Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, kusema: ‘Ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, yeye ambaye alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake!’” (Ufunuo 14:8, NW)

  • “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 3. Inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka?

      3 Huenda ukauliza, ‘Kwa kuwa dini ingali inatumia uvutano mkubwa katika dunia, kwa nini malaika anatangaza kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka?’ Basi, kulitokea nini baada ya 539 K.W.K. wakati Babuloni la kale lilipoanguka? Kwani, Israeli aliwekwa huru arudi kwenye bara la nyumbani kwake na kurudisha ibada ya kweli kule! Kwa hiyo urudisho wa Israeli wa kiroho katika 1919 kwenye ufanisi wa kiroho wenye kung’aa, ambao unaendelea na kupanuka hadi leo hii, unasimama ukiwa ithibati kwamba Babuloni Mkubwa alianguka mwaka huo. Yeye hana nguvu tena za kuzuia watu wa Mungu. Zaidi, yeye ameingia katika matata yenye kina ndani yake mwenyewe. Tangu 1919 ufisadi, utovu wa haki, na utovu wa adili wake umefunuliwa sana. Katika sehemu kubwa ya Ulaya watu wachache ndio huenda kanisani, na baadhi ya mabara ya kisoshalisti, dini inaonwa kuwa “kasumba ya watu.” Akiwa ameaibishwa machoni pa wote wapendao Neno la Mungu la ukweli, sasa Babuloni Mkubwa, ni kana kwamba yu kwenye mstari wa kifo, akingojea Yehova atekeleze juu yake hukumu yake ya uadilifu.

      Anguko Lenye Aibu la Babuloni

      4-6. Ni jinsi gani “Babuloni Mkubwa . . . alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake”?

      4 Acheni tuchunguze kirefu zaidi hali zenye kuzunguka anguko lenye aibu la Babuloni Mkubwa. Malaika anatuambia hapa kwamba “Babuloni Mkubwa . . . alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake.” Hii humaanisha nini? Huhusiana na ushindi. Mathalani, Yehova alimwambia Yeremia: “Chukua kikombe hiki cha divai ya hasira-kali kutoka mkono wangu, na wewe lazima ufanye mataifa yote ambayo kwayo mimi ninatuma wewe yanywe hicho. Na wao lazima wanywe na kuyumbayumba na kutenda kama watu wenye kichaa kwa sababu ya upanga ambao mimi ninapeleka miongoni mwao.” (Yeremia 25:15, 16, NW) Katika karne ya sita na ya saba K.W.K, Yehova alitumia Babuloni ya kale kumwaga kikombe cha ufananisho cha dhiki kwa ajili ya mataifa mengi yanywe kutia na Yuda yenye kuasi imani, hivi kwamba hata watu wake mwenyewe walipelekwa katika uhamisho. Kisha, kwa zamu yayo, Babuloni ikaanguka kwa sababu ya mfalme wayo kujitukuza mwenyewe dhidi ya Yehova, “Bwana ya zile mbingu.”—Danieli 5:23, NW.

      5 Babuloni Mkubwa amefanya ushindi mwingi, lakini kwa sehemu iliyo kubwa, huo umekuwa wa werevu zaidi. Yeye ‘amefanya mataifa yote yanywe’ kwa kutumia ujanja wa kahaba, kufanya uasherati wa kidini pamoja nao. Yeye ametongoza watawala wa kisiasa waingie ndani ya mafungamano na urafiki pamoja naye. Kupitia vivuta-macho vya kidini, yeye amefanya njama ya uonevu wa kisiasa, wa kibiashara na wa kiuchumi. Yeye amechochea minyanyaso ya kidini na vita na krusedi, pamoja na vita vya kitaifa, kwa sababu tu za kisiasa na za kiuchumi. Naye ametakasa vita hivyo kwa kusema eti ni mapenzi ya Mungu.

      6 Kujiingiza kwa dini katika vita na siasa za karne ya 20 ni jambo linalojulikana na watu wote—kama katika Japani ya Shinto, India ya Hindu, Vietnamu ya Kibudha, Ailandi Kaskazini ya Ukristo” Amerika ya Kilatini, na nyinginezo—bila kusahau wale makasisi wa kijeshi pande zote mbili za vita viwili vya ulimwengu katika kuhimiza wanaume vijana wachinjane. Kielelezo kimoja bora cha kujiingiza kwa Babuloni Mkubwa ni hisa aliyokuwa nayo katika Vita ya Hispania ya Wenyewe kwa Wenyewe ya 1936-39, ambayo katika hiyo angalau watu 600,000 waliuawa. Umwagaji-damu huu ulichochewa na waungaji-mkono wa viongozi wa kidini Wakatoliki na wafungamani wao, kwa sehemu, kwa sababu ukwasi na cheo cha kanisa vilitishwa na serikali halali ya Hispania.

      7. Ni nani ambaye amekuwa shabaha kuu ya Babuloni Mkubwa, naye ametumia njia zipi dhidi ya shabaha hii?

      7 Kwa kuwa Babuloni Mkubwa ndiyo sehemu ya kidini ya mbegu ya Shetani, sikuzote yeye amefanya “mwanamke” wa Yehova “Yerusalemu juu,” kuwa shabaha yake kuu. Katika karne ya kwanza, kundi la Wakristo wapakwa-mafuta lilitambulishwa waziwazi kuwa mbegu ya mwanamke. (Mwanzo 3:15; Wagalatia 3:29; 4:26, NW) Babuloni Mkubwa alijaribu sana kushinda kundi hilo safi kwa kulitongoza lifanye uasherati wa kidini. Mitume Paulo na Petro walionya kwamba wengi wangeshindwa na uasi-imani mkubwa ungetokea. (Matendo 20:29, 30; 2 Petro 2:1-3) Jumbe za Yesu kwa makundi saba zilionyesha kwamba kuelekea mwisho wa maisha ya Yohana, Babuloni Mkubwa alikuwa akifanya maendeleo fulani katika jitihada zake za kufisidi. (Ufunuo 2:6, 14, 15, 20-23) Lakini Yesu alikuwa tayari ameonyesha kadiri ambayo angeruhusiwa afike.

      Ngano na Magugu

      8, 9. (a) Fumbo la maneno la Yesu kuhusu ngano na magugu lilionyesha nini? (b) Ikawaje “wakati watu walikuwa wakilala”?

      8 Katika fumbo la maneno lake la ngano na magugu, Yesu alisema juu ya mtu ambaye alipanda mbegu nzuri katika shamba lake. Lakini “wakati watu walikuwa wakilala,” adui alikuja akapanda magugu kwa wingi. Kwa sababu hiyo, ngano ikaja kufichwa na magugu. Yesu alifafanua fumbo la maneno lake kwa maneno haya: “Mpanzi wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu; shamba ni ulimwengu; kwa habari ya mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme; lakini magugu ni wana wa mwovu, na adui aliyeyapanda ni Ibilisi.” Kisha akaonyesha kwamba “mbegu nzuri” na “magugu” vingeruhusiwa vikue pamoja mpaka “umalizio wa mfumo wa mambo,” wakati malaika ‘wangekusanya ili kuondoa’ magugu ya ufananisho.—Mathayo 13:24-30, 36-43, NW.

      9 Walichoonya Yesu na mitume Paulo na Petro kikawako. “Wakati watu walikuwa wakilala,” ama baada ya mitume kulala usingizi katika kifo ama wakati waangalizi Wakristo waliposinzia katika kulinda kondoo za Mungu, uasi-imani wa Kibabuloni ulichipuka mle mle ndani ya kundi. (Matendo 20:31) Upesi magugu yakazidi wingi wa ngano na kuificha isionekane. Kwa karne kadhaa huenda ikawa ilionekana kwamba mbegu ya mwanamke ilikuwa imefunikwa kabisa na marinda makubwa ya Babuloni Mkubwa.

      10. Ni nini kilichotukia kufikia miaka ya 1870, naye Babuloni Mkubwa alitendaje kuitikia hilo?

      10 Kufikia miaka ya 1870 Wakristo wapakwa-mafuta walianza kufanya jitihada za bidii wajiondoe wenyewe kutoka ushirika wa njia za kikahaba za Babuloni Mkubwa. Wao waliachana na mafundisho bandia ambayo Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imeingiza kutoka upagani na kwa ujasiri wakatumia Biblia katika kuhubiri kwamba majira ya Mataifa yangekwisha 1914. Chombo kikuu cha Babuloni Mkubwa, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, kilipinga vichocheo hivi vya kurudisha ibada ya kweli. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza wao walitumia kwa faida yao ukichaa wa wakati wa vita wakajaribu kufutilia mbali kikundi hicho kidogo cha Wakristo waaminifu. Katika 1918, wakati utendaji wao ulikuwa karibu umekomeshwa kabisa, ilionekana kama Babuloni Mkubwa alikuwa amefaulu. Alionekana kama amewashinda.

      11. Ni nini kilichotokezwa na anguko la Babuloni wa kale?

      11 Kama tulivyoona wakati uliopita, jiji la Babuloni lenye kiburi lilipatwa na anguko la nguvu lenye msiba katika 539 K.W.K. Ndipo kilio hiki kikasikika: “Ameanguka! Babuloni ameanguka!” Kiti kikubwa cha milki ya ulimwengu kilikuwa kimeanguka kwa majeshi ya Umedi na Uajemi chini ya Sairasi Mkuu. Ijapokuwa jiji lenyewe liliokoka ushindi huo, anguko la nguvu zalo lilikuwa halisi, na lilitokeza kuachiliwa kwa mateka walo Wayahudi. Walirudi Yerusalemu wakarudishe ibada safi kule.—Isaya 21:9; 2 Nyakati 36:22, 23; Yeremia 51:7, 8.

      12. (a) Katika nyakati zetu, inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova amekatalia mbali kabisa Jumuiya ya Wakristo?

      12 Katika nyakati zetu pia kilio kimesikika kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka! Ufaulu wa kitambo wa Jumuiya ya Wakristo ya Kibabuloni katika 1918 uligeuzwa upesi sana katika 1919 wakati baki la wale wapakwa-mafuta, jamii ya Yohana, liliporudishwa kupitia ufufuo wa kiroho. Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka kwa habari ya kuwa na uwezo wa kushikilia mateka ya watu wa Mungu. Kama nzige, ndugu wapakwa-mafuta wa Kristo walitoka mabumba-mabumba katika abiso, wakiwa tayari kwa tendo. (Ufunuo 9:1-3; 11:11, 12, NW) Wao walikuwa ndiye “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu” wa ki-siku-hizi, na Bwana-Mkubwa aliwaweka rasmi juu ya mali yake yote duniani. (Mathayo 24:45-47, NW) Kutumiwa kwao katika njia hii kulithibitisha kwamba Yehova alikuwa ametupilia mbali kabisa Jumuiya ya Wakristo lijapokuwa dai layo la kuwa ndiyo mwakilishi wake duniani. Ibada safi iliimarishwa tena, na njia ilifunguliwa kwa kazi ya kukamilisha kutia muhuri baki la wale 144,000—wabakio wa mbegu ya mwanamke, adui wa zamani wa Babuloni Mkubwa. Yote haya yaliashiria ushinde wenye kuponda-ponda wa hilo tengenezo la kidini la kishetani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki