Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutia Muhuri Israeli wa Mungu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 19

      Kutia Muhuri Israeli wa Mungu

      Njozi ya 4—Ufunuo 7:1-17

      Habari: Wale 144,000 watiwa muhuri, na umati mkubwa unaonwa umesimama mbele ya kiti cha ufalme cha Yehova na mbele ya Mwana-Kondoo

      Wakati wa utimizo: Tangu kuketishwa katika kiti cha ufalme kwa Kristo Yesu katika 1914 na kuendelea kuingia Utawala wa Mileani wake

      1. “Ni nani anaweza kusimama” wakati wa siku kubwa ya hasira-kisasi ya kimungu?

      “NI NANI anaweza kusimama?” (Ufunuo 6:17, NW) Ndiyo, ni nani kweli kweli? Wakati siku kubwa ya hasira-kisasi ya kimungu inapokumba mfumo wa Shetani, watawala na watu wa ulimwengu huenda kwa kufaa wakauliza swali hilo. Itaonekana kwao kwamba kumbo hilo kubwa linalokuja litazima uhai wote wa kibinadamu. Lakini je! litafanya hivyo? Kwa furaha, nabii wa Mungu anatuhakikishia: “Kila mmoja ambaye anaita juu ya jina la Yehova ataponyoka akiwa salama.” (Yoeli 2:32, NW) Mitume Petro na Paulo wathibitisha uhakika huo. (Matendo 2:19-21; Warumi 10:13) Ndiyo, wale wanaoita juu ya jina la Yehova watakuwa waokokaji. Hao ni akina nani? Kadiri njozi inayofuata ikunjulikavyo, sisi tutaona.

      2. Ni kwa nini ni jambo la kushangaza kwamba kutakuwa na waokokaji wa siku ya hukumu ya Yehova?

      2 Kwa kweli ni jambo lenye kushangaza kwamba yapasa yeyote apitie siku ya Yehova ya hukumu akiwa hai, kwa kuwa mwingine wa manabii wa Mungu anaieleza kwa maneno haya: “Tazama! Upepo-dhoruba wa Yehova, hasira kali yenyewe, imetoka ikaenda nje, tufani yenye kwenda mbele ikifagia. Juu ya kichwa cha waovu itazunguka vuruvuru. Kasirani yenye kuwaka ya Yehova haitarudi nyuma mpaka yeye awe ameua na mpaka yeye awe ametekeleza mawazo ya moyo wake.” (Yeremia 30:23, 24, NW) Ni jambo la uharaka kwamba sisi tuchukue hatua za kusalimika katika dhoruba hiyo!—Mithali 2:22; Isaya 55:6, 7; Sefania 2:2, 3.

      Zile Pepo Nne

      3. (a) Ni utumishi gani wa pekee unaofanywa na malaika anaouona Yohana? (b) Ni nini kinachofananishwa na “pepo nne”?

      3 Kabla ya Yehova kuachilia kiruu hiki, malaika wa kimbingu wanafanya utumishi wa pekee. Sasa Yohana anaona hilo katika njozi: “Baada ya hili mimi niliona malaika wanne wakisimama juu ya kona nne za dunia, wakishika sana pepo nne za dunia, kwamba upepo wowote usipate kupuliza juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote.” (Ufunuo 7:1, NW) Hili linamaanisha nini kwa sisi leo? Hizi “pepo nne” ni ufananisho halisi wa hukumu yenye kuharibu inayokaribia kuachiliwa juu ya jamii mbovu ya kidunia, juu ya “bahari” yenye kusukasuka ya binadamu waasi-sheria, na juu ya watawala walioinuka mfano wa miti ambao wanapata uungaji-mkono na utegemezo kutoka kwa watu wa dunia.—Isaya 57:20; Zaburi 37:35, 36.

      4. (a) Malaika wanne wanawakilisha nini? (b) Tokeo linakuwa nini juu ya tengenezo la kidunia la Shetani wakati pepo nne zinapoachiliwa?

      4 Hapana shaka, hawa malaika wanne wanawakilisha vikundi vinne vya kimalaika, ambavyo Yehova anatumia kuzuia utekelezo wa hukumu yake mpaka wakati uliowekwa. Malaika hao waachiliapo pepo nne za hasira-kisasi zizunguke vuruvuru wakati ule ule mmoja kutoka kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi, kumbo hilo litakuwa kubwa mno. Litafanana, lakini kwa kadiri kubwa mno, na utumiaji wa Yehova wa pepo nne kutawanya Waelamu, akiwavunjavunja na kuwaulia mbali kabisa. (Yeremia 49:36-38) Itakuwa dhoruba ya upepo mkubwa mno yenye kukumba zaidi ya ile “tufani” ambayo kwayo Yehova alifutilia mbali taifa la Amoni. (Amosi 1:13-15, NW) Hakuna sehemu ya tengenezo la Shetani duniani ambayo itaweza kusimama katika siku ya kiruu cha Yehova, wakati yeye anapotetea enzi kuu yake kwa umilele wote utakaokuja.—Zaburi 83:15, 18; Isaya 29:5, 6.

      5. Unabii wa Yeremia unatusaidiaje kuelewa kwamba hukumu za Mungu zitaenea dunia yote nzima?

      5 Je! sisi tunaweza kuwa na hakika kwamba hukumu za Yehova zitakumba dunia nzima? Sikiliza tena nabii wake Yeremia: “Tazama! Afa moja linaenda kutoka taifa moja kwenda kwenye jingine, na tufani kubwa yenyewe itaamshwa juu kutoka sehemu za mbali zaidi sana za dunia. Na wale wenye kuuawa na Yehova kwa hakika watakuja kuwa katika siku hiyo kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi kufika mwisho mwingine kabisa wa dunia.” (Yeremia 25:32, 33, NW) Ni wakati wa dhoruba hii yenye tufani kwamba giza litagharikisha ulimwengu huu. Mawakili wao wenye kutawala watatikiswa waingie ndani ya utowesho. (Ufunuo 6:12-14) Lakini wakati ujao hautakuwa wenye giza kwa kila mmoja. Basi, ni kwa ajili ya nani zile pepo nne zinazuiwa?

      Kuwatia Muhuri Watumwa wa Mungu

      6. Ni nani anayeambia malaika wazuie pepo nne, na hilo linaruhusu wakati kwa ajili ya nini?

      6 Yohana anaendelea kueleza jinsi baadhi ya watu wanavyotiwa alama kwa ajili ya kuokoka, akisema: “Na mimi nikaona malaika mwingine akipanda juu kutoka kwenye zukio la jua, akiwa na muhuri wa Mungu anayeishi; na yeye alilia kwa sauti kubwa kwa wale malaika wanne ambao kwao ruhusa ilipewa ya kudhuru dunia na bahari, akisema: ‘Msidhuru dunia au bahari au miti, mpaka baada ya sisi tuwe tumetia muhuri watumwa wa Mungu wetu katika vipaji vya nyuso zao.’”—Ufunuo 7:2, 3, NW.

      7. Ni nani hasa aliye malaika wa tano, na ni ithibati gani inayotusaidia tuthibitishe utambulisho wake?

      7 Ingawa huyu malaika wa tano hatajwi jina, ithibati yote inaonyesha kwamba lazima awe Bwana Yesu aliyetukuzwa. Kupatana na kuwa kwa Yesu Malaika Mkuu, yeye anaonyeshwa hapa akiwa na mamlaka juu ya wale malaika wengine. (1 Wathesalonike 4:16; Yuda 9) Yeye anapanda juu kutoka mashariki, kama “wafalme kutoka zukio la jua”—Yehova na Kristo wake—ambao wanakuja kutekeleza hukumu, kama walivyofanya wafalme Dario na Sairasi wakati waliponyenyekeza Babuloni wa kale. (Ufunuo 16:12; Isaya 45:1; Yeremia 51:11; Danieli 5:31, NW) Malaika huyu anashabihi Yesu katika njia ya kwamba yeye ameaminishwa kazi ya kutia muhuri Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 1:13, 14) Na zaidi, wakati pepo zinapoachiliwa, ni Yesu anayeongoza majeshi ya kimbingu katika kutekeleza hukumu juu ya mataifa. (Ufunuo 19:11-16) Basi, kimantiki, Yesu angekuwa ndiye wa kuamuru kwamba uharibifu kwa tengenezo la kidunia la Shetani uzuiwe mpaka watumwa wa Mungu wawe wametiwa muhuri.

      8. Kutia muhuri ni nini, nako kulianza wakati gani?

      8 Huku kutia muhuri ni nini, na hawa watumwa wa Mungu ni nani? Kutia muhuri huku kulianza katika Pentekoste 33 W.K. wakati Wakristo Wayahudi wa kwanza walipopakwa mafuta kwa roho takatifu. Baadaye, Mungu aliendelea kuita na kupaka mafuta “watu wa mataifa.” (Warumi 3:29; Matendo 2:1-4, 14, 32, 33; 15:14, NW) Mtume Paulo aliandika juu ya Wakristo wapakwa-mafuta wakiwa na uhakikisho wa kwamba wao ‘ni wa Kristo’ na akaongeza kwamba Mungu “pia ametia muhuri wake juu yetu na ametupa sisi dalili ya kitu ambacho kitakuja, yaani, roho, katika mioyo yetu.” (2 Wakorintho 1:21, 22; linga Ufunuo 14:1, NW.) Hivyo, wakati watumwa hawa wanapolelewa kuwa wana wa kiroho wa Mungu, wanapokea dalili yenye kutangulia urithi wao wa kimbingu—muhuri au rehani. (2 Wakorintho 5:1, 5; Waefeso 1:10, 11) Ndipo wanapoweza kusema: “Roho yenyewe hutoa ushuhuda pamoja na roho yetu kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Ikiwa, basi, sisi ni watoto, sisi ni warithi pia: warithi kweli kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo, iwapo sisi tunateswa pamoja ili kwamba sisi tuweze pia kutukuzwa pamoja.”—Waroma 8:15-17, NW.

      9. (a) Ni uvumilivu gani unaotakwa upande wa mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho? (b) Kutahiniwa kwa wale wapakwa-mafuta kutaendelea mpaka lini?

      9 “Iwapo sisi tunateswa pamoja”—hiyo inamaanisha nini? Ili kupokea taji la uhai, Wakristo wapakwa-mafuta lazima wavumilie, wakiwa waaminifu mpaka kifo. (Ufunuo 2:10) Si shauri la ‘wakiisha okolewa, wanaokolewa daima.’ (Mathayo 10:22; Luka 13:24) Badala ya hivyo, wao wanapewa onyo hili la upole: “fanyeni yoteyote mwezayo mfanye kuitwa na kuchaguliwa kwa nyinyi kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe.” Kama vile mtume Paulo, mwishowe kabisa ni lazima wao waweze kusema: “Mimi nimepiga vita nzuri, mimi nimekimbia katika shindano mpaka mwisho, mimi nimeshika imani.” (2 Petro 1:10, 11; 2 Timotheo 4:7, 8, NW) Hivyo hapa duniani kule kutahiniwa na kupepetwa kwa yale mabaki ya wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho lazima kuendelee mpaka Yesu na malaika wanaoandamana naye wawe wamekwisha kuutia kikiki muhuri ‘katika kipaji cha uso’ wa hawa wote, kuwatambulisha kabisa kabisa, bila kutanguka, kuwa “watumwa wa Mungu wetu” waliojaribiwa na waaminifu. Ndipo muhuri unapokuwa alama ya daima. Kwa wazi, wakati pepo nne za dhiki zinapoachiliwa, Waisraeli wote wa kiroho watakuwa wamekwisha tiwa muhuri kabisa kabisa, hata ingawa wachache watakuwa wangali wanaishi katika mnofu. (Mathayo 24:13; Ufunuo 19:7) Hesabu nzima ya washiriki itakuwa imekamilika!—Warumi 11:25, 26.

      Ni Wangapi Wanatiwa Muhuri

      10. (a) Ni maandiko gani yanaonyesha kwamba hesabu ya watiwa muhuri ina kikomo? (b) Ni nini jumla ya hesabu iliyotiwa muhuri, na wao wanaorodheshwaje?

      10 Yesu aliambia wale waliokuwa katika mstari wa huku kutiwa muhuri: “Msiwe na hofu, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu ametoa kibali cha kuwapa nyinyi ufalme.” (Luka 12:32, NW) Maandiko mengine, kama vile Ufunuo 6:11 na Warumi 11:25, huonyesha kwamba hesabu ya hili kundi dogo ina kikomo kweli kweli na, kwa hakika, ilikusudiwa kimbele. Maneno ya Yohana yanayofuata yanathibitisha hili: “Na mimi nikasikia hesabu ya wale ambao walitiwa muhuri, mia na arobaini na nne elfu, waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli: Kutoka kabila la Yuda elfu kumi na mbili walitiwa muhuri; kutoka kabila la Reubeni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Gadi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Asheri elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Naftali elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Manase elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Simeoni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Lawi elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Isakari elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Zebuloni elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Yosefu elfu kumi na mbili; kutoka kabila la Benyamini elfu kumi na mbili walitiwa muhuri.”—Ufunuo 7:4-8, NW.

      11. (a) Ni kwa nini lile rejezo kwa makabila 12 halingeweza kutumika kuhusu Israeli halisi, wa mnofu? (b) Ni kwa nini Ufunuo huorodhesha makabila 12? (c) Ni kwa nini hakuna kabila ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani katika Israeli wa Mungu?

      11 Je! hii haingeweza kuwa inarejeza kwa Israeli halisi, wa mnofu? La, kwa kuwa Ufunuo 7:4-8 hutofautiana na ile orodha ya kawaida ya kikabila. (Hesabu 1:17, 47) Kwa wazi, orodha hii hapa si kwa kusudi la kutambulisha Wayahudi wa mnofu kwa makabila yao bali ni kuonyesha muundo wa kitengenezo kama huo kwa Israeli wa kiroho. Hili linasawazika. Wanapaswa waweko washiriki 144,000 wa hili taifa jipya—12,000 kutoka kila mojapo makabila 12. Hakuna kabila katika huyu Israeli wa Mungu ambalo hilo pekee ndilo la kifalme au la kikuhani. Taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa wafalme, na taifa lote kwa ujumla litatawala likiwa makuhani.—Wagalatia 6:16; Ufunuo 20:4, 6.

      12. Ni kwa nini inafaa kwamba wale wazee 24 wanaimba mbele ya Mwana-Kondoo maneno ya ule wimbo wa Ufunuo 5:9, 10?

      12 Ijapokuwa Wayahudi asilia na waongofu wa Kiyahudi walipewa fursa ya kwanza ili wachaguliwe kwa ajili ya kuwa Israeli wa kiroho, ni wachache tu wa taifa hilo walioitikia. Kwa hiyo Yehova aliwatolea mwaliko wale wasio Wayahudi. (Yohana 1:10-13; Matendo 2:4, 7-11; Warumi 11:7) Kama vile kwa habari ya Waefeso, ambao hapo kwanza walikuwa “wametenganishwa na dola la Israeli,” sasa watu wasio Wayahudi wangeweza kutiwa muhuri kwa roho ya Mungu na kuwa sehemu ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 2:11-13; 3:5, 6; Matendo 15:14) Basi, inafaa wazee 24 kuimba mbele za Mwana-Kondoo: “Kwa damu yako wewe ulinunua watu kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na kikundi cha watu na taifa, na wewe ulifanya wao kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao wanapaswa kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”—Ufunuo 5:9, 10, NW.

      13. Ni kwa nini ilifaa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote”?

      13 Kundi la Kikristo ni “jamii teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu.” (1 Petro 2:9, NW) Likichukua mahali pa Israeli asilia likiwa taifa la Mungu, linakuwa Israeli mpya ambaye ni “‘Israeli’ kikweli.” (Warumi 9:6-8; Mathayo 21:43, NW)a Kwa sababu hii, ilifaa kabisa Yakobo ndugu-nusu ya Yesu aandike barua yake ya kiuchungaji “kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika kotekote,” yaani, kwa kundi la ulimwenguni pote la Wakristo wapakwa-mafuta ambalo baadaye hesabu yalo ingekuwa 144,000.—Yakobo 1:1, NW.

      Israeli wa Mungu Leo

      14. Ni nini linaloonyesha kwamba bila ugeugeu Mashahidi wa Yehova wameshikilia kwamba 144,000 ni hesabu halisi ya wale wanaojumlika kuwa Israeli wa kiroho?

      14 Kwa kupendeza, Charles T. Russell, alitambua 144,000 kuwa hesabu halisi ya watu mmoja mmoja wanaojumlika kuwa Israeli wa kiroho. Katika The New Creation, Buku 6 la mfululizo wake wa Studies in the Scriptures, kilichotangazwa 1904, yeye aliandika: “Sisi tuna kila sababu kuitikadi kwamba ile hesabu dhahiri, iliyo imara ya wateule [wapakwa-mafuta waliochaguliwa] ni ile ambayo imetaarifiwa mara kadhaa katika Ufunuo (7:4; 14:1); yaani, 144,000 ‘waliokombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu.’” Katika Light, Kitabu cha Kwanza, kilichotangazwa katika 1930 na Wanafunzi wa Biblia, ilitaarifiwa hali kadhalika hivi: “Hivyo washiriki 144,000 wa mwili wa Kristo wako katika kusanyiko wakionyeshwa kuwa wamechaguliwa na kupakwa mafuta, au kutiwa muhuri.” Bila ugeugeu Mashahidi wa Yehova wameshikilia oni la kwamba kihalisi Wakristo wapakwa-mafuta 144,000 wanajumlika kuwa Israeli wa kiroho.

      15. Kabla tu ya siku ya Bwana, wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walifikiri Wayahudi asilia wangefurahia nini baada ya Majira ya Mataifa kuisha?

      15 Hata hivyo, je! Waisraeli asilia leo hawastahili kadiri fulani ya upendeleo wa pekee? Katika pindi iliyokuwa kabla tu ya siku ya Bwana, wakati wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe walipokuwa wakigundua tena nyingi za kweli za msingi za Neno la Mungu, ilidhaniwa kwamba Majira ya Mataifa yakiisha, Wayahudi wangefurahia tena msimamo wenye kibali mbele za Mungu. Hivyo, kitabu cha C. T. Russell The Time Is at Hand (Buku 2 la Studies in the Scriptures), kilichotangazwa 1889, kilitumia Yeremia 31:29-34 kuhusu Wayahudi asilia, na kueleza: “Ulimwengu ni shahidi wa uhakika wa kwamba adhabu ya Israeli chini ya utawala wa wasio Wayahudi imekuwa ikiendelea tangu K.K. [607], kwamba ingali inaendelea, na kwamba hakuna sababu ya kutazamia mtengenezo mpya wa kitaifa upesi zaidi ya M.B. 1914, kile kikomo cha ‘nyakati saba’ zao—miaka 2520.” Ilielekea kwamba wakati huo Wayahudi wangepata urudisho wa kitaifa, na kwa wazi tazamio hilo lilitiwa uangavu 1917, wakati Julisho-Wazi la Balfour lilipoahidi kuunga mkono Uingereza kwa kufanya Palestina kuwa kao la kitaifa kwa ajili ya Wayahudi.

      16. Ni jitihada gani walizofanya Mashahidi wa Yehova kufikia Wayahudi asilia wakiwa na ule ujumbe wa Kikristo, na kukawa na tokeo gani?

      16 Kufuata vita ya kwanza ya ulimwengu, Palestina ikawa eneo chini ya usimamizi wa Uingereza, na njia ikafunguka Wayahudi warudi kwenye bara hilo. Katika 1948 Dola la kisiasa la Israeli lilitokezwa. Je! hiyo haikuonyesha kwamba Wayahudi walikuwa katika mstari wa kupata baraka za kimungu? Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova waliitikadi kwamba ilikuwa hivyo. Hivyo, katika 1925 walitangaza kitabu chenye kurasa 128, Comfort for the Jews. Katika 1929 walitoa buku lenye kuvutia la kurasa 360, Life, ambalo lilikusudiwa livutie Wayahudi na pia lilishughulika na kitabu cha Biblia cha Ayubu. Jitihada kubwa zilifanywa, hasa katika Jiji la New York, kufikia Wayahudi kwa huu ujumbe wa Kimesiya. Kwa furaha, watu wachache mmoja mmoja waliitikia, lakini Wayahudi kwa ujumla, kama babu zao wa karne ya kwanza, waliikataa ithibati ya kuwapo kwa Mesiya.

      17, 18. Watumwa wa Mungu walikuja kuelewa nini kuhusu agano jipya na unabii wa Biblia wa urudisho?

      17 Ilikuwa wazi kwamba Wayahudi, wakiwa taifa, hawakuwa yule Israeli aliyeelezwa katika Ufunuo 7:4-8 au katika unabii mwingine wa Biblia unaohusu siku ya Bwana. Wakifuata pokeo, Wayahudi waliendelea kuepuka kutumia jina la kimungu. (Mathayo 15:1-3, 7-9) Kikizungumzia Yeremia 31:31-34, kitabu Jehovah, kilichotangazwa na Mashahidi wa Yehova katika 1934, kilitaarifu hivi kwa mkataa: “Lile agano jipya halihusiani kwa vyovyote na wazao asilia wa Israeli pamoja na aina ya binadamu kwa ujumla, bali . . . lina mpaka kwa Israeli wa kiroho tu.” Unabii wa Biblia juu ya urudisho hauhusu wala Wayahudi asilia wala Israeli ya kisiasa, ambayo ni mshiriki wa Umoja wa Mataifa na ni sehemu ya ulimwengu ambao Yesu alizungumzia kwenye Yohana 14:19, 30 na 18:36.

      18 Katika 1931 watumwa wa Mungu duniani walikuwa wamepokea, kwa shangwe kubwa, jina Mashahidi wa Yehova. Wao waliweza kukubaliana kwa moyo wote na maneno ya Zaburi 97:11, NW: “Nuru yenyewe imemeta juu ya mwadilifu, na kushangilia hata kwa ajili ya wale walio wanyoofu katika moyo.” Wao wangeweza kufahamu kwamba Israeli wa kiroho pekee walikuwa wameletwa ndani ya agano jipya. (Waebrania 9:15; 12:22, 24) Waisraeli asilia wasioitikia hawakuwa na sehemu humo, wala aina ya binadamu kwa ujumla. Uelewevu huu ulifungulia njia mmeto mwangavu wa nuru ya kimungu, wenye kutokeza sana katika habari ya tarehe za historia ya kitheokrasi. Huo ungefunua jinsi Yehova atoavyo kwa wingi sana rehema, fadhili za upendo, na ukweli kwa wanadamu wote ambao wanamkaribia yeye. (Kutoka 34:6; Yakobo 4:8) Ndiyo, wengine mbali na Israeli wa Mungu wangenufaishwa na uzuifu wa malaika wa pepo nne za uharibifu. Hao wangekuwa nani? Je! wewe ungeweza kuwa mmoja wao? Acheni tuone sasa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kwa kufaa, jina Israeli humaanisha “Mungu Hushindana; Mwenye Kushindana (Mwendelevu) Pamoja na Mungu.”—Mwanzo 32:28, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

  • Kutia Muhuri Israeli wa Mungu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 114]

      [Picha katika ukurasa wa 116, 117]

      Uteuzi wa ujumla wa Israeli wa kweli wa Mungu uliendelea kuanzia siku ya Pentekoste 33 W.K. kufika 1935 wakati, kwenye mkusanyiko wenye kufanyiza historia wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C., mkazo uligeuzwa ukaelekezwa kwenye kukusanywa kwa umati mkubwa wenye matazamio ya uhai wa kidunia (Ufunuo 7:9)

  • Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 20

      Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi Sana

      1. Baada ya kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa wale 144,000, Yohana anaona kikundi gani kingine?

      AKIISHA kueleza habari ya kutiwa muhuri kwa 144,000, Yohana anaendelea kuripoti mmojapo mafunuo yenye kutaharakisha zaidi sana katika Andiko lote. Lazima moyo wake uwe uliruka-ruka kwa shangwe alipokuwa akiuripoti, akisema: “Baada ya vitu hivi mimi nikaona, na, tazama! umati mkubwa ambao hakuna binadamu aliyeweza kuhesabu kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevalia majoho meupe; na kulikuwa na matawi ya mitende katika mikono yao.” (Ufunuo 7:9, NW) Ndiyo, kuzuiliwa kwa zile pepo nne kunaruhusu wakati kwa ajili ya wokovu wa kikundi kingine mbali na washiriki 144,000 wa Israeli wa kiroho: umati mkubwa wa lugha nyingi, wa kimataifa.a—Ufunuo 7:1.

      2. Waelezaji wa kilimwengu wameelezaje umati mkubwa, na hata Wanafunzi wa Biblia zamani walionaje kikundi hiki?

      2 Waelezaji wa kilimwengu wamefasiri huu umati mkubwa kuwa watu wa mnofu wasio Wayahudi ambao wameongolewa kwenye Ukristo au kuwa Wakristo wafia-imani wanaoelekea mbinguni. Zamani, hata Wanafunzi wa Biblia waliwaona kuwa jamii ya pili ya kimbingu, kama ilivyotajwa katika 1886 katika Buku I la Studies in the Scriptures, The Divine Plan of the Ages: “Wao wanapoteza zawadi ya kiti cha ufalme, na ile asili ya kimungu, lakini mwishowe watafikia uzawa wakiwa viumbe wa roho wa hali ya chini zaidi ya asili ya kimungu. Ingawa hawa ni wakfu kikweli, wao wanashindwa na roho ya ulimwengu kwa kadiri ya kwamba wao wanakosa kutoa maisha yao kuwa dhabihu.” Hata karibuni zaidi kama 1930, hilo wazo lilitolewa katika Light, Kitabu cha Kwanza: “Wale wanaojumlika kuwa huu umati mkubwa wanashindwa kuitikia mwaliko wa kuwa mashahidi wenye bidii kwa ajili ya Bwana.” Ilielezwa kuwahusu kuwa kikundi cha wenye uadilifu wa kujifanyia wenyewe waliokuwa na maarifa ya ukweli lakini walifanya kidogo sana kuuhubiri. Walipaswa kwenda mbinguni wakiwa jamii ya pili ambayo haingeshiriki kutawala pamoja na Kristo.

      3. (a) Ni tumaini gani walilotolewa wengine wa wale wenye mioyo inayofaa ambao baadaye walikuwa wenye bidii katika kazi ya kuhubiri? (b) Katika 1923 Mnara wa Mlinzi ulielezaje mfano wa kondoo na mbuzi?

      3 Hata hivyo, kulikuwako wengine walioshirikiana na Wakristo wapakwa-mafuta ambao baadaye walikuwa wenye bidii zaidi sana katika kazi ya kuhubiri. Wao hawakuwa na tamaa za kwenda mbinguni. Kweli kweli, tumaini lao lilipatana na kichwa cha hotuba iliyotolewa na Mashahidi wa Yehova kuanzia 1918 kufika 1922. Mwanzoni kabisa, hiyo ilikuwa “Ulimwengu Umekoma—Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Kamwe.”b Upesi baada ya hapo gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1923, lilieleza mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi (Mathayo 25:31-46), likataarifu: “Kondoo huwakilisha vikundi vyote vya mataifa, si vilivyozaliwa kwa roho lakini vyenye mwelekeo wa uadilifu, ambavyo kiakili hukiri Yesu Kristo kuwa Bwana na ambavyo hutazamia na kutumaini wakati ulio bora chini ya utawala wake.”

      4. Nuru kuhusu jamii ya kidunia ilipataje kuwa nyangavu zaidi katika 1931? katika 1932? katika 1934?

      4 Miaka kadhaa baadaye, katika 1931, Vindication, Kitabu cha Kwanza, kilizungumzia Ezekieli sura ya 9 kikitambulisha wale watu wenye kutiwa alama juu ya kipaji cha uso kwa ajili ya kuhifadhiwa kwenye mwisho wa ulimwengu kuwa kondoo wa huo mfano wa juu. Vindication, Kitabu cha Tatu, kilichotolewa 1932, kilieleza habari ya unyoofu wa mwelekeo wa moyoni wa mtu asiye Mwisraeli, Yehonadabu, aliyejiunga na Mfalme mpakwa-mafuta, Yehu Mwisraeli katika gari lake akaenda naye akaone bidii ya Yehu katika kufisha wanadini bandia. (2 Wafalme 10:15-17) Kitabu hicho kilitoa elezo hili: “Yehonadabu aliwakilisha au akatangulia kuweka kivuli cha jamii ya watu ambao wako duniani leo katika wakati ambao kazi ya Yehu [ya kujulisha wazi hukumu za Yehova] inaendelea, ambao ni wa nia njema, hawapatani na tengenezo la Shetani, ambao wanachukua msimamo wao katika upande wa uadilifu, na ndio ambao Bwana atahifadhi hai wakati wa Har–Magedoni awachukue kupitia taabu hiyo, na kuwapa uhai wa milele duniani. Hao wanajumlika kuwa ‘jamii ya kondoo.’ Katika 1934 Mnara wa Mlinzi ulieleza wazi kwamba Wakristo hawa walio na matumaini ya kidunia wapaswa wajiweke wakfu kwa Yehova na wabatizwe. Nuru kuhusu hii jamii ya kidunia ilikuwa iking’aa kwa uangavu zaidi na zaidi.—Mithali 4:18.

      5. (a) Ni utambulisho gani wa umati mkubwa uliofanywa katika 1935? (b) Wakati J. F. Rutherford katika 1935 alipouliza wanamkusanyiko waliokuwa na tumaini la kuishi milele duniani wasimame, kulitukia nini?

      5 Ule uelewevu wa Ufunuo 7:9-17 ulikuwa sasa unakaribia kububujika pamoja na uangavu wao wote wenye kumeremeta! (Zaburi 97:11) Kwa kurudiarudia gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa limeonyesha tumaini la kwamba mkusanyiko mmoja uliokuwa umeratibiwa Mei 30 kufika Juni 3, 1935, katika Washington D.C., U.S.A., ungekuwa “faraja halisi na manufaa” kwa wale waliotolewa picha na Yehonadabu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa! Katika hotuba yenye kusisimua juu ya “Mkutano Mkubwa” iliyotolewa kwa wanamkusanyiko wapatao 20,000, J. F. Rutherford, ambaye wakati huo alikuwa akielekeza kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote, alitoa uthibitisho wa Kimaandiko kwamba kondoo wengine wa ki-siku-hizi ni jamii ile ile ya umati mkubwa wa Ufunuo 7:9. Kwenye upeo wa hotuba hii, msemaji huyo aliuliza: “Wale wote ambao wana tumaini la kuishi milele juu ya dunia tafadhali mnaweza kusimama?” Sehemu kubwa ya hadhirina ilipokuwa ikisimama, msemaji alitangaza: “Tazameni! Mkutano mkubwa!” Kukawa na kimya, kikifuatwa na vigelegele vyenye mngurumo. Ilifurahi kama nini jamii ya Yohana—na pia kikundi cha Yehonadabu! Keshoye, Mashahidi wapya 840 walibatizwa, walio wengi zaidi wa hawa wakidai kuwa wa huo umati mkubwa.

      Kuthibitisha Utambulisho wa Umati Mkubwa

      6. (a) Ni kwa nini sisi tunaweza kuelewa waziwazi kwamba umati mkubwa ni kikundi cha ki-siku-hizi cha Wakristo walio wakfu ambao wanatumaini kuishi milele duniani? (b) Yale majoho meupe ya huo umati mkubwa yanafananisha nini?

      6 Sisi tunaweza kutaarifuje tukiwa na uhakika sana hivyo kwamba ule umati mkubwa ni kikundi hiki cha ki-siku-hizi cha Wakristo waliojiweka wakfu ambao wanatumaini kuishi milele juu ya dunia ya Mungu? Wakati uliotangulia, Yohana alikuwa ameona katika njozi kikundi cha kimbingu ‘ambacho kilinunuliwa kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na vikundi vya watu na taifa.’ (Ufunuo 5:9, 10, NW) Umati mkubwa una chanzo kinachofanana na hicho lakini wanakoenda ni tofauti. Tofauti na Israeli wa Mungu, hesabu yao haikukusudiwa kimbele. Hakuna mtu anayeweza kusema mapema watakuwa wangapi. Majoho yao meupe yameoshwa kwa damu ya yule Mwana-Kondoo, kufananisha kwamba wao wana msimamo wenye uadilifu mbele za Yehova kwa sababu ya imani yao katika dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:14) Nao wanapungapunga matawi ya mitende, wakimshangilia Mesiya kuwa Mfalme wao.

      7, 8. (a) Kule kupungwapungwa kwa matawi ya mitende bila shaka kulimkumbusha mtume Yohana juu ya matukio gani? (b) Ni nini maana ya uhakika wa kwamba hao wa umati mkubwa wanapungapunga matawi ya mitende?

      7 Anapotazama katika njozi hii, mawazo ya Yohana lazima yawe yanamrudisha nyuma zaidi ya miaka 60 kwenye juma la mwisho la Yesu duniani katika Nisani 9, 33 W.K., wakati umati ulipokuja makundi makundi ili kumkaribisha Yesu ndani ya Yerusalemu, wao “walichukua matawi ya mitende wakatoka nje kumlaki. Na wao wakaanza kupaaza sauti: ‘Okoa, sisi twaomba wewe! Mbarikiwa ni yeye ambaye anakuja katika jina la Yehova, hata mfalme wa Israeli!’” (Yohana 12:12, 13, NW) Hali moja na hiyo, kule kupungapunga matawi ya mitende na kupaaza sauti upande wa umati mkubwa huonyesha shangwe yao isiyozuilika katika kumkubali Yesu kuwa Mfalme wa Yehova aliyewekwa rasmi.

      8 Pasipo shaka, hayo matawi ya mitende na vilio vya kuchachawa pia vinamkumbusha Yohana ile Sikukuu ya Vibanda ya kale ya Israeli. Kwa ajili ya sikukuu hii Yehova aliamuru: “Na ni lazima nyinyi mjichukulie kwa ajili yenu wenyewe katika siku ya kwanza tunda la miti mizuri sana, na matagaa ya mitende na matanzu ya miti yenye matawi na mipopla ya bonde la mvo, na ni lazima nyinyi mshangilie mbele za Yehova Mungu wenu siku saba.” Matawi ya mitende yalitumiwa kuwa alama ya kushangilia. Vibanda vya muda vilikuwa kikumbusha kwamba Yehova alikuwa amewaokoa watu wake kutoka Misri, waishi katika mahema katika jangwa. “Mkazi mgeni na mvulana asiye na baba na mjane” walishiriki hii sikukuu. Waisraeli wote walipaswa ‘wawe si kitu ila wenye kujawa na shangwe.’—Walawi 23:40; Kumbukumbu 16:13-15, NW.

      9. Umati mkubwa unajiunga katika kilio gani cha shangwe?

      9 Basi, inafaa kwamba, umati mkubwa, ingawa si sehemu ya Israeli wa kiroho, upungepunge matawi ya mitende kwa kuwa wanaonyesha kwa shangwe na asante kwamba ushindi na wokovu hutoka kwa Mungu na Mwana-Kondoo kama Yohana anavyoona hapa: “Nao hufuliza kulia kwa sauti kubwa, kusema: ‘Wokovu wetu ni kwa Mungu wetu, ambaye ameketi juu ya kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’” (Ufunuo 7:10, NW) Ijapokuwa wao wametengwa kutoka vikundi vyote vya kikabila, huo umati mkubwa unalia kwa hiyo “sauti kubwa” moja tu. Wao wanawezaje kufanya hivi, wajapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?

      10. Umati mkubwa unaweza kuliaje kwa umoja kwa “sauti kubwa” moja ijapokuwa ni wa mataifa na lugha mbalimbali?

      10 Huu umati mkubwa ni sehemu ya tengenezo la mataifa mengi ambalo ndilo pekee lina umoja kweli kweli duniani leo. Wao hawana viwango tofauti-tofauti kwa nchi tofauti-tofauti bali wanatumia kwa ajili ya upatani kanuni za Biblia zinazofaa kokote wanakoishi. Wao hawajiingizi katika harakati za kitaifa, zenye kutaka mapinduzi bali wao ‘wamefua panga zao zikawa majembe ya plau.’ (Isaya 2:4, NW) Wao hawana mgawanyiko wa mafarakano au vikundi vya kidini, hivi kwamba wanapaaza sauti zilizovurugika au jumbe za pamoja zenye kupingana-pingana kama zinavyofanya dini za Jumuiya ya Wakristo; wala wao hawaachii jamii ya viongozi wa kidini wenye kulipwa mshahara wafanye kusifu kwa ajili yao. Wao hawapaazi sauti kwamba wokovu wao hutoka kwa roho takatifu kwa kuwa wao si watumishi wa kamungu ka utatu. Katika maeneo ya kijiografia 200 kuzunguka dunia, wao wana umoja katika kuita juu ya jina la Yehova wanaposema lugha safi ya ukweli. (Sefania 3:9) Kwa kufaa, wao wanakiri peupe kwamba wokovu wao unakuja kutoka kwa Yehova Mungu wa wokovu, kupitia Yesu Kristo, Wakili Mkuu Wake wa wokovu.—Zaburi 3:8; Waebrania 2:10.

      11. Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidiaje wale wa umati mkubwa kufanya sauti yao kubwa iwe kubwa hata zaidi?

      11 Tekinolojia ya ki-siku-hizi imesaidia kufanya sauti kubwa ya umati mkubwa wenye umoja ivume kwa ukubwa hata zaidi. Hakuna kikundi kinginecho cha kidini duniani ambacho kina uhitaji wa kuchapisha misaada ya kujifunza Biblia katika lugha zaidi ya 400, kwa maana hakuna kikundi kinginecho ambacho kinapendezwa na kufikia vikundi vyote vya watu wa dunia kwa ujumbe mmoja wenye umoja. Kama msaada zaidi katika jambo hili, chini ya uangalizi wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova lililopakwa mafuta mfumo uitwao, Multilanguage Electronic Phototypesetting System (MEPS) uliundwa. Kufikia wakati kitabu hiki kilipochapishwa, namna tofauti-tofauti za MEPS zinatumiwa katika maeneo zaidi ya 125 kuzunguka dunia, na jambo hili limesaidia kufanya iwezekane utangazaji sawia wa jarida la mara mbili kwa mwezi, Mnara wa Mlinzi, katika lugha zaidi ya 130. Pia watu wa Yehova wanatangaza kisawia, vitabu kama hiki, kwa lugha kadhaa. Hivyo, Mashahidi wa Yehova, ambao ule umati mkubwa ndio walio wengi sana, wanaweza kila mwaka kugawa mamia ya mamilioni ya vichapo katika lugha zote zinazojulikana vizuri zaidi, wakiwezesha misongamano mingi zaidi ya kutoka makabila yote na lugha wajifunze Neno la Mungu na kuunga sauti zao kwenye ile sauti kubwa ya umati mkubwa.—Isaya 42:10, 12.

      Mbinguni au Duniani?

      12, 13. Ni katika njia gani umati mkubwa ‘umesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo’?

      12 Sisi tunajuaje kwamba ‘kusimama mbele ya kiti cha ufalme’ hakumaanishi kwamba umati mkubwa umo mbinguni? Kuna ithibati nyingi iliyo wazi juu ya jambo hili. Mathalani, neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa “mbele” (e·noʹpi·on) humaanisha kihalisi “katika [mwono wa]” nalo linatumiwa mara kadhaa kuhusu wanadamu duniani ambao wako “mbele” au “katika mwono wa” Yehova. (1 Timotheo 5:21; 2 Timotheo 2:14; Warumi 14:22; Wagalatia 1:20, NW) Katika pindi moja wakati Waisraeli walipokuwa katika jangwa, Musa alimwambia Haruni hivi: “Sema kwa kusanyiko zima la wana wa Israeli, ‘Njooni karibu mbele za Yehova, kwa sababu yeye amesikia manung’uniko yenu.’” (Kutoka 16:9, NW) Waisraeli hao hawakulazimika kusafirishwa mpaka mbinguni ili wakasimame mbele za Yehova katika pindi hiyo. (Linga Walawi 24:8.) Badala ya hivyo, uko huko jangwani walisimama katika mtazamo wa Yehova, na uangalifu wake ukawa juu yao.

      13 Kwa kuongezea, sisi tunasoma hivi: “Wakati Mwana wa binadamu anapowasili katika utukufu wake . . . mataifa yote yatakusanywa mbele ya yeye.”c Jamii ya kibinadamu kwa ujumla haitakuwamo katika mbingu wakati unabii huu unapotimizwa. Bila shaka, wale ambao ‘huondoka kwenda kuingia katika kukatiliwa mbali milele’ hawatakuwamo katika mbingu. (Mathayo 25:31-33, 41, 46, NW) Badala ya hivyo, aina ya binadamu husimama duniani katika mtazamo wa Yesu, naye hugeuza uangalifu wake awahukumu. Hali kadhalika, umati mkubwa uko “mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo” katika maana ya kwamba huo husimama katika mtazamo wa Yehova na Mfalme wake, Kristo Yesu, ambao kutoka kwao unapokea hukumu yenye kupendeleka.

      14. (a) Ni nani wanaosimuliwa kuwa wako “kuzunguka kiti cha ufalme” na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu? (b) Ingawa umati mkubwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake,” ni kwa sababu gani hilo haliwafanyi kuwa jamii ya kikuhani?

      14 Wazee 24 na kikundi cha wapakwa-mafuta 144,000 wanasimuliwa kuwa wako ‘kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova pande zote’ na “juu ya Mlima Sayuni” wa kimbingu. (Ufunuo 4:4; 14:1, NW) Umati mkubwa si jamii ya kikuhani nao haufikii cheo hicho kilichokwezwa. Kweli, baadaye unasimuliwa katika Ufunuo 7:15 kuwa unatumikia Mungu “katika hekalu lake.” Lakini hekalu hili halirejezei patakatifu pa ndani zaidi, pale Patakatifu Zaidi Sana. Badala ya hivyo, ni ua wa kidunia wa hekalu la Mungu la kiroho. Neno la Kigiriki na·osʹ, linalotafsiriwa hapa “hekalu,” mara nyingi huwasilisha maana pana ya jengo zima lote lililojengwa kwa ajili ya ibada ya Yehova. Leo, hili ni jengo la kiroho ambalo hutia ndani mbingu na dunia pia.—Linga Mathayo 26:61; 27:5, 39, 40; Marko 15:29, 30; Yohana 2:19-21, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      Vigelegele vya Sifa vya Ulimwengu Wote Mzima

      15, 16. (a) Kunakuwa na tendo-itikio gani katika mbingu kwa kuonekana kwa umati mkubwa? (b) Uumbaji wa roho wa Yehova unatendaje kwa kuitikia kila ufunuo mpya wa kusudi lake? (c) Sisi tuliopo duniani tunaweza kujiungaje kuimba wimbo wa sifa?

      15 Umati mkubwa unamsifu Yehova, lakini wengine pia wanaimba sifa zake. Yohana anaripoti: “Na malaika wote walikuwa wakisimama kuzunguka kiti cha ufalme na wazee na viumbe hai wanne, na wao walianguka nyuso zao chini mbele ya kiti cha ufalme na wakaabudu Mungu, kusema: ‘Ameni! Baraka na utukufu na hekima na utoaji-shukrani na heshima na nguvu na imara ziwe kwa Mungu wetu milele na milele. Ameni.’”—Ufunuo 7:11, 12, NW.

      16 Wakati Yehova alipoumba dunia, malaika zake wote watakatifu ‘walipiga kilio kikuu kwa shangwe pamoja, na wana wote wa Mungu wakaanza kupaaza sauti kwa vifijo.’ (Ayubu 38:7, NW) Kila ufunuo mpya wa kusudi la Yehova lazima uwe ulitokeza mipaazo ya sifa ya kimalaika jinsi iyo hiyo. Wakati wazee 24—144,000 katika utukufu wao wa kimbingu—wanapolia kwa sauti kubwa katika kumtambua Mwana-Kondoo, wengine wote wa viumbe wa kimbingu huitikia kwa kusifu Yesu na Yehova Mungu. (Ufunuo 5:9-14) Tayari, viumbe hawa wamekuwa na shangwe mno kuona utimizo wa kusudi la Yehova katika kufufua kwake wanadamu wapakwa-mafuta waaminifu kwenye mahali penye utukufu katika milki ya kiroho. Sasa, viumbe wote waaminifu wa Yehova wa kimbingu wanabubujika kwa sifa za kimelodia wakati umati mkubwa unapoonekana. Kwa kweli, kwa watumishi wote wa Yehova, siku ya Bwana ni wakati wenye kusisimua kuishi humo. (Ufunuo 1:10) Hapa duniani, sisi ni wenye pendeleo kama nini kushiriki kuimba wimbo wa sifa kwa kuutolea Ufalme wa Yehova ushuhuda!

      Umati Mkubwa Wajionyesha

      17. (a) Ni swali gani linalozushwa na mmoja wa wazee 24, na uhakika wa kwamba mzee angeweza kupata mahali pa jibu unadokeza nini? (b) Swali la mzee lilijibiwa lini?

      17 Tangu wakati wa mtume Yohana na kundelea mpaka ndani ya siku ya Bwana, Wakristo wapakwa-mafuta walitatizika wakitaka kujua utambulisho wa umati mkubwa. Basi, inafaa kwamba, mmoja wa wazee 24, akiwakilisha wapakwa-mafuta ambao tayari wako katika mbingu, achochee kufikiri kwa Yohana kwa kuzusha swali hususa: “Na katika kuitikia mmoja wa wazee akasema kwangu mimi: ‘Hawa ambao wamevalia majoho meupe, wao ni akina nani na wao walitoka wapi?’ Kwa hiyo mara hiyo mimi nikasema kwa yeye: ‘Bwana yangu, wewe ndiwe mmoja ambaye anajua.’” (Ufunuo 7:13, 14a, NW) Ndiyo, huyo mzee angeweza kupata mahali pa jibu na kumpa Yohana. Hiyo inadokeza kwamba waliofufuliwa wa kikundi cha wazee 24 huenda wakawa wanahusika katika kuwasilisha kweli za kimungu leo. Kwa upande wao, wale wa jamii ya Yohana waliomo duniani walipata kujua utambulisho wa umati mkubwa kwa kutazama kwa ukaribu sana alichokuwa akifanya Yehova katikati yao. Wao walikuwa wenye uharaka wa kuthamini mmeto wenye kutia kiwi wa nuru ya kimungu ambao ulipamba anga la kitheokrasi katika 1935, wakati barabara wa Yehova.

      18, 19. (a) Ni tumaini gani lililokaziwa na jamii ya Yohana wakati wa miaka ya 1920 na 1930, lakini ni nani walioitikia ujumbe kwa hesabu yenye kuongezeka? (b) Ule utambulisho wa umati mkubwa katika 1935 ulionyesha nini kwa habari ya 144,000? (c) Takwimu za Ukumbusho zinafunua nini?

      18 Wakati wa miaka ya 1920 na 1930, jamii ya Yohana ilikuwa imekazia tumaini la kimbingu, katika vichapo na katika kazi ya kuhubiri pia. Kwa wazi hesabu kamili ya 144,000 ilikuwa bado kutimia. Lakini hesabu iliyokuwa ikiongezeka ya wale waliotii ujumbe na wakaonyesha bidii katika kazi ya kutoa ushuhuda wakaja kudhihirisha kuwa wanapendezwa na kuishi milele katika dunia Paradiso. Wao hawakuwa na tamaa ya kwenda mbinguni. Huo haukuwa mwito wao. Wao hawakuwa sehemu ya kundi dogo bali ya kondoo wengine. (Luka 12:32; Yohana 10:16) Kutambulishwa kwao katika 1935 kuwa umati mkubwa wa wale kondoo wengine kilikuwa kionyeshi cha kwamba wakati huo kuchaguliwa kwa 144,000 kulikuwa karibu kumekamilika.

      19 Je! takwimu zinaunga mkono mkataa huu? Ndiyo. Katika 1938, ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova 59,047 walishiriki katika huduma. Kati ya hao 36,732 walishiriki mifano kwenye mwadhimisho wa kila mwaka wa Ukumbusho wa kifo cha Yesu, hivyo wakionyesha kwamba walikuwa na mwito wa kimbingu. Katika miaka iliyofuata tangu hapo, hesabu ya washiriki hao imeendelea kupungua, hasa kwa sababu Mashahidi waaminifu wa Yehova walimaliza mwendo wa maisha yao ya kidunia katika kifo. Katika 2005 ni 8,524 pekee walioshiriki mifano ya Ukumbusho—asilimia 0.05 tu ya wale 16,390,116 waliohudhuria mwadhimisho huo wa pote katika tufe.

      20. (a) Wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, ni elezo gani alilotoa faraghani J. F. Rutherford kwa habari ya umati mkubwa? (b) Ni uhakika gani sasa unaoonyesha kwamba umati mkubwa ni mkubwa kweli kweli?

      20 Wakati vita ya pili ya ulimwengu ilipofyatuka, Shetani alitia jitihada kali azuie kuvunwa kwa umati mkubwa. Kazi ya Yehova ilizuiwa katika nchi nyingi. Siku hizo zilizokuwa ngumu, na muda mfupi kabla ya kifo chake katika Januari 1942, J. F. Rutherford alisikiwa akisema: “Basi . . . inaonekana kama umati mkubwa hautakuwa mkubwa sana hata hivyo.” Lakini baraka za kimungu zilielekeza vingine! Kufikia 1946 hesabu ya Mashahidi waliokuwa wakitumikia ulimwenguni pote ilikuwa imeruka kufikia 176,456—walio wengi wa hao wakiwa wa umati mkubwa. Katika 2005 walikuwako Mashahidi 6,390,022 waliokuwa wakitumikia Yehova kiaminifu katika mabara mbalimbali 235—UMATI MKUBWA kweli kweli! Na hesabu inazidi kuongezeka.

      21. (a) Kuvunwa kwa watu wa Mungu wakati wa siku ya Bwana kumekuwaje katika upatani kamili na njozi ya Yohana? (b) Unabii fulani wa maana ulianza kutimizwaje?

      21 Hivyo kuvunwa kwa watu wa Mungu wakati wa siku ya Bwana kumekuwa katika upatani kamili na njozi ya Yohana: kwanza kazi ya kukusanya mabaki ya 144,000; kisha kukusanywa kwa umati mkubwa. Kama Isaya alivyotoa unabii, sasa “katika sehemu ya mwisho kabisa ya siku,” watu wa mataifa yote wanamiminika kushiriki ibada safi ya Yehova. Na, kweli kweli, sisi tunachachawa katika uthamini wa uumbaji wa Yehova wa “mbingu mpya na dunia mpya.” (Isaya 2:2-4; 65:17, 18, NW) Mungu anakusanya “tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu katika mbingu na vitu juu ya dunia.” (Waefeso 1:10, NW) Warithi wapakwa-mafuta wa Ufalme wa kimbingu—waliochaguliwa katika muda wa karne zilizopita tangu siku ya Yesu—ndio “vitu katika mbingu.” Na sasa, umati mkubwa wa kondoo wengine wanatokea wakiwa wa kwanza wa “vitu juu ya dunia.” Kutumikia kwako kupatana na mpango huo kunaweza kumaanisha furaha ya milele kwa ajili ya wewe.

      Baraka za Umati Mkubwa

      22. Ni habari gani zaidi anayopokea Yohana kuhusu umati mkubwa?

      22 Kupitia mfereji wa kimungu Yohana anapokea habari zaidi kuhusu huu umati mkubwa: “Na yeye [mzee] akasema kwangu mimi: ‘Hawa ndio wale ambao huja kutoka dhiki kubwa, na wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Hiyo ndiyo sababu wao wako mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu; na wao wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Mmoja anayeketi juu ya kiti cha ufalme atatanda hema yake juu yao.’”—Ufunuo 7:14b, 15, NW.

      23. Ni nini iliyo dhiki kubwa ambayo umati mkubwa “huja kutoka” hiyo?

      23 Katika pindi ya mapema zaidi, Yesu alikuwa amesema kwamba kuwapo kwake katika utukufu wa Ufalme kungefikia upeo katika “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, 22, NW) Katika utimizo wa unabii huo, wale malaika wataachilia pepo nne za dunia zikumbe mfumo wa ulimwengu wa Shetani. Cha kwanza kwenda kitakuwa ni Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Kisha, kwenye upeo wa dhiki hiyo, Yesu ataokoa mabaki duniani ya 144,000, pamoja na umati mkubwa wenye watu wengi sana.—Ufunuo 7:1; 18:2.

      24. Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka?

      24 Watu mmoja mmoja wa umati mkubwa wanastahilije kwa ajili ya kuokoka? Yule mzee anamwambia Yohana kwamba “wamefua majoho yao na wameyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Kwa maneno mengine, wao wamezoea imani katika Yesu akiwa Mkombozi wao, wamejiweka wakfu kwa Yehova, nao wameonyesha wakfu wao kwa ubatizo wa maji, na ‘wanashika dhamiri njema’ kwa mwenendo wao mnyoofu. (1 Petro 3:16, 21; Mathayo 20:28, NW) Hivyo, wao ni safi na waadilifu katika macho ya Yehova. Na wanajiweka wenyewe “bila doa kutoka ulimwengu.”—Yakobo 1:27, NW.

      25. (a) Umati mkubwa unamtoleaje Yehova “utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake”? (b) Yehova ‘anatandaje hema lake’ juu ya umati mkubwa?

      25 Na zaidi, wao wamekuwa Mashahidi wenye bidii wa Yehova—“wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.” Je! wewe ni mmoja wa huu umati mkubwa ulio wakfu? Ikiwa ndivyo, ni pendeleo lako kutumikia Yehova bila kuacha katika ua wake wa kidunia wa hekalu lake kubwa la kiroho. Leo, chini ya mwelekezo wa wapakwa-mafuta, umati mkubwa unafanya sehemu iliyo kubwa zaidi ya kazi ya kutoa ushuhuda. Wajapokuwa na madaraka ya kimwili, mamia ya maelfu wanautafutia nafasi ule utumishi wa wakati wote wakiwa mapainia. Lakini uwe wewe ni wa kikundi hicho au la, ukiwa mshiriki aliye wakfu wa umati mkubwa, wewe unaweza kushangilia ukiwa rafiki ya Mungu na mgeni anayekaribishwa katika hema yake. (Zaburi 15:1-5; Yakobo 2:21-26) Hivyo Yehova ‘anatanda hema yake’ juu ya wale ambao wanampenda yeye na, akiwa mkaribishaji-wageni mwema, anawapa himaya.—Mithali 18:10.

      26. Ni baraka gani nyingine utakazofurahia umati mkubwa?

      26 Yule mzee anaendelea: “Wao hawataona njaa tena wala kuona kiu tena, wala jua halitapiga juu yao tena wala joto lolote lenye kuunguza, kwa sababu Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha ufalme, atachunga wao, na ataelekeza wao kwenye vibubujiko vya maji ya uhai. Na Mungu atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao.” (Ufunuo 7:16, 17, NW) Ndiyo, Yehova ni mkaribishaji-wageni kikweli! Lakini kuna maana gani yenye kina kirefu katika maneno haya?

      27. (a) Isaya alitoaje unabii wa jambo linalofanana na maneno ya mzee? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba unabii wa Isaya ulianza kutimizwa juu ya kundi la Kikristo katika siku ya Paulo?

      27 Acheni sisi tufikirie unabii ulio na maneno yanayofanana na hayo: “Hivi ndivyo Yehova amesema: ‘Katika wakati wa nia njema mimi nilijibu wewe, na katika siku ya wokovu mimi nimekusaidia wewe . . . Wao hawataenda njaa, wala hawataenda kiu, wala joto lenye kukausha au jua halitapiga wao. Kwa kuwa Mmoja ambaye ana sikitikio juu yao ataendesha wao, na kando ya chemchemi za maji yeye ataongoza wao.’” (Isaya 49:8, 10, NW; ona pia Zaburi 121:5, 6.) Mtume Paulo alinukuu sehemu ya unabii huu na akautumia kuhusu “siku ya wokovu” iliyoanza Pentekoste 33 W.K. Yeye aliandika: “Kwa maana yeye [Yehova] asema: ‘Katika wakati uliokubalika mimi nilisikia wewe, na katika siku ya wokovu mimi nilisaidia wewe.’ Tazama! Sasa ndio hasa wakati uliokubalika. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”—2 Wakorintho 6:2, NW.

      28, 29. (a) Maneno ya Isaya yalitimizwaje katika karne ya kwanza? (b) Maneno ya Ufunuo 7:16 yanatimizwaje kwa habari ya umati mkubwa? (c) Ni nini litakalokuwa tokeo la kuelekezwa kwa umati mkubwa kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai”? (d) Ni kwa nini umati mkubwa utakuwa usio na kifani miongoni mwa aina ya binadamu?

      28 Ile ahadi ya kutoona njaa au kiu au kutaabishwa na joto lenye kukausha ilitumikaje wakati huo huko nyuma? Hakika, Wakristo katika karne ya kwanza walitaabishwa na njaa na kiu halisi nyakati nyingine. (2 Wakorintho 11:23-27) Ingawa hivyo, katika maana ya kiroho, wao walikuwa na chakula tele. Wao waliandaliwa kwa wingi hivi kwamba wao hawakwenda njaa au kiu kwa vitu vya kiroho. Zaidi ya hilo, Yehova hakuruhusu joto la kasirani yake liwake dhidi yao wakati yeye alipoharibu mfumo wa mambo wa Kiyahudi katika 70 W.K. Maneno ya Ufunuo 7:16 yana utimizo wa kiroho unaofanana na huo kwa ajili ya umati mkubwa leo. Pamoja na Wakristo wapakwa-mafuta, wao wanafurahia wingi wa maandalizi ya kiroho.—Isaya 65:13; Nahumu 1:6, 7.

      29 Ikiwa wewe ni mmoja wa ule umati mkubwa, hali yako njema ya moyo itakufanya wewe “upige kilio kikuu kwa shangwe,” si kitu ulazimike kuvumilia nini kwa habari ya manyimo na mikazo wakati wa miaka hii ya gizagiza ya mfumo wa Shetani. (Isaya 65:14, NW) Katika maana hiyo, hata sasa, Yehova anaweza ‘kupangusa kabisa kila chozi kutoka macho yako.’ “Jua” lenye joto jingi la Mungu au hukumu mbaya halikutishi wewe tena, na pepo nne za uharibifu ziachiliwapo, huenda wewe ukakingwa na “joto lenye kuunguza” la kutopendezwa kwa Yehova. Baada ya uharibifu huo kwisha, yule Mwana-Kondoo atakuelekeza wewe unufaishwe kikamili na “vibubujiko vya maji ya uhai” vyenye kutia uhai mpya, hivyo vikiwa vinawakilisha maandalizi yote ambayo Yehova anakufanyia wewe upate uhai wa milele. Imani yako katika damu ya Mwana-Kondoo itatetewa katika maana ya kwamba wewe utainuliwa polepole ufikie ukamilifu wa kibinadamu. Nyinyi wa umati mkubwa mtakuwa bila kifani miongoni mwa aina ya binadamu mkiwa yale “mamilioni” ambayo hayakulazimika hata kufa! Katika maana iliyo kamili zaidi, kila chozi litakuwa limekwisha panguswa kabisa kutoka macho yenu.—Ufunuo 21:4.

      Kufanya Ule Mwito Uwe Hakika

      30. Ni mandhari gani nzuri mno inayofunguka kwetu katika njozi ya Yohana, na ni nani ambaye ataweza “kusimama”?

      30 Lo! maneno haya yanatufungulia mandhari nzuri mno kama nini! Yehova mwenyewe yu katika kiti cha ufalme chake, na watumishi wake wote, wa kimbingu na wa kidunia, wanaungana katika kumsifu yeye. Watumishi wake wa kidunia wanathamini ni pendeleo lenye kutia hofu kama nini walilo nalo kushiriki katika hii korasi ya sifa inayoongezeka. Karibuni sana, Yehova na Kristo Yesu watatekeleza hukumu, nacho kilio hiki kitasikika: “Siku kubwa ya hasira-kisasi yao imekuja, na ni nani anaweza kusimama?” (Ufunuo 6:17, NW) Na jibu? Ni sehemu ndogo tu ya aina ya binadamu, kutia na wowote kati ya 144,000 waliotiwa muhuri ambao huenda wangali wanabaki katika mnofu na umati mkubwa wa kondoo wengine ndio ‘watasimama,’ yaani, wataokoka pamoja nao.—Yeremia 35:19; 1 Wakorintho 16:13.

      31. Utimizo wa njozi ya Yohana wapasa uathirije Wakristo, wa wapakwa-mafuta na wa ule umati mkubwa pia?

      31 Kwa sababu ya uhakika huu, Wakristo wapakwa-mafuta wa jamii ya Yohana hujipinda wenyewe kisulubu katika ‘kufuatilia kuteremka kuelekea mradi kwa ajili ya tuzo la mwito wa kuelekea juu wa Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.’ (Wafilipi 3:14, NW) Wao wanafahamu kabisa kwamba matukio wakati wa siku hizi hutaka uvumilivu wa pekee upande wao. (Ufunuo 13:10) Baada ya kutumikia Yehova kishikamanifu kwa miaka mingi, wao wanashikilia sana imani, wakishangilia kwamba majina yao “yamechorwa katika mbingu.” (Luka 10:20; Ufunuo 3:5, NW) Wale wa umati mkubwa vilevile wanajua kwamba ni “yeye ambaye amevumilia hadi mwisho ndiye ambaye ataokolewa.” (Mathayo 24:13, NW) Ingawa umati mkubwa ukiwa kikundi umetiwa alama utoke katika dhiki kubwa, watu mmoja mmoja wa huo lazima wajipinde wenyewe wabaki wakiwa safi na wenye kutenda.

      32. Ni hali gani yenye umuhimu inayokaziwa na uhakika wa kwamba ni vikundi viwili tu ndivyo vitaweza “kusimama” katika siku ya hasira-kisasi ya Yehova?

      32 Hakuna ithibati kwamba yeyote kando na hivi vikundi viwili ‘atasimama’ katika siku ya hasira-kisasi ya Yehova. Hii humaanisha nini kwa yale mamilioni ambayo kila mwaka huonyesha staha fulani kwa dhabihu ya Yesu kwa kuhudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo chake lakini ambao bado hawajajizoeza imani katika dhabihu ya Yesu kufikia hatua ya kuwa watumishi wa Yehova walio wakfu na waliobatizwa, wenye kutenda katika utumishi wake? Na zaidi, namna gani wale ambao hapo zamani walikuwa watendaji lakini ambao wameruhusu mioyo yao ‘ilemewe na mahangaikio ya maisha?’ Wote hao na waamke, na wakae wakiwa macho, ili ‘wafaulu katika kuponyoka mambo hayo yote ambayo yamekusudiwa yatukie na katika kusimama mbele ya Mwana wa binadamu’—Yesu Kristo. Wakati ni mfupi!—Luka 21:34-36, NW.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      b The Watch Tower, Aprili 1, 1918, ukurasa 98.

      c Kihalisi, “katika mbele ya yeye,” The Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures.

  • Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 121]

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki