-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwishoni mwa miaka ya 1800, Warumania wengi walihamia nchi nyingine ili watafute kazi kwa sababu ya hali ngumu za kijamii na za kiuchumi nchini kwao, na baadhi yao walienda Marekani. Mbali na faida za kimwili, wengine kati yao walipata ujuzi sahihi wa kweli ya Biblia. Károly Szabó na József Kiss ni baadhi yao. Wanaume hao walipendezwa na mambo ya kiroho na walisikiliza hotuba kadhaa za Biblia zilizotolewa na Ndugu Russell.
Ndugu Russell alitambua kwamba wanaume hao wawili walipendezwa kikweli na Biblia naye akajitambulisha na kuongea nao. Walipokuwa wakizungumza aliwapendekezea Károly na József warudi Rumania wakawaeleze watu wao wa ukoo na marafiki wao kuhusu Ufalme. Wote wawili walikubali na wakasafiri kwa meli hadi Rumania mwaka wa 1911. Waliamua kwenda kuishi mjini Tirgu-Mures huko Transylvania.
-
-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 69]
Károly Szabó na József Kiss walirudi nchini kwao mwaka wa 1911, ili wahubiri ujumbe wa Ufalme
-