-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na katika kiti cha ufalme zinatoka meme na sauti na ngurumo.” (Ufunuo 4:5a, NW) Lo! jinsi inavyokumbusha madhihirisho mengine yenye kutia hofu ya uwezo wa kimbingu wa Yehova! Mathalani, wakati Yehova ‘aliposhuka’ juu ya Mlima Sinai, Musa aliripoti hivi: “Katika siku ya tatu wakati ilipokuwa asubuhi, ikawa kwamba ngurumo na meme zikaanza kutukia, na wingu zito juu ya mlima na sauti kubwa sana ya pembe. . . . Wakati sauti ya pembe iliendelea kuwa kubwa zaidi na zaidi, Musa akaanza kunena, na Mungu wa kweli akaanza kujibu yeye kwa sauti.”—Kutoka 19:16-19, NW.
-
-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
14. Sauti zimevumaje leo?
14 Namna gani zile sauti? Wakati wa kushuka kwa Yehova juu ya Mlima Sinai, sauti ilinena kwa Musa. (Kutoka 19:19) Sauti kutoka mbinguni zilitoa nyingi za zile amri na mbiu katika kitabu cha Ufunuo. (Ufunuo 4:1; 10:4, 8; 11:12; 12:10; 14:13; 16:1, 17; 18:4; 19:5; 21:3) Leo, Yehova ametoa pia amri na mbiu kwa watu wake, akimulikia kuelewa kwao unabii na kanuni za Biblia. Habari yenye kutoa nuru ya elimu mara nyingi imejulishwa kwenye mikusanyiko ya kimataifa, kisha, mbiu ya kweli hizo za Biblia imepigwa ulimwenguni pote. Mtume Paulo alisema hivi juu ya wahubiri waaminifu wa habari njema: “Kwani, kwa hakika, ‘katika dunia yote mvumo wao ulitoka ukaenda, na kwenye ncha za dunia inayokaliwa matamko yao.’”—Warumi 10:18, NW.
-