhahabu akiwa na nyota saba katika mkono wake wa kulia. (Ufunuo 1:12, 13, 16) Sasa Yesu anaeleza hilo: “Kwa habari ya siri takatifu ya zile nyota saba ambazo wewe uliona juu ya mkono wangu wa kulia, na ya vile vinara vya taa saba vya dhahabu: Zile nyota saba humaanisha malaika wa yale makundi saba, na vile vinara vya taa saba humaanisha makundi saba.”—Ufunuo 1:20, NW.

      6. Ni kitu gani kinachowakilishwa na hizo nyota saba, na ni kwa sababu gani jumbe zilielekezwa hasa kwa hizo?

      6 Zile “nyota” ni “malaika wa yale makundi saba.” Katika Ufunuo, nyakati nyingine nyota hufananisha malaika halisi, lakini haielekei kwamba Yesu angetumia mwandikaji wa kibinadamu awaandikie viumbe wa roho wasioonekana. Kwa hiyo zile “nyota” lazima ziwe wale waangalizi wa kibinadamu, au wazee, katika makundi, wakionwa kuwa wajumbe wa Yesu.b Hizo nyota zinapelekewa jumbe, kwa kuwa hizo zina daraka la kuangalia kundi la Yehova.—Matendo 20:28.

      7. (a) Ni jambo gani linaloonyesha kwamba Yesu anaposema kwa malaika mmoja hilo halimaanishi kwamba kila kundi lina mzee mmoja tu? (b) Ni nani, kwa kweli, wanaowakilishwa na zile nyota saba katika mkono wa kulia wa Yesu?

      7 Kwa kuwa Yesu anasema kwa “malaika” mmoja tu katika kila kundi, je! hilo linamaanisha kwamba kila kundi lina mzee mmoja tu? La. Mapema kama siku ya Paulo, kundi la Efeso lilikuwa na wazee kadhaa, si mmoja tu. (Ufunuo 2:1; Matendo 20:17) Kwa hiyo katika siku ya Yohana, wakati nyota saba zilipopelekewa jumbe zikasomwe kwenye yale makundi (kutia na kundi la Efeso), nyota hizo lazima ziwe zilisimama badala ya wale wote waliotumikia katika mabaraza ya wazee ndani ya kundi lililopakwa mafuta la Yehova. Hali kadhalika, waangalizi leo husomea makundi barua zinazopokewa kutoka Baraza Linaloongoza, ambalo washiriki walo ni waangalizi wapakwa-mafuta wanaotumikia chini ya ukichwa wa Yesu. Mabaraza ya wazee ya kienyeji yapaswa yahakikishe kwamba shauri la Yesu linafuatwa na makundi yao. Bila shaka, shauri linatolewa kwa manufaa ya wale wote wanaoshirikiana na kundi, na si wazee tu.—Ona Ufunuo 2:11a.

      8. Ni jambo gani linaloonyeshwa na wazee kuwa katika mkono wa kulia wa Yesu?

      8 Kwa kuwa Yesu ndiye Kichwa cha kundi, wazee wanasemwa kwa kufaa kuwa wamo katika mkono wake wa kulia, yaani, chini ya udhibiti na mwelekezo wake. (Wakolosai 1:18) Yeye ndiye Mchungaji Mkuu, nao ni wachungaji walio chini yake.—1 Petro 5:2-4.

      9. (a) Vile vinara vya taa saba vinawakilisha nini, na ni kwa nini vinara vya taa ni mfano unaofaa kwa hao? (b) Ile njozi ingeelekea kumkumbusha mtume Yohana kitu gani?

      9 Vile vinara vya taa saba ni makundi saba ambayo kwayo Yohana anaelekeza kitabu cha Ufunuo: Efeso, Smirna, Pargamamu, Thiatira, Sardisi, Filadelfia, na Laodikia. Ni kwa nini makundi yanafananishwa na vinara vya taa? Ni kwa sababu Wakristo, wawe mmoja mmoja au kwa ujumla kama kundi, sharti ‘waache taa zao ziangaze mbele ya watu’ katika huu ulimwengu wenye kutiwa giza. (Mathayo 5:14-16) Kwa kuongezea, vinara vya taa vilikuwa miongoni mwa samani za hekalu la Solomoni. Kuyaita makundi vinara vya taa inaelekea kungemkumbusha Yohana kwamba, katika maana ya kielezi, kila kundi la kienyeji, la wapakwa-mafuta ni “hekalu la Mungu,” mahali pa kukaliwa na roho ya Mungu. (1 Wakorintho 3:16) Zaidi ya hilo, katika mpango wa kinachofananishwa na hekalu la Kiyahudi, washiriki wa kundi la wapakwa-mafuta wanatumikia wakiwa “ukuhani wa kifalme” katika mpango mkubwa wa hekalu la kiroho la Yehova, ambalo Yesu ndiye Kuhani Mkuu na ambamo Yehova anakaa kibinafsi katika Patakatifu Zaidi Sana pa kimbingu.—1 Petro 2:4, 5, 9; Waebrania 3:1; 6:20; 9:9-14, 24.

      Ule Uasi-Imani Mkubwa

      10. Ni jambo gani lililoupata mfumo wa Kiyahudi na wategemezaji wao wasiotubu katika 70 W.K.?

      10 Wakati Yohana alipoandika Ufunuo, Ukristo ulikuwa na umri wa zaidi ya miaka 60. Mwanzoni, ulikuwa umeokoka miaka 40 ya upinzani wa daima kutoka dini ya Kiyahudi. Kisha mfumo wa Kiyahudi ukapokea pigo la kifo katika 70 W.K. wakati Wayahudi wasiotubu walipopoteza utambulishi wao wa kuwa taifa pamoja na kile ambacho kwao kilikaribia sana kuwa sanamu ya kuabudiwa—lile hekalu katika Yerusalemu.

      11. Kwa nini ilifaa sana yule Mchungaji Mkuu ayaonye makundi juu ya miendo iliyokuwa ikisitawi?

      11 Hata hivyo, mtume Paulo alikuwa ametabiri kwamba kungekuwako uasi-imani miongoni mwa Wakristo wapakwa-mafuta, na jumbe za Yesu huonyesha kwamba katika umri wa uzee wa Yohana uasi-imani huu ulikuwa tayari ukisitawi. Yohana alikuwa wa mwisho wa wale waliokuwa wakitenda wakiwa kizuizi katika jaribio hili la kupindukia la Shetani la kufisidi ile mbegu ya mwanamke. (2 Wathesalonike 2:3-12; 2 Petro 2:1-3; 2 Yohana 7-11) Kwa hiyo ulikuwa wakati unaofaa kwa Mchungaji Mkuu wa Yehova kuandikia wazee katika makundi, akiwaonya juu ya miendo iliyokuwa ikisitawi na kuwatia moyo wale wenye mioyo iliyo sawa wasimame imara kwa ajili ya uadilifu.

      12. (a) Ule uasi-imani ulisitawije katika karne za baada ya siku ya Yohana? (b) Jumuiya ya Wakristo ilipataje kuwako?

      12 Sisi hatujui jinsi makundi yalivyoitikia jumbe za Yesu katika 96 W.K. Lakini tunalojua ni kwamba ule uasi-imani ulisitawi kwa haraka sana baada ya kifo cha Yohana. “Wakristo” waliacha kutumia jina Yehova na badala yalo wakaweka “Bwana” au “Mungu” katika hati za Biblia. Kufikia karne ya nne, lile fundisho bandia la Utatu lilikuwa limepenya kisirisiri katika makundi. Katika pindi ii hii ya wakati, lile wazo la kutokufa kwa nafsi lilikuwa likikubaliwa. Hatimaye, Konstantino Maliki Mroma aliipa dini ya “Kikristo” idhini rasmi ya Serikali, nayo hatua hiyo ikatokeza Jumuiya ya Wakristo, ambamo Kanisa na Serikali ziliunganisha kani zao katika kutawala kwa miaka elfu moja. Lilikuwa jambo rahisi kuwa “Mkristo” wa mtindo mpya. Makabila kwa ujumla yalirekebisha zile itikadi za mapema za kipagani zikawa namna za dini hii. Walio wengi wa viongozi katika Jumuiya ya Wakristo wakawa watawala wa kisiasa wenye kuonea, wakishurutisha watu wakubali maoni yao ya uasi-imani kwa kutumia upanga.

      13. Ijapokuwa onyo la Yesu juu ya kufanyiza mafarakano, Wakristo waliokuwa wakiasi imani walichukua mwendo gani?

      13 Maneno ya Yesu kwa yale makundi saba yalipuuzwa kabisa na Wakristo hao waliokuwa wakiasi imani. Yesu alikuwa amewaonya Waefeso waupate tena ule upendo waliokuwa nao hapo kwanza. (Ufunuo 2:4) Hata hivyo, washiriki wa Jumuiya ya Wakristo, bila kuwa wameungana tena katika upendo kwa ajili ya Yehova, walipiga vita vikali sana na wakanyanyasana vibaya sana. (1 Yohana 4:20) Yesu alikuwa amelionya kundi katika Pargamamu juu ya kufanyiza mafarakano. Hata hivyo, mafarakano yalitokea hata katika karne ya pili, na leo Jumuiya ya Wakristo ina maelfu ya mafarakano na dini zenye kuzozana.—Ufunuo 2:15.

      14. (a) Ingawa Yesu alionya dhidi ya kuwa mfu kiroho, ni mwendo gani uliochukuliwa na wale waliojidai kuwa Wakristo? (b) Ni katika njia zipi wale waliodai kuwa Wakristo walishindwa kutii onyo la Yesu dhidi ya ibada ya sanamu na ukosefu wa adili?

      14 Yesu alikuwa amelionya kundi katika Sardisi dhidi ya kuwa mfu kiroho. (Ufunuo 3:1) Kama hao katika Sardisi, waliodai kuwa Wakristo walisahau upesi juu ya kazi za Kikristo na bila kukawia wakakabidhi kazi ya maana zaidi ya kuhubiri kwa kikundi kidogo, cha jamii ya viongozi wa kidini wenye kulipwa mshahara. Yesu alikuwa amelionya kundi katika Thiatira dhidi ya ibada ya sanamu na uasherati. (Ufunuo 2:20) Hata hivyo, Jumuiya ya Wakristo ilikubali waziwazi utumizi wa sanamu, pamoja na kuendeleza ibada ya sanamu yenye werevu zaidi ya utukuzo wa taifa na upendo wa vitu vya kimwili. Na ukosefu wa adili, ingawa nyakati fulani mahubiri ya kuupinga yalitolewa, sikuzote umekuwa ukivumiliwa kotekote.

      15. Maneno ya Yesu kwa yale makundi saba yanafichua nini kuhusu dini za Jumuiya ya Wakristo, nao makasisi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamethibitika kuwa nini?

      15 Kwa sababu hiyo, maneno ya Yesu kwa yale makundi saba yanafichua kule kushindwa kabisa kwa dini za Jumuiya ya Wakristo kuwa watu wa pekee wa Yehova. Kweli kweli, viongozi wa dini za Jumuiya ya Wakristo wamekuwa ndio washiriki wenye kutokeza zaidi wa ile mbegu ya Shetani. Akisema juu ya hao kuwa ‘yule mtu wa uasi-sheria,’ mtume Paulo alitabiri kwamba ‘kuwapo kwao ni kulingana na utendaji wa Shetani pamoja na kila kazi yenye nguvu na ishara za kusema uwongo na maajabu na pamoja na kila danganyo lisilo la uadilifu.’—2 Wathesalonike 2:9, 10, NW.

      16. (a) Viongozi wa Jumuiya ya Wakristo walionyesha uchukivu wa pekee kwa nani? (b) Ni jambo gani lililotukia katika Jumuiya ya Wakristo katika kile kipindi cha zile Enzi za Katikati? (c) Je! ule uasi au Mapinduzi Makuu ya Kiprotestanti, yalibadili njia za uasi-imani za Jumuiya ya Wakristo?

      16 Huku wakidai kuwa wachungaji wa kundi la Mungu, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo, wa kidini na wa kiserikali, walionyesha uchukivu wa pekee kwa yeyote aliyejaribu kutia moyo usomaji wa Biblia au yeyote aliyefichua mazoea yao yasiyo ya kimaandiko. John Hus na mtafsiri Biblia William Tyndale, walinyanyaswa na wakauawa kwa sababu ya imani yao. Katika kile kipindi chenye kutiwa giza cha Enzi za Katikati, utawala wa wenye kuasi imani ulifikia upeo wao kwa lile Baraza la Kuhukumia Wazushi wa Kidini lenye ukatili mwingi la Kikatoliki. Watu wowote waliopinga mafundisho au mamlaka ya kanisa walikandamizwa bila rehema, na maelfu yasiyohesabika ya wale walioitwa eti wazushi wa kidini waliteswa-teswa mpaka kifo au wakachomwa penye nguzo. Hivyo Shetani alijitahidi kuhakikisha kwamba mbegu yoyote ya kweli ya tengenezo la Yehova lililo mfano wa mwanamke ingepondwa-pondwa kwa haraka sana. Wakati ule uasi au Mapinduzi Makuu ya Kiprotestanti yalipotukia (kuanzia 1517 na kuendelea), makanisa mengi ya Kiprotestanti yalidhihirisha roho ile ile ya kutovumilia. Hayo vilevile yakawa yenye hatia ya damu kwa kuwaua kwa sababu ya imani yao wale wote waliojaribu kuwa washikamanifu kwa Mungu na Kristo. Kweli kweli, “damu ya watakatifu” ilimwagwa kwa wingi sana!—Ufunuo 16:6; linga Mathayo 23:33-36.

      Ile Mbegu Yavumilia

      17. (a) Fumbo la maneno la Yesu la ngano na magugu lilitabiri nini? (b) Ni jambo gani lililotukia katika 1918, likitokeza kukataliwa gani na kuwekwa rasmi gani?

      17 Katika fumbo lake la maneno la ngano na magugu, Yesu alitabiri ule wakati wa giza ambao ungekuwako wakati Jumuiya ya Wakristo ilitawala ikiwa na mamlaka yote. Hata hivyo, kupitia karne zote za uasi-imani, kungekuwako Wakristo mmoja mmoja wa mfano wa ngano, wapakwa-mafuta halisi. (Mathayo 13:24-29, 36-43) Hivyo, wakati siku ya Bwana ilipopambazuka katika Oktoba 1914, Wakristo wa kweli walikuwa wangali wapo duniani. (Ufunuo 1:10) Inaonekana kwamba Yehova alikuja kwenye hekalu lake la kiroho kwa ajili ya kuhukumu karibu miaka mitatu na nusu baadaye, katika 1918, akiandamana na Yesu akiwa “mjumbe wa agano” wake. (Malaki 3:1; Mathayo 13:47-50) Ulikuwa wakati wa kukataa hatimaye wale Wakristo bandia na kuweka rasmi ‘yule mtumwa mwaminifu na mwenye akili juu ya mali yake yote.’—Mathayo 7:22, 23; 24:45-47.

      18. Ni “saa” ipi iliyokuja katika 1914, nao ulikuwa wakati wa yule mtumwa kufanya nini?

      18 Pia ulikuwa wakati wa mtumwa huyu kutoa uangalifu wa pekee kwa vile vitu vilivyoandikwa katika zile jumbe za Yesu zilizopelekwa kwa makundi saba, kama tunavyoona kutokana na mambo yaliyotaarifiwa humo. Mathalani, Yesu anarejeza kwenye kuja kwake kuhukumu makundi, hukumu ambayo ilianza katika 1918. (Ufunuo 2: 5, 16, 22, 23; 3:3) Yeye anasema juu ya kulipa himaya kundi la Filadelfia juu ya “ile saa ya mtihani ambayo yapasa ije juu ya dunia yote nzima inayokaliwa.” (Ufunuo 3:10, 11, NW) Hii “saa ya mtihani” inawasili inapopambazuka tu siku ya Bwana katika 1914, ambayo baada ya hiyo Wakristo walitahiniwa kwa habari ya ushikamanifu wao kwa Ufalme wa Mungu uliosimamishwa.—Linga Mathayo 24:3, 9-13.

      19. (a) Yale makundi saba yanafananisha nini leo? (b) Ni nani ambao wameshirikiana na Wakristo wapakwa-mafuta wakiwa hesabu kubwa-kubwa na kwa nini lile shauri la Yesu na hali anazoeleza Yesu huhusu wao pia? (c) Imetupasa sisi tuzioneje zile jumbe za Yesu kwa yale makundi saba ya karne ya kwanza?

      19 Kwa sababu hii, maneno ya Yesu kwa yale makundi yamekuwa na utumizi wayo mkubwa tangu 1914. Katika mazingira haya, yale makundi saba yanafananisha makundi yote ya Wakristo wapakwa-mafuta katika kipindi cha hii siku ya Bwana. Zaidi ya hilo, katika kipindi cha ile miaka 70 iliyopita na zaidi, hesabu kubwa za waamini ambao tumaini lao ni kuishi milele katika Paradiso duniani wamejiunga na wale Wakristo wapakwa-mafuta waliofananishwa na Yohana. Lile shauri la Yesu Kristo aliyetukuzwa na zile hali alizopata kuona katika yale makundi saba likiwa ni tokeo la ukaguzi wake vinatumika kwa nguvu ile ile kwa makundi haya, kwa kuwa kuna kiwango kimoja tu cha uadilifu na uaminifu kwa watumishi wote wa Yehova. (Kutoka 12:49; Wakolosai 3:11) Hivyo, jumbe za Yesu kwa yale makundi saba ya karne ya kwanza katika Esia Ndogo si madadisi ya kihistoria tu. Zinamaanisha uhai au kifo kwa kila mmoja wetu sisi. Basi, acheni sisi tusikilize kwa makini maneno ya Yesu.

      [Maelezo ya Chini]

      a Katika Kiebrania cha awali kwenye Isaya 44:6, hakuna neno dhihirisho pamoja na maneno “wa kwanza” na “wa mwisho,” hali katika elezeo la Yesu kuhusu yeye binafsi katika Kigiriki cha awali kwenye Ufunuo 1:17, linapatikana lile neno dhihirisho. Kwa hiyo, kisarufi, Ufunuo 1:17 huonyesha mtajo wa cheo, hali Isaya 44:6 huelezea Uungu wa Yehova.

      b Lile neno la Kigiriki agʹge·los (linalotamkwa “anʹge·los”) humaanisha “mjumbe” na vilevile “malaika.” Kwenye Malaki 2:7, kuhani Mlawi anarejezewa kuwa “mjumbe” (Kiebrania, “mal·’akhʹ”).—Ona kielezi cha chini cha New World Translation Reference Bible.

  • Washa Upya Upendo wa Kwanza!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 7

      Washa Upya Upendo wa Kwanza!

      EFESO

      1. Ujumbe wa Yesu wa kwanza unaelekezewa kundi gani, naye anawakumbusha waangalizi nini?

      UJUMBE wa Yesu wa kwanza ni kwa kundi la Efeso, wakati ule likiwa jiji lenye kusitawi la pwani ya Esia Ndogo karibu na kile kisiwa cha Patmosi. Yeye amwamuru Yohana hivi: “Kwa malaika wa kundi katika Efeso andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo yeye anasema ambaye hushika zile nyota saba katika mkono wake wa kulia, yeye ambaye hutembea katikati ya vile vinara vya taa saba vya dhahabu.” (Ufunuo 2:1, NW) Kama ilivyo katika zile jumbe nyingine sita, hapa Yesu anavuta fikira kwenye jambo moja linaloonyesha cheo chake chenye mamlaka. Yeye anakumbusha wale waangalizi wa Efeso kwamba wazee wote wako chini ya uangalizi wake mwenyewe wenye himaya na kwamba yeye anakagua makundi yote. Kuteremka kuingia ndani ya nyakati zetu wenyewe, yeye ameendelea kutumia ukichwa huu wenye upendo, akiwalinda wazee na akichunga kwa fadhili wote wanaoshirikiana na kundi. Wakati kwa wakati, yeye hurekebisha mipango ya kundi ili kuwezesha nuru ing’ae kwa uangavu zaidi. Ndiyo, Yesu ndiye Mchungaji Mkuu juu ya kundi la Mungu.—Mathayo 11:28-30; 1 Petro 5:2-4.

      2. (a) Yesu alisifu kundi la Efeso kwa sababu ya mambo gani mema? (b) Kwa wazi wazee Waefeso walikuwa wametii shauri gani la mtume Paulo?

      2 Kisha Yesu anaweka kigezo kwa zote ila mbili za jumbe zake saba kwa kufungua kwa maneno machangamfu ya kusifu. Kwa Waefeso, yeye ana ujumbe huu: “Mimi najua matendo yako, na kazi ngumu yako na uvumilivu, na ya kwamba wewe huwezi kuhimili watu wabaya, na ya kwamba uliwaweka kwenye mtihani wale ambao husema wao ni mitume, lakini wao sio, nawe uliwapata kuwa waongo. Pia wewe unaonyesha uvumilivu, na wewe umevumilia kwa minajili ya jina langu nawe hujapata kuchoka.” (Ufunuo 2:2, 3, NW) Miaka fulani kabla ya hapa, mtume Paulo alikuwa ameonya wale wazee wa Efeso juu ya “mbwa-mwitu waonezi,” wasumbuaji wa kundi waasi-imani, naye alikuwa amewaambia wazee hao ‘waendelee kuamka,’ wakifuata kielelezo chake mwenyewe cha kutochoka. (Matendo 20:29, 31, NW) Kwa kuwa sasa Yesu anawasifu kwa ajili ya kazi ngumu yao na uvumilivu na kwa ajili ya kutopata kuchoka, lazima wawe walitumia shauri hilo.

      3. (a) “Mitume bandia” wametafutaje kudanganya waaminifu katika siku zetu? (b) Petro alitoa onyo gani juu ya waasi-imani?

      3 Katika kipindi cha ile siku ya Bwana, pia, wametokea “mitume bandia” ambao “husema mambo yaliyopopotoka ili kuvuta mbali wale wanafunzi baada yao wenyewe.” (2 Wakorintho 11:13; Matendo 20:30; Ufunuo 1:10, NW) Wao wanaona wema katika zile dini zote za kimafarakano, wakidai kwamba Mungu hana tengenezo, na kukana kwamba Yesu hakupokea uwezo wa Ufalme katika 1914. Wao hutimiza ule unabii kwenye 2 Petro 3:3, 4, NW: “Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki pamoja na dhihaka yao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe na kusema: ‘Ku wapi huku kuwapo kwake kulikoahidiwa? Kwani, tangu ile siku mababu wetu walipolala usingizi katika kifo, mambo yote yaendelea sawasawa kama yalivyokuwa tangu mwanzo wa kuumba.’”

      4. (a) Kiburi na uasi wa wadhihaki unadhihirishwaje? (b) Wakristo leo wanaonyesha kwamba wao wako kama Waefeso kwa kuchukua tendo gani dhidi ya wapinzani waongo?

      4 Wadhihaki hawa wanaasi lile wazo la kufanya tangazo la peupe la imani yao. (Warumi 10:10) Wao wametumia uungaji-mkono wa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo na msaada wa majarida ya habari na stesheni za TV ili kueneza ripoti za uwongo kuhusu washirika wao wa hapo zamani. Upesi wale waaminifu wanapata kuona kwamba usemi na mwenendo wa wadanganyaji hawa hauna mlio wa ukweli. Kama vile Waefeso, Wakristo leo ‘hawawezi kuhimili watu wabaya,’ kwa hiyo wanawatenga na ushirika watoke katika makundi yao.a

      5. (a) Yesu alisema Waefeso walikuwa na udhaifu gani? (b) Ni onyo gani ambalo Waefeso wangalipaswa kukumbuka?

      5 Hata hivyo, sasa, kama afanyavyo na matano ya yale makundi saba, Yesu anachagua tatizo moja zito. Yeye anasema kwa Waefeso hivi: “Hata hivyo, mimi nina hili dhidi yako wewe, ya kwamba wewe umeacha upendo ambao wewe ulikuwa nao hapo kwanza.” (Ufunuo 2:4, NW) Haingaliwapasa kushindwa katika hili, kwa kuwa Paulo alikuwa amewaandikia miaka 35 mapema akielekeza kwenye “upendo mkubwa [wa Mungu] ambao kwa huo yeye alitupenda sisi,” naye alikuwa amewahimiza hivi: “Iweni waigaji wa Mungu, mkiwa watoto wapendwa, na mzidi kutembea katika upendo, sawa na vile Kristo pia alivyopenda nyinyi.” (Waefeso 2:4; 5:1, 2, NW) Zaidi, maneno ya Yesu yangalipaswa kuandikwa bila kufutika juu ya mioyo yao: “Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote mzima na kwa nafsi yako yote nzima na kwa akili zako zote nzima na kwa uthabiti wako wote mzima.” (Marko 12:29-31, NW) Waefeso walikuwa wamepoteza upendo huo wa kwanza.

      6. (a) Tuwe sisi ni wakale au washiriki wapya katika kundi, ni lazima sisi tujilinde na hatari na maelekeo gani? (b) Upendo wetu kwa Mungu wapaswa utusukume tufanye nini?

      6 Tuwe sisi ni wakale au washiriki wapya katika kundi, lazima sisi tulinde dhidi ya kupoteza upendo wetu wa kwanza kwa Yehova. Ni jinsi gani upotezi huu unaweza kutukia? Tungeweza sisi kuruhusu ufungamano kwa kazi yetu ya kimwili, ile tamaa ya kuchuma pesa nyingi, au ule mfuatilio wa anasa uwe ndicho kitu kikubwa katika maisha zetu. Hivyo sisi tungeweza kuwa watu wenye akili za kimnofu badala ya kuwa wenye akili za kiroho. (Warumi 8:5-8; 1 Timotheo 4:8; 6:9, 10) Upendo wetu kwa Yehova wapasa usukume sisi kusahihisha mielekeo yoyote kama hiyo na ‘tufulize kutafuta Ufalme wa Mungu kwanza na uadilifu wake,’ ili ‘tujiwekee hazina katika mbingu kwa ajili yetu wenyewe.’—Mathayo 6:19-21, 31-33, NW.

      7. (a) Utumishi wetu kwa Yehova wapasa kusukumwa na kitu gani? (b) Yohana alisema nini kwa habari ya upendo?

      7 Acheni utumishi wetu kwa Yehova uwe sikuzote unasukumwa na upendo wenye kina kirefu kwake. Acheni sisi tuwe na uthamini wenye idili kwa yote ambayo Yehova na Kristo wametufanyia sisi. Kama Yohana mwenyewe alivyoandika baadaye: “Upendo uko hivi, si kwamba sisi tumependa Mungu, bali yeye alipenda sisi naye akatuma Mwana wake akiwa dhabihu ya kufunika kwa ajili ya madhambi yetu.” Yohana anaendelea kutuambia sisi hivi: “Mungu ni upendo, na yeye ambaye hubaki katika upendo hubaki katika muungano pamoja na Mungu na Mungu hubaki katika muungano pamoja na yeye.” Sisi tusiache kamwe ufifie upendo wetu kwa Yehova, kwa Bwana Yesu Kristo, na kwa lile Neno la Mungu lenye uhai! Upendo huu tunaweza kuonyesha si katika utumishi wa bidii tu kwa Mungu bali pia kwa utii “kwa amri hii tuliyo nayo kutoka kwake, kwamba mmoja ambaye hupenda Mungu amepaswa kuwa akipenda ndugu yake pia.”—1 Yohana 4:10, 16, 21, NW; Waebrania 4:12; ona pia 1 Petro 4:8; Wakolosai 3:10-14; Waefeso 4:15.

      “Kufanya Yale Matendo ya Hapo Kwanza”

      8. Yesu alisema inawapasa Waefeso kutendaje?

      8 Waefeso hao lazima wawashe upya ule upendo waliokuwa nao wakati mmoja ikiwa wao hawataki kupata hasara. “Kwa hiyo,” Yesu anawaambia, “kumbuka ni kutoka nini wewe umeanguka, na utubu na kufanya yale matendo ya hapo kwanza. Usipofanya, mimi ninakuja kwako wewe, nami nitaondoa kinara cha taa chako kutoka mahali pacho, isipokuwa wewe unatubu.” (Ufunuo 2:5, NW) Wakristo katika kundi la Efeso walipokeaje maneno hayo? Sisi hatujui. Sisi tunatumaini kwamba wao walitubu na kufaulu katika kuamsha tena upendo wao kwa ajili ya Yehova. Ikiwa hawangefanya hivyo, basi taa yao ingezimwa na kinara cha taa chao kingeondolewa. Wao wangepoteza pendeleo lao la kuangaza ule ukweli.

      9. (a) Ni neno gani la kutia moyo ambalo Yesu alikuwa nalo kwa ajili ya Waefeso? (b) Makundi baada ya siku ya Yohana yalishindwaje kutii shauri la Yesu kwa Waefeso?

      9 Hata hivyo, Yesu ana neno hili la kutia moyo kwa Waefeso: “Ingawa hivyo, wewe una hili, ya kwamba wewe unachukia vile vitendo vya lile farakano la Nikolausi, ambalo mimi pia nachukia.” (Ufunuo 2:6, NW) Angalau wao walichukia mgawanyiko wa kimafarakano, kama na Bwana Yesu Kristo huuchukia. Hata hivyo, miaka ilipozidi kupita, makundi mengi yalishindwa kutii maneno hayo ya Yesu. Ukosefu wa upendo kwa ajili ya Yehova, kwa ajili ya ukweli, na kwa ajili ya mmoja na mwenzake ulitokeza kupeperushwa kwao na kuingizwa ndani ya giza la kiroho. Wakavunjika-vunjika kuwa mafarakano mengi-mengi yenye kugombana. Wanukuaji “Wakristo” ambao hawakuwa na upendo kwa ajili ya Yehova waliondoa jina lenyewe la Mungu kutoka hati za Kigiriki za Biblia. Ukosefu huo wa upendo pia uliruhusu nafasi ya kufundisha mafundisho ya Kibabuloni na Kigiriki kama vile moto wa mateso, pargatori, na Utatu, kwa jina la Ukristo. Kwa kutokuwa na upendo kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya ukweli, walio wengi wa wale ambao walidai kuwa Wakristo waliacha kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu. Wakaja kutawalwa na jamii ya viongozi wa kidini yenye ubinafsi ambayo ikafanya ufalme wayo yenyewe hapa duniani.—Linga 1 Wakorintho 4:8.

      10. Hali ya kidini katika Jumuiya ya Wakristo ilikuwaje katika 1918?

      10 Hukumu ilipoanza na nyumba ya Mungu katika 1918, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wenye farakano walikuwa wakitoa waziwazi uungaji-mkono wao kwa Vita ya Ulimwengu 2, wakihimiza Wakatoliki na Waprotestanti katika pande zote mbili kuchinjana. (1 Petro 4:17) Tofauti na kundi la Efeso ambalo lilichukia yaliyokuwa yakifanywa na farakano la Nikolausi, kwa muda mrefu dini za Jumuiya ya Wakristo zilikuwa zimejawa na mafundisho yenye kupinga Mungu, yanayohitilafiana, nao viongozi wazo walikuwa wanajiunga na ulimwengu, ambao Yesu alisema wanafunzi wake lazima wasiwe sehemu yao. (Yohana 15:17-19) Makundi yao, kwa kutojua kile kichwa cha Biblia, Ufalme wa Mungu, hayakuwa vinara vya taa vyenye kuangaza ukweli wa Kimaandiko, wala washiriki wayo hawakuwa sehemu ya hekalu la kiroho la Yehova. Wanaume (na wanawake) wayo wenye kuongoza hawakuwa nyota bali walifunuliwa kuwa washiriki wa “yule mtu wa kuasi.”—2 Wathesalonike 2:3; Malaki 3:1-3.

      11. (a) Ni kikundi gani cha Kikristo kwenye mandhari ya ulimwengu katika 1918 kilichozoea maneno ya Yesu kwa Waefeso? (b) Jamii ya Yohana ilifanya nini tokea 1919 na kuendelea?

      11 Hata hivyo, ile jamii ya Yohana, iliibuka katika zile siku zenye msukosuko za vita ya kwanza ya ulimwengu ikiwa na upendo kwa ajili ya Yehova na kwa ajili ya ukweli ambao uliwasukuma kumtumikia kwa bidii yenye kuwaka mwali. Wao waliwapinga wale waliojaribu kuingiza faraka kupitia tendo lililokaribia sana kumfanya Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, awe sanamu ya kuabudiwa, kufuatia kifo chake katika 1916. Wakiwa wametiwa nidhamu kwa minyanyaso na misiba, kikundi hiki cha Kikristo kwa wazi kilipokea hukumu ya kupongezwa “umefanya vema” kutoka kwa Bwana-Mkubwa wao pamoja na mwaliko wa kuingia katika shangwe yake. (Mathayo 25:21, 23, NW) Wao walitambua katika mwendo wa matukio ya ulimwengu na katika mambo waliyojionea wenyewe, utimizo wa ile ishara ambayo Yesu alikuwa ametoa ya kutia alama kuwapo kwake kusikoonekana katika uwezo wa Ufalme. Kutoka 1919 na kuendelea, wao walisonga mbele washiriki utimizo zaidi wa unabii mkubwa wa Yesu: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 6:9, 10; 24:3-14, NW) Ikiwa upendo wao kwa Yehova ulikuwa umepungukiwa katika njia fulani, ulipepewa tokea wakati huo na kuendelea ukawa mwali wa moto.

      12. (a) Kwenye mkusanyiko wa kihistoria katika 1922, ni mwito gani uliotokezwa? (b) Ni jina gani walilokubali Wakristo wa kweli katika 1931, na walitubia nini?

      12 Kwenye mkusanyiko wa kihistoria, uliohudhuriwa na 18,000 wa hawa Wakristo, kwenye Sida Pointi, Ohaiyo, U.S.A., Septemba 5-13, 1922, mwito ulitokezwa: “Rudini shambani, Enyi wana wa Mungu aliye juu zaidi sana! . . . Lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. . . . Kwa hiyo vumisheni habari, vumisheni habari, vumisheni habari, ya Mfalme na ufalme wake.” Jina la Yehova lenye thamani kubwa lilikuwa linafanywa kuwa mashuhuri zaidi na zaidi. Katika 1931 Wakristo hawa, wakikusanyika katika mkusanyiko huko Kolumbasi, Ohaiyo, U.S.A., walishangilia kulikubali na kuchukua lile jina alilolionyesha Mungu katika unabii wa Isaya—Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10, 12, NW) Kwa toleo lalo la Machi 1, 1939, jina la jarida kuu la tengenezo hilo lilibadilishwa kuwa Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova, hivyo kumpa heshima ya kwanza Muumba wetu na serikali yake ya kifalme. Mashahidi wa Yehova, wakiwa na upendo kwake uliofanywa upya, wametubia kushindwa kokote ambako huenda wakawa walikuwa nako wakati uliopita katika kuheshimu na kukuza jina lake tukufu na Ufalme wake.—Zaburi 106:6, 47, 48.

      “Yeye Ambaye Hushinda”

      13. (a) Ni baraka gani iliyongojea Waefeso ikiwa ‘wangeshinda’? (b) Wakristo Waefeso ‘wangeshindaje’?

      13 Kwa kumalizia, kama afanyavyo pia katika jumbe zake nyingine, Yesu anavuta fikira kwenye roho ya Mungu kuwa inajulisha kupitia Yesu zile thawabu kwa ajili ya uaminifu. Kwa Waefeso yeye anasema hivi: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye hushinda mimi nitaruhusu ale ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu.” (Ufunuo 2:7, NW) Wale walio na masikio ya kusikia wangekuwa na hamu nyingi ya kutii ujumbe huo muhimu, wakijua kwamba haukuja kwa kuanzishwa na Yesu bali kwamba huo ulishuka kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Mkuu Yehova mwenyewe kupitia roho takatifu Yake, au kani-tendaji. Wao wangeweza ‘kushindaje’? Kwa kufuata kwa ukaribu hatua za Yesu, ambaye alishika ukamilifu mpaka kifo na hivyo angeweza kusema: “Jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu!”—Yohana 8:28; 16:33; ona pia 1 Yohana 5:4.

      14. Ni lazima “paradiso ya Mungu” aliyotaja Yesu iwe ilirejezea nini?

      14 Kwa kuwa hao hawana tazamio la kuishi katika paradiso ya kidunia, Wakristo watiwa-mafuta, kama hao Waefeso, wanathawabishwaje kwa kula “ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu”? Hiyo haingeweza kuwa Paradiso iliyorudishwa duniani, kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta 144,000, kutia na wale wa kundi la Efeso, wananunuliwa kutoka wanadamu wakatawale pamoja na Mwana-Kondoo, Kristo Yesu, juu ya Mlima Sayuni wa kimbingu wakiwa wana wa kiroho. (Efeso 1:5-12; Ufunuo 14:1, 4) Kwa sababu hiyo, lile rejezo hapa lazima liwe kwenye makao ya kimbingu mithili ya bustani wanayorithi hao washindi. Humo, “katika paradiso ya Mungu,” ndiyo, katika kuwapo halisi kwa Yehova mwenyewe, washindi hawa ambao wameruhusiwa wawe na kutokufa wataendelea kuishi milele, kama inavyofananishwa hapa na kula kwao ya mti wa uhai.

      15. Kwa nini kitia-moyo cha Yesu kwamba washinde ni chenye upendezi wa muhimu kwa umati mkubwa wa leo?

      15 Namna gani, basi, wale waungaji mkono wa kidunia washikamanifu wa wapakwa-mafuta 144,000? Umati mkubwa wa hawa Mashahidi waandamani wanashinda pia. Lakini tumaini lao hutegemea kuingia katika paradiso ya kidunia ambayo katika hiyo wao watakunywa kutoka “mto wa maji ya uhai” na kupata ponyo kutoka “majani ya miti” iliyopandwa kando-kando za mto huo. (Ufunuo 7:4, 9, 17; 22:1, 2, NW) Ikiwa wewe ni mmoja wa kikundi hiki, wewe pia na uonyeshe upendo wako mchangamfu kwa Yehova na kushinda katika ushindi wa imani. Hivyo wewe huenda ukafikia ile furaha ya uhai wa milele katika dunia Paradiso.—Linga 1 Yohana 2:13, 14.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kwa habari zaidi ya kihistoria juu ya kutokea kwa mitume bandia, ona kurasa 360-367 za kile kitabu cha mafundisho Kutoa Sababu Kwa Kutumia Maandiko, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

  • Kujitahidi Kuwa Washindi
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 8

      Kujitahidi Kuwa Washindi

      SMIRNA

      1. (a) Ni kundi gani linalofuata kupokea ujumbe kutoka kwa Yesu aliyetukuzwa? (b) Kwa kujiita mwenyewe “wa Kwanza na wa Mwisho,” Yesu aliwakumbusha nini Wakristo katika kundi hilo?

      LEO, Efeso la kale linalala likiwa magofu. Lakini kule ambako Yesu alipeleka ujumbe wake wa pili kungali ni mahali penye jiji lenye kuvuma shughuli nyingi. Kilometa zapata 56 kaskazini mwa magofu ya Efeso kuna jiji la Kituruki la Izmiri, ambako makundi manne yenye bidii ya Mashahidi wa Yehova yanapatikana hata leo. Hapo, katika karne ya kwanza, lilikuwako Smirna. Angalia, sasa, maneno yafuatayo ya Yesu: “Na kwa malaika wa kundi katika Smirna andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo anasema, ‘yule wa Kwanza na wa Mwisho,’ ambaye akapata kuwa mfu na akaja kwenye uhai tena.” (Ufunuo 2:8, NW) Kwa kuwataarifu hivi Wakristo hao katika Smirna, Yesu anawakumbusha kwamba yeye alikuwa ndiye mshika ukamilifu wa kwanza ambaye Yehova alifufua moja kwa moja kwenye uhai wa kiroho usioweza kufa na ndiye wa mwisho kuinuliwa hivyo. Yesu mwenyewe angefufua Wakristo wengine wote wapakwa-mafuta. Yeye anastahili vizuri hivyo kuwapa shauri ndugu zake, ambao wanatumaini kushiriki naye uhai wa kimbingu usioweza kufa.

      2. Ni kwa sababu gani Wakristo wote wanafarijiwa na maneno ya Mmoja ambaye “alipata kuwa mfu na akaja kwenye uhai tena”?

      2 Yesu aliongoza njia katika kuvumilia minyanyaso kwa ajili ya uadilifu, naye alipokea thawabu aliyostahili. Uaminifu wake mpaka kifo na ufufuo uliofuata ndio msingi wa tumaini kwa Wakristo wote. (Matendo 17:31) Uhakika wa kwamba Yesu “akapata kuwa mfu na akaja kwenye uhai tena” unathibitisha kwamba lolote ambalo ni lazima livumiliwe katika kusudi la ukweli si kazi bure. Ufufuo wa Yesu ni chanzo cha kitia-moyo chenye kina kirefu kwa Wakristo wote, hasa wakati wanapoitwa wateseke kwa ajili ya imani yao. Je! hii ndiyo hali yako? Basi wewe unaweza kujipa moyo pia kutokana na maneno yanayofuata ya Yesu kwa kundi la Smirna.

      3. (a) Ni kitia-moyo gani ambacho Yesu aliwapa Wakristo katika Smirna? (b) Ingawa Wakristo katika Smirna walikuwa maskini, ni kwa nini Yesu alisema wao walikuwa ‘matajiri’?

      3 “Mimi najua dhiki na umaskini wako—lakini wewe u tajiri—na kufuru la wale ambao husema wao wenyewe ni Wayahudi, na kumbe wao sio bali ni sinagogi la Shetani.” (Ufunuo 2:9, NW) Yesu hana uchambuzi kwa ndugu zake katika Smirna, ana pongezi changamfu tu. Wao wamepatwa na dhiki nyingi sana kwa sababu ya imani yao. Kimwili wao ni maskini, yaelekea kwa sababu ya uaminifu wao. (Waebrania 10:34) Hangaikio lao kuu, hata hivyo, ni vitu vya kiroho, nao wamejiwekea akiba hazina katika mbingu, kama Yesu alivyoshauri. (Mathayo 6:19, 20) Kwa sababu hiyo, Mchungaji Mkuu anawaona wao kuwa “tajiri.”—Linga Yakobo 2:5.

      4. Wakristo katika Smirna walipatwa na upinzani mwingi sana kutoka kwa nani, naye Yesu aliwaonaje wapinzani hao?

      4 Yesu anataja hasa kwamba Wakristo katika Smirna wamechukuana na upinzani mwingi mikononi mwa Wayahudi wa kimnofu. Katika siku za mapema zaidi, wengi wa dini hii walipinga kwa dhati kuenea kwa Ukristo. (Matendo 13:44, 45, 14:19) Sasa, miongo michache tu baada ya Yerusalemu kuanguka, Wayahudi hao katika Smirna wanaonyesha roho ile ile ya kishetani. Si ajabu kwamba Yesu anawaona hao kuwa “sinagogi la Shetani”!a

      5. Ni majaribu gani yaliyokuwa mbele kwa ajili ya Wakristo katika Smirna?

      5 Wakikabiliwa na chuki kama hiyo, Wakristo katika Smirna wanafarijiwa na Yesu hivi: “Usiwe mwenye kuogopa vitu ambavyo wewe u karibu kupatwa navyo. Tazama! Ibilisi atafuliza kutupa baadhi ya nyinyi ndani ya gereza ili nyinyi mtiwe kenyekenye kwenye mtihani, na ili nyinyi muwe na dhiki siku kumi. Jithibitishe mwenyewe kuwa mwaminifu mpaka hata kifo, na mimi nitakupa wewe taji la uhai.” (Ufunuo 2:10, NW) Hapa Yesu mara tatu anatumia namna ya wingi wa Kigiriki kwa “nyinyi,” kuonyesha kwamba maneno yake yanatia ndani kundi kwa ujumla. Yesu hawezi kuahidi kwamba majaribu ya Wakristo katika Smirna yatakoma karibuni. Baadhi yao wataendelea kunyanyaswa na kutupwa gerezani. Wao watakuwa na dhiki kwa “siku kumi.” Kumi ni nambari ambayo huonyesha ukamili au uzima wote wa kidunia. Hata hao washika ukamilifu walio matajiri kiroho watapokea kutahiniwa kikamili wakati wamo katika mnofu.

      6. (a) Ni kwa nini Wakristo katika Smirna hawakupaswa kuogopa? (b) Yesu alimaliziaje ujumbe wake kwa kundi katika Smirna?

      6 Hata hivyo, hao Wakristo katika Smirna hawapaswi kuogopa au kuacha msimamo wao. Ikiwa wao wanabaki waaminifu mpaka mwisho, wamewekewa “taji la uhai” kuwa thawabu, kwao ikiwa ni uhai usioweza kufa katika mbingu. (1 Wakorintho 9:25; 2 Timotheo 4:6-8, NW) Mtume Paulo aliiona zawadi hii yenye thamani kubwa kuwa inastahili kudhabihiwa kila kitu kinginecho chote, hata uhai wake wa kidunia. (Wafilipi 3:8) Kwa wazi, hao waaminifu katika Smirna wanahisi jinsi iyo hiyo. Yesu anamalizia ujumbe wake kwa kusema: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye hushinda hatadhuriwa kwa vyovyote na kifo cha pili.” (Ufunuo 2:11, NW) Washindi wanahakikishiwa uhai wa kimbingu usioweza kufa ambao hauwezi kuguswa na kifo.—1 Wakorintho 15:53, 54.

      “Dhiki Siku Kumi”

      7, 8. Kama vile kundi katika Smirna, kundi la Kikristo ‘lilitiwaje kenyekenye kwenye mtihani’ katika 1918?

      7 Sawasawa na Wakristo katika Smirna, ile jamii ya Yohana na waandamani wao leo wamekuwa na wanaendelea “kutiwa kenyekenye kwenye mtihani.” Uaminifu wao chini ya jaribu huwatia alama ya kuwa watu wa Mungu mwenyewe. (Marko 13:9, 10) Muda mfupi baada ya siku ya Bwana kuanza, maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Smirna yalileta faraja halisi kwa kikundi kidogo cha kimataifa cha watu wa Yehova. (Ufunuo 1:10) Tangu 1879, hao walikuwa wamekuwa wakichimbua kutoka Neno la Mungu utajiri wa kiroho ambao wao walishiriki na wengine bila malipo. Lakini wakati wa Vita ya Ulimwengu 1, walikutana na chuki na upinzani mkali, kwa sehemu kwa sababu wao hawakujitia katika ile harara ya vita na kwa sehemu kwa sababu wao walikuwa wakifunua wazi bila woga makosa ya Jumuiya ya Wakristo. Ule mnyanyaso ambao wao walipokea ukichochewa na baadhi ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo ulifikia upeo katika 1918 na ulilinganika na ule waliopokea Wakristo katika Smirna kutoka jamii ya Kiyahudi iliyokuwa huko.

      8 Wimbi moja la mnyanyaso katika United States ya Amerika lilifikia upeo wakati yule msimamizi mpya wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, Joseph F. Rutherford, na washiriki saba walipelekwa kwenye gereza katika Juni 22, 1918, walio wengi wao wakiwa na hukumu za kifungo cha miaka 20. Waliachiliwa kwa dhamana miezi tisa baadaye. Mei 14, 1919, mahakama ya rufani ilibadili hatia walizowekewa kimakosa; ilionyeshwa kulikuwako makosa 130 katika jaribio hilo. Jaji Manton, Mroma Katoliki, mwenye daraja la utawa wa Mtakatifu Gregori Mkuu, ambaye katika 1918 alikuwa amekataa dhamana kwa hao Wakristo, baadaye katika 1939, alihukumiwa kifungo cha miaka miwili na faini ya dola 10,000 kwa mashtaka sita ya kuomba na kupokea rushwa.

      9. Mashahidi wa Yehova katika Ujeremani wa Nazi walitendwaje na Hitla, na kukiwa tendo-mwitikio gani kutoka viongozi wa kidini?

      9 Wakati wa utawala wa Nazi katika Ujeremani, Hitla alipiga marufuku kabisa kabisa kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova. Kwa miaka kadhaa, maelfu ya Mashahidi walifungwa ndani ya kambi za mateso na magereza kikatili, ambako wengi walikufa, huku wanaume vijana 200 ambao walikataa kupigana katika jeshi la Hitla wakifishwa kwa amri ya serikali. Uungaji-mkono wa viongozi wa kidini wa yote haya unathibitishwa na maneno ya padri Mkatoliki, yaliyochapishwa katika ile nyusipepa The German Way ya Mei 29, 1938. Kwa sehemu, yeye alisema: “Sasa kuna nchi moja duniani ambako wale wanaoitwa eti . . . Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] wamekatazwa. Hiyo ni Ujeremani! . . . Wakati Adolf Hitla alipochukua mamlaka, nayo Episkopati ya Kikatoliki katika Ujeremani ikarudia ombi lao, Hitla akasema: ‘Hawa wanaoitwa eti Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] Wenye Bidii ni wafanyiza matata; . . . mimi nawaona kuwa wadanganyaji; mimi sivumilii kwamba Wakatoliki Wajeremani watatupiwa matope jinsi hiyo na huyu Mwamerika Jaji Rutherford. Mimi nafumua [Mashahidi wa Yehova] katika Ujeremani.’” Kwa hayo, yule padri akaongeza: “Hongera!”

      10. (a) Kadiri ile siku ya Bwana imeendelea, Mashahidi wa Yehova wamekabili mnyanyaso gani? (b) Mara nyingi tokeo lilikuwa nini wakati Wakristo walipopigania uhuru wa kidini katika mahakama?

      10 Kadiri ile siku ya Bwana imesonga mbele, yule Nyoka na mbegu yake hawakukoma kamwe kupiga vita dhidi ya Wakristo wapakwa-mafuta na waandamani wao. Wengi wa hawa wametiwa gerezani na kunyanyaswa kikatili sana. (Ufunuo 12:17) Maadui hao wameendelea ‘kutunga madhara kwa njia ya sheria,’ lakini watu wa Yehova kwa uthabiti husisitiza: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” (Zaburi 94:20; Matendo 5:29, NW) Katika 1954 gazeti Mnara wa Mlinzi liliripoti: “Zaidi ya nchi sabini katika wakati mmoja au mwingine katika muda wa miaka arobaini iliyopita zimefanyiza amri zuifu nazo zimenyanyasa Mashahidi wa Yehova.” Mahali ambako imewezekana kupigania uhuru wa kidini katika mahakama, Wakristo hawa wamefanya hivyo na katika nchi kadha wa kadha wamepata ushindi mwingi wenye mshindo mkubwa. Katika Mahakama Kuu Zaidi ya United States pekee, Mashahidi wa Yehova wameshinda maamuzi 50 yenye kupendeleka.

      11. Ni unabii gani wa Yesu kuhusu ile ishara ya kuwapo kwake ambao umetimizwa juu ya Mashahidi wa Yehova wakati wa hii siku ya Bwana?

      11 Hakuna kikundi kinginecho chote kimekuwa chenye kudhamiria kadiri hiyo katika kutii amri ya Yesu ya kulipa Kaisari vitu vya Kaisari. (Luka 20:25; Warumi 13:1, 7) Hata hivyo, hakuna kikundi kinginecho chote kimekuwa na washiriki waliotiwa gerezani katika mabara mengi hivyo chini ya namna nyingi hivyo mbalimbali za serikali, na jambo hili linaendelea mpaka wakati uu huu katika zile bara za Amerika, katika Europa, katika Afrika, na katika Esia. Unabii mkubwa wa Yesu kuhusu ile ishara ya kuwapo kwake ulitia ndani maneno haya: “Kisha watu watakabidhi nyinyi katika dhiki na wataua nyinyi, na nyinyi mtakuwa vitu vya kuchukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.” (Mathayo 24:3, 9, NW) Bila shaka hilo limetimizwa juu ya Mashahidi Wakristo wa Yehova wakati wa hii siku ya Bwana.

      12. Jamii ya Yohana imeimarishaje watu wa Mungu dhidi ya mnyanyaso?

      12 Ili kuwaimarisha watu wa Mungu dhidi ya dhiki, ile jamii ya Yohana kwa kuendelea imewakumbusha maana ya maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Smirna. Kwa mfano, mnyanyaso wa Kinazi ulipoanza, Mnara wa Mlinzi katika 1933 na 1934 ulikuwa na makala kama vile “Msiwaogope,” ambayo ilizungumzia Mathayo 10:26-33; “Lile Tanuri,” iliyotegemea Danieli 3:17, 18; na “Makanwa ya Simba,” Danieli 6:22 lilikuwa andiko kuu. Katika miaka ya muda wa tangu 1980, mwongo ambao katika huo kitabu hiki kilichapishwa kwa mara ya kwanza na Mashahidi wa Yehova wakanyanyaswa vikali katika mabara zaidi ya 40, Mnara wa Mlinzi uliimarisha watu wa Mungu kwa makala kama vile “Wenye Furaha Wajapoteswa!” na “Wakristo Wanaelekeana na Mateso kwa Uvumilivu.”b

      13. Kama vile Wakristo katika Smirna, ni kwa nini Mashahidi Wakristo wa Yehova hawajakuwa wakiogopa mnyanyaso?

      13 Kweli kweli, Mashahidi wa Yehova Wakristo wanapata mnyanyaso wa kimwili na mitihani mingine kwa siku kumi za mfano. Kama vile Wakristo huko nyuma katika Smirna, wao hawakuwa wakiogopa; wala hakuna yeyote wetu anayehitaji kuogopa taabu zizidipo kuwa mbaya hapa duniani. Sisi tuko tayari kuvumilia chini ya mateso na hata ‘kukubali kunyang’anywa mali zetu kwa furaha.’ (Waebrania 10:32-34) Kwa kujifunza Neno la Mungu na kulifanya liwe letu wenyewe, sisi tutatayarishwa tusimame tukiwa thabiti katika imani. Uwe na hakika kwamba Yehova anaweza kulinda na atalinda wewe katika ukamilifu wako. ‘Tupia yeye mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakujali wewe.’—1 Petro 5:6-11, NW.

      [Maelezo ya Chini]

      a Yapata miaka 60 baada ya Yohana kufa, Polycarp mwenye umri wa miaka 86 aliteketezwa mpaka kifo katika Smirna kwa sababu yeye hangeweza kukana itikadi yake katika Yesu. The Martyrdom of Polycarp, kitabu kinachoitikadiwa kuwa cha wakati ule ule mmoja na tukio hili, hutaarifu kwamba wakati kuni zilipokuwa zikikusanywa za kuteketeza yeye, “wale Wayahudi walikuwa na bidii kupita kiasi, kama ilivyo desturi yao, katika kusaidia katika hili”—hata ingawa kufishwa huko kulitukia katika “siku kubwa ya Sabato.”

      b Ona The Watchtower ya Novemba 1, 1933; Oktoba 1 na 15, Desemba 1 na 15, 1934; Mnara wa Mlinzi Oktoba 1, 1983.

  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 9

      Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu

      PARGAMAMU

      1. Ni kundi gani lililofuata kupokea ujumbe wa Yesu, na Wakristo hao waliishi katika jiji la aina gani?

      TUKISAFIRI kilometa 80 kaskazini kufuata barabara ya pwani kutoka Smirna kisha kilometa 24 kuingia ndani ya bara kupitia bonde la Mto Kaikusi, tunakuja Pargamamu, linaloitwa Bargama sasa. Jiji hilo lilisifika sana kwa sababu ya hekalu lalo la Zeusi, au Jupita. Katika muda wa miaka ya 1800 na kitu wachimbuzi wa mambo ya kale walisafirisha madhabahu ya hekalu hilo kuipeleka Ujeremani, ambako ingali inaweza kutazamwa, pamoja na sanamu na michoro mingi ya miungu ya kipagani, kwenye Pergamon Museum katika Berlin. Ni ujumbe gani ambao Bwana Yesu angepelekea kundi linaloishi katikati ya ibada hii yote ya sanamu?

      2. Yesu anathibitishaje utambulisho wake, na ni nini maana ya yeye kuwa na ‘upanga wenye makali mawili’?

      2 Kwanza, Yesu anathibitisha utambulisho wake, akisema: “Na kwa malaika wa kundi katika Pargamamu andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo yeye anasema ambaye ana upanga mkali mrefu, wenye makali mawili.” (Ufunuo 2:12, NW) Hapa Yesu anarudia yale maelezo yaliyotolewa kuhusu yeye kwenye Ufunuo 1:16. Akiwa Jaji na Mfishaji, yeye atawapiga na kuangusha chini wale ambao hunyanyasa wanafunzi wake. Uhakikishio huo ni wenye kufariji kama nini! Kwa habari ya hukumu, hata hivyo, acheni wale walio ndani ya kundi wapate onyo pia kwamba Yehova, akitenda kupitia huyu “mjumbe wa agano,” Yesu Kristo, “atakuwa shahidi mwepesi” dhidi ya wote wanaodai kuwa Wakristo ambao huzoea ibada-sanamu, ukosefu wa adili, kusema uwongo, na ukosefu wa haki na ambao hushindwa kuangalia wahitaji. (Malaki 3:1, 5; Waebrania 13:1-3, NW) Ni lazima kutii lile shauri na karipio ambalo Mungu anafanya Yesu atoe!

      3. Ni ibada gani ya bandia iliyofanyika katika Pargamamu, na inaweza kusemwaje kwamba “kiti cha ufalme cha Shetani” kilikuwa huko?

      3 Sasa Yesu analiambia kundi hivi: “Mimi najua mahali unapokaa, yaani, palipo na kiti cha ufalme cha Shetani.” (Ufunuo 2:13a, NW) Kweli kweli, Wakristo hao walizungukwa na ibada ya kishetani. Kuongezea lile hekalu la Zeusi, palikuwapo patakatifu pa Eskulapiusi, kale kamungu ka maponyo. Pargamamu lilisifika pia kuwa kitovu cha lile dhehebu la ibada ya mfalme wa milki. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “Shetani” linamaanisha “Mkinzani,” na “kiti cha ufalme” chake kinawakilisha utawala wake wa ulimwengu kama unavyoruhusiwa kimungu kwa muhula fulani. (Ayubu 1:6, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini) Wingi wa ibada ya sanamu katika Pargamamu ulionyesha kwamba “kiti cha ufalme” cha Shetani kilikuwa kimeimarishwa sana katika jiji hilo. Ni lazima Shetani awe alihisi hasira jinsi gani kwamba Wakristo huko hawakumwinamia katika ibada ya utukuzo wa taifa!

      4. (a) Yesu anawapa pongezi gani Wakristo katika Pargamamu? (b) Mjumbe wa Kiroma Plini aliandikia Maliki Trajani nini kwa habari ya kutendewa kwa Wakristo? (c) Ijapokuwa hatari, Wakristo katika Pargamamu walichukua mwendo gani?

      4 Ndiyo, “kiti cha ufalme cha Shetani” kimo mle mle Pargamamu. “Na hata hivyo,” Yesu aendelea, “wewe unafuliza kushikilia kwa imara jina langu, nawe hukukana imani yako katika mimi hata katika siku za Antipasi, shahidi wangu, mwaminifu, ambaye aliuawa kando yako, anapokaa Shetani.” (Ufunuo 2:13b, NW) Lo, ni pongezi lenye kuchochea nafsi kama nini! Bila shaka kifo cha imani cha Antipasi kilitokana na kukataa kwake kufuatana na mazoea ya kishetani na ibada ya maliki wa Kiroma. Si muda mrefu baada ya Yohana kupokea unabii huu, Plini, Mchanga, mjumbe wa kibinafsi wa Maliki Trajani wa Roma, alimwandikia Trajani na kueleza njia yake ya kushughulikia watu walioshtakiwa kuwa Wakristo—njia ambayo maliki alikubali. Wale waliokana kuwa Wakristo waliachiliwa wakati, kama Plini alivyosema, “wao walikuwa wamerudia baada ya mimi sala kwa tumiungu, wameutolea mfano wako [Trajani] uvumba na divai . . . na kwa kuongezea, wakalaani Kristo.” Wowote waliopatikana wakiwa Wakristo walifishwa. Hata ingawa walikabiliwa na hatari hiyo, Wakristo katika Pargamamu hawakukana imani yao. Wao ‘walishikilia kwa imara jina la Yesu’ katika maana ya kwamba wao waliendelea kuheshimu cheo chake kitukufu akiwa Mteteaji wa Yehova na Jaji aliyewekwa rasmi. Kishikamanifu, wao walifuata hatua za Yesu wakiwa mashahidi wa Ufalme.

      5. (a) Ni kifano gani cha ki-siku-hizi cha dhehebu la ibada ya maliki ambacho kimesababisha mitihani mikali kwa Wakristo katika nyakati zetu? (b) Ni msaada gani ambao Mnara wa Mlinzi umeandalia Wakristo?

      5 Pindi mbalimbali, Yesu alikuwa amejulisha kwamba Shetani hutawala ulimwengu mbovu uliopo, lakini kwa sababu ya ukamilifu wa Yesu, Shetani hakuwa na nguvu juu yake. (Mathayo 4:8-11; Yohana 14:30) Katika nyakati zetu mataifa yenye nguvu, hasa yule “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini,” wameng’ang’ania utawala wa ulimwengu. (Danieli 11:40) Harara ya kizalendo imechochewa, nalo dhehebu la ibada ya maliki lina kifano cha ki-siku-hizi kwa namna ya wimbi la utukuzo wa taifa ambao umeenea pote duniani. Makala juu ya kutokuwamo katika The Watchtower ya Novemba 1, 1939, na tena Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1980, na Septemba 1, 1986, zimetaarifu waziwazi fundisho la Biblia juu ya suala hili, zikiandaa miongozo kwa ajili ya Wakristo wanaotaka kutembea katika jina la Yehova na kuushinda ulimwengu, kama Yesu alivyofanya kwa ujasiri sana.—Mika 4:1, 3, 5; Yohana 16:33; 17:4, 6, 26; 18:36, 37; Matendo 5:29.

      6. Kama vile Antipasi, Mashahidi wa Yehova wamechukuaje msimamo thabiti katika nyakati za ki-siku-hizi?

      6 Shauri kama hilo limekuwa likihitajiwa kwa uharaka sana. Usoni mwa harara ya uzalendo wenye kupita kiasi, Mashahidi wa Yehova, wapakwa-mafuta na pia waandamani wao, wamekuwa sharti wasimame wakiwa thabiti katika imani. Katika United States, mamia ya watoto na walimu walifukuzwa shuleni kwa sababu hawakusalimu bendera ya kitaifa, hali katika Ujeremani Mashahidi walinyanyaswa vikali kwa kukataa kusalimu swastika. Kama ilivyokwisha kuonyeshwa, Wanazi wa Hitla waliua watumishi washikamanifu wa Yehova kwa sababu walikataa kushiriki ibada ya sanamu kama hiyo ya kitaifa. Katika miaka ya 1930, wakati wa usitawi mwingi wa ibada ya Shinto ya maliki wa Japani, wahudumu wawili mapainia walipanda mbegu nyingi za Ufalme katika Taiwani iliyokaliwa na Wajapani. Watawala wa kivita waliwatupa gerezani, ambamo mmoja wao alikufa kwa sababu ya kutendwa kikatili. Yule mwingine aliachiliwa baadaye, akaja tu kupigwa risasi mgongoni—Antipasi wa ki-siku-hizi. Mpaka leo hii, kuna mabara ambamo ibada ya mifano ya kitaifa na kujitoa kabisa kabisa kwenye serikali ni mambo yanayodaiwa. Mashahidi wengi vijana wametiwa gerezani, na si wachache wakafishwa, kwa sababu ya msimamo wao wa ushujaa wakiwa Wakristo wasiokuwamo. Ikiwa wewe ni kijana anayekabili masuala kama hayo, jifunze neno la Mungu kila siku ili wewe uweze ‘kuwa na imani ya kuhifadhi hai nafsi’ kwa kutazamia uhai wa milele.—Waebrania 10:39–11:1, NW; Mathayo 10:28-31.

      7. Vijana wachanga katika India walikabilije suala la ibada ya utukuzo wa taifa, na kwa tokeo gani?

      7 Walio wachanga wameelekeana na masuala kama hayo shuleni. Katika 1985 katika mkoa wa Kerala, India, watoto watatu wachanga wa Mashahidi wa Yehova walikataa kuacha msimamo wao uliotegemea imani ya Biblia, wakikataa kuimba wimbo wa kutukuza taifa. Wao walisimama kwa heshima huku wengine wakiimba, lakini hata hivyo walifukuzwa shuleni. Baba yao alikata rufani ya tendo hilo moja kwa moja mpaka Mahakama Kuu Zaidi ya India ambako majaji wawili waliamua kwa kupendelea watoto, wakitaarifu hivi kwa ujasiri: “Pokeo letu hufundisha uvumiliano, falsafa yetu hufundisha uvumiliano; katiba yetu huzoea uvumiliano; acheni sisi tusiipunguze nguvu.” Utangazaji wa nyusipepa na tahariri zenye kupendeleka zilizotokana na kesi hii zilijulisha taifa zima, ambalo wakati huo idadi yake ilikaribia sehemu moja kwa tano ya idadi ya dunia, kwamba kuna Wakristo katika bara lile ambao huabudu Mungu wa kweli Yehova na kwamba hawa wanasimama kishikamanifu kwa kanuni za Biblia.

      Mavutano Yenye Kufisidi

      8. Ni laumu gani ambalo Yesu anaona linahitajiwa kabisa Wakristo kupewa katika Pargamamu?

      8 Ndiyo, Wakristo katika Pargamamu ni washika-ukamilifu. “Hata hivyo,” asema Yesu, “mimi nina vitu vichache dhidi yako.” Wao wamefanya nini kustahili laumu? Yesu anatuambia sisi: “Wewe unao hapo wale wanaoshikilia kwa imara lile fundisho la Balaamu, aliyeenda akifundisha Balaki kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, kula vitu vilivyodhabihiwa kwa sanamu na kufanya uasherati.”—Ufunuo 2:14, NW.

      9. Balaamu alikuwa nani, na shauri lake liliwekaje “kikwazo mbele ya wana wa Israeli”?

      9 Katika siku ya Musa, Mfalme Balaki wa Moabu alikuwa amemwajiri Balaamu, nabii asiye Mwisraeli aliyejua habari juu ya njia za Yehova, alaani Israeli. Yehova alimpinga Balaamu, akimshurutisha atangaze baraka kwa ajili ya Waisraeli na ole kwa ajili ya adui zao. Balaamu alituliza chukio ambalo lilitoka kwa Balaki kwa kudokeza shambulio la hila zaidi. Acha wanawake Wamoabi watongoze wanaume wa Israeli na kuwaingiza katika ukosefu wa maadili na ibada ya sanamu mbaya sana ya mungu bandia Baali wa Peori! Hila hii ilikuwa na matokeo. Hasira yenye uadilifu ya Yehova iliwaka, alipokuwa akipeleka pigo ambalo liliua Waisraeli hao waasherati 24,000—pigo ambalo lilikomeshwa tu wakati kuhani Finehasi alipochukua tendo lenye kufaa kuondoa ubaya kutoka kwa Israeli.—Hesabu 24:10, 11; 25:1-3, 6-9; 31:16.

      10. Ni vikwazo gani ambavyo vimepenya ndani ya kundi katika Pargamamu, na ni kwa nini yamkini Wakristo hao wangeweza kuhisi kwamba Mungu angeachilia makosa yao?

      10 Sasa, katika siku ya Yohana, je! kuna vikwazo hali moja na hivyo katika Pargamamu? Viko! Ukosefu wa adili na ibada ya sanamu vimepenya ndani ya kundi. Wakristo hao hawakutii maonyo ya Mungu yaliyotolewa kupitia mtume Paulo. (1 Wakorintho 10:6-11) Kwa kuwa wao wamevumilia mnyanyaso, pengine wao wanahisi kwamba Yehova ataachilia makosa yao ya kingono. Kwa hiyo Yesu anawaambia waziwazi kwamba ni lazima wao waepuke uovu kama huo.

      11. (a) Inawapasa Wakristo walinde dhidi ya nini, na ni kufikiri kwa namna gani ambako lazima kuepukwe? (b) Kwa muda wa miaka iliyopita, ni wangapi waliotengwa na ushirika wa kundi la Kikristo, na zaidi sana ni kwa sababu zipi?

      11 Hali moja na hiyo leo, Wakristo lazima walinde dhidi ya ‘kugeuza fadhili zisizostahiliwa za Mungu wetu kuwa kisababu cha mwenendo mlegevu.’ (Yuda 4, NW) Sisi tunawajibishwa kuchukia lililo baya na ‘kupiga-piga ngumi miili yetu’ ili tufuatilie mwendo wa wema wa Kikristo. (1 Wakorintho 9:27, NW; Zaburi 97:10; Warumi 8:6) Haitupasi kamwe kufikiri kwamba bidii katika utumishi wa Mungu na ukamilifu chini ya mnyanyaso hutupa sisi leseni ya kujitia katika mwenendo mbaya wa kingono. Katika muda wa miaka iliyopita, wakosaji waliotengwa na ushirika wa kundi la Kikristo la ulimwenguni pote, zaidi sana kwa sababu za ukosefu wa adili kingono, wamefikia hesabu ya makumi ya maelfu. Katika miaka fulani kumekuwako hata wengi zaidi ya wale walioanguka katika Israeli wa kale kwa sababu ya Baali wa Peori. Sisi na tufulize kulinda ili tusije kuanguka kamwe katika mashirika hayo!—Warumi 11:20; 1 Wakorintho 10:12.

      12. Kama ilivyokuwa kwa watumishi wa Mungu katika nyakati za mapema, ni kanuni zipi zinazotumika kwa Wakristo leo?

      12 Pia Yesu anawakemea Wakristo katika Pargamamu kwa ‘kula vitu vilivyodhabihiwa kwa sanamu.’ Hilo lingetia ndani nini? Kwa sababu ya maneno ya Paulo kwa Wakorintho, labda wengine walikuwa wakitumia vibaya uhuru wao wa Kikristo na kukosea kimakusudi dhamiri za wengine. Hata hivyo, linalowezekana zaidi ni kwamba wao walikuwa wakishiriki kwa njia fulani katika sherehe halisi za sanamu. (1 Wakorintho 8:4-13; 10:25-30) Wakristo waaminifu leo lazima waonyeshe upendo usio na ubinafsi katika kutumia kwao uhuru wa Kikristo, wakiwa waangalifu wasiwakwaze wengine. Hakika, lazima wao waepuke namna za ki-siku-hizi za ibada ya sanamu, kama vile kuabudu wachezaji mashuhuri wa TV, sinema, na michezo, au kufanya pesa kuwa kamungu, au hata tumbo lao wenyewe!—Mathayo 6:24; Wafilipi 1:9, 10; 3:17-19.

      Epuka Farakano!

      13. Ni maneno gani ya karipio ambayo Yesu anafuata kuwatolea Wakristo katika Pargamamu, na ni kwa nini kundi hilo liliyahitaji?

      13 Yesu anakaripia zaidi Wakristo katika Pargamamu, akisema: “Vivyo wewe, pia, unao hao wanaoshikilia kwa imara lile fundisho la lile farakano la Nikolausi hali kadhalika.” (Ufunuo 2:15, NW) Hapo kwanza, Yesu amesifu Waefeso kwa kuchukia kwao matendo ya farakano hili. Lakini Wakristo katika Pargamamu wanahitaji shauri juu ya kufuliza kutunza kundi likiwa bila farakano. Uthabiti zaidi unahitajiwa katika kutegemeza viwango vya Kikristo ili ule umoja ambao Yesu alisali kwenye Yohana 17:20-23 uhifadhiwe. Inahitajiwa kabisa “kutia moyo kwa fundisho ambalo ni lenye afya na kukaripia pia wale wanaopinganisha maneno.”—Tito 1:9, NW.

      14. (a) Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limelazimika kushindana na akina nani, na mtume Paulo aliwaelezaje? (b) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kutiiwa na yeyote ambaye huenda ikawa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali?

      14 Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limekuwa halina budi kushindana na waasi-imani wenye kiburi, ambao kwa usemi laini, wenye kudanganya “husababisha migawanyiko na sababu za kukwaza kinyume cha fundisho” lililoandaliwa kupitia mfereji wa Yehova. (Waroma 16:17, 18, NW) Mtume Paulo alionya juu ya tisho hili karibu katika barua zake zote.a Katika nyakati za ki-siku-hizi, wakati ambapo Yesu amerudishia kundi la Kikristo la kweli usafi na umoja walo, hatari ya farakano inabaki. Kwa sababu hiyo, yeyote ambaye huenda alikuwa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali, hivyo kufanyiza farakano, apaswa atii maneno yafuatayo ya Yesu: “Kwa hiyo tubu. Usipofanya hivyo, mimi naja kwako upesi, nami nitapiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa changu.”—Ufunuo 2:16, NW.

      15. Farakano linaanzishwaje?

      15 Farakano linaanzishwaje? Pengine mwalimu fulani wa kujifanya anapanda mashaka, akibishia ukweli fulani wa Biblia (Kama vile kuwa kwetu sisi katika siku za mwisho), na hivyo kikundi kilicho kisehemu kinavunjika na kutoka kumfuata yeye. (2 Timotheo 3:1; 2 Petro 3:3, 4) Au mtu fulani anachambua ile njia ambayo katika hiyo Yehova anafanyiza kazi yake naye anavuta ile roho ya kutofanya mengi sana kwa kudai kwamba kwenda nyumba kwa nyumba na ujumbe wa Ufalme si njia ya Kimaandiko wala haihitajiwi kabisa. Kushiriki utumishi kama huo kufuatia kielelezo cha Yesu na mitume wake kungewaendeleza hawa wakiwa wanyenyekevu; hata hivyo, wao wanaona ni afadhali wajitenge na kujistarehesha, pengine wakisoma Biblia tu pindi kwa pindi wakiwa kikundi cha faragha. (Mathayo 10:7, 11-13; Matendo 5:42; 20:20, 21) Watu kama hao wanabuni mawazo yao wenyewe juu ya Ukumbusho wa Kifo cha Yesu, ile amri ya Kimaandiko ya kuepukana na damu, kusherehekea sikukuu, na tumizi la tumbako. Zaidi ya hilo, wao wanashushia heshima jina la Yehova; upesi sana wanaanguka na kurudi ndani ya njia zenye kuendekeza za Babuloni Mkubwa. Hata vibaya zaidi, baadhi yao wanasukumwa na Shetani wageukie na ‘kupiga watumwa wenzao,’ ambao wakati mmoja walikuwa ndugu zao.—Mathayo 24:49; Matendo 15:29; Ufunuo 17:5, NW.

      16. (a) Kwa nini wale wanaoyumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani inawapasa watubu upesi? (b) Ni nini litakalopata wale wanaokataa kutubu?

      16 Wowote ambao wanayumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani wapaswa wawe wepesi kutii mwito wa Yesu wa kutubu! Propaganda ya waasi-imani lazima ikataliwe kuwa ni sumu! Msingi wayo ni husuda na chuki, tofauti na zile kweli zenye uadilifu, safi, na zenye kupendeka ambazo Yesu analisha kundi lake. (Luka 12:42; Wafilipi 1:15, 16; 4:8, 9) Kwa habari ya wale wanaokataa kutubu kweli kweli Bwana Yesu ‘hupiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa chake.’ Yeye anapepeta watu wake ili kuhifadhi ule umoja ambao kwa ajili yao yeye alisali wakati wa jioni yake ya mwisho pamoja na wanafunzi wake duniani. (Yohana 17:20-23, 26) Kwa kuwa waasi-imani wanakataa lile shauri lenye upendo na msaada unaotolewa na zile nyota zilizo kwenye mkono wake wa kulia, Yesu anawahukumu na kuwaadhibu “kwa ukali ulio mkubwa zaidi sana,” akiwaweka kwenye “giza nje.” Wanatengwa na ushirika, wasitende tena kama chachu miongoni mwa watu wa Mungu.—Mathayo 24:48-51; 25:30; 1 Wakorintho 5:6, 9, 13; Ufunuo 1:16, NW.

      ‘Mana Iliyofichwa na Kijiwe cha Mviringo Cheupe’

      17. Ni thawabu gani inayongojea Wakristo wapakwa-mafuta ‘wanaoshinda,’ na ni nini ambacho Wakristo katika Pargamamu walihitaji kushinda?

      17 Thawabu tukufu inawangojea wote ambao hutii shauri la Yesu, linalotolewa kwa mwelekezo wa roho takatifu ya Yehova. Sikiliza! “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye anashinda mimi nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa kijiwe cha mviringo cheupe, na juu ya kijiwe cha mviringo cheupe jina mpya lililoandikwa ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.” (Ufunuo 2:17, NW) Hivyo, Wakristo katika Pargamamu kama vile wale Wakristo katika Smirna, wanatiwa moyo ‘washinde.’ Ikiwa watafanikiwa, wale walioko Pargamamu, ambako kuna kiti cha ufalme cha Shetani, lazima waepuke ibada ya sanamu. Lazima washinde ukosefu wa adili, farakano, na uasi-imani unaounganishwa na Balaki, Balaamu, na lile farakano la Nikolausi. Wakifanya hivyo, Wakristo hao wapakwa-mafuta wataalikwa wale baadhi ya “ile mana iliyofichwa.” Hii inamaanisha nini?

      18, 19. (a) Ni nini iliyokuwa mana ambayo Yehova aliandalia Waisraeli? (b) Ni mana gani iliyofichwa? (c) Ni nini linalofananishwa na kula baadhi ya ile mana iliyofichwa?

      18 Katika siku ya Musa, Yehova aliandaa mana kuendeleza Waisraeli wakati wa safari yao ya jangwani. Mana hiyo haikufichwa, kwa kuwa kila asubuhi—isipokuwa Sabato—ilitokea kimuujiza, kama sakitu yenye vipande vipande vyembamba vyenye kufunika ardhi. Lilikuwa andalio la kimungu ili kuendeleza hai Waisraeli. Ili iwe ukumbusho, Yehova alimwamuru Musa aweke baadhi ya huu “mkate” katika chupa ya dhahabu ndani ya lile sanduku takatifu la agano “katika vizazi vyote [vya Israeli].”—Kutoka 16:14, 15, 23, 26, 33; Waebrania 9:3, 4, NW.

      19 Ni mfano wenye kufaa kama nini! Mana hii ilifichwa ndani ya chumba cha Patakatifu Zaidi Sana cha ile hema, ambamo ile nuru ya kimuujiza ambayo ilining’inia juu ya kifuniko cha lile sanduku ilifananisha kuwapo kwenyewe kwa Yehova. (Kutoka 26:34) Hakuna mmoja aliyeruhusiwa kupenya ndani ya mahali hapo patakatifu ili ale mana hiyo iliyofichwa. Hata hivyo, Yesu alisema kwamba wafuasi wake wapakwa-mafuta wanaoshinda wangekula “ile mana iliyofichwa.” Kama vile Kristo aliyewatangulia, wao wanapata kuingia, “[si] katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali . . . mbinguni hasa.” (Waebrania 9:12, 24) Wakati wa ufufuo wao, wanavaa kutofisidika na kutokufa—andalio zuri ajabu la Yehova, linalofananishwa na kupewa kwao ile “mana iliyofichwa” isiyoweza kuharibika. Lo! kundi hilo dogo la washindi ni lenye pendeleo kama nini!—1 Wakorintho 15:53-57.

      20, 21. (a) Ni nini inayofananishwa na kuwapa Wakristo wapakwa-mafuta kijiwe cha mviringo cheupe? (b) Kwa kuwa kuna vijiwe vya mviringo vyeupe 144,000 tu, ni tumaini gani ulilo nalo ule umati mkubwa?

      20 Hawa pia wanapokea “kijiwe cha mviringo cheupe.” Katika mahakama za Kiroma vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa katika kupitisha hukumu.b Kijiwe cha mviringo cheupe kilimaanisha ondoleo la hatia, hali kijiwe cha mviringo cheusi kilimaanisha hukumu ya laana, mara nyingi ni ya kifo. Kwa kuwapa Wakristo katika Pargamamu “kijiwe cha mviringo cheupe” Yesu angeonyesha kwamba yeye anawahukumu wao kuwa wasio na hatia, wenye kutakata, na walio safi. Lakini maneno ya Yesu huenda yakawa na maana zaidi. Katika nyakati za Kiroma, vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa pia kuwa tikiti za kupata ruhusa ya kuingia kwenye matukio ya maana. Kwa hiyo kijiwe cha mviringo cheupe huenda kikaonyesha kitu fulani cha pekee sana kwa Mkristo mpakwa-mafuta mwenye kushinda—kuruhusiwa kwake kuingia mahali penye heshima katika mbingu kwenye arusi ya Mwana-Kondoo. Ni vijiwe vya mviringo vyeupe kama hivyo 144,000 tu vinavyoandaliwa.—Ufunuo 14:1; 19:7-9.

      21 Je! hii inamaanisha kwamba wewe umeachwa bila kufikiriwa ikiwa wewe ni mmoja wa waabudu waandamani wa ule umati mkubwa? Sivyo hata kidogo! Ingawa hupokei kile kijiwe cha mviringo cheupe cha ruhusa ya kuingia mbinguni, huenda wewe, ukivumilia, ukatoka katika dhiki kubwa uwe na sehemu katika kazi yenye kujaa furaha ya kurudisha Paradiso duniani. Watakaoshiriki pamoja nawe kazi hiyo ni waaminifu watakaofufuliwa wa tangu nyakati za kabla ya Ukristo na wale wa kondoo wengine ambao huenda wakawa walikufa hivi majuzi zaidi. Mwishowe, wafu wengine wote waliokombolewa watapendelewa wawe na ufufuo kwenye uhai katika dunia paradiso.—Zaburi 45:16; Yohana 10:16; Ufunuo 7:9, 14.

      22, 23. Ni nini maana ya lile jina lililoandikwa juu ya kijiwe cha mviringo cheupe wanalopewa Wakristo wapakwa-mafuta, na hilo lapasa liandae kitia-moyo gani?

      22 Ni nini lile jina jipya lenye kuandikwa juu ya kile kijiwe cha mviringo cheupe? Jina ni njia ya kutambulisha mtu na kumtofautisha huyo na wengine. Hawa Wakristo wapakwa-mafuta wanapokea kile kijiwe cha mviringo cheupe baada ya wao kumaliza mwendo wao wa kidunia wakiwa washindi. Kwa wazi, basi, lile jina juu ya kijiwe cha mviringo cheupe linahusiana na pendeleo lao la kuwa wameunganishwa na Yesu mbinguni—cheo cha ukaribu zaidi sana cha utumishi wa kifalme kinachopasa kuthaminiwa kabisa kabisa na kufurahiwa na wale tu wanaorithi Ufalme wa kimbingu. Kwa sababu hiyo, ni jina au mtajo wa ofisi, “ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.”—Linga Ufunuo 3:12.

      23 Lo! ni kichocheo kama nini kwa jamii ya Yohana ‘isikie ambacho roho husema kwa makundi’ na kukitumia! Na jinsi hilo linavyowatia moyo washirika wenzao, ule umati mkubwa, watumikie kiaminifu pamoja nao wakati wanapoweza kufurahia uandamani wao hapa duniani na kushiriki pamoja nao kuujulisha Ufalme wa Yehova!

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona pia 1 Wakorintho 3:3, 4, 18, 19; 2 Wakorintho 11:13; Wagalatia 4:9; Waefeso 4:14, 15; Wafilipi 3:18, 19; Wakolosai 2:8; 1 Wathesalonike 3:5; 2 Wathesalonike 2:1-3; 1 Timotheo 6:3-5; 2 Timotheo 2:17; 4:3, 4; Tito 1:13, 14; 3:10; Waebrania 10:26, 27.

      b Ona Matendo 26:10 na kielezi cha chini, New World Translation Reference Bible.

  • Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 10

      Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”

      THIATIRA

      1. Thiatira lilikuwa mahali gani kuhusiana na makundi mengine, na lilikuwa na mazingira ya kidini ya namna gani?

      KILOMETA zapata 68 kusini-mashariki mwa Bargama (Pargamamu) kuna Akhisari, mji wa Kituruki wenye kusitawi. Yapata miaka 1,900 iliyopita, mji huu ndipo mahali lilipokuwa Thiatira. Mwangalizi asafiriye angeweza kwa urahisi kufikia Thiatira kwa barabara ya barani kutoka Pargamamu na kisha azunguke kwenye makundi yanayobaki ya Ufunuo sura ya 3—Sardisi, Filadelfia, na Laodikia. Tofauti na Pargamamu, Thiatira halionekani kuwa lilikuwa kitovu chenye maana cha ibada ya maliki, lakini lilikuwa na vihekalu na mahekalu yaliyowekwa wakfu kwa tumungu twa kipagani. Thiatira lilikuwa na sifa ya kuwa kitovu cha biashara ya kiuchumi.

      2, 3. (a) Ni nini lililokuwa limeandikwa mapema zaidi juu ya Mthiatira mmoja aliyepata kuwa Mkristo? (b) Kuna umaana gani kwa Wakristo katika Thiatira kwamba Yesu ni “Mwana wa Mungu” na kwamba yeye ana “macho kama mwali wenye moto”?

      2 Paulo alipokuwa akihubiri Makedonia, alikutana na mwanamke wa Thiatira aliyeitwa Lidia, muuza zambarau. Lidia pamoja na watu wote wa nyumba yake walikubali kwa mteremo ujumbe aliokuwa akihubiri Paulo na akaonyesha ukaribishaji-wageni usio wa kawaida. (Matendo 16:14, 15) Akawa Mthiatira wa kwanza kutiwa kwenye maandishi aliyekubali Ukristo. Baada ya muda fulani, jiji lenyewe likaja kuwa na kundi la Wakristo. Yesu anaelekeza huko ujumbe wake ulio mrefu kupita zote: “Na kwa malaika wa kundi katika Thiatira andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo Mwana wa Mungu asema, yeye ambaye ana macho yake kama mwali wa moto, na nyayo zake kama shaba safi.”—Ufunuo 2:18, NW.

      3 Huu ndio wakati pekee ambapo usemi “Mwana wa Mungu” unaonekana katika Ufunuo, ingawa mahali kwingine Yesu humtaja Yehova kuwa “Baba yangu.” (Ufunuo 2:27; 3:5, 21) Tumizi la jina hilo la cheo hapa inaelekea linakumbusha Wakristo wa Thiatira juu ya uhusiano wa karibu alio nao Yesu pamoja na Yehova. Mwana huyu “ana macho yake kama mwali wa moto”—onyo kwa Wakristo katika Thiatira kwamba hukumu yake itawaka dhidi ya chochote anachoona kuwa kinachafua kundini. Kwa kurejeza mara ya pili kwenye nyayo zake zenye kuwaka, zilizo kama shaba, yeye anakazia kielelezo chake mwenyewe cha uaminifu wenye kung’aa alipokuwa akiitembea dunia hii. Wale Wakristo katika Thiatira bila shaka walitii shauri hili, na ndivyo nasi lazima tutii leo!—1 Petro 2:21.

      4, 5. (a) Ni kwa nini Yesu angeweza kusifu Wakristo katika Thiatira? (b) Kundi katika Thiatira ni kifananishi jinsi gani leo cha makundi ya Mashahidi wa Yehova?

      4 Kwa furaha, Yesu anaweza kusifu hao waliomo Thiatira. Yeye anasema: “Mimi najua matendo yako, na upendo wako na imani na huduma na uvumilivu, na kwamba matendo yako ya baadaye yanazidi yale ya hapo kwanza.” (Ufunuo 2:19, NW) Tofauti na Waefeso, Wakristo wapakwa-mafuta huko hawakupoteza ule upendo wao wa kwanza kwa ajili ya Yehova. Imani yao ni thabiti. Zaidi ya hilo, matendo yao yanazidi yale ya hapo kwanza, na kama vile yale makundi matatu yaliyotangulia, Wakristo katika Thiatira wanavumilia. Ni kifananishi kama nini cha yale makundi karibu 100,000 ya Mashahidi wa Yehova kotekote duniani leo! Upendo kwa ajili ya Yehova unang’aa kwa kupenya, kwa kuwa roho ya bidii katika huduma inaenea pote katika tengenezo, ikichochea wachanga na wazee. Nambari inayozidi kuongezeka wanajitumikisha wenyewe wakiwa mapainia, hivyo wakitumia kwa hekima ule wakati ambao ungali unabaki kutangaza tumaini tukufu la Ufalme wa Yehova unaokuja!—Mathayo 24:14; Marko 13:10.

      5 Kwa miongo fulani, waaminifu wengi, wa mabaki ya wapakwa-mafuta na ule umati mkubwa pia, wamekuwa wakionyesha kielelezo kizuri cha uvumilivu katika utumishi wa Mungu, huku ulimwengu unaowazunguka ukiwa umekuwa ukizidi kutumbukia ndani ya giza zito lisilo na tumaini. Lakini acheni sisi tuwe na ushujaa! Ufunuo unathibitisha ule ushahidi wa manabii wa Mungu wakati wa mapema zaidi. “Hiyo siku ya Bwana [Yehova, NW] iliyo kuu i karibu; i karibu, nayo inafanya haraka sana.”—Sefania 1:14; Joeli 2:1; Habakuki 2:3; Ufunuo 7:9; 22:12, 13.

      “Huyo Mwanamke Yezebeli”

      6. (a) Yajapokuwa mambo yenye kusifika, ni tatizo gani analoona Yesu katika kundi la Thiatira linalohitaji uangalifu wa mara moja? (b) Yezebeli alikuwa nani, na je! yeye alikuwa na dai halali la kuwa nabii wa kike?

      6 Macho yenye moto ya Yesu yamepenya zaidi. Yeye anaona jambo linalohitaji uangalifu wa mara moja. “Hata hivyo,” yeye anawaambia Wakristo katika Thiatira, “mimi nina hili dhidi yako, kwamba wewe wavumilia huyo mwanamke Yezebeli, ambaye hujiita mwenyewe nabii wa kike, naye huwafundisha na kuongoza vibaya watumwa wangu wafanye uasherati na kula vitu vilivyodhabihiwa kwa sanamu.” (Ufunuo 2:20, NW) Katika karne ya kumi K.W.K., Malkia Yezebeli, mke mwabudu Baali wa Mfalme Ahabu wa Israeli, alikuwa amekuwa mwenye sifa mbaya sana kwa sababu ya njia zake za kuua kimakusudi, kufanya uzinzi na za kutawala. Yehu, akiwa mpakwa-mafuta wa Yehova, aliagiza auawe. (1 Wafalme 16:31; 18:4; 21:1-16; 2 Wafalme 9:1-7, 22, 30, 33) Yezebeli mwabudu-sanamu hakuwa na dai la kuwa nabii wa kike. Yeye hakuwa kama Miriamu na Debora, waliotumikia wakiwa manabii wa kike waaminifu katika Israeli. (Kutoka 15:20, 21; Waamuzi 4:4; 5:1-31) Na roho ya Yehova haikumsukuma atoe unabii kama ilivyosukuma Ana mwenye umri wa uzee na wale mabinti wanne wa Filipo mweneza-evanjeli.—Luka 2:36-38; Matendo 21:9.

      7. (a) Kwa kutaja “huyo mwanamke Yezebeli,” kwa wazi Yesu anarejezea uvutano gani? (b) Huenda wanawake washiriki fulani wakawa waliteteaje mwendo wao wa kujitakia yao?

      7 Kwa wazi, basi, “huyo mwanamke Yezebeli” anayedai kuwa nabii wa kike katika Thiatira ni bandia. Yeye hana utegemezo wa roho ya Mungu. Yeye ni nani? Inaelekea, yeye ni mwanamke au kikundi cha wanawake wanaotenda wakiwa uvutano wenye kufisidi na usio na haya katika kundi lile. Wanawake washiriki fulani huenda wakawa walikuwa wakiwahusisha washiriki katika ukosefu wa adili, huku wakitetea kwa ukavu wa macho mwendo wao wa kujitakia yao kwa kutumia maandiko kimakosa. Kutoa unabii kibandia kweli kweli! Wangevuta wengine waangukie njia zao wenyewe za “uasherati, ukosefu wa usafi, hamu ya ngono, tamaa yenye kudhuru, na uchoyo, ambao ni ibada ya sanamu.” (Wakolosai 3:5, NW) Wangetaka wale waliomo kundini washiriki katika mtindo wa maisha wenye ukosefu wa adili, kujitafutia yao wenyewe kwa namna ile ambayo sasa inakubaliwa, au kuachiliwa, katika dini zilizo nyingi za Jumuiya ya Wakristo.

      8. (a) Ni nini tamko la hukumu la Yesu juu ya yule “Yezebeli” katika Thiatira? (b) Uvutano wa kike usiofaa umehisiwaje katika nyakati za ki-siku-hizi?

      8 Yesu anaendelea kuwaambia wazee katika Thiatira hivi: “Na mimi nilimpa wakati wa kutubu, lakini yeye hataki kutubu uasherati wake. Tazama! Mimi niko karibu kutupa yeye katika kitanda cha ugonjwa, na wale wanaofanya uasherati pamoja na yeye katika dhiki kubwa, wasipotubu matendo yake.” (Ufunuo 2:21, 22, NW) Kama vile yule Yezebeli wa kwanza kabisa kwa wazi alivyomtawala Ahabu na kisha akamkaidi Yehu, mfishaji wa Mungu, ndivyo uvutano huu wa kike huenda ukawa unajaribu kutumia hila juu ya waume na wazee. Inaonekana kwamba wazee katika Thiatira wanavumilia uvutano huu usio na kiasi wa Yezebeli. Hapa Yesu anatoa onyo kali kwao, pamoja na kwa kundi lililo kwenye tufe lote la watu wa Yehova leo. Katika nyakati za ki-siku-hizi, baadhi ya wanawake kama hao wenye nia ngumu wameshawishi waume zao wawe waasi-imani na hata wamechukua hatua ya kimahakama dhidi ya watumishi waaminifu wa Yehova.—Linga Yuda 5-8.

      9. (a) Ni kwa nini maneno ya Yesu juu ya Yezebeli hayaonyeshi sifa mbaya juu ya wanawake wote katika kundi? (b) Ni wakati gani tu uvutano wa Kiyezebeli unapozuka?

      9 Hili kwa vyovyote halionyeshi sifa mbaya juu ya wanawake waaminifu katika kundi la Kikristo. Siku hizi, sehemu kubwa ya kazi ya kutoa ushuhuda inatimizwa na akina dada waaminifu; kupitia mafunzo ya Biblia ya nyumbani wanayoongoza, wanaleta ndani ya kundi misongamano ya watu wapya. Mungu mwenyewe anabariki mpango huu, kama inavyoonyeshwa na Zaburi 68:11, NW: “Yehova mwenyewe hutoa usemi; wanawake wanaosimulia habari njema ni jeshi kubwa.” Huenda waume wakavutwa kwa mema na mwenendo wa upole, wenye staha wa wake zao, ambao “ni wenye thamani kubwa katika macho ya Mungu.” (1 Petro 3:1-4, NW) Mke hodari, mwenye bidii ya kufanya kazi anasifiwa na Mfalme Lemueli. (Mithali 31:10-31, NW) Ni wakati tu wanawake wanaporuka mpaka kwa kutongoza wanaume au kwa kukaidi au kupuuza ukichwa ndipo uvutano wa Kiyezebeli unapozuka.—Waefeso 5:22, 23; 1 Wakorintho 11:3.

      10. (a) Ni kwa nini Yezebeli na watoto wake walipokea hukumu? (b) Wale wanaokuwa watoto wa Yezebeli wako katika hali gani ya hatari, na watu kama hao imewapasa wafanye nini?

      10 Akirejezea “huyo mwanamke Yezebeli,” Yesu anaendelea: “Na watoto wake mimi nitaua kwa tauni yenye kufisha, ili makundi yote yajue kwamba mimi ndiye ambaye huchunguza figo na mioyo, na mimi nitatoa kwa nyinyi mmoja mmoja kulingana na matendo yenu.” (Ufunuo 2:23, NW) Yesu ameruhusu Yezebeli na watoto wake wakati wa kutubu, lakini wao wanaendelea katika njia zao za ukosefu wa adili na kwa sababu hiyo lazima wapokee hukumu. Hapa pana ujumbe wenye nguvu nyingi kwa Wakristo leo. Wale wanaoiga Yezebeli, wawe ni wanaume au wanawake, na hivyo wamekuwa watoto wake kwa kuhalifu kanuni za Biblia juu ya ukichwa na maadili au kwa kuwa wenye kichwa kigumu hivi kwamba wanapuuza utaratibu wa kitheokrasi, kwa njia ya kiroho wamo katika hali yenye hatari sana ya ugonjwa. Ni kweli, ikiwa mmoja kama huyo anawaita wazee katika kundi wakamwombee, hiyo “sala ya imani itafanya huyo asiye na maelekeo mazuri ahisi vema, na Yehova atainua yeye”—maadamu yeye anatenda kwa unyenyekevu kupatana na sala hizo. Lakini yeyote asifikiri kwamba yeye anaweza kudanganya Mungu au Kristo kwa kujaribu kuficha matendo ya ukosefu wa adili au kwa kujivika wonyesho wa nje-nje wa utumishi wenye bidii.—Yakobo 5:14, 15, NW.

      11. Makundi leo yanasaidiwa jinsi gani yakae macho ili yaone upenyezi wa uvutano wa kike usio halali?

      11 Kwa furaha, yaliyo mengi ya makundi ya Mashahidi wa Yehova leo yako macho kuona hatari hii. Wazee wanalinda waone miendo ya mielekeo isiyo ya kitheokrasi na utendaji makosa. Wanajaribu kusaidia wanaume na wanawake walio katika njia ya hatari ili hao wajenge hali ya kiroho na kurekebishwa kabla haijawa kuchelewa mno. (Wagalatia 5:16; 6:1) Kwa upendo na kwa uthabiti, waangalizi hawa Wakristo wanazuia jitihada yoyote ya kike ya kufanyiza vikundi vikundi vya kuendeleza miendo kama ile ya ukombozi wa wanawake. Zaidi ya hilo, pindi kwa pindi shauri la wakati wenye kufaa linatolewa katika vichapo vya Mashahidi wa Yehova.a

      12. Ni kwa njia gani jamii ya Yohana leo inaonyesha bidii kama ile ya Yehu?

      12 Hata hivyo, kunapokuwa na ukosefu wa adili mbaya sana, na hasa hilo linapokuwa ni zoea, watenda dhambi wasiotubu lazima watengwe na ushirika. Sisi tunakumbuka bidii ya Yehu katika kuondolea mbali dalili zote za uvutano wa Kiyezebeli katika Israeli. Hali moja na hiyo, ile jamii ya Yohana leo inachukua tendo thabiti, ikiwawekea kielelezo waandamani wenzao wa jamii ya “Yonadabu” na kujionyesha wenyewe kuwa tofauti kwa mbali sana na wahudumu wenye kuendekeza wa Jumuiya ya Wakristo.—2 Wafalme 9:22, 30-37; 10:12-17.

      13. Ni nini litakalowapata wale wanaoshindwa na uvutano wenye makosa wa kike?

      13 Akiwa Mjumbe na Hakimu wa Yehova, Mwana wa Mungu anatenda kwa usahihi katika kutambulisha Yezebeli wa ki-siku-hizi na kumtupa ndani ya kitanda cha ugonjwa, kwa kuwa ugonjwa wake wa kiroho ni wenye kusendeka kweli kweli. (Malaki 3:1, 5) Wale ambao wameshindwa na uvutano huu wenye makosa wa kike pia watapatwa na dhiki kubwa—ile huzuni ya kutengwa na ushirika, kukatiliwa mbali na kundi la Kikristo kama kwamba ni wafu. Isipokuwa hawa wanatubu, wanageuka, na wanakubaliwa tena ndani ya kundi, wanakabili pia kifo cha kimwili kwa “tauni yenye kufisha”—mwishowe kabisa, katika ile dhiki kubwa. Kwa wakati huu, kurudishwa kunawezekana ikiwa wanatubia kabisa matendo yao yenye kosa.—Mathayo 24:21, 22; 2 Wakorintho 7:10.

      14. (a) Yesu anatumiaje wazee katika kushughulikia matatizo fulani, kama vile uvutano wowote wa Kiyezebeli? (b) Imelipasa kundi liungeje mkono wazee wanaoshughulikia matatizo kama hayo?

      14 “Makundi yote” lazima yaje kujua kwamba Yesu anachunguza “figo,” zile hisia zenye kina kirefu zaidi sana, na ‘moyo,’ yule mtu wa ndani-ndani zaidi, kutia na makusudio yaliyo chinichini. Kutimiza hilo, yeye anatumia nyota, au wazee wenye kuitibarika, katika kushughulikia matatizo fulani fulani, kama vile uvutano wowote wa Kiyezebeli unaotokea. (Ufunuo 1:20, NW) Baada ya hawa wazee kuchunguza kikamili jambo fulani la aina hii na hukumu imekwisha pitishwa, si juu ya watu mmoja mmoja kuchungua-chungua ni kwa sababu gani na kwa nini hatua ilichukuliwa vile. Wote wamepaswa kukubali kwa unyenyekevu kumalizwa kwa mambo na wazee na kuendelea kuunga mkono nyota hizi za kundi. Ushikamanifu kwa Yehova na kwa mipango yake ya kitengenezo utathawabishwa. (Zaburi 37:27-29; Waebrania 13:7, 17) Kwa upande wako mwenyewe, fungu lako na liwe baraka wakati Yesu anampa kila mtu mmoja mmoja kulingana na matendo yake.—Wagalatia 5:19-24; 6:7-9.

      ‘Shikilia kwa Imara Ulicho Nacho’

      15. (a) Yesu alikuwa na vitu gani vya kusema kwa wale ambao hawakufisidiwa na Yezebeli? (b) Ni jambo gani linaloonyesha kwamba si wote waliodai kuwa Wakristo huko nyuma katika 1918 walikuwa wamefisidiwa na Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani?

      15 Maneno yanayofuata ya Yesu yanaleta faraja: “Hata hivyo, mimi nasema kwa nyinyi wengine mliomo Thiatira, wale wote ambao hawana fundisho hili, wale hasa ambao hawakupata kujua ‘vitu vyenye kina kirefu vya Shetani,’ kama wasemavyo: Mimi siweki juu yenu nyinyi mzigo mwingine wowote. Hata hivyo, shikilieni kwa imara kile mlicho nacho mpaka mimi nije.” (Ufunuo 2:24, 25, NW) Kuna nafsi zenye uaminifu katika Thiatira ambazo hazikuvutwa na Yezebeli. Hali moja na hiyo, kwa miaka 40 kabla ya 1918 na tangu hapo, si Wakristo wote waliovumilia njia za ukosefu wa adili, zenye ufisadi ambazo zimeenea sana katika Jumuiya ya Wakristo. Kile kikosi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia, kinachojulikana sasa kuwa Mashahidi wa Yehova, kilichojaribu kusaidia washiriki wa kanisa waone asili isiyo ya Kikristo ya mengi ya mafundisho ya Jumuiya ya Wakristo, kimechukua hatua ya kujiondolea itikadi zote za Kibabuloni na mazoea yaliyopokewa kupitia Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani. Hii inatia ndani fundisho lenye kuendekeza la “huyo mwanamke Yezebeli.”

      16. Ingawa Yesu na baraza lenye kuongoza la Kikristo la karne ya kwanza hakuongeza mzigo zaidi, ni vitu gani ambavyo lazima viepukwe?

      16 Ile jamii ya Yohana leo imetia moyo pia waandamani wao, ule umati mkubwa, kujihadhari na mavutano ya ukosefu wa adili, kama yale yaliyomo katika ulimwengu wa matumbuizo wenye kushusha tabia. Hakuna haja ya kuona au kujaribu ufisadi kwa sababu ya udadisi au ili kujifunza cha kuepuka. Ni mwendo wa hekima kukaa mbali sana na “vitu vyenye kina kirefu vya Shetani.” Kama asemavyo Yesu: “Mimi siweki juu yenu nyinyi mzigo mwingine wowote.” Hili linatukumbusha ile amri ya baraza lenye kuongoza la Kikristo la karne ya kwanza. “Roho takatifu na sisi wenyewe tumependelea tusiongeze mzigo zaidi kwenu nyinyi, isipokuwa vitu hivi vya lazima, kuendelea kushika mwiko wa vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na wa damu na wa vitu vilivyonyongwa na wa uasherati. Ikiwa kwa uangalifu mnajiepusha nyinyi wenyewe na vitu hivyo, mtafanikiwa.” (Matendo 15:28, 29, NW) Kwa ajili ya ufanisi wa kiroho, epuka dini bandia, tumizi baya la damu (kama vile kutiwa damu mishipani) na ukosefu wa adili! Na yaelekea afya yako ya kimwili itapewa himaya vilevile.

      17. (a) Shetani ameshawishije watu leo kwa “vitu vyenye kina kirefu”? (b) Mwelekeo wetu umepaswa kuwa nini juu ya “vitu vyenye kina kirefu” vya ulimwengu wa Shetani wenye kutatanisha?

      17 Shetani ana “vitu vyenye kina kirefu” vingine leo, kama vile makisio-makisio magumu na falsafa ambazo husifu-sifu mno ule uwezo wa akili. Kuongezea masababio ya ukosefu wa adili na yenye kuendekeza, hivi hutia ndani kuwasiliana na roho na ile nadharia ya mageuzi. Muumba mwenye hekima yote anaonaje hivi “vitu vyenye kina kirefu”? Mtume Paulo anamnakili kuwa akisema: “Mimi nitaharibu hekima ya wenye hekima.” Tofauti na hayo, “vitu vyenye kina kirefu vya Mungu” ni sahili, ni vyenye kueleweka, na vyenye kuchangamsha moyo. Wakristo wenye hekima huepuka “vitu vyenye kina kirefu” vya ulimwengu wa Shetani wenye kutatanisha. Kumbuka, “ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.”—1 Wakorintho 1:19, Kingdom Interlinear; 2:10; 1 Yohana 2:17, NW.

      18. Ni baraka gani ambazo Yesu aliwaahidi Wakristo wapakwa-mafuta wanaobaki kuwa waaminifu kuteremka mpaka mwisho, na ni pendeleo gani ambalo hawa wafufuliwa watakuwa nalo kwenye Har–Magedoni?

      18 Kwa Wakristo hao katika Thiatira, sasa Yesu anasema maneno yenye kuchangamsha moyo. Hayo yanawatia moyo pia Wakristo wapakwa-mafuta leo: “Na yeye ambaye hushinda na kushika matendo yangu kuteremka mpaka mwisho mimi nitampa mamlaka juu ya mataifa, na yeye atachunga watu kwa ufito wa chuma hivi kwamba watavunjwa vipande vipande kama vyombo vya udongo wa mfinyanzi, sawasawa na ambavyo mimi nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufunuo 2:26, 27, NW) Ni pendeleo zuri ajabu kweli kweli. Mamlaka hii ambayo washindi wapakwa-mafuta wanapokea kwenye ufufuo wao ni ushiriki pamoja na Yesu katika kupunga “ufito wa chuma” wa uharibifu dhidi ya mataifa yenye kuasi kwenye Har–Magedoni. Zikifanikiwa zaidi sana, zile nguvu-moto za nyukilia za mataifa zitalialia kama fataki zilizolowa maji wakati Kristo atavunja vipande vipande adui zake kama vile angefanyia vyombo vya udongo wa mfinyanzi.—Zaburi 2:8, 9; Ufunuo 16:14, 16; 19:11-13, 15.

      19. (a) Ni nani aliye “ile nyota ya asubuhi,” naye atapewaje kwa wale ambao hushinda? (b) Ni kitia-moyo gani unachotolewa ule umati mkubwa?

      19 Yesu anaongeza hivi: “Na mimi nitampa ile nyota ya asubuhi.” (Ufunuo 2:28, NW) Yesu mwenyewe anaeleza baadaye hiyo “nyota” ni nini, akisema: “Mimi ndiye ule mzizi na mzao wa Daudi, na ile nyota nyangavu ya asubuhi.” (Ufunuo 22:16, NW) Ndiyo, Yesu ndiye anayetimiza ule unabii ambao Yehova alilazimisha utoke katika midomo isiyo na nia ya Balaamu: “Nyota itatokea katika Yakobo; na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli.” (Hesabu 24:17) Yesu atawapaje “nyota ya asubuhi” wale ambao hushinda? Kwa wazi, ni kwa kujipa mwenyewe kwao, kwa kuwachukua ndani ya uhusiano ulio wa karibu zaidi sana, ulio wa usiri zaidi sana naye. (Yohana 14:2, 3) Hakika ni kichocheo chenye nguvu nyingi cha kuvumilia! Vilevile, ni jambo lenye kuchochea kwa ule umati mkubwa kujua kwamba “ile nyota nyangavu ya asubuhi” karibuni itatumia mamlaka yayo ya Ufalme ili kurudisha Paradiso hapa duniani!

      Dumisha Ukamilifu

      20. Ni matukio gani katika Jumuiya ya Wakristo yanayotukumbusha baadhi ya udhaifu katika kundi la Thiatira?

      20 Ujumbe huu lazima uwe ulitia moyo sana Wakristo katika Thiatira. Ebu wazia—yule Mwana wa Mungu aliyetukuzwa katika mbingu alikuwa amesema ana kwa ana kwa Wakristo katika Thiatira juu ya baadhi ya matatizo yao! Hakika, angalau baadhi yao katika kundi lile waliitikia uchungaji kama huo wa upendo. Ujumbe huu ulio mrefu kupita zote za jumbe saba unatusaidia pia kulitambua kundi la kweli la Kikristo leo. Katika 1918 wakati Yesu alipokuja hekaluni kuhukumu, yaliyo mengi zaidi ya matengenezo yaliyodai kuwa ya Kikristo yalikuwa yamechafuliwa na ibada ya sanamu na ukosefu wa adili kiroho. (Yakobo 4:4) Baadhi yayo yaliweka msingi wa itikadi zao juu ya mafundisho ya wanawake wenye akili ngumu wa karne ya 19, kama vile Ellen White wa Waadventisti wa Siku ya Sabato na Mary Baker Eddy wa Wanasayansi wa Kikristo, na hivi majuzi zaidi wanawake wamekuwa wakihubiri kutoka mimbara. (Tofautisha 1 Timotheo 2:11, 12.) Miongoni mwa namna tofautitofauti za Ukatoliki, mara nyingi, Maria ndiye wa mbele kuheshimiwa kuliko Mungu na Kristo. Yesu hakumheshimu hivyo. (Yohana 2:4; 19:26) Je! matengenezo yanayoruhusu uvutano wa kike usio halali kama huo yangeweza kweli kukubaliwa kuwa ya Kikristo?

      21. Kuna masomo gani kwa watu mmoja mmoja katika ujumbe wa Yesu aliopelekea Thiatira?

      21 Wakristo mmoja mmoja, wawe wale wa jamii ya Yohana au wa kondoo wengine, watafanya vema kufikiria ujumbe huo. (Yohana 10:16) Huenda wengine wakaliona kuwa jambo lenye kushawishi kufuata mwendo rahisi, kama walivyofanya wale wanafunzi wa Yezebeli wa Thiatira. Pia kuna kishawishi cha kuacha msimamo unaofaa. Leo, kunakuwa na lazima ya kukabili masuala kama vile kula vitu vilivyofanyizwa kwa damu au kukubali kutiwa damu mishipani. Huenda wengine wakahisi kwamba bidii katika utumishi wa shambani au kutoa hotuba kunawapa haki ya kutokuwa waangalifu sana katika maeneo mengine, kama vile kutazama sinema na kanda za vidio zenye kuonyesha jeuri na ukosefu wa adili, au kujifurahisha mno kileo. Onyo la Yesu kwa Wakristo katika Thiatira linatuambia sisi ni lazima tusifanye mambo kama hayo yasiyofaa. Yehova anatutaka sisi tuwe safi, wenye nafsi kamili, si waliogawanyika, kama walivyokuwa Wakristo wengi katika Thiatira.

      22. Yesu anakaziaje umaana wa kuwa na sikio lenye kusikia?

      22 Kwa kumalizia, Yesu anatangaza hivi: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi.” (Ufunuo 2:29, NW) Kwa mara ya nne, Yesu anarudia hapa kibwagizo hiki chenye kuamsha, nacho kitamalizia jumbe zote tatu ambazo zingali zinakuja. Je! wewe una sikio lenye kuitikia? Basi endelea kusikiliza kwa makini kadiri Mungu, kwa roho yake aendeleavyo kuandaa shauri kupitia mfereji wake.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona, mathalani, ile makala “Wanawake Wakristo Waaminifu Ni Waabudu wa Mungu Wenye Thamani” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2003.

  • Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 11

      Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?

      SARDISI

      1. Ni nini iliyo hali ya kiroho ya kundi katika Sardisi, naye Yesu anaanzaje ujumbe wake?

      KILOMETA zapata 48 kusini mwa Akhisari (Thiatira) wa ki-siku-hizi, ndipo mahali pa kundi linalofuata kupokea ujumbe kutoka kwa Yesu aliyetukuzwa: Sardisi. Katika karne ya sita kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, jiji hili lilikuwa ndilo jiji kuu lenye kiburi la ufalme wa kale wa Lidia na kao la Mfalme Kroeso mwenye utajiri mwingi sana. Kufikia siku ya Yohana, limeingia katika nyakati ngumu, na ile fahari yalo chini ya Kroeso ni historia tu. Hali moja na hiyo, kundi la Kikristo la huko limekuwa maskini kiroho. Kwa mara ya kwanza, Yesu haanzi ujumbe wake kwa neno la pongezi. Badala ya hiyo, yeye anasema: “Na kwa malaika wa kundi katika Sardisi andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo husema yeye ambaye ana roho saba za Mungu na nyota saba, ‘Mimi najua matendo yako, ya kwamba wewe una jina la kwamba wewe u hai, lakini wewe u mfu.’”—Ufunuo 3:1, NW.

      2. (a) Kuna umaana gani kwa Wakristo katika Sardisi kwamba Yesu ana “roho saba”? (b) Kundi la Sardisi lilikuwa na sifa gani, lakini mambo ya hakika yalikuwa nini?

      2 Ni kwa nini Yesu ajitambulisha kuwa yeye “ambaye ana roho saba”? Kwa sababu roho hizi huwakilisha roho takatifu ya Yehova ikitiririka kwa ujazi wayo. Baadaye, Yohana anazieleza pia kuwa “macho saba,” kuonyesha mwono wenye kupenya ambao roho takatifu inampa Yesu. (Ufunuo 5:6, NW) Hivyo, yeye anaweza kugubua na kushughulikia hali yoyote ambayo huenda ikawako. (Mathayo 10:26; 1 Wakorintho 4:5) Lile kundi katika Sardisi lina sifa ya kuwa hai, lenye kutenda. Lakini Yesu anaweza kuona kwamba limekufa kiroho. Kwa wazi, walio wengi wa washiriki walo wamerudia utepetevu unaofanana na hali waliyokuwa nayo kabla ya kuwa Wakristo.—Linga Waefeso 2:1-3; Waebrania 5:11-14.

      3. (a) Ni kwa nini imempasa “malaika wa kundi katika Sardisi” aangalie kwa njia maalumu uhakika wa kwamba Yesu ana “nyota saba”? (b) Ni shauri gani kali ambalo Yesu analipa kundi katika Sardisi?

      3 Yesu anamkumbusha pia “malaika wa kundi katika Sardisi,” kwamba Yeye ndiye ambaye ana “nyota saba.” Yeye anashika hao wazee wa kundi katika mkono wake wa kulia, akiwa na mamlaka kuwaelekeza katika kazi yao ya kuchunga. Inawapasa wao kuweka mioyo yao katika ‘kujua hakika mwonekano wa kundi.’ (Mithali 27:23, NW) Kwa sababu hiyo, afadhali wasikilize kwa makini maneno ya Yesu yanayofuata: “Uwe mwenye kulinda, na kuimarisha vitu vinavyobaki vilivyokuwa tayari kufa, kwa kuwa mimi sikupata kuona matendo yako yakiwa yamefanywa kwa ukamili mbele za Mungu wangu. Kwa hiyo, endelea kukumbuka jinsi wewe umepokea na jinsi wewe ulisikia, na kuzidi kukishika, na kutubu. Kwa hakika usipoamka, mimi nitakuja kama mwivi, na wewe hutajua hata kidogo ni kwenye saa gani mimi nitakuja juu yako wewe.”—Ufunuo 3:2, 3, NW.

      4. Maneno ya Petro yangesaidiaje kundi katika Sardisi “kuimarisha vitu vinavyobaki”?

      4 Wazee katika Sardisi wanahitaji kukumbuka ile furaha waliyokuwa nayo kwanza wakati walipojifunza ule ukweli na zile baraka walizopokea wakati huo. Lakini sasa wao ni wafu kwa habari ya utendaji wa kiroho. Taa yao ya kikundi ilikuwa ikiwaka na kuzimika kwa kukosa kazi za imani. Miaka mingi huko nyuma, mtume Petro aliandikia makundi katika Esia (yaelekea kutia na Sardisi) wajenge uthamini kwa ajili ya zile habari njema tukufu ambazo Wakristo walikuwa wamekubali na zilizokuwa zimetangazwa “kwa roho takatifu iliyotumwa kutoka mbinguni”—kama inavyowakilishwa na zile roho saba za njozi ya Yohana. Petro alikumbusha pia Wakristo hao wa Esia kwamba wao walikuwa ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya mali ya pekee, ili wapate kutangaza kotekote sifa bora za mmoja ambaye aliwaita kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’ (1 Petro 1:12, 25; 2 Petro 2:9, NW) Kutafakari juu ya kweli hizo za kiroho kutasaidia kundi katika Sardisi litubu na ‘kuimarisha vitu vinavyobaki.’—Linga 2 Petro 3:9, NW.

      5. (a) Ni jambo gani lililoupata uthamini wa Wakristo katika Sardisi? (b) Ni jambo gani litakalotukia ikiwa Wakristo wa Sardisi hawaitikii shauri la Yesu?

      5 Kwa wakati uliopo, uthamini na upendo wao kwa ajili ya ukweli ni kama moto ambao karibu umepoa. Ni makaa machache tu yanayoendelea kuwaka. Yesu anawatia moyo wapulize, wachochee moto huo, watubu dhambi ambazo katika hizo uzembe wao umewaongoza, na kuwa kundi hai kiroho tena. (Linga 2 Timotheo 1:6, 7.) La sivyo, wakati Yesu ajapo bila kutazamiwa—“kama mwivi”—kutekeleza hukumu, kundi katika Sardisi litakuwa haliko tayari.—Mathayo 24:43, 44.

      Kuja “Kama Mwivi”

      6. Yesu alikujaje “kama mwivi” katika 1918, na alikuta hali gani miongoni mwa waliodai kuwa wafuasi wake?

      6 Onyo la Yesu kwamba yeye angekuja “kama mwivi” linafika mpaka ndani ya nyakati za ki-siku-hizi. Lilikuwa na tumizi la pekee kwa Wakristo walioishi mpaka kuingia katika siku ya Bwana. Upesi baada ya 1914, kulikuwako utimizo wa unabii wa Malaki: “‘Kwa ghafula Bwana wa kweli atakuja kwenye hekalu Lake, ambaye nyinyi watu mnatafuta, na mjumbe wa agano ambaye katika yeye nyinyi mnapendezwa. Tazama! Yeye atakuja kwa hakika,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Malaki 3:1, NW; Ufunuo 1:10) Akiwa “mjumbe wa agano,” Yesu alikuja kukagua na kuhukumu wale waliodai kuwa wafuasi wake. (1 Petro 4:17) Wakati huo, katika 1918, Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imejitia katika umwagaji-damu katika Vita ya Ulimwengu 1, na ilikuwa mfu kabisa, kiroho. Hata Wakristo wa kweli, ambao kabla ya vita walikuwa wamehubiri kwa bidii, walipitia wakati wa lepe la usingizi wa kiroho. Baadhi ya wazee wao mashuhuri walitiwa gerezani, na utendaji wa kuhubiri ukakaribia kukoma. Wakati roho ya Yehova ilipoamsha Wakristo hawa mwaka uliofuata, si wote waliokuwa tayari. Baadhi yao, kama wale wanawali wapumbavu wa mfano wa Yesu, hawakutayarishwa kwa vifaa kiroho kwa ajili ya pendeleo la kumtumikia Yehova. Hata hivyo, kwa furaha, walikuwako wengi ambao, kama wale wanawali waangalifu, walikuwa wametii onyo la Yesu: “Fulizeni kulinda, basi, kwa sababu nyinyi hamjui wala siku yenyewe wala saa yenyewe.”—Mathayo 25:1-13, NW.

      7. Ni kwa nini Wakristo leo wanahitaji kukaa hali wameamka?

      7 Uhitaji wa Mkristo kuendelea kuwa chonjo haukumalizika mapema katika siku ya Bwana. Katika unabii wake mkubwa kuhusu “ile ishara wakati mambo yote haya yamekusudiwa kuja kwenye umalizio,” Yesu alitoa onyo lenye mkazo: “Kuhusu siku hiyo au saa hakuna mtu anayejua . . . Fulizeni kutazama, fulizeni kuamka, kwa maana nyinyi hamjui wakati uliowekwa ni lini. Lakini kitu ninachoambia nyinyi ninaambia wote, fulizeni kulinda.” (Marko 13:4, 32, 33, 37, NW) Ndiyo, mpaka saa ii hii, kila mmoja wetu, awe ni wa wapakwa-mafuta au wa ule umati mkubwa, anahitaji kukaa chonjo na kupiga vita dhidi ya kupeperushwa kuingia ndani ya usingizi wa kiroho. Siku ya Yehova ijapo ‘kama mwivi usiku,’ sisi na tupatikane tukiwa tumeamka kabisa ili tupokee hukumu yenye upendeleo.—1 Wathesalonike 5:2, 3; Luka 21:34-36, NW; Ufunuo 7:9.

      8. Jamii ya Yohana imechocheaje watu wa Mungu leo wafulize kuwa hai kiroho?

      8 Ile jamii ya Yohana leo yenyewe imeamka kuona uhitaji wa kuchochea watu wa Mungu waendelee kuwa hai kiroho. Kwa kusudi hilo, makusanyiko ya pekee hupangwa kotekote duniani mara kadhaa kila mwaka. Katika mwaka mmoja wa majuzi, hadhirina kwenye mikusanyiko ya wilaya 2,981 ilijumlika kuwa 10,953,744, na waumini wapya 122,701 wakabatizwa. Kwa zaidi ya miaka mia moja, ile jamii ya Yohana imetumia gazeti Mnara wa Mlinzi katika kutangaza jina na kusudi la Yehova. Katika kuitikia minyanyaso mikali wakati wa vile vita viwili vya ulimwengu, Mnara wa Mlinzi uliwaamsha Mashahidi wa Yehova kwenye bidii mpya kwa kutangaza makala kama vile “Wabarikiwa ni Wasioogopa” (1919), “Mwito Kwenye Tendo” (1925), na “Kushindwa kwa Mnyanyaso” (1942).

      9. (a) Imewapasa Wakristo wote wawe wakijiuliza wenyewe nini? (b) Ni kitia-moyo gani kimetolewa na Mnara wa Mlinzi?

      9 Kama vile katika Sardisi, ndivyo ilivyo katika makundi leo, uchunguzi mwendelevu wa kibinafsi ni wa muhimu kwa Wakristo wote. Sisi sote inatupasa tuendelee kujiuliza wenyewe: Je! ‘matendo yetu yamefanywa kikamili’ mbele za Mungu wetu? Bila ya kuhukumu wengine, je! sisi kibinafsi tunasitawisha ile roho ya kujidhabihu na kujitahidi kutoa utumishi wa nafsi yote kwa Mungu? Kuhusiana na hili gazeti Mnara wa Mlinzi limetoa kitia-moyo kwa kuzungumzia habari kama vile “Endeleeni Kuthibitisha Ninyi Wenyewe Jinsi Mlivyo” na “Kuishi Si kwa Ajili Yetu Wenyewe Tena.”a Tukiwa na misaada kama hiyo ya Kimaandiko, acheni sisi tuchungue utu wetu wa ndani-ndani zaidi tunapojaribu kutembea kwa unyenyekevu na kwa sala katika ukamilifu mbele za Yehova.—Zaburi 26:1-3; 139:23, 24.

      “Majina Machache”

      10. Ni jambo gani lenye kutia-moyo aliloona Yesu katika kundi katika Sardisi, na hilo limepasa lituathirije sisi?

      10 Maneno ya Yesu yanayofuata kwa kundi la Sardisi yanatia moyo zaidi sana. Yeye anasema: “Hata hivyo, wewe una majina machache katika Sardisi ambayo hayakuchafua mavazi yao ya nje, nao watatembea pamoja na mimi katika meupe, kwa sababu wao wanastahiki. Yeye ambaye hushinda atapambwa hivyo mavazi ya nje meupe; na mimi kwa njia yoyote sitafuta jina lake kutoka kitabu cha uhai, bali mimi nitakiri jina lake mbele za Baba yangu na mbele ya malaika zake.” (Ufunuo 3:4, 5, NW) Je! maneno haya hayatuamshi na kuimarisha azimio letu la kuwa waaminifu? Kwa sababu ya uzembe upande wa baraza la wazee, kundi kwa ujumla huenda likaingia ndani ya usingizi wa kiroho. Hata hivyo, baadhi ya watu mmoja mmoja humo huenda wakajitahidi kishujaa kutunza utambulisho wao wa Kikristo ukiwa safi na bila kutiwa madoa na hivyo waendelee kuwa na jina zuri pamoja na Yehova.—Mithali 22:1.

      11, 12. (a) Hata katika pindi ya ule uasi-imani mkubwa, ni lazima wengine wawe walikuwaje kama yale “majina machache” yenye uaminifu katika Sardisi? (b) Ni kitulizo gani kilichowajia Wakristo wa mfano wa ngano wakati wa siku ya Bwana?

      11 Ndiyo, hayo “mavazi ya nje” yanarejeza kwenye utambulisho wa uadilifu wa mtu akiwa Mkristo. (Linga Ufunuo 16:15; 19:8.) Ni lazima Yesu achangamke moyo kuona kwamba, kujapokuwa utepetevu wa idadi iliyo kubwa, “majina machache,” Wakristo wapakwa-mafuta wachache katika Sardisi, bado wanafaulu kuendeleza utambulisho huu. Vivyo hivyo, wakati waliodai kuwa Wakristo walipovama katika Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia, wakati wa zile karne ndefu za ule uasi-imani mkubwa, ni lazima kuwe sikuzote kulikuwako watu wachache mmoja mmoja waliojaribu kufanya mapenzi ya Mungu, ijapokuwa vipingamizi vikubwa. Hawa walikuwa waadilifu kama ngano iliyofichwa kati ya mvuvumuko wa magugu ya kifarakano.—Ufunuo 17:3-6; Mathayo 13:24-29.

      12 Yesu aliahidi kwamba yeye angekuwa pamoja na Wakristo hao mfano wa ngano “sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” Yeye anajua wao ni akina nani na ni jina gani zuri walilojifanyia wenyewe. (Mathayo 28:20, NW; Mhubiri 7:1) Ebu wazia shangilio la hao waaminifu ‘wachache’ ambao walikuwa wangali hai mwanzoni mwa siku ya Bwana! Mwishowe walitenganishwa na Jumuiya ya Wakristo iliyokufa kiroho nao walikusanywa wakaingizwa ndani ya kundi lenye uadilifu linalofanana zaidi na lile kundi katika Smirna.—Mathayo 13:40-43.

      13. Ni baraka gani zilizo akibani kwa Wakristo wapakwa-mafuta ambao ‘hawachafui mavazi yao ya nje’?

      13 Wale katika Sardisi ambao ni waaminifu mpaka mwisho na hawachafui utambulisho wao wa Kikristo wanafikia utimizo wa tumaini zuri ajabu. Baada ya kusimamishwa kwa Ufalme wa Kimesiya katika 1914, wanafufuliwa kwenye uhai wa kiroho na wakiwa washindi hupambwa mavazi meupe ya nje yakiwa ufananisho wa uadilifu wao usio na kasoro, wala waa. Wakiwa wamekwisha tembea katika ile njia yenye kusonga iongozayo kwenye uhai, watafurahia thawabu ya milele.—Mathayo 7:14; Ona pia Ufunuo 6:9-11.

      Milele Katika Kitabu cha Uhai!

      14. Kitabu cha uhai ni nini, na ni majina ya akina nani yaliyorekodiwa humo?

      14 “Kitabu cha uhai,” ni nini na ni majina ya akina nani yatakayotunzwa humo? Kitabu, au hati-kunjo, cha uhai hurejezea rekodi ya watumishi wa Yehova wanaokuja katika mstari wa kupokea tuzo la uhai wa milele. (Malaki 3:16) Humu katika Ufunuo rejezo mahususi limefanywa kwenye majina ya Wakristo wapakwa-mafuta. Lakini majina ya wale walio katika mstari wa uhai wa milele duniani yamerekodiwa pia humo. Zaidi ya hilo, majina yanaweza ‘kufutwa’ katika kitabu hicho. (Kutoka 32:32, 33) Hata hivyo, wale wa jamii ya Yohana ambao majina yao yanabaki katika kile kitabu cha uhai mpaka kifo chao wanapokea uhai usioweza kufa katika mbingu. (Ufunuo 2:10) Haya ndiyo majina ambayo Yesu anakiri hasa mbele za Baba yake na mbele ya malaika Zake. Lo! ni kubwa mno jinsi gani thawabu hiyo!

      15. Washiriki wa ule umati mkubwa wataandikishaje majina yao bila kufutika katika kitabu cha uhai?

      15 Ule umati mkubwa, ambao majina yao yameandikwa pia katika kitabu cha uhai, watatoka katika dhiki kubwa wakiwa hai. Kwa kuzoea imani muda wote wa Utawala wa Mileani wa Yesu na wakati wa mtihani wenye kukata maneno unaofuata, hawa watathawabishwa na uhai wa milele katika Paradiso duniani. (Danieli 12:1; Ufunuo 7:9, 14; 20:15; 21:4) Ndipo majina yao yatakapobaki yameandikwa bila kufutika katika kitabu cha uhai. Kwa kujua kinachotolewa hapa kwa njia ya roho takatifu, je! wewe huitikii kwa idili waadhi hii ya Yesu yenye kurudiwarudiwa: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi”?—Ufunuo 3:6, NW.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona Mnara wa Mlinzi Julai 15, 2005, na Machi 15, 2005.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 12

      “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”

      FILADELFIA

      1. Ujumbe wa Yesu wa sita ulielekezwa kwenye kundi katika jiji gani, na jina la jiji hilo humaanisha nini?

      SHAUKU YA KIDUGU—ni sifa ya kutamanika kama nini! Pasipo shaka Yesu ana hiyo akilini wakati anapotoa ujumbe wake wa sita, ambao unaelekezwa kwenye kundi katika Filadelfia, kwa kuwa jina hilo humaanisha “Shauku ya Kidugu.” Yohana aliye mwenye umri wa uzee angali anakumbuka ile pindi, zaidi ya miaka 60 mapema, wakati Petro alipomsisitizia Yesu mara tatu kwamba yeye, Petro, alikuwa ana shauku changamfu kwa Bwana yake. (Yohana 21:15-17) Je! Wakristo katika Filadelfia, kwa upande wao, wanaonyesha shauku ya kidugu? Yaonekana wanafanya hivyo!

      2. Filadelfia lilikuwa jiji la namna gani, ni kundi la aina gani lilikuwa kule, na Yesu anasema nini kwa malaika wa kundi hili?

      2 Likiwa mahali zapata kilometa 48 kusini-mashariki mwa Sardisi (lilipo jiji la ki-siku-hizi la Alasehiri la Kituruki), Filadelfia la siku ya Yohana ni jiji lenye ufanisi wa kadiri. Hata hivyo, unaostahili kuangaliwa zaidi, ni ule ufanisi wa kundi la Kikristo lililo huko. Ni lazima wawe walimpokea kwa shangwe iliyoje yule mhudumu aliyekuja akisafiri kwao, inaelekea kupitia Sardisi! Ujumbe anaopeleka una shauri lenye kuchochea kwa ajili yao. Lakini kwanza unarejezea mamlaka ya Mtumaji wao mtukufu. Yeye husema hivi: “Na kwa malaika wa kundi katika Filadelfia andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo husema yeye ambaye ni mtakatifu, aliye wa kweli, ambaye ana ufunguo wa Daudi, ambaye hufungua hivi kwamba hakuna mmoja ambaye atafunga, na hufunga hivi kwamba hakuna mmoja ambaye hufungua.”—Ufunuo 3:7, NW.

      3. Ni kwa nini inafaa Yesu aitwe “mtakatifu,” na inaweza kusemwaje kwamba yeye ni “wa kweli”?

      3 Yohana alikuwa amesikia Petro akisema kwa binadamu Yesu Kristo hivi: “Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiye Mtakatifu wa Mungu.” (Yohana 6:68, 69) Kwa kuwa Yehova Mungu ndiye asili yenyewe ya utakatifu, Mwanaye mzaliwa-pekee lazima pia awe “mtakatifu.” (Ufunuo 4:8) Pia Yesu ni “wa kweli.” Neno la Kigiriki linalotumiwa hapa (a·le·thi·nosʹ) linadokeza uhalisi. Katika maana hii, Yesu ndiye nuru ya kweli na ule mkate wa kweli ulioshuka kutoka mbinguni. (Yohana 1:9; 6:32) Yeye ndiye mzabibu wa kweli. (Yohana 15:1) Yesu ni wa kweli pia katika maana ya kwamba yeye ni mwenye kuitibarika. Sikuzote yeye husema ukweli. (Ona Yohana 8:14, 17, 26.) Mwana huyu wa Mungu anastahili kweli kweli kutumikia akiwa Mfalme na Jaji.—Ufunuo 19:11, 16.

      “Ufunguo wa Daudi”

      4, 5. “Ufunguo wa Daudi” ulishirikishwa na agano gani?

      4 Yesu ana “ufunguo wa Daudi.” Akiutumia, yeye “hufungua hivi kwamba hakuna mmoja ambaye atafunga, na hufunga hivi kwamba hakuna mmoja ambaye hufungua.” Ni nini huu “ufunguo wa Daudi”?

      5 Yehova alifanya agano la Ufalme wa milele na Mfalme Daudi wa Israeli. (Zaburi 89:1-4, 34-37) Nyumba ya Daudi ilitawala kutoka kiti cha ufalme cha Yehova katika Yerusalemu tangu 1070 mpaka 607 K.W.K., lakini ndipo hukumu ya Mungu ikafikilizwa juu ya ufalme huo kwa sababu uligeuka ukawa mbovu. Hivyo Yehova akaanza kutimiza unabii wake kwenye Ezekieli 21:27, NW: “Magofu, magofu, magofu mimi nitalifanya liwe [Yerusalemu la kidunia]. Na kwa habari ya hii pia, hiyo [fimbo ya umaliki katika nasaba ya Daudi] hakika haitakuwa ya mwingine mpaka ajapo ambaye ana haki halali, nami lazima nimpe hiyo.”

      6, 7. Ni wakati gani na jinsi gani yule aliye na “haki halali” angetokea?

      6 Ni wakati gani na jinsi gani huyu mmoja mwenye “haki halali” angetokea? Ni jinsi gani yeye angepewa fimbo ya ufalme wa Daudi?

      7 Yapata miaka 600 baadaye, mzao wa Mfalme Daudi, yule msichana Myahudi Mariamu, akapata mimba kwa roho takatifu. Mungu alimtuma malaika Gabrieli kumwambia Mariamu kwamba yeye angepata mwana, ambaye angeitwa Yesu. Gabrieli aliongeza hivi: “Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana [Yehova, NW] Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Atamiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.”—Luka 1:31-33.

      8. Yesu alijithibitishaje kuwa anastahili kurithi ufalme wa Kidaudi?

      8 Wakati Yesu alipobatizwa katika mto Yordani na kupakwa mafuta kwa roho takatifu katika 29 W.K., akawa Mfalme-Mchaguliwa katika nasaba ya Daudi. Yeye alionyesha bidii iliyo kielelezo chema katika kuhubiri habari njema za Ufalme na akawapa utume wanafunzi wake wahubiri vivyo hivyo. (Mathayo 4:23; 10:7, 11) Yesu alijinyenyekeza, hata mpaka kifo kwenye nguzo ya mateso, akijithibitisha hivyo kustahili kabisa kurithi ule umaliki wa Kidaudi. Yehova alimfufua Yesu akiwa roho asiyeweza kufa akamkweza kwenye mkono wa kulia Wake katika mbingu. Huko alirithi haki zote za ufalme wa Kidaudi. Wakati uwadiapo Yesu angetumia haki yake ‘aende akitiisha katikati ya adui zake.’—Zaburi 110:1, 2, NW; Wafilipi 2:8, 9; Waebrania 10:13, 14.

      9. Ni jinsi gani Yesu anatumia ufunguo wa Daudi kufungua na kufunga?

      9 Kwa wakati uliopo Yesu angetumia ule ufunguo wa Daudi, akifungua nafasi na mapendeleo yanayohusiana na Ufalme wa Mungu. Kupitia Yesu, Yehova angekomboa Wakristo wapakwa-mafuta duniani “kutoka mamlaka ya lile giza,” na kuwahamisha awaingize “ndani ya ufalme wa Mwana wa upendo wake.” (Wakolosai 1:13, 14, NW) Ufunguo ule ungetumiwa pia kuzuia wasipate mapendeleo hayo wowote ambao wangethibitika kuwa wasioaminika. (2 Timotheo 2:12, 13) Kwa kuwa mrithi huyu wa kudumu wa ufalme wa Daudi ana utegemezo wa Yehova, hakuna kiumbe anayeweza kumzuia asitimize wajibu huo ulio mwingi.—Linga Mathayo 28:18-20.

      10. Ni kitia-moyo gani anachotoa Yesu kwa kundi katika Filadelfia?

      10 Yakija kutoka chanzo kama hicho chenye mamlaka, maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Filadelfia lazima yawe yenye kufariji hasa! Yeye anawasifu, akisema: “Mimi najua matendo yako—tazama! mimi nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, ambao hakuna mmoja awezaye kufunga—kwamba wewe una nguvu chache, na wewe ulishika neno langu na hukuthibitika kuwa bandia kwa jina langu.” (Ufunuo 3:8, NW) Kundi limekuwa lenye kutenda, nao mlango umefunguliwa mbele yalo—bila shaka mlango wa nafasi ya utumishi wa kihuduma. (Linga 1 Wakorintho 16:9; 2 Wakorintho 2:12.) Kwa hiyo, Yesu analitia moyo kundi litumie kwa faida kamili ile nafasi ya kuhubiri. Wao wamevumilia na kuonyesha kwamba wana nguvu za kutosha, kwa msaada wa roho ya Mungu, kuendelea kufanya “matendo” zaidi katika utumishi wa Yehova. (2 Wakorintho 12:10; Zekaria 4:6) Wametii amri za Yesu nao hawakumkana Kristo ama kwa neno ama kwa tendo.

      “Watainama Mbele Yako Wewe”

      11. Ni baraka gani ambayo Yesu anaahidi Wakristo, nayo ilitimizwaje?

      11 Kwa sababu hiyo, Yesu anawaahidi tunda: “Tazama! Mimi nitatoa wale kutoka lile sinagogi la Shetani ambao wanasema ni Wayahudi, na hata hivyo wao sio bali wanasema uwongo—tazama! mimi nitafanya wao waje na kusujudu mbele ya nyayo zako na kufanya wao wajue mimi nimekupenda wewe.” (Ufunuo 3:9, NW) Labda, kama vile katika Smirna, lile kundi limekuwa na matatizo na Wayahudi wenyeji. Yesu anawataja hawa kuwa “sinagogi la Shetani.” Hata hivyo, angalau baadhi ya Wayahudi hao wanakaribia kung’amua kwamba yale ambayo Wakristo hawa wamekuwa wakihubiri juu ya Yesu ni ukweli. ‘Kusujudu’ kwao inaelekea kutakuwa kwa jinsi ile ambayo Paulo alieleza kwenye 1 Wakorintho 14:24, 25, hivi kwamba kwa kweli wao wanatubu na kuwa Wakristo, wakithamini kikamili upendo mkubwa wa Yesu katika kutoa hata nafsi yake kwa ajili ya wanafunzi wake.—Yohana 15:12, 13.

      12. Ni kwa nini washiriki wa sinagogi la Kiyahudi katika Filadelfia inaelekea wangeshtuka kujifunza kwamba baadhi yao ‘wangeinamia’ jamii ya Kikristo ya mahali hapo?

      12 Washiriki wa Sinagogi la Kiyahudi katika Filadelfia inaelekea wangeshtuka kujifunza kwamba baadhi yao ‘wangesujudia’ jamii ya Kikristo ya mahali hapo. Kwa sababu ya uhakika wa kwamba bila shaka kuna wasio Wayahudi wengi katika kundi hilo, wao wangetazamia jambo lililo kinyume kabisa litukie. Kwa nini? Kwa sababu Isaya alitabiri hivi: “Wafalme [wasio Wayahudi] lazima wawe watunzi kwa ajili yako wewe [watu wa Israeli], na mabinti-wafalme wao wanawake wa kulea kwa ajili yako wewe. Nyuso zikiwa kwenye dunia watainama mbele yako wewe.” (Isaya 49:23, NW; 45:14; 60:14) Katika maana iyo hiyo, Zekaria alivuviwa kuandika hivi: “Itakuwa siku hizo kwamba wanaume [wasio Wayahudi] kumi kutoka lugha zote za mataifa watashika, ndiyo, hakika watashika rinda la mwanamume aliye Myahudi, wakisema: ‘Sisi tutaenda na nyinyi watu, kwa maana sisi tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na nyinyi watu.’” (Zekaria 8:23, NW) Ndiyo, watu wasio Wayahudi wangeinamia Wayahudi, si kinyume cha hivyo!

      13. Ni nani waliokuwa Wayahudi ambao wangeona utimizo wa unabii uliosemwa kwa Israeli wa kale?

      13 Unabii huo ulielekezwa kwa taifa chaguliwa la Mungu. Ulipotamkwa, Israeli wa mnofu walikuwa na cheo hicho chenye kuheshimiwa. Lakini wakati taifa la Kiyahudi lilipomkataa Mesiya, Yehova aliwatupilia mbali. (Mathayo 15:3-9; 21:42, 43; Luka 12:32; Yohana 1:10, 11) Kwenye Pentekoste 33 W.K., alichagua mahali pao yule Israeli wa Mungu wa kweli, kundi la Kikristo. Washiriki walo ndio Wayahudi wa kiroho walio na tohara halisi ya moyo. (Matendo 2:1-4, 41, 42; Warumi 2:28, 29; Wagalatia 6:16) Kwa hiyo, ile njia pekee ambayo katika hiyo Wayahudi wa mnofu mmoja mmoja wangeweza kurudia uhusiano wenye kibali pamoja na Yehova ungekuwa kwa kuweka imani yao katika Yesu akiwa Mesiya. (Mathayo 23:37-39) Kwa wazi, hilo lilikuwa karibu kutukia kwa baadhi ya watu mmoja mmoja katika Filadelfia.a

      14. Ni jinsi gani Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 yamekuwa na utimizo wa maana katika nyakati za ki-siku-hizi?

      14 Katika nyakati za ki-siku-hizi, unabii kama vile Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 umekuwa na utimizo wenye umaana sana. Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b Walio wengi wa hawa wametoka katika Jumuiya ya Wakristo, ambayo dini zayo hudai kwa ubandia kuwa Waisraeli wa kiroho. (Linga Warumi 9:6.) Hawa, wakiwa umati mkubwa, wanafua mavazi yao na kuyafanya meupe kwa kutumia imani katika damu ya dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:9, 10, 14) Kwa kutii utawala wa Kristo wa Ufalme, wanatumaini kurithi baraka zao hapa duniani. Wanakuja kwa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta na ‘kuwainamia,’ kiroho, kwa sababu ‘wamesikia kwamba Mungu yu pamoja nao.’ Wanahudumia hawa wapakwa-mafuta, ambao pamoja nao wanakuwa wenye umoja katika ushirika wa ndugu ulimwenguni pote.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 5:9.

      “Ile Saa ya Mtihani”

      15. (a) Yesu aliwaahidi nini Wakristo katika Filadelfia, nao walitiwa moyo kufanya nini? (b) Wakristo walitazamia kupokea “taji” gani?

      15 Yesu anaendelea kusema: “Kwa sababu wewe ulishika lile neno juu ya uvumilivu wangu, mimi pia nitakinga wewe na ile saa ya mtihani, inayopasa kuja juu ya dunia yote kwa ujumla inayokaliwa, ili kuweka mtihani juu ya wale wanaokaa juu ya dunia. Mimi ninakuja upesi. Fuliza kushikilia kwa imara kile ulicho nacho, ili kusiwe mmoja wa kuchukua taji lako.” (Ufunuo 3:10, 11, NW) Ijapokuwa Wakristo wa siku ya Yohana hawangeendelea kuishi mpaka siku ya Bwana (kuanzia 1914), uhakika wa kwamba Yesu alikuwa akija ungewapa uwezo waendelee kuhubiri. (Ufunuo 1:10; 2 Timotheo 4:2) Lile “taji,” au zawadi ya uhai wa milele, linawangojea mbinguni. (Yakobo 1:12; Ufunuo 11:18) Ikiwa wangekuwa waaminifu mpaka kifo, hakuna mmoja ambaye angeweza kuwapokonya thawabu hiyo.—Ufunuo 2:10.

      16, 17. (a) Ni ipi “ile saa ya mtihani, inayopasa kuja juu ya dunia yote kwa ujumla inayokaliwa”? (b) Hali ya wapakwa-mafuta ilikuwa nini mwanzoni mwa “ile saa ya mtihani”?

      16 Hata hivyo, ni ipi “ile saa ya mtihani”? Pasipo shaka, Wakristo hao katika Esia walipaswa wakabiliane na wimbi jingine la mnyanyaso mbaya sana kutoka Roma yenye milki.c Hata hivyo, ule utimizo ulio mkubwa ni ile saa ya kupepeta na kuhukumu ambayo mwishowe iliwasili katika kipindi cha siku ya Bwana, ikifikia upeo tangu 1918 na kuendelea. Ule mtihani umekuwa wa kuamulia kama mmoja anaunga mkono Ufalme wa Mungu uliosimamishwa au ulimwengu wa Shetani. Ni wa kipindi kifupi kwa kulinganisha, “saa” moja, lakini haujakwisha. Mpaka uishe, ni lazima sisi tusisahau kamwe kwamba tunaishi katika “ile saa ya mtihani.”—Luka 21:34-36.

      17 Katika 1918 jamii ya Yohana ya Wakristo wapakwa-mafuta—kama kundi hilo mathubuti katika Filadelfia—ilikuwa sharti ikabili upinzani kutoka “sinagogi la Shetani” la ki-siku-hizi. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao hudai kuwa Wayahudi wa kiroho, waliongoza kwa hila watawala wakandamize Wakristo wa kweli. Hata hivyo, hao walijaribu sana ‘kushika neno la uvumilivu wa Yesu’; kwa sababu hiyo, kwa msaada wa kiroho, “nguvu chache” zenye maana, waliokoka na wakaamshwa waingie kupitia mlango ambao sasa ulifunguliwa mbele yao. Katika njia gani?

      “Mlango Uliofunguliwa”

      18. Ni kuweka rasmi gani alikofanya Yesu katika 1919, na hivyo mwekwa alikuwaje kama mtumishi wa nyumba mwaminifu wa Hezekia?

      18 Katika 1919 Yesu alitimiza ahadi yake na kukitambua kile kikosi kidogo cha Wakristo wapakwa-mafuta cha kweli kuwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wake. (Mathayo 24:45-47) Hao waliingia ndani ya pendeleo linalofanana na lile alilofurahia Eliakimu mtumishi wa nyumba mwaminifu katika wakati wa Hezekia.d Yehova alisema hivi kwa habari ya Eliakimu: “Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.” Eliakimu alibeba begani madaraka mazito kwa ajili ya Hezekia, yule mwana wa kifalme wa Daudi. Hali moja na hiyo leo, jamii ya Yohana ya wapakwa-mafuta imewekelewa begani mwayo “ufunguo wa nyumba ya Daudi” katika maana ya kwamba wameaminishwa masilahi ya kidunia ya Ufalme wa Kimesiya. Yehova ameimarisha watumishi wake kwa ajili ya pendeleo hili, akiongezea nguvu chache zao kuwa nishati yenye msukumo inayotosha kwa ushuhuda mkubwa wa tufe lote.—Isaya 22:20, 22; 40:29.

      19. Jamii ya Yohana ilishughulikiaje madaraka ambayo ilipewa na Yesu katika 1919, kukiwa na tokeo gani?

      19 Tangu 1919 na kuendelea mabaki ya wapakwa-mafuta, wakifuata kielelezo cha Yesu, walianzisha kampeni yenye bidii ya kutangaza kotekote habari njema za Ufalme. (Mathayo 4:17; Warumi 10:18) Kama tokeo, wengine wa lile sinagogi la Shetani la ki-siku-hizi, Jumuiya ya Wakristo, walijia baki hili la wapakwa-mafuta, wakatubu na ‘wakainama,’ wakikiri mamlaka ya mtumwa huyo. Wao vilevile walikuja kutumikia Yehova katika muungano na wale wazee-wazee wa jamii ya Yohana. Hilo liliendelea mpaka hesabu kamili ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu wakakusanywa. Kufuatia hili, “umati mkubwa . . . kutoka mataifa yote” umekuja ‘ukainamia’ mtumwa mpakwa-mafuta. (Ufunuo 7:3, 4, 9, NW) Pamoja, mtumwa huyu na huu umati mkubwa wanatumikia wakiwa kundi moja la Mashahidi wa Yehova.

      20. Ni kwa nini hasa leo lazima Mashahidi wa Yehova wawe thabiti katika imani na watendaji katika utumishi wa Mungu?

      20 Wakiwa na umoja kama wale Wakristo katika Filadelfia katika kifungo cha shauku halisi ya kidugu, Mashahidi wa Yehova leo wanathamini kwamba kazi yao ya kuhubiri lazima ifanywe kwa hima. Upesi, ile dhiki kubwa itavua pazia la ulimwengu mbovu wa Shetani. Wakati huo, kila mmoja wetu na apatikane akiwa mwenye nguvu katika imani na akitenda katika utumishi wa Mungu, ili majina yetu yasifutwe kutoka kitabu cha uhai cha Yehova. (Ufunuo 7:14) Acheni tulichukue kwa uzito sana onyo ambalo Yesu alilipa kundi katika Filadelfia ili tuweze kushikilia kwa imara mapendeleo yetu ya utumishi na kufikilia thawabu ya uhai wa milele.

      Baraka za Washindi

      21. Wakristo wapakwa-mafuta leo ‘wameshikaje neno juu ya uvumilivu wa Yesu,’ na ni tazamio gani linalowangojea?

      21 Ile jamii ya Yohana leo ‘imeshika neno juu ya uvumilivu wa Yesu,’ yaani, wamefuata kielelezo chake wakavumilia. (Waebrania 12:2, 3; 1 Petro 2:21) Hivyo wametiwa moyo sana sana na maneno mengine haya ya Yesu kwa kundi katika Filadelfia: “Yeye ambaye hushinda—mimi nitafanya yeye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na yeye hatatoka nje yalo tena kwa vyovyote.”—Ufunuo 3:12a, NW.

      22. (a) Ni nini lile hekalu la Mungu wa Yesu? (b) Wakristo wapakwa-mafuta wanaoshinda watakuwaje nguzo katika hekalu hili?

      22 Lo! ni pendeleo kama nini kwa mmoja kuwa nguzo katika hekalu la Yehova! Katika Yerusalemu la kale, lile hekalu halisi lilikuwa kitovu cha ibada ya Yehova. Ndani ya hekalu hilo, kuhani mkuu alitoa damu ya wanyama wa dhabihu, mara moja kila mwaka, mbele ya ile nuru ya muujiza iliyowakilisha kuwapo kwa Yehova katika “Patakatifu Zaidi Sana.” (Waebrania 9:1-7, NW) Wakati wa ubatizo wa Yesu, likaja kuwako hekalu jingine, mpango mkubwa wa kiroho ulio kama hekalu kwa ajili ya kumwabudu Yehova. Pale patakatifu pa patakatifu pote pa hekalu hili pako mbinguni, ambapo kwa wakati wake Yesu alionekana “mbele ya utu wa Yehova.” (Waebrania 9:24, NW) Yesu ndiye Kuhani Mkuu, na kuna dhabihu moja tu iliyotolewa kwa kufunika kabisa dhambi: ile damu iliyomwagwa ya Yesu binadamu mkamilifu. (Waebrania 7:26, 27; 9:25-28; 10:1-5, 12-14) Maadamu wanadumu kuwa waaminifu, Wakristo wapakwa-mafuta duniani wanatumikia wakiwa makuhani wadogo katika nyua za kidunia za hekalu hili. (1 Petro 2:9) Lakini mara washindapo, wao pia wanaingia hapo patakatifu pa patakatifu pote katika mbingu nao wanakuwa mihimili isiyoondoleka, kama nguzo, za ule mpango ulio kama hekalu kwa ajili ya ibada. (Waebrania 10:19; Ufunuo 20:6) Hakuna hatari kwamba wao ‘watatoka nje yalo tena.’

      23. (a) Kisha Yesu anatoa ahadi gani kwa Wakristo wapakwa-mafuta wanaoshinda? (b) Ni nini tokeo la kuandikwa kwa jina la Yehova na jina la Yerusalemu jipya juu ya Wakristo washindi?

      23 Yesu anaendelea, akisema: “Na mimi nitaandika juu yake yeye jina la Mungu wangu na jina la jiji la Mungu wangu, Yerusalemu jipya ambalo hushuka toka mbinguni kutoka kwa Mungu wangu, na hilo jina jipya langu.” (Ufunuo 3:12b, NW) Ndiyo, washindi hawa wanakuwa na jina la Yehova likiwa limeandikwa juu yao—Mungu wao na Mungu wa Yesu. Hilo laonyesha waziwazi kwamba Yehova na Yesu ni watu wawili walio mbalimbali na si sehemu mbili za Mungu wa Utatu. (Yohana 14:28; 20:17) Uumbaji wote lazima uje kuona kwamba Wakristo hawa wapakwa-mafuta ni wa Yehova. Wao ni Mashahidi wake. Pia wanaandikwa na jina la Yerusalemu Jipya juu yao, lile jiji la kimbingu lishukalo toka mbinguni katika maana ya kwamba linatandaza utawala walo wenye hisani juu ya wanadamu wote waaminifu. (Ufunuo 21:9-14) Hivyo, kondoo wote wa Kristo wa kidunia watajua pia kwamba washindi hao wapakwa-mafuta ni wenyeji wa ule Ufalme, Yerusalemu la kimbingu.—Zaburi 87:5, 6; Mathayo 25:33, 34; Wafilipi 3:20; Waebrania 12:22.

      24. Ni nini kinachowakilishwa na jina jipya la Yesu, nalo linaandikwaje juu ya Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu?

      24 Mwishowe, washindi wapakwa-mafuta wanaandikwa jina la Yesu jipya juu yao. Hilo larejezea ofisi mpya ya Yesu na yale mapendeleo yasiyo na kifani aliyopewa na Yehova. (Wafilipi 2:9-11; Ufunuo 19:12) Hakuna mwingine apataye kujua jina hilo, katika maana ya kwamba hakuna mwingine aliye na majioneo hayo au anayeaminishwa mapendeleo hayo. Hata hivyo, wakati Yesu aandikapo jina lake juu ya hao ndugu zake waaminifu, wanakuja ndani ya uhusiano wa karibu sana pamoja naye katika milki hiyo ya kimbingu na hata wanashiriki mapendeleo yake. (Luka 22:29, 30) Si ajabu kwamba Yesu anamalizia ujumbe wake kwa wapakwa-mafuta kwa kurudia waadhi hii: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi.”—Ufunuo 3:13, NW.

      25. Kila Mkristo mmoja mmoja leo anaweza kutumiaje kanuni iliyo katika shauri ambalo Yesu alitoa kwa kundi katika Filadelfia?

      25 Lo! ujumbe huo lazima uwe ulikuwa kitia-moyo kama nini kwa Wakristo waaminifu katika Filadelfia! Na hakika kuna somo lenye nguvu nyingi kwa ajili ya jamii ya Yohana sasa, wakati wa siku ya Bwana. Lakini kanuni zao ni za maana kwa kila Mkristo mmoja mmoja, awe ni wa wapakwa-mafuta au wa kondoo wengine. (Yohana 10:16) Kila mmoja wetu angefanya vema kufuliza kuzaa tunda la Ufalme kama walivyofanya hawa Wakristo katika Filadelfia. Sote tuna angalau nguvu chache. Sisi sote tunaweza kufanya jambo fulani katika utumishi wa Yehova. Acheni tuitumie nguvu hii! Kwa habari ya mapendeleo ya Ufalme yaliyoongezeka, acheni sisi tuwe chonjo kuingia mlango wowote unaofunguliwa kwetu. Sisi hata tunaweza kusali kwa Yehova afungue mlango kama huo. (Wakolosai 4:2, 3) Tunapofuata kigezo cha Yesu cha uvumilivu na kujithibitisha kuwa wa kweli kwa jina lake, tutaonyesha kwamba sisi, vilevile, tuna sikio la kusikia kile ambacho roho ya Mungu husema kwa makundi.

      [Maelezo ya Chini]

      a Katika wakati wa Paulo, Sosthene, ofisa msimamizi wa sinagogi la Kiyahudi katika Korintho, akawa ndugu Mkristo.—Matendo 18:17; 1 Wakorintho 1:1.

      b Gazeti Mnara wa Mlinzi linalotangazwa na jamii ya Yohana, limeendelea kukazia umuhimu wa kutwaa nafasi hii na kushiriki kikamilifu kadiri iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri; mathalani, ona makala “Wote na Wautangaze Utukufu wa Yehova” na “Sauti Yao Ilifika Katika Dunia Yote” katika toleo la Januari 1, 2004. Katika toleo la Juni 1, 2004, katika makala “Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa,” mkazo uliwekwa juu ya kuingia “mlango uliofunguliwa” ndani ya utumishi wa wakati wote. Kulikuwako kilele cha mapainia 1,093,552 walioripoti utumishi kama huo katika pindi ya mwezi mmoja katika 2005.

      c Cyclopedia ya McClintock na Strong (Buku la 10, uku. 519) huripoti: “Wamaliki walilazimishwa wauone Ukristo na ghasia zilizochochewa miongoni mwa raia na makuhani wapagani ambao walitazama kwa hofu maendeleo yenye kustaajabisha ya imani hiyo, naye Trajani [98-117 W.K.] kwa sababu hiyo aliongozwa atoe amri za kukandamiza polepole hilo fundisho jipya lililogeuza watu kuwa wachukiaji wa tumungu. Usimamizi wa Plini mchanga akiwa gavana wa Bithinia [iliyopakana na mkoa wa Kiroma wa Esia upande wa kaskazini] ulitatizwa na mambo yaliyotokana na mweneo wa haraka sana wa Ukristo na hasira kali ya raia wa kipagani ndani ya jimbo lake.”

      d Jina Hezekia lamaanisha “Yehova Huimarisha.” Ona 2 Wafalme 16:20, kielezi cha chini, New World Translation Reference Bible.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 63]

      Kusaidia Wengi Wainame Chini

      Kati ya wale wapakwa-mafuta 144,000 ambao watarithi Ufalme wa kimbingu, inaonekana kwamba baki, ile jamii ya Yohana, ya walio punde kuliko 9,000 wangali watamaliza mwendo wao duniani. Wakati ule ule, umati mkubwa umepanuka ukawa 6,600,000 na zaidi. (Ufunuo 7:4, 9) Ni kitu gani kimesaidia kutokeza ongezeko hili kubwa mno? Zile shule mbalimbali zinazoongozwa na Mashahidi wa Yehova zimetoa mchango mkubwa. Tofauti sana na seminari za Jumuiya ya Wakristo ambazo hufundisha falsafa za kilimwengu na kushusha heshima ya Biblia, shule hizi za Mashahidi hukaza kikiki imani yenye kina katika Neno la Mungu. Zinaonyesha utumizi walo wenye mafaa kwa habari ya maisha safi ya adili na utumishi ulio wakfu kwa Mungu. Ulimwenguni pote tangu 1943, kila kundi la Mashahidi wa Yehova huongoza Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika Jumba la Ufalme lalo la mahali pao. Mamilioni huhudhuria shule hii kila juma, wakifuata programu yenye umoja ya elimu ya Biblia.

      Tangu 1959 Mashahidi wa Yehova wameongoza pia Shule za Huduma ya Ufalme kwa ajili ya kuzoeza wazee na watumishi wa huduma wa kundi. Na tangu 1977, ile Shule ya Utumishi wa Painia imezoeza mamia ya maelfu ya akina ndugu na dada ambao, wakiwa na roho ya kweli ya Kifiladelfia, wanatumikia Yehova wakati wote katika kazi ya kuhubiri. Katika 1987 ile Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ilianzishwa kwa ajili ya kuzoeza Mashahidi wa kiume kwa ajili ya migawo ya pekee katika shamba la ulimwengu.

      Yenye kutokeza miongoni mwa shule zinazoendeshwa na Mashahidi wa Yehova imekuwa ile Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi. Tangu 1943 shule hii ya misionari, iliyoko Mkoa wa New York imehitimisha vikundi viwili vya wanafunzi karibu kila mwaka. Kwa ujumla, imezoeza wahudumu wa Yehova zaidi ya 7,000 kwa ajili ya utumishi wa misionari wa nchi za kigeni. Wahitimu wa shule hii wametumikia katika mabara zaidi ya 100, katika mengi yayo walisaidia sana katika kufungua kazi ya Ufalme. Baada ya miaka yapata 60, wengi wa wale wamisionari wa mapema wangali kazini, wakishiriki pamoja na wamisionari wapya zaidi katika kusogeza mbele katika tufe lote mpanuko wa tengenezo la Yehova. Lo! huo umekuwa mpanuko mzuri ajabu kama nini!

      [Chati katika ukurasa wa 64]

      Katika 1919 yule Mfalme anayetawala Yesu alifungua mlango wa nafasi kwa utumishi wa Kikristo. Nambari yenye kuongezeka ya Wakristo waliojitoa wametumia kwa faida nafasi hiyo.

      Mabara Wakristo Wahubiri

      Yaliyofikiwa Walioshiriki wa Wakati

      Mwaka kwa Kuhubiri Katika Kuhubirie Wotef

      1918 14 3,868 591

      1928 32 23,988 1,883

      1938 52 47,143 4,112

      1948 96 230,532 8,994

      1958 175 717,088 23,772

      1968 200 1,155,826 63,871

      1978 205 2,086,698 115,389

      1988 212 3,430,926 455,561

      1998 233 5,544,059 698,781

      2005 235 6,390,022 843,234

      [Maelezo ya Chini]

      e Tarakimu zilizo juu ni wastani wa kila mwezi.

      f Tarakimu zilizo juu ni wastani wa kila mwezi.

      [Picha katika ukurasa wa 65]

      Utendaji wa Mashahidi wa Yehova unatolewa kwa moyo mzima wote. Mathalani, fikiria zile saa ambazo wametumia katika kuhubiri na kufundisha na ile hesabu kubwa mno ya mafunzo ya Biblia bila malipo ambayo wameongoza katika nyumba za watu.

      Saa Zilizotumiwa Mafunzo ya Biblia

      Kuhubiri Yaliyoongozwa

      Mwaka (Jumla ya Mwaka) (Wastani wa Mwezi)

      1918 19,116 Hayakurekodiwa

      1928 2,866,164 Hayakurekodiwa

      1938 10,572,086 Hayakurekodiwa

      1948 49,832,205 130,281

      1958 110,390,944 508,320

      1968 208,666,762 977,503

      1978 307,272,262 1,257,084

      1988 785,521,697 3,237,160

      1998 1,186,666,708 4,302,852

      2005 1,278,235,504 6,061,534

  • Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 13

      Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto

      LAODIKIA

      1, 2. Kundi la mwisho la yale saba kupokea ujumbe kutoka kwa Yesu aliyetukuzwa, lipo mahali gani, na ni nini baadhi ya mambo ya jiji hilo?

      LAODIKIA ndilo la mwisho la yale makundi saba kupokea ujumbe kutoka kwa Yesu aliyefufuliwa. Nao ujumbe huo unapeleka habari yenye kufungua macho na yenye kuchochea kama nini!

      2 Leo, ungeweza kuona magofu ya Laodikia karibu na Denizli, kilometa zapata 88 kusini-mashariki mwa Alasehiri. Katika karne ya kwanza, Laodikia lilikuwa jiji lenye ufanisi. Likikaa kwenye njia panda kuu, lilikuwa kitovu kikuu cha kazi ya benki na biashara. Uuzaji wa dawa ya macho yenye kujulikana sana uliongezea utajiri walo, na pia lilijulikana sana kwa sababu ya mavazi yalo ya hali ya juu sana yaliyotengenezewa huko kutokana na sufi nyeusi nzuri. Ukosefu wa maji uliokuwa tatizo kubwa kwa jiji hilo, ulikuwa umeshindwa kwa kuleta maji kupitia mifereji kutoka visima vyenye maji moto vilivyokuwa umbali fulani. Hivyo, maji yangekuwa yenye uvuguvugu tu kufikia wakati ambao yangewasili katika jiji hilo.

      3. Yesu anafunguaje ujumbe wake kwa kundi katika Laodikia?

      3 Laodikia lilikuwa karibu na Kolosai. Katika kuandikia Wakolosai, mtume Paulo anataja barua aliyokuwa amewapelekea Walaodikia. (Wakolosai 4:15, 16) Sisi hatujui mambo ambayo Paulo aliandika katika barua hiyo, lakini ujumbe ambao Yesu anawapelekea Walaodikia sasa unaonyesha kwamba wameanguka katika hali mbaya sana ya kiroho. Ingawa hivyo, kama kawaida, Yesu ataja kwanza vitambulisho vyake mwenyewe, akisema: “Na kwa malaika wa kundi katika Laodikia andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo Ameni asema, yule shahidi mwaminifu na wa kweli, aliye mwanzo wa uumbaji wa Mungu.”—Ufunuo 3:14, NW.

      4. Yesu ni “Ameni” jinsi gani?

      4 Ni kwa nini Yesu anajiita “Ameni”? Jina hili la cheo linaongeza uzito wa kihukumu kwenye ujumbe wake. “Ameni” ni neno la Kiebrania lililotoholewa kumaanisha “kwa uhakika,” “na iwe hivyo,” nalo linatumiwa mwishoni mwa sala kuthibitisha hisia zilizoonyeshwa ndani yazo. (1 Wakorintho 14:16) Yesu ndiye “Ameni” kwa sababu ukamilifu usio na kasoro na kifo cha dhabihu chake vilithibitisha na vikahakikisha utimizo wa ahadi zote za Yehova zenye thamani kubwa. (2 Wakorintho 1:20) Tangu wakati huo, kwa kufaa sala zote hupelekewa Yehova kupitia Yesu.—Yohana 15:16; 16:23, 24.

      5. Ni katika njia gani Yesu ndiye “shahidi mwaminifu na wa kweli”?

      5 Pia Yesu ndiye “shahidi mwaminifu na wa kweli.” Katika unabii, mara nyingi yeye anashirikishwa na uaminifu, ukweli, na uadilifu, kwa kuwa yeye ni mwenye kustahili itibari kabisa kabisa akiwa mtumishi wa Yehova Mungu. (Zaburi 45:4; Isaya 11:4, 5; Ufunuo 1:5; 19:11, NW) Yeye ndiye Shahidi mkubwa zaidi sana kwa ajili ya Yehova. Kwa kweli, akiwa “mwanzo wa uumbaji wa Mungu,” Yesu ametangaza utukufu wa Mungu tangu mwanzo wenyewe. (Mithali 8:22-30) Akiwa binadamu duniani, yeye alishuhudia ukweli. (Yohana 18:36, 37; 1 Timotheo 6:13) Baada ya ufufuo wake, yeye aliahidi wanafunzi wake roho takatifu na akawaambia hivi: “Nyinyi mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Yudea yote na Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” Tangu Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, Yesu alielekeza Wakristo hawa wapakwa-mafuta katika kuhubiri habari njema “katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu.” (Matendo 1:6-8; Wakolosai 1:23, NW) Kweli kweli, Yesu anastahili kuitwa shahidi mwaminifu na wa kweli. Wale Wakristo wapakwa-mafuta katika Laodikia wangenufaika kwa kusikiliza maneno yake.

      6. (a) Yesu anaelezaje hali ya kiroho ya kundi katika Laodikia? (b) Ni kielelezo gani kizuri cha Yesu ambacho kundi la Laodikia limeshindwa kufuata?

      6 Yesu ana ujumbe gani kwa Walaodikia? Yeye hana neno la pongezi. Yeye anawaambia waziwazi hivi: “Mimi najua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala moto. Mimi naona laiti ungekuwa baridi au sivyo moto. Kwa hiyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu na wala si moto wala baridi, mimi nitatapika wewe utoke katika kinywa changu.” (Ufunuo 3:15, 16, NW) Wewe ungeitikiaje ujumbe kama huo kutoka kwa Bwana Yesu Kristo? Je! wewe hungeamka ujichunguze mwenyewe? Kwa hakika, Walaodikia hao wanahitaji kujiamsha wenyewe, kwa kuwa wamekuwa wavivu kiroho, kwa wazi wakichukua mambo mengi mno vivi hivi tu. (Linga 2 Wakorintho 6:1.) Yesu, ambaye wao wakiwa Wakristo iliwapasa kuiga, sikuzote anaonyesha bidii yenye kuwaka moto kwa ajili ya Yehova na utumishi wake. (Yohana 2:17) Zaidi ya hilo, wasikivu wamempata sikuzote akiwa mwanana na mpole, mwenye kuburudisha kama kikombe cha maji baridi katika siku yenye joto la kutosha jasho jingi. (Mathayo 11:28, 29) Lakini Wakristo katika Laodikia si moto wala baridi. Kama yale maji yanayotiririka kuingia jiji lao, wao wamevuvuwaa, wamekuwa vuguvugu. Wao wanaelekea kukataliwa kabisa na Yesu, ‘kutapikwa watoke katika kinywa chake’! Sisi kwa upande wetu na tujitahidi kwa bidii sikuzote, kuwaandalia wengine burudisho la kiroho, kama alivyofanya Yesu.—Mathayo 9:35-38.

      “Wewe Wasema: ‘Mimi Ni Tajiri’”

      7. (a) Yesu anatambulishaje mzizi wa tatizo la Wakristo katika Laodikia? (b) Ni kwa nini Yesu anasema kwamba Wakristo Walaodikia ni “vipofu na uchi”?

      7 Ni nini hasa kilicho mzizi wa tatizo la Walaodikia hao? Sisi tunapata wazo zuri kutoka kwa maneno yanayofuata ya Yesu: “Kwa sababu wewe wasema: ‘Mimi ni tajiri nami nimepata utajiri na sihitaji kitu chochote kabisa,’ lakini wewe hujui u mwenye taabu na mwenye kusikitikiwa na maskini na kipofu na uchi.” (Ufunuo 3:17, NW; linga Luka 12:16-21.) Wakiishi katika jiji lenye utajiri, wanahisi kuwa na uhakika kwa sababu ya utajiri wao. Yaelekea, njia yao ya maisha imeathiriwa na ule uwanja wa michezo, majumba ya maonyesho, na nyanja za mazoezi ya mwili, hivi kwamba wamekuwa “wapenda raha kuliko kuwa wapenda Mungu.”a (2 Timotheo 3:4, NW) Lakini Walaodikia hao waliokuwa matajiri katika vitu vya kimwili ni maskini kiroho. ‘Hazina walizojiwekea mbinguni’ ni chache ikiwa wana zozote. (Mathayo 6:19-21) Wao hawakutunza jicho lao likiwa sahili, wakiupa Ufalme wa Mungu mahali pa kwanza katika maisha zao. Wao kwa kweli wamo gizani, ni vipofu, bila mwono wa kiroho. (Mathayo 6:22, 23, 33) Waaidha, yajapokuwa mavazi mazuri ambayo huenda utajiri wao wa kimwili ulinunua, machoni pa Yesu wao wako uchi. Hawana mavazi ya kiroho ya kuwatambulisha kuwa Wakristo.—Linga Ufunuo 16:15.

      8. (a) Ni katika njia gani hali inayofanana na ile iliyokuwako Laodikia iko pia leo? (b) Wakristo wengine wamejidanganyaje wenyewe katika ulimwengu huu wenye pupa?

      8 Ni hali yenye kugutusha kama nini! Lakini je! sisi hatuoni mara nyingi hali inayofanana na hiyo leo? Ni nini kilicho mzizi wenye kusababisha? Ni mwelekeo wa kujitumainia unaotokana na kutegemea miliki za kimwili na nyenzo za kibinadamu. Kama wale waenda-kanisani wa Jumuiya ya Wakristo, baadhi ya watu wa Yehova wamejidanganya wenyewe, wakifikiri wanaweza kumpendeza Mungu kwa kuhudhuria mikutano tu pindi kwa pindi. Wao wanajaribu kutosheka na dalili tu ya kuwa “watendaji wa neno.” (Yakobo 1:22) Yajapokuwa maonyo yenye kurudiwarudiwa kutoka jamii ya Yohana, wao wanaweka moyo wao juu ya mavazi ya mitindo-mitindo, magari, na nyumba, na juu ya maisha yenye kutegemea tafrija na anasa. (1 Timotheo 6:9, 10; 1 Yohana 2:15-17) Yote hayo yanatokeza ufahamu wa kiroho uliopumbazwa. (Waebrania 5:11, 12) Badala ya kuwa wenye uvuguvugu usiochangamsha, wanahitaji kuuwasha tena “moto wa roho” waonyeshe hamu nyingi yenye kuburudisha katika ‘kuhubiri lile neno.’—1 Wathesalonike 5:19; 2 Timotheo 4:2, 5, NW.

      9. (a) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kugutusha Wakristo wenye uvuguvugu, na kwa nini? (b) “Kondoo” wanaopotoka wanaweza kusaidiwaje na kundi?

      9 Yesu anawaonaje Wakristo wenye uvuguvugu? Maneno yake ya unyofu yapasa yawagutushe: “Wewe hujui u mwenye taabu na mwenye kusikitikiwa na maskini na kipofu na uchi.” Dhamiri zao zimekufa ganzi kufikia hatua ya kwamba wao hata hawang’amui hali yao yenye kufadhaisha sana. (Linga Mithali 16:2; 21:2.) Hali hii nzito katika kundi haiwezi kusukumiwa kando vyepesi. Kwa kuweka kielelezo chema cha bidii na kwa uchungaji wa upendo, wazee na wengine waliopewa migawo nao wanaweza kuwaamsha kwenye shangwe yao ya hapo kwanza ya utumishi wa moyo wote mzima “kondoo” hawa wanaopotoka.—Luka 15:3-7.

      Shauri Juu ya “Kuwa Tajiri”

      10. Ni “dhahabu” ipi ambayo Yesu anaambia Wakristo wa Laodikia wanunue kutoka kwake?

      10 Je! kuna ponyo la hali hii yenye huzuni katika Laodikia? Ndiyo, ikiwa Wakristo hao watafuata shauri la Yesu: “Mimi nashauri wewe kununua kutoka kwangu mimi dhahabu iliyosafishwa sana kwa moto ili wewe upate kuwa tajiri.” (Ufunuo 3:18a, NW) “Dhahabu” ya kweli ya Kikristo, iliyosafishwa sana kwa moto na uchafu wote ukiwa umeondolewa, itawafanya kuwa “tajiri kuelekea Mungu.” (Luka 12:21, NW) Wanaweza kununua wapi dhahabu kama hiyo? Si kutoka kwa wanabenki wenyeji bali kutoka kwa Yesu! Mtume Paulo alieleza dhahabu hiyo ni nini alipomwambia Timotheo atoe maagizo kwa Wakristo matajiri “watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo; huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao.” Kwa kujitumikisha wenyewe hivyo ndipo tu wangeweza ‘kupata uzima ulio kweli kweli.’ (1 Timotheo 6:17-19) Walaodikia hao matajiri wangalipaswa kufuata shauri la Paulo na hivyo wawe matajiri kiroho.—Ona pia Mithali 3:13-18.

      11. Sisi tuna vielelezo gani vya wale wanaonunua “dhahabu iliyosafishwa sana kwa moto”?

      11 Je! kuna vielelezo vya ki-siku-hizi vya wale wanaonunua “dhahabu iliyosafishwa sana kwa moto”? Ndiyo, vipo! Hata ile siku ya Bwana ilipokuwa ikikaribia, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia kilikuwa kikiamka kuona ubandia wa mengi ya mafundisho ya Kibabuloni ya Jumuiya ya Wakristo, kama vile Utatu, kutokufa kwa nafsi, moto wa mateso, ubatizo wa vitoto vichanga, na ibada ya sanamu (kutia na msalaba na zile za Maria). Katika kupigania ukweli wa Biblia, Wakristo hawa walitangaza Ufalme wa Yehova kuwa tumaini pekee kwa aina ya binadamu na dhabihu ya ukombozi ya Yesu kuwa ndiyo msingi kwa ajili ya wokovu. Karibu miaka 40 kabla ya wakati, walielekeza kwenye 1914 kuwa ule mwaka uliotiwa alama katika unabii wa Biblia kuwa ndio mwisho wa majira ya Mataifa, pamoja na matukio ya ajabu duniani.—Ufunuo 1:10.

      12. Ni nani aliyekuwa mmoja wa wale waliokuwa wakichukua uongozi miongoni mwa Wakristo waliokuwa wakiamka, naye aliwekaje kielelezo chenye kutokeza katika kujiwekea hazina katika mbingu?

      12 Charles Taze Russell ndiye aliyekuwa akichukua uongozi miongoni mwa Wakristo hawa waliokuwa wakiamka, na ambaye, mapema katika miaka ya 1870, alianzisha darasa la kujifunza Biblia katika Allegheny (sasa ni sehemu ya Pittsburgh), Pennsylvania, U.S.A. Alipoanza utafutaji wake wa ukweli, Russell alikuwa katika biashara-shirika pamoja na baba yake na alikuwa akielekea kuwa milionea. Lakini yeye aliuza faida za biashara yake ya duka moja baada ya jingine na kutumia utajiri wake katika kusaidia kifedha kazi ya kuhubiri Ufalme wa Mungu katika dunia yote. Katika 1884 Russell akawa msimamizi wa kwanza wa lile shirika linalojulikana sasa kuwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Katika 1916 yeye alikufa akiwa ndani ya garimoshi karibu na Pampa, Teksasi, njiani kwenda New York, akiwa amemalizwa nguvu kabisa na safari yake ya mwisho ya kuhubiri magharibi mwa United States. Yeye aliweka kielelezo chenye kutokeza cha kujiwekea hazina za kiroho katika mbingu, kielelezo ambacho leo kinafuatwa na mamia ya maelfu ya wahudumu mapainia wenye kujidhabihu.—Waebrania 13:7; Luka 12:33, 34; linga 1 Wakorintho 9:16; 11:1.

      Kutumia Dawa ya Macho ya Kiroho

      13. (a) Dawa ya kiroho ya macho itaendelezaje hali ya Walaodikia? (b) Yesu anapendekeza mavazi ya aina gani, na kwa nini?

      13 Pia Yesu anawapa kwa uthabiti Walaodikia hao onyo la upole: “Nunua . . . mavazi ya nje meupe ili wewe upate kuwa mwenye kuvishwa na kwamba aibu ya uchi wako isipate kuwa dhahiri, na dawa ya macho ili kusugua katika macho yako kwamba wewe upate kuona.” (Ufunuo 3:18b, NW) Imewapasa watafute ponyo kwa ajili ya upofu wao wa kiroho kwa kununua dawa ya macho yenye kuponya, si ile ya waponyaji wenyeji, bali ile ya aina ambayo ni Yesu tu awezaye kuandaa. Hiyo ingewasaidia kupata utambuzi wa kiroho, ikiwasaidia watembee katika “kile kijia cha waadilifu” na macho yao yenye kung’aa yakiwa yanalenga juu ya kufanya mapenzi ya Mungu. (Mithali 4:18, 25-27, NW) Hivyo, huenda wakavaa, si yale mavazi ya sufi nyeusi yenye bei yaliyotengenezewa huko Laodikia, bali “mavazi ya nje meupe,” mazuri, yanayotangaza utambulisho wao wenye pendeleo wakiwa wafuasi wa Yesu Kristo.—Linga 1 Timotheo 2:9, 10; 1 Petro 3:3-5.

      14. (a) Ni dawa gani ya kiroho ya macho ambayo imekuwa ikipatikana tangu 1879? (b) Ni kipi kimekuwa chanzo kikuu kabisa cha kutegemeza Mashahidi wa Yehova kifedha? (c) Katika utumiaji wa michango, Mashahidi wa Yehova wanatofautianaje na wengine?

      14 Je! dawa ya kiroho ya macho inapatikana katika nyakati za ki-siku-hizi? Hakika inapatikana! Katika 1879 Pasta Russell, kama alivyoitwa kwa shauku ya upendo, alianza kutangaza kwa kuutetea ukweli gazeti linalojulikana ulimwenguni pote leo kuwa Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Katika toleo lalo la pili, yeye alitangaza hivi: “Tunaitikadi kwamba [Gazeti hili] lina YEHOVA akiwa mtegemezaji walo, na maadamu ndivyo ilivyo halitaomba-omba kamwe wala kuomba rasmi wanadamu kwa ajili ya kusaidiwa. Wakati Yeye anayesema: ‘Dhahabu yote na fedha yote ya milimani ni zangu,’ anashindwa kutoa pesa zinazohitajiwa, sisi tutaelewa kuwa ni wakati wa kusimamisha uchapaji.” Baadhi ya waeneza-evanjeli wa televisheni wamerundika utajiri mwingi sana na wakaishi katika anasa isiyo na aibu (na nyakati nyingine yenye ukosefu wa adili). (Ufunuo 18:3) Katika kutofautisha, Wanafunzi wa Biblia, wanaojulikana leo kuwa Mashahidi wa Yehova, wametumia michango yote isiyo ya kuombwa-ombwa wanayopokea ili kupanga kitengenezo na kusogeza mbele kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote Ufalme wa Yehova unaokuja. Ile jamii ya Yohana kufikia leo hii inaelekeza kutangazwa kwa Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, magazeti ambayo yalikuwa na mwenezo wa pamoja wa nakala zaidi ya milioni 59 katika 2006. Mnara wa Mlinzi linapatikana katika lugha 150 hivi. Ndilo jarida rasmi la kundi la Wakristo zaidi ya milioni sita ambao wametumia dawa ya macho kama hiyo ya kiroho katika kufungua macho yao yaone dini bandia na ule uharaka wa kuhubiri zile habari njema katika mataifa yote.—Marko 13:10.

      Kunufaishwa na Karipio na Nidhamu

      15. Ni kwa nini Yesu anatoa shauri kali kwa Wakristo katika Laodikia, na imelipasa kundi liliitikieje?

      15 Acheni turudi kwa Walaodikia. Wao wataitikiaje lile shauri kali kutoka kwa Yesu? Je! wavunjike moyo na kuhisi kwamba Yesu hawataki tena wakiwa wanafunzi wake? La, sivyo ilivyo kabisa. Ule ujumbe unaendelea kusema: “Wale wote ambao mimi naonea shauku mimi nakaripia na kunidhamu. Kwa hiyo uwe mwenye bidii na kutubu.” (Ufunuo 3:19, NW) Kama vile nidhamu kutoka kwa Yehova, nidhamu ya Yesu ni ishara ya upendo. (Waebrania 12:4-7) Kundi la Laodikia lapaswa lijifaidi na hangaikio lake lenye shauku na kutumia shauri lake. Inawapasa watubu wakitambua kwamba uvuguvugu wao ni kutenda dhambi. (Waebrania 3:12, 13; Yakobo 4:17) Acha wazee walo waweke nyuma njia za kufuatilia vitu vya kimwili na ‘kuchochea kama moto’ ile karama waliyo nayo kutoka kwa Mungu. Ile dawa ya macho ikiwa inafanya kazi, acha wote waliomo katika kundi hilo wapate burudisho kama lile linalotokana na kinywaji cha maji baridi kutoka chemchemi ya maji.—2 Timotheo 1:6; Mithali 3:5-8; Luka 21:34.

      16. (a) Upendo na shauku ya Yesu huonyeshwaje leo? (b) Sisi tukipokea shauri kali, inatupasa tuliitikieje?

      16 Namna gani sisi leo? Yesu huendelea ‘kupenda wale walio wake mwenyewe ambao wako katika ulimwengu.’ Yeye atafanya hivyo “sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Yohana 13:1; Mathayo 28:20, NW) Upendo na shauku yake huonyeshwa kupitia ile jamii ya Yohana ya ki-siku-hizi na zile nyota, au wazee, katika kundi la Kikristo. (Ufunuo 1:20) Katika siku hizi zenye kujaribu, wazee wanapendezwa sana katika kutusaidia sisi sote, wenye umri na vijana, tuendelee kukaa ndani ya mipaka ya zizi la kitheokrasi, tukipinga kule kijitegemea, ile pupa ya vitu vya kimwili, na ule uchafu wa ukosefu wa adili wa ulimwengu. Ikiwa nyakati nyingine sisi tunapokea shauri au nidhamu kali, kumbuka kwamba “yale makaripio ya nidhamu ni njia ya uhai.” (Mithali 6:23, NW) Sisi sote ni wasiokamilika na inatupasa tuwe wenye bidii katika kutubu inapohitajiwa kabisa ili tuweze kurekebishwa na kubaki katika upendo wa Mungu.—2 Wakorintho 13:11.

      17. Utajiri unaweza kuwaje hatari kwetu kiroho?

      17 Lazima sisi tusiruhusu ufuatiaji wa vitu vya kimwili, mali, au ukosefu wa mali utufanye sisi tuwe wenye uvuguvugu. Utajiri unaweza kusaidia kufungulia uwezekano mpya ulio mwingi wa utumishi, lakini pia unaweza kuwa hatari. (Mathayo 19:24) Mtu mwenye mali huenda akahisi kwamba yeye hahitaji kuwa mwenye bidii katika kazi ya kuhubiri kama wengine, mradi yeye anatoa michango mikubwa wakati kwa wakati. Au huenda akahisi kwamba kuwa tajiri kunampa haki ya kupata mapendeleo. Kwa kuongezea, kuna raha na maburudisho ambayo yako wazi kwa mtu tajiri ambayo wengine hawawezi kuyapata. Lakini tafrija hizo huchukua wakati na zaweza kuvuta mtu asiyejihadhari mbali na huduma ya Kikristo, hivyo kumfanya huyo asiye mwangalifu kuwa mwenye uvuguvugu. Sisi na tujiepushe na mitego hiyo yote na tuendelee “kufanya kazi sana na kujipinda wenyewe” kwa moyo wote, tukiutazamia uhai wa milele.—1 Timotheo 4:8-10; 6:9-12, NW.

      “Kutwaa Mlo wa Jioni”

      18. Ni fursa gani ambayo Yesu anaweka mbele ya Wakristo katika Laodikia?

      18 Yesu anaendelea kusema: “Tazama! Mimi ninasimama penye mlango na kubisha. Ikiwa ye-yote asikia sauti yangu na kufungua mlango, mimi nitaingia ndani ya nyumba yake na kutwaa mlo wa jioni pamoja na yeye na yeye pamoja na mimi.” (Ufunuo 3:20, NW) Ikiwa Wakristo hao Walaodikia wanamkaribisha Yesu ndani ya kundi lao, yeye atawasaidia washinde uvuguvugu wao!—Mathayo 18:20.

      19. Yesu anadokeza nini anapoahidi kutwaa mlo wa jioni pamoja na kundi katika Laodikia?

      19 Bila shaka mtajo wa Yesu wa mlo wa jioni unawakumbusha Walaodikia hao zile nyakati ambapo yeye alikula milo pamoja na wanafunzi wake. (Yohana 12:1-8) Sikuzote pindi hizo ziliwaletea wale waliokuwapo baraka za kiroho. Vilevile, zilikuwako pindi zisizosahaulika zilizowatia nguvu sana baada ya ufufuo wa Yesu wakati alipokuwapo kwenye mlo pamoja na wanafunzi wake. (Luka 24:28-32; Yohana 21:9-19) Kwa sababu hiyo, ahadi yake ya kuja ndani ya kundi la Laodikia na kutwaa mlo wa jioni pamoja nao ni ahadi ya kuwaletea manufaa zenye utajiri mwingi wa kiroho ikiwa tu watamkaribisha.

      20. (a) Mwanzoni mwa ile siku ya Bwana, ni jambo gani lililotokezwa na uvuguvugu wa Jumuiya ya Wakristo? (b) Hukumu ya Yesu imeathirije Jumuiya ya Wakristo?

      20 Waidha lenye upendo la Yesu kwa Walaodikia lina maana kubwa kwa mabaki ya Wakristo wapakwa-mafuta leo. Wengine wao wanakumbuka kwamba, ile siku ya Bwana ilipokuwa ikianza, wanadini wa Jumuiya ya Wakristo walikuwa wenye uvuguvugu kwa kiwango chenye kusikitisha sana. Badala ya kukaribisha kurudi kwa Bwana yetu katika 1914, viongozi wa kidini wayo walijiingiza sana katika ule mchinjo wa Vita ya Ulimwengu 1, ambayo katika hiyo mataifa 24 kati ya yale 28 yaliyokuwa yakipigana yalidai kuwa ya Kikristo. Lo! hatia ya damu yayo ni kubwa kama nini! Wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, ambayo pia ilipiganwa hasa ndani ya Jumuiya ya Wakristo, kwa mara nyingine tena dhambi za dini bandia ‘zilikuwa nyingi mno, zikarundamana mpaka mbinguni.’ (Ufunuo 18:5, HNWW) Zaidi ya hilo, viongozi wa kidini wameupa kisogo Ufalme wa Yehova unaokuja kwa kuunga mkono Ushirika wa Mataifa, Umoja wa Mataifa, na harakati zenye kutaka mapinduzi, zenye kutukuza taifa, ambazo hakuna mojapo inayoweza kutatua matatizo ya aina ya binadamu. Kwa muda mrefu Yesu amekwisha kataa viongozi wa kidini, akiwahukumu vibaya na kuwatupilia mbali, kama vile mvua-samaki atupavyo samaki wasiofaa wanaokamatwa katika wavu-mvuto wake. Ile hali yenye kusikitisha ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo leo inashuhudia hukumu hiyo yayo. Angamio layo la mwisho linalokuja na litumike kuwa onyo kwetu sisi!—Mathayo 13:47-50.

      21. Kutoka 1919 na kuendelea, Wakristo katika kundi la kweli wameitikiaje maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Laodikia?

      21 Hata ndani ya lile kundi la kweli, mmekuwamo watu mmoja mmoja ambao wako kama kinywaji ambacho si chenye moto wenye kuchochea wala chenye baridi yenye kuburudisha. Lakini Yesu angali anapenda kichangamfu kundi lake. Yeye anajifanya mwenyewe apatikane kwa Wakristo wanaoitikia kwa ukaribishaji-wageni, na wengi wamemkaribisha, kana kwamba kwa mlo wa jioni. Kama tokeo, tangu 1919 na kuendelea macho yao yamefunguliwa yaone maana ya unabii wa Biblia. Wao wamefurahia kipindi cha nuru ya elimu kubwa.—Zaburi 97:11; 2 Petro 1:19.

      22. Huenda akilini Yesu alikuwa na mlo wa jioni upi wa wakati ujao, na ni nani watakaoushiriki?

      22 Alipokuwa akihutubia Walaodikia, huenda Yesu akawa pia alikuwa akilini na mlo wa jioni mwingine. Baadaye katika Ufunuo tunasoma hivi: “Wenye furaha ni wale walioalikwa kwenye mlo wa jioni wa ndoa ya Mwana-Kondoo.” Hii ni ile karamu tukufu ya ushindi kwa sifa ya Yehova baada ya yeye kuwa ametekeleza hukumu juu ya dini bandia—karamu anayoishiriki Yesu pamoja na bibi-arusi wake aliyekamilika wa 144,000 katika mbingu. (Ufunuo 19:1-9, NW) Washiriki waitikivu wa hilo kundi la kale la Laodikia—ndiyo, na ndugu za Yesu Kristo waaminifu wa leo, ambao wanavaa mavazi safi ya utambulisho kuwa wao ni Wakristo wapakwa-mafuta halisi—wote watakula karamu pamoja na Bwana-arusi wao kwenye huo mlo wa jioni. (Mathayo 22:2-13) Lo! ni kichocheo chenye nguvu kama nini cha kuwa na bidii na kutubu!

      Kiti cha Ufalme kwa Washindi

      23, 24. (a) Yesu anasema juu ya thawabu gani zaidi? (b) Yesu aliketi lini juu ya kiti cha ufalme chake, na alianza lini kuhukumu wale waliodai kuwa Wakristo? (c) Ni ahadi gani nzuri ajabu aliyofanya Yesu kwa wanafunzi wake wakati alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake?

      23 Yesu anazungumza juu ya thawabu zaidi, akisema: “Yeye ambaye hushinda mimi nitaruhusu kuketi chini pamoja na mimi juu ya kiti cha ufalme changu, hata kama vile mimi nilivyoshinda na nikaketi chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti cha ufalme chake.” (Ufunuo 3:21, NW) Katika utimizo wa maneno ya Daudi kwenye Zaburi 110:1, 2, Yesu mshika-ukamilifu, akiisha kuushinda ulimwengu, alifufuliwa katika 33 W.K. na kukwezwa akaketi chini pamoja na Baba yake juu ya kiti cha ufalme Chake cha kimbingu. (Matendo 2:32, 33) Katika mwaka mwingine wenye maana kubwa, 1914, Yesu aliwasili aketi chini juu ya kiti cha ufalme chake mwenyewe cha Kimesiya akiwa Mfalme na Jaji. Inaonekana kwamba hukumu ilianza katika 1918 na wale waliodai kuwa Wakristo. Washindi wapakwa-mafuta waliokufa kabla ya wakati huo ndipo wangefufuliwa na kujiunga na Yesu katika Ufalme wake. (1 Petro 4:17) Yeye alikuwa amewaahidi jambo hilo alipokuwa akianzisha Ukumbusho wa kifo chake, akiwaambia wanafunzi wake hivi: “Mimi nafanya agano pamoja na nyinyi, kama vile Baba yangu amefanya agano pamoja na mimi, kwa ajili ya ufalme, kwamba nyinyi mpate kula na kunywa katika meza yangu katika ufalme wangu, na kuketi juu ya viti vya ufalme kuhukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”—Luka 22:28-30, NW.

      24 Ni mgawo mzuri ajabu kama nini—kuketi pamoja na Mfalme anayetawala wakati wa “uumbaji upya” na kushiriki pamoja naye, kwa msingi wa dhabihu yake kamilifu, katika kuinua kwenye ukamilifu wa Kiedeni ulimwengu wa aina ya binadamu yenye utii! (Mathayo 19:28; 20:28, NW) Kama Yohana anavyotutaarifu, Yesu huwafanya wale wanaoshinda kuwa “ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake,” wakalie viti vya ufalme kuzunguka kiti cha ufalme chenye utukufu cha Yehova mwenyewe cha kimbingu. (Ufunuo 1:6; 4:4, NW) Acheni sisi sote—tuwe wapakwa-mafuta au wa jamii ya ile dunia mpya ambayo inatumaini kushiriki katika kurudisha Paradiso—tuzingatie maneno ya Yesu kwa Walaodikia!—2 Petro 3:13; Matendo 3:19-21, NW.

      25. (a) Kama ilivyo kwa zile jumbe zilizotangulia, Yesu anamaliziaje ujumbe wake kwa Walaodikia? (b) Imewapasa Wakristo mmoja mmoja leo waitikieje maneno ya Yesu kwa kundi katika Laodikia?

      25 Kama ilivyo kwa zile jumbe zinazotangulia, Yesu anamalizia ujumbe huu kwa maneno ya kusihi: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi.” (Ufunuo 3:22, NW) Sisi tunaishi ndani sana ya wakati wa mwisho. Ithibati inatuzunguka kotekote kwamba Jumuiya ya Wakristo ni baridi kwa habari ya kuwa na upendo. Kwa kutofautisha, sisi tukiwa Wakristo wa kweli na tuitikie kwa bidii ya moyo ujumbe wa Yesu kwa kundi la Laodikia, ndiyo, jumbe zote saba za Bwana yetu kwa yale makundi. Sisi tunaweza kufanya hivyo kwa kushiriki kisulubu katika utimizo wa unabii mkubwa wa Yesu kwa ajili ya siku yetu: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.”—Mathayo 24:12-14, NW.

      26. Ni wakati gani Yesu anaposema tena kwa Yohana moja kwa moja, lakini yeye hushiriki katika nini?

      26 Shauri la Yesu kwa yale makundi saba limekwisha. Yeye hasemi na Yohana tena katika Ufunuo mpaka ile sura ya kumalizia; lakini yeye hushiriki katika nyingi za zile njozi, mathalani, katika kutekeleza hukumu za Yehova. Acheni sasa sisi tujiunge na jamii ya Yohana katika kuchunguza ile njozi ya pili yenye kustaajabisha inayofunuliwa na Bwana Yesu Kristo.

      [Maelezo ya Chini]

      a Mahali hapa pamefukuliwa na machimbuzi ya kiarkiolojia mahali ulipokuwa Laodikia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki