Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Kwa mara ya kwanza, lakini si ya mwisho, Ufunuo unakaza uangalifu juu ya Babuloni Mkubwa. Yeye ni nani? Kama tutakavyoona, yeye ni milki ya tufe lote, yeye ni wa kidini, naye ni mfumo bandia wa Shetani ambao yeye hutumia kupiga vita dhidi ya mbegu ya mwanamke wa Mungu. (Ufunuo 12:17, NW) Babuloni Mkubwa ni mfumo wa ulimwengu mzima wote wa dini bandia. Yeye anatia ndani dini zote ambazo huhifadhi mafundisho na mazoea ya Babuloni la kale na zinazodhihirisha roho yalo.

      2. (a) Ikawaje kwamba dini ya Kibabuloni ikatawanywa kwenye sehemu zote za dunia? (b) Ni kisehemu kipi chenye kutokeza zaidi sana cha Babuloni Mkubwa, nacho kiliibuka lini kikiwa tengenezo lenye nguvu?

      2 Ilikuwa kwenye Babuloni, zaidi ya miaka 4,000 iliyopita, kwamba Yehova akavuruga ndimi za wale ambao wangekuwa wajenzi wa Mnara wa Babeli. Vikundi mbalimbali vya lugha vilitawanywa kwenye miisho ya dunia, vikichukua pamoja navyo itikadi na mazoea ya uasi-imani ambayo ndiyo misingi ya dini zilizo nyingi leo hii. (Mwanzo 11:1-9) Babuloni Mkubwa ndiyo sehemu ya kidini ya tengenezo la Shetani. (Linga Yohana 8:43-47.) Kisehemu chenye kutokeza zaidi sana ni Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani, ambayo iliibuka katika karne ya nne baada ya Kristo, ikiwa tengenezo lenye nguvu, lenye kuasi sheria, likiwa na itikadi na kawaida zinazotokana, si na Biblia, bali sana sana na dini ya Kibabuloni.—2 Wathesalonike 2:3-12.

  • “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Yeye ‘amefanya mataifa yote yanywe’ kwa kutumia ujanja wa kahaba, kufanya uasherati wa kidini pamoja nao. Yeye ametongoza watawala wa kisiasa waingie ndani ya mafungamano na urafiki pamoja naye. Kupitia vivuta-macho vya kidini, yeye amefanya njama ya uonevu wa kisiasa, wa kibiashara na wa kiuchumi. Yeye amechochea minyanyaso ya kidini na vita na krusedi, pamoja na vita vya kitaifa, kwa sababu tu za kisiasa na za kiuchumi. Naye ametakasa vita hivyo kwa kusema eti ni mapenzi ya Mungu.

      6 Kujiingiza kwa dini katika vita na siasa za karne ya 20 ni jambo linalojulikana na watu wote—kama katika Japani ya Shinto, India ya Hindu, Vietnamu ya Kibudha, Ailandi Kaskazini ya Ukristo” Amerika ya Kilatini, na nyinginezo—bila kusahau wale makasisi wa kijeshi pande zote mbili za vita viwili vya ulimwengu katika kuhimiza wanaume vijana wachinjane. Kielelezo kimoja bora cha kujiingiza kwa Babuloni Mkubwa ni hisa aliyokuwa nayo katika Vita ya Hispania ya Wenyewe kwa Wenyewe ya 1936-39, ambayo katika hiyo angalau watu 600,000 waliuawa. Umwagaji-damu huu ulichochewa na waungaji-mkono wa viongozi wa kidini Wakatoliki na wafungamani wao, kwa sehemu, kwa sababu ukwasi na cheo cha kanisa vilitishwa na serikali halali ya Hispania.

      7. Ni nani ambaye amekuwa shabaha kuu ya Babuloni Mkubwa, naye ametumia njia zipi dhidi ya shabaha hii?

      7 Kwa kuwa Babuloni Mkubwa ndiyo sehemu ya kidini ya mbegu ya Shetani, sikuzote yeye amefanya “mwanamke” wa Yehova “Yerusalemu juu,” kuwa shabaha yake kuu. Katika karne ya kwanza, kundi la Wakristo wapakwa-mafuta lilitambulishwa waziwazi kuwa mbegu ya mwanamke. (Mwanzo 3:15; Wagalatia 3:29; 4:26, NW) Babuloni Mkubwa alijaribu sana kushinda kundi hilo safi kwa kulitongoza lifanye uasherati wa kidini. Mitume Paulo na Petro walionya kwamba wengi wangeshindwa na uasi-imani mkubwa ungetokea. (Matendo 20:29, 30; 2 Petro 2:1-3) Jumbe za Yesu kwa makundi saba zilionyesha kwamba kuelekea mwisho wa maisha ya Yohana, Babuloni Mkubwa alikuwa akifanya maendeleo fulani katika jitihada zake za kufisidi. (Ufunuo 2:6, 14, 15, 20-23) Lakini Yesu alikuwa tayari ameonyesha kadiri ambayo angeruhusiwa afike.

      Ngano na Magugu

      8, 9. (a) Fumbo la maneno la Yesu kuhusu ngano na magugu lilionyesha nini? (b) Ikawaje “wakati watu walikuwa wakilala”?

      8 Katika fumbo la maneno lake la ngano na magugu, Yesu alisema juu ya mtu ambaye alipanda mbegu nzuri katika shamba lake. Lakini “wakati watu walikuwa wakilala,” adui alikuja akapanda magugu kwa wingi. Kwa sababu hiyo, ngano ikaja kufichwa na magugu. Yesu alifafanua fumbo la maneno lake kwa maneno haya: “Mpanzi wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu; shamba ni ulimwengu; kwa habari ya mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme; lakini magugu ni wana wa mwovu, na adui aliyeyapanda ni Ibilisi.” Kisha akaonyesha kwamba “mbegu nzuri” na “magugu” vingeruhusiwa vikue pamoja mpaka “umalizio wa mfumo wa mambo,” wakati malaika ‘wangekusanya ili kuondoa’ magugu ya ufananisho.—Mathayo 13:24-30, 36-43, NW.

      9 Walichoonya Yesu na mitume Paulo na Petro kikawako. “Wakati watu walikuwa wakilala,” ama baada ya mitume kulala usingizi katika kifo ama wakati waangalizi Wakristo waliposinzia katika kulinda kondoo za Mungu, uasi-imani wa Kibabuloni ulichipuka mle mle ndani ya kundi. (Matendo 20:31) Upesi magugu yakazidi wingi wa ngano na kuificha isionekane. Kwa karne kadhaa huenda ikawa ilionekana kwamba mbegu ya mwanamke ilikuwa imefunikwa kabisa na marinda makubwa ya Babuloni Mkubwa.

      10. Ni nini kilichotukia kufikia miaka ya 1870, naye Babuloni Mkubwa alitendaje kuitikia hilo?

      10 Kufikia miaka ya 1870 Wakristo wapakwa-mafuta walianza kufanya jitihada za bidii wajiondoe wenyewe kutoka ushirika wa njia za kikahaba za Babuloni Mkubwa. Wao waliachana na mafundisho bandia ambayo Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imeingiza kutoka upagani na kwa ujasiri wakatumia Biblia katika kuhubiri kwamba majira ya Mataifa yangekwisha 1914. Chombo kikuu cha Babuloni Mkubwa, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, kilipinga vichocheo hivi vya kurudisha ibada ya kweli. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza wao walitumia kwa faida yao ukichaa wa wakati wa vita wakajaribu kufutilia mbali kikundi hicho kidogo cha Wakristo waaminifu. Katika 1918, wakati utendaji wao ulikuwa karibu umekomeshwa kabisa, ilionekana kama Babuloni Mkubwa alikuwa amefaulu. Alionekana kama amewashinda.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki