Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Mchungaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • 13. Daudi anazungumzaje kwa hisia nyingi zaidi kwenye Zaburi 23:4, na kwa nini hilo halishangazi?

      13 Daudi anataja sababu ya pili iliyomfanya awe na uhakika: Yehova huwalinda kondoo wake. Tunasoma hivi: “Hata ingawa nitatembea katika bonde lenye kivuli kizito, siogopi chochote kibaya, kwa maana wewe uko pamoja nami; fimbo yako na gongo lako ndivyo vitu vinavyonifariji.” (Zaburi 23:4) Sasa Daudi anazungumza kwa hisia nyingi zaidi, akiongea na Yehova kwa kutumia neno “wewe.” Hilo halishangazi kwa kuwa Daudi anazungumzia jinsi Mungu alivyomsaidia kuvumilia matatizo. Daudi alikuwa amepitia mabonde mengi yenye giza, yaani, uhai wake ulipokuwa hatarini. Lakini hakuruhusu woga umtawale, kwa kuwa alihisi kwamba Mungu, akiwa tayari na “fimbo” na “gongo” Lake, alikuwa pamoja naye. Bila shaka, Daudi alifarijika kujua kwamba analindwa na hivyo akamkaribia Yehova zaidi.b

  • Yehova Ni Mchungaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • 15, 16. (a) Yehova hutusaidia kwa njia gani kushughulikia matatizo ambayo huenda tukakabili? (b) Toa mfano unaoonyesha jinsi Yehova anavyotusaidia wakati wa majaribu.

      15 Yehova haahidi kuingilia kati kimuujiza.c Lakini tunaweza kuwa na uhakika wa jambo hili: Yehova atatusaidia tushinde tatizo lolote ambalo huenda tukakabili. Anaweza kutupa hekima ya kukabili “majaribu ya namna mbalimbali.” (Yakobo 1:2-5) Mbali na kutumia fimbo au gongo lake kuwafukuza wawindaji, mchungaji huzitumia pia kuwaelekeza kondoo kwa wororo upande unaofaa. Yehova anaweza “kutuelekeza kwa wororo,” labda kupitia mwabudu mwenzetu, ili tutumie shauri la Biblia ambalo linaweza kutusaidia sana. Isitoshe, Yehova anaweza kutupa nguvu za kuvumilia. (Wafilipi 4:13) Kupitia roho yake takatifu, anaweza kutupa “nguvu zinazopita zile za kawaida.” (2 Wakorintho 4:7) Roho ya Mungu inaweza kutusaidia kuvumilia jaribu lolote ambalo huenda Shetani akatuletea. (1 Wakorintho 10:13) Je, haifariji kujua kwamba sikuzote Yehova yuko tayari kutusaidia?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki