-
Tumeimarishwa Kukataa Kutenda KosaMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 1
-
-
Yesu alisema: “Ingieni kupitia lango jembamba; kwa sababu ni pana na yenye nafasi barabara inayoongoza kuingia katika uharibifu, na wengi ndio wanaoingia kupitia hiyo; lakini lango ni jembamba na barabara ni yenye kufinyana inayoongoza kuingia katika uhai, na wachache ndio wanaoipata.”—Mathayo 7:13, 14.
-
-
Tumeimarishwa Kukataa Kutenda KosaMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 1
-
-
Lakini, kwa nini Yesu alisema kwamba ni wachache tu waliochagua barabara iliyofinyana? Hasa kwa sababu ni wachache tu wanaotaka sheria za Mungu na kanuni zake ziongoze maisha zao na kuwasaidia kukinza vishawishi vingi na fursa zinazowakabili za kutenda kosa. Tena, ni wachache tu kwa kulinganisha ambao wako tayari kukinza tamaa mbaya, msongo wa marika, hofu ya kwamba huenda wakadhihakiwa kwa sababu ya njia ambayo wameamua kufuata.—1 Petro 3:16; 4:4.
-