Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Panga Ratiba Inayofaa ya Familia
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Panga Ratiba Inayofaa ya Familia

      1 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu aliwahimiza hivi wasikilizaji wake: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” (Mt. 6:33) Njia inayofaa ya kupanga shughuli za familia ili mambo ya kiroho yatangulizwe, ni kuwa na ratiba iliyoandikwa. Tumieni dakika chache kupanga ratiba ya kila juma ya familia mkitumia ratiba ambayo haijajazwa, iliyo katika ukurasa wa 6 wa nyongeza hii. Mnaweza kuandika shughuli za familia yenu kwenye ratiba hiyo, au kukata visehemu vilivyo chini ya ratiba iliyo katika ukurasa wa 6 na kuvibandika kwenye ratiba ya familia yenu.

      2 Ratiba iliyo hapa chini inaweza kuwasaidia kupanga ratiba yenu. Mtaona kwamba inahusisha mambo manne tu yaliyo muhimu: (1) kuhudhuria mikutano ya kutaniko, (2) huduma ya shambani ya familia, (3) funzo la familia, na (4) kuchunguza andiko la siku. Kupanga mambo hayo katika ratiba yenu kutawasaidia “kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mapendekezo zaidi kuhusu mambo hayo manne yamo katika ukurasa wa 4-5.

      3 Ratiba yenu ya familia haihitaji kuhusisha mambo hayo manne tu. Ikiwa ninyi hutayarisha mikutano fulani mkiwa pamoja, mnaweza kuandika jambo hilo katika ratiba yenu. Iwapo mnasoma sehemu fulani ya Biblia mkiwa pamoja baada ya kuchunguza andiko la siku au katika pindi nyingine, andikeni jambo hilo katika ratiba. Ikiwa ninyi huwa na tafrija fulani huenda mkaona kuwa inafaa kuandika jambo hilo katika ratiba yenu.

      4 Pangeni ratiba ya familia kupatana na mahitaji na hali za kila mmoja katika familia yenu. Mara kwa mara, chunguzeni ikiwa ratiba yenu bado inafaa hali zenu, na mfanye marekebisho yoyote yanayohitajika.

      [Chati katika ukurasa wa 3]

      Ratiba ya Mfano ya Familia

      Asubuhi Alasiri Jioni

      J2. Andiko la Siku

      Hotuba ya Watu Wote na

      Funzo la Mnara wa Mlinzi

      J3. Andiko la Siku Funzo la Familia

      J4. Andiko la Siku Funzo la Kitabu

      la Kutaniko

      J5. Andiko la Siku

      Al. Andiko la Siku Shule ya Huduma

      ya Kitheokrasi

      na Mkutano

      wa Utumishi

      Ij. Andiko la Siku

      J1. Andiko la Siku

      Huduma ya Shambani

      ya Familia

      (Siku ya Magazeti)

      [Chati katika ukurasa wa 6]

      Ratiba ya Familia

      Asubuhi Alasiri Jioni

      J2.

      J3.

      J4.

      J5.

      Al.

      Ij.

      J1.

      ..................................................................

      Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko

      la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku

      Hotuba Shule ya Funzo Funzo Huduma Usomaji Tafrija

      ya watu Huduma la kitabu la Fami- ya Sha- wa Biblia ya

      wote na ya Kith- la Kuta- lia mbani wa Familia Familia

      Funzo la eokrasi niko ya Familia

      Mnara wa na Mku-

      Mlinzi tano wa

      Utumishi

  • Ratiba ya Familia—Mikutano ya Kutaniko
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Ratiba ya Familia—Mikutano ya Kutaniko

      1 Ikiwa wewe ni mzazi Mkristo, bila shaka unataka watoto wako wawe watu wazima wanaompenda Yehova na kumtumikia, na hatimaye wapate uzima wa milele katika ulimwengu mpya ambao Mungu ameahidi. Unaweza kuwasaidiaje kutanguliza ibada ya Yehova maishani mwao? Njia moja muhimu ni kuwawekea mfano. (Met. 20:7) Akikumbuka mfano wa mama yake aliye Shahidi, dada mmoja alisema hivi: “Tulienda mikutanoni, tupende tusipende.” Hajasahau jambo hilo.

      2 Je, familia yako inaelewa kusudi la mikutano? Mafundisho tunayopata katika mikutano hiyo hutuchochea kuendelea kufanya mapenzi ya Mungu, na ushirika tunaofurahia pamoja na ndugu zetu hututia moyo sana. (Isa. 54:13; Rom. 1:11, 12) Hata hivyo, kusudi muhimu zaidi la mikutano yetu ni kumsifu Yehova “kati ya makundi yaliyokutanika.” (Zab. 26:12) Mikutano ya Kikristo hutupa nafasi ya kuonyesha upendo wetu kwa Yehova na kumwabudu.

      3 “Endeleeni Kuangalia Sana”: Kuthamini kusudi takatifu la mikutano yetu kutatuchochea ‘kuendelea kuangalia sana’ ili pole kwa pole tusisitawishe desturi ya kukosa mikutano kwa sababu ya mambo yasiyo muhimu. (Efe. 5:15, 16; Ebr. 10:24, 25) Unapopanga ratiba ya familia, unaweza kuanza kwa kupangia wakati wa mikutano ya kutaniko. Kisha hakikisha kwamba huruhusu mambo mengine yavuruge ratiba hiyo ya mikutano. Hakikisha kwamba uhudhuriaji wa mikutano unatangulizwa katika familia yako.

      4 Je, hatuchochewi tunaposoma jinsi ndugu zetu wanavyokabiliana na magumu ili wahudhurie mikutano na makusanyiko? Huenda hukabili hali ngumu sana, hata hivyo, yaelekea unakabili magumu fulani. Shetani hufanya iwe vigumu zaidi kwa watu wa Mungu kumwabudu Yehova. Lakini, uwe na hakika kwamba, bila shaka, watoto wako wataona jinsi familia yenu inavyojitahidi kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Kwa kweli, kwa kufanya hivyo unaweza kuwapa zawadi ya kiroho ambayo hawataisahau kamwe.

  • Ratiba ya Familia—Utumishi wa Shambani wa Familia
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Ratiba ya Familia—Utumishi wa Shambani wa Familia

      1 Yehova hushangilia kuwaona vijana wakilisifu jina lake. (Zab. 148:12, 13) Katika siku za Yesu hata ‘watoto na wanaonyonya walimsifu’ Mungu. (Mt. 21:15, 16) Hivyo ndivyo ilivyo leo. Wazazi, mnaweza kuwasaidiaje watoto wenu wawe watu wanaomsifu Yehova kwa bidii katika huduma ya Kikristo? Kama ilivyokaziwa katika makala iliyo juu, inayozungumzia mikutano ya kutaniko, mfano wenu ni muhimu sana. Baba mmoja alisema jambo ambalo wazazi wengi wamejionea. Alisema hivi: “Watoto hufuata mfano wako wala si maneno yako!”

      2 Dada mmoja aliyelelewa na wazazi wanaomcha Mungu anasema hivi: “Hatukuamka kamwe Jumamosi asubuhi na kujiuliza ikiwa tungeenda kwenye huduma. Tulijua kwamba tungeenda.” Ninyi pia, mnaweza kukazia umuhimu wa kazi ya kuhubiri kwa kuhubiri pamoja na familia zenu kwa ukawaida. Hilo haliwawezeshi watoto wenu kuiga mfano wenu tu, bali pia huwawezesha ninyi kuchunguza mtazamo wao, tabia, na maendeleo yao.

      3 Kuwazoeza Hatua kwa Hatua: Ili watoto wafurahie utumishi, ni lazima wazoezwe kuhubiri vizuri. Dada aliyenukuliwa mapema alisema hivi: ‘Hatukuandamana tu na wazazi wetu katika kazi yao. Tulijua kuwa tunapaswa kufanya jambo fulani, hata ikiwa ilikuwa tu kubisha mlango na kuacha kikaratasi cha mwaliko. Kwa kutayarishwa vema kabla ya utendaji wa kila mwisho-juma, tulijua kile ambacho tungesema.’ Unaweza kuwazoeza watoto wako kwa kutumia dakika chache kila juma kuwatayarisha kwa ajili ya huduma ya shambani, iwe wakati wa funzo la familia au katika pindi nyingine.

      4 Kuhubiri pamoja mkiwa familia huwapa nafasi nyingine ya kuwafundisha watoto wenu kweli. Baba mmoja aliandamana na binti yake alipotembea kilometa 20 (safari ya kwenda na kurudi) ili kuwaachia wanakijiji katika bonde fulani trakti za Biblia. Binti huyo anasema hivi: ‘Baba yangu alikazia kweli moyoni mwangu tulipokuwa tukitembea.’ (Kum. 6:7) Yehova na awabariki kwa kupanga huduma ya shambani katika ratiba ya kila juma ya familia zenu.

  • Ratiba ya Familia—Funzo la Familia
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Ratiba ya Familia—Funzo la Familia

      1 Ukiwa mzazi Mkristo, zawadi bora zaidi unayoweza kuwapa watoto wako ni kuwasaidia kumpenda Yehova kama wewe unavyompenda. Nafasi muhimu ya kufanya hivyo hupatikana “unapoketi katika nyumba yako” kwa ajili ya funzo la Biblia la familia la kila juma. (Kum. 6:5-7) Iwe una mwenzi wa ndoa anayeamini, familia yenu imegawanyika kidini, au uwe mzazi asiye na mwenzi, unaweza kuwasaidia watoto wako kumkaribia Yehova kwa kuwa na funzo la familia linaloongozwa kwa ukawaida.

      2 Kuanzisha Funzo la Familia: Kwanza mnapaswa kuwa na desturi ya kujifunza mkiwa familia. Ikiwa hujui ni wakati gani unaofaa kuwa na funzo hilo, kwa nini msizungumzie jambo hilo mkiwa familia? (Met. 15:22) Ikiwa una watoto wachanga, huenda ukapendelea kuwa na vipindi vifupi vya kujifunza mara kadhaa kila juma. Panga ratiba itakayofaa zaidi hali ya familia yako. Weka wakati hususa wa funzo hilo katika ratiba ya familia yenu, na mhakikishe kwamba mnaufuata.

      3 Mnaweza kujifunza mambo gani? Familia fulani hutayarisha habari itakayozungumziwa katika Funzo la Kitabu la Kutaniko au Funzo la Mnara wa Mlinzi litakalofuata. Wengine hujifunza habari inayohusu vijana. Baba mmoja aliye na mwana mchanga na binti mchanga, asema: ‘Sisi huigiza masimulizi ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na hilo hufanya watoto wetu waone funzo la familia kuwa jambo muhimu sana katika juma. Ufahamu na ueleweji tunaopata ni muhimu sana kuliko kusoma tu mafungu mengi.’

      4 Jifunzeni Kila Juma: Funzo la familia linapaswa kufanywa kwa ukawaida na kutazamiwa kwa hamu na kila mmoja katika familia. Huenda mkabadili siku na saa ya funzo hilo ili kushughulikia mambo ya dharura. Pia, huenda kukawa na uhitaji wa kuzungumzia jambo tofauti. Lakini mabadiliko hayo hayapaswi kuvuruga ratiba ya funzo la familia kwa muda mrefu. Ikiwa kuna unahitaji wa kubadilisha wakati wa funzo, baba mmoja huandika ujumbe mfupi unaoonyesha wakati funzo litakapofanywa na kuuweka mahali ambapo wote katika familia wanaweza kuuona. Jitihada kama hizo za kuhakikisha kwamba funzo la familia linafanywa kwa ukawaida zinafaa sana. Unapoendelea kuwalea watoto wako “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova,” utakuwa ukionyesha jinsi unavyowapenda na pia jinsi unavyompenda Baba yetu wa mbinguni.—Efe. 6:4.

  • Ratiba ya Familia—Andiko la Siku
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Ratiba ya Familia—Andiko la Siku

      1 Kila siku, wazazi wenye upendo hujitahidi sana kuwaandalia watoto wao chakula kizuri. Kuwaandalia chakula cha kiroho kutoka katika neno la Mungu ni muhimu zaidi. (Mt. 4:4) Njia moja ya kuwasaidia watoto wako kusitawisha hamu ya chakula cha kiroho ili ‘wakue kufikia wokovu’ ni kuchunguza andiko la siku na maelezo yake kila siku mkiwa familia. (1 Pet. 2:2) Mnaweza kuchunguza andiko la siku wakati gani?

      2 Wakati wa Mlo: Kuanza siku kwa kuzungumzia andiko la siku kutaiwezesha familia yenu kumfikiria Yehova mchana kutwa. (Zab. 16:8) Mama mmoja alizoea kusoma na kuzungumzia andiko la siku na maelezo yake pamoja na mwana wake alipokuwa akila kiamsha kinywa na kusali naye kabla mwana huyo hajaondoka kwenda shuleni. Hilo lilimwimarisha kusimama imara alipokabili suala la uzalendo, kupinga vishawishi vya ukosefu wa maadili, na kuwahubiria kwa ujasiri wanafunzi na walimu. Hakuhisi upweke licha ya kuwa Shahidi pekee katika shule hiyo.

      3 Ikiwa hamwezi kulichunguza andiko la siku asubuhi mkiwa familia, mnaweza kulichunguza baadaye, pengine mnapokula chakula cha jioni siku hiyo. Wengine huzungumzia mambo yaliyoonwa katika huduma ya shambani na mambo waliyofurahia katika usomaji wao wa Biblia. Wengi hukumbuka pindi kama hizo nao huziona kuwa pindi walizofurahia zaidi wakiwa pamoja na familia zao.

      4 Usiku: Familia fulani huona kwamba muda mfupi kabla ya kwenda kulala ndio wakati bora wa kulichunguza andiko la siku. Hiyo inaweza pia kuwa pindi nzuri ya kusali pamoja. Watoto wenu humwona Yehova kuwa mtu halisi wanapowasikia mkiongea kumhusu na kusali kwake kila siku.

      5 Yehova na abariki jitihada zenu za kuwafundisha watoto wenu kweli mnapotumia vizuri kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki