-
Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
Biblia inaonyesha kwamba Yosefu na Maria walikuwa maskini. Tunajua namna gani? Kati ya mambo machache ambayo vitabu vya Injili—Mathayo, Marko, Luka, na Yohana—vinatuambia kuhusu wenzi hawa wa ndoa ni kwamba siku 40 baada ya Maria kuzaa, yeye na Yosefu walienda katika hekalu ili kutoa dhabihu iliyohitajiwa, yaani, “njiwa-tetere wawili au hua wachanga wawili.”a (Luka 2:22-24) Walioruhusiwa kutoa dhabihu hiyo ni wale tu waliokuwa maskini sana hivi kwamba hawangeweza kutoa kondoo-dume mchanga. Kwa hiyo, yaelekea kwamba, Yosefu na Maria walijitahidi ili kujiruzuku. Hata hivyo, walifaulu sana kuandaa mazingira ya familia yenye upendo. Bila shaka, walitanguliza mambo ya kiroho maishani.—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.
-
-
Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
a Ndege mmoja alitolewa kuwa toleo la dhambi. (Mambo ya Walawi 12:6, 8) Kwa kuitoa, Maria alionyesha kwamba yeye kama wanadamu wengine wote wasio wakamilifu alikuwa amerithi matokeo ya dhambi ya Adamu, mwanadamu wa kwanza.—Waroma 5:12.
-