Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Rumania
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Waangalizi Wanaosafiri Wazoezwa

      Roberto Franceschetti na Andrea Fabbi kutoka ofisi ya tawi ya Italia walitumwa Rumania mwaka wa 1990 kwa kusudi la kusaidia kupanga upya kazi. Ndugu Franceschetti anasema: “Nilikuwa na miaka 57, na hali ya uchumi haikuwa nzuri nchini Rumania wakati huo, kwa hiyo, ilikuwa vigumu kwangu na kwa mke wangu Imelda kuzoea maisha nchini humo.

      “Tulipofika Bucharest saa 1:00 jioni, Desemba 7, 1990, halijoto ilikuwa nyuzi 12 Selsiasi chini ya kiwango cha kuganda na theluji ilitanda kotekote jijini. Tulikutana na ndugu fulani katikati ya jiji na tukawauliza kuhusu mahali pa kulala. Walisema: ‘Hatujui bado.’ Lakini mwanamke kijana ambaye mama na nyanya yake ni Mashahidi alisikia mazungumzo yetu na akatukaribisha mara moja nyumbani kwake. Tulikaa kwake kwa majuma kadhaa hadi tulipopata makao yanayofaa jijini. Ndugu wenyeji walitutia moyo, na hilo lilitusaidia kuzoea hali hizo mpya.”

      Roberto, aliyehitimu darasa la 43 la Shule ya Gileadi mwaka wa 1967, alikaa Rumania pamoja na mke wake kwa miaka tisa hivi, na ndugu walinufaika sana kutokana na uzoefu wao katika utumishi wa Yehova. Roberto anasema: “Mnamo Januari 1991, Halmashauri ya Nchi ilipanga mkutano pamoja na waangalizi wote 42 wanaosafiri. Mizunguko mingi ilikuwa na makutaniko sita au saba tu. Waangalizi walikuwa wakitumia siku nne kwa ajili ya kila ziara katika makutaniko, yaani, miisho ya juma miwili. Kwa kawaida hawakuandamana na wake zao. Nyakati hizo waangalizi wa mzunguko walikuwa wakifanya kazi ya kujiruzuku ili wasishukiwe na wenye mamlaka. Lakini sasa ndugu hao wangeweza kufuata ratiba ileile ya waangalizi katika nchi nyingine na kutembelea makutaniko kuanzia Jumanne hadi Jumapili.

      “Baada ya kueleza mpango huo niliwaambia wale ndugu 42 hivi: ‘Ikiwa mnataka kuendelea kuwa waangalizi wa mzunguko, tafadhali inueni mikono.’ Hakuna hata mmoja aliyeinua mkono! Papo hapo tukapoteza waangalizi wote wanaosafiri nchini mwetu! Hata hivyo, baada ya kusali na kutafakari kuhusu jambo hilo, baadhi yao walikubali kuendelea. Ndugu ambao walikuwa wamehitimu Shule ya Mazoezi ya Kihuduma kutoka Austria, Italia, Marekani, Ufaransa, na Ujerumani, walikuja kusaidia pia.”

  • Rumania
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 152]

      Roberto na Imelda Franceschetti

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki