-
Rwanda2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Rwanda
RWANDA ni mojawapo ya nchi ndogo zaidi barani Afrika. Pia ni mojawapo ya nchi maridadi sana. Nchi hii inayoitwa Nchi ya Milima Elfu Moja ina milima, misitu, maziwa, na maporomoko ya maji, na vilevile unamna-namna wa mimea na wanyama. Milima mikubwa ya Virunga, iko katika eneo lenye milima lililo katika sehemu ya magharibi inayopakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongoa na katika sehemu ya kaskazini ya Uganda. Mlima Karisimbi, ambao mara nyingi huwa umefunikwa na theluji, ni mlima wa volkano isiyotenda na ndio mrefu zaidi katika safu hii ya milima. Una urefu wa mita 4,480. Sehemu za chini ya milima hiyo, kuna msitu wa mvua wenye mianzi mingi, ambamo tumbili walio katika hatari ya kutoweka hubembea kwa uhuru kwenye matawi na mizabibu. Ni katika mazingira haya yenye miti mingi ambamo pia mojawapo ya hazina zenye thamani nchini Rwanda inapatikana, yaani, sokwe wa milimani.
Mimea ya kipekee na majani yenye kunawiri huenea hadi fuo za Ziwa Kivu na Msitu wa Nyungwe. Kuna sokwe, kima wa rangi nyeusi na nyeupe, na wanyama wengine zaidi ya 70 katika msitu huo. Kuna spishi 270 hivi za miti na karibu spishi 300 za ndege. Vipepeo wengi na okidi huchangia uzuri wa hifadhi hiyo.
Kutoka katikati mwa Msitu wa Nyungwe, kuna kijito cha maji kinachotiririka kuelekea upande wa mashariki. Hatua kwa hatua vijito na mito mingine hujiunga nacho na hatimaye maji yake hutiririka katika Ziwa Viktoria. Kutoka hapo, maji hayo huteremka kwa nguvu na kwa kasi sana ili kuendelea na safari yake ndefu kuelekea upande wa kaskazini kupitia Ethiopia, Sudan, na mwishowe Misri, ambapo yanaingia katika Bahari ya Mediterania. Mto Nile unaoanza ukiwa kijito katika milima yenye miti mingi ya Afrika ya kati, husafiri umbali wa kilomita 6,825 hivi, na hivyo kuufanya Mto huo kuwa mmoja wa mito mirefu zaidi duniani.
-
-
Rwanda2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 166]
Maelezo Mafupi Kuhusu Rwanda
Nchi
Rwanda ina ukubwa wa kilomita 177 tu kutoka kaskazini hadi kusini na kilomita 233 kutoka mashariki hadi magharibi. Nchi hii inakadiriwa kuwa na watu 11,000,000. Hata hivyo, hiyo ni idadi kubwa sana kwa nchi ndogo hivyo. Mji mkuu ni Kigali.
Watu
Wakaaji ni Wahutu, Watutsi, Watwa, Wahindi na Wazungu. Zaidi ya nusu ya idadi ya watu nchini Rwanda ni Wakatoliki zaidi ya robo moja ni Waprotestanti, kutia ndani Waadventisti wengi. Hao wengine ni Waislamu na watu wa imani nyinginezo.
Lugha
Lugha rasmi ni Kinyarwanda, Kiingereza, na Kifaransa. Wanatumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano wanapofanya biashara na watu wa nchi jirani.
Kazi
Wanyarwanda wengi ni wakulima. Kwa sababu mashamba mengi hayana rutuba, wengi hukuza chakula cha kutosha familia zao tu. Mimea inayokuzwa ni pareto—mmea unaotumiwa kutengeneza dawa za kuua wadudu—chai, na vilevile kahawa, ambayo huuzwa nje ya nchi kwa wingi.
Chakula
Vyakula vya msingi vinatia ndani viazi, ndizi, na maharagwe.
Hali ya hewa
Kuna hali nzuri ya hewa licha ya kwamba Rwanda iko karibu na ikweta. Hali ya joto katika maeneo ya nyanda za juu yaliyo ndani zaidi ni wastani wa nyuzi 21 Selsiasi, na inapata mvua ya kadiri kila mwaka.
-
-
Rwanda2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 164, 165]
Kuvua samaki katika Ziwa Kivu
-