Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na wakati wao waona jinsi hayawani-mwitu alikuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo, wale ambao hukaa juu ya dunia watastaajabu kwa kusifu mno, lakini majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” (Ufunuo 17:8b, NW)

  • Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 8, 9. (a) Ni kwa nini UM hauna jawabu kwa matatizo ya ulimwengu, nao utapatwa na nini kulingana na amri ya Mungu? (b) Ni kwa nini waasisi na wasifaji wa UM hawakuandikisha majina yao katika “hati-kunjo ya uhai” ya Mungu? (c) Ufalme wa Yehova utatimiza jambo gani kwa kufaulu?

      8 UM hauna jawabu. Na kwa nini? Kwa sababu Mpaji uhai wa aina ya binadamu yote siye mpaji-uhai wa UM. Urefu wa maisha yao utakuwa mfupi, kwa kuwa kulingana na amri ya Mungu, ‘wapaswa kwenda zao ndani ya uharibifu.’ Waasisi na wasifaji mno wa UM hawakuandikisha majina yao katika hati-kunjo ya uhai ya Mungu. Watu wenye dhambi, wenye kufa, wengi wao wakiwa wadhihaki wa jina la Mungu, wangewezaje kufanikiwa kupata kupitia UM kitu ambacho Yehova Mungu amejulisha wazi kwamba yeye yu karibu kutimiza, si kwa njia za kibinadamu, bali kupitia Ufalme wa Kristo wake?—Danieli 7:27; Ufunuo 11:15.

      9 Kwa kweli UM ni kitu bandia chenye makufuru cha Ufalme wa Kimesiya wa Mungu kupitia Yesu Kristo, Mwana-Mfalme wa Amani wake—ambaye utawala wake wa kifalme hautakuwa na mwisho. (Isaya 9:6, 7, NW) Hata kama UM ungeweza kutiatia kama viraka amani fulani ya kitambo, vita vingefyatuka tena. Hiyo ni asili ya watu wenye dhambi. “Majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” Ufalme wa Yehova kupitia Kristo hautasimamisha tu amani ya milele duniani bali, juu ya msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu, utainua wafu, waadilifu na wasio waadilifu ambao wamo katika kumbukumbu la Mungu. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Hii inatia ndani kila mmoja ambaye amebaki akiwa imara ijapokuwa mashambulizi ya Shetani na mbegu yake, na wengine ambao wangali watajionyesha wenyewe kuwa watiifu. Kwa wazi, hati-kunjo ya uhai ya Mungu haitakuwa kamwe na majina ya wafuasi washupavu wa Babuloni Mkubwa au ya wowote wanaoendelea kuabudu hayawani-mwitu.—Kutoka 32:33, NW; Zaburi 86:8-10; Yohana 17:3; Ufunuo 16:2; 17:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki