-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndugu walifanya makusanyiko mengi huko Baia-Mare, Cluj-Napoca, Tirgu-Mures, na Ocna Mureş, na mamia ya Mashahidi na watu waliopendezwa wakahudhuria. Ubatizo ndilo jambo lililovutia hasa kwenye kusanyiko lililofanywa Baia-Mare, mnamo Juni 1945, nao ulifanywa kwenye mto uliokuwa umbali wa kilometa kumi kutoka mji huo. Baada ya hotuba kutolewa katika bustani ya ndugu fulani, watu 118 walibatizwa katika Mto Lăpuşul, karibu na bustani hiyo. Ubatizo huo katika mazingira hayo mazuri ulikuwa wa pekee sana.
Mjini Tirgu-Mures, ndugu walikodi jumba la maonyesho lililotoshea watu 3,000. Baadhi ya ndugu walitembea kwa miguu na wengine wakasafiri kwa gari-moshi, magari yanayokokotwa na farasi, na baiskeli. Walifika siku iliyotangulia kusanyiko na wengine kati yao wakaanza kuhubiri mara moja na kuwaalika watu kwenye hotuba ya watu wote iliyozungumzia safina ya Noa. Ndugu wengi walitokwa na machozi walipoona kotekote mjini mabango yenye maandishi maridadi yaliyotangaza hotuba. Hawakufikiri kamwe kwamba wangekuwa na uhuru huo wa kuhubiri habari njema!
Jitihada za ndugu zilibarikiwa sana. Watu wengi sana walihudhuria hivi kwamba iliwabidi kuweka vipazasauti viwili nje kwa ajili ya wale ambao hawakupata nafasi ndani ya jumba. Jambo hilo liliwawezesha majirani wengi kusikia hotuba wakiwa kwenye madirisha yao. Wakuu wa mji na watu wengi mashuhuri walialikwa ili wajionee mwenendo wa Mashahidi wa Yehova na kusikiliza mafundisho yao. Jambo la ajabu ni kwamba sehemu iliyotengwa kwa ajili yao ilijaa, na wakajiunga na ndugu kuimba.
-
-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 102]
Kusanyiko la mzunguko huko Baia-Mare mwaka wa 1945
-