-
Endeleeni Kuutafuta Kwanza “Uadilifu Wake”Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
-
-
Hatari ya Kujiona Wenyewe Kuwa Waadilifu
5. Tunapaswa kuepuka hatari gani?
5 Akiwaandikia Wakristo huko Roma, mtume Paulo alikazia hatari ambayo sisi sote tunahitaji kuepuka ikiwa tunataka kufanikiwa katika kuutafuta kwanza uadilifu wa Mungu. Paulo alisema hivi kuhusu Wayahudi wenzake: “Nawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi; kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu bali wakitafuta kujiwekea uadilifu wao wenyewe, hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.” (Rom. 10:2, 3) Kulingana na Paulo, waabudu hao hawakuelewa uadilifu wa Mungu kwa sababu walikuwa na bidii sana wakijaribu kujiwekea viwango vyao wenyewe vya uadilifu.a
6. Tunapaswa kuepuka mtazamo gani, na kwa nini?
6 Njia moja ambayo tunaweza kuanguka katika mtego huo ni kuuona utumishi wetu kwa Yehova kuwa mashindano, tukijilinganisha na wengine. Mtazamo huo unaweza kwa urahisi kutufanya tujitumaini kupita kiasi kwa sababu ya uwezo wetu. Lakini kwa kweli, tukitenda hivyo, tutakuwa tunausahau uadilifu wa Yehova. (Gal. 6:3, 4) Nia nzuri ambayo inapaswa kutuchochea kufanya mambo yanayofaa ni upendo wetu kwa Yehova. Tukijaribu kwa njia yoyote ile kuthibitisha uadilifu wetu wenyewe tutakuwa tukipinga dai letu la kwamba tunampenda Yehova.—Soma Luka 16:15.
-
-
Endeleeni Kuutafuta Kwanza “Uadilifu Wake”Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
-
-
a Kulingana na msomi mmoja, neno la lugha ya awali ambalo lilitafsiriwa kuwa “kujiwekea” linaweza pia kumaanisha ‘kusimamisha mnara wa ukumbusho.’ Hivyo, Wayahudi hao kwa kweli walikuwa wakisimamisha mnara wa mfano wa ukumbusho ili wajiletee sifa badala ya kumletea Mungu sifa.
-