-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
George Scipio,g mmoja wa wana wa Tom, anakumbuka mojawapo ya magumu waliyokabili ili kumfikisha kila mtu mikutanoni: “Kulikuwa na magari mawili tu. Njia zilikuwa mbovu na zenye milima mingi, na ni barabara chache tu zilizokuwa nzuri wakati huo. . . . Wengine walianza kutembea mapema asubuhi. Nilibeba watu watatu katika gari langu na kuwaacha mahali fulani barabarani. Waliendelea kutembea, huku nikirudi kuwachukua wengine watatu, na kuwaacha baada ya muda fulani, na kurudi. Mwishowe wote walifika mkutanoni kwa njia hiyo.” Baadaye, ingawa George alikuwa na mke na watoto wanne, alitumikia akiwa painia kwa miaka 14. Watatu kati ya wana wake ni wazee kutanikoni.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
g Masimulizi ya maisha ya George Scipio yalikuwa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi, la Februari 1, 1999, ukurasa wa 25-29.
-