-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Baada ya Mashahidi kama 1,200 kufungwa katika Ujerumani mapema katika enzi ya Nazi kwa kukataa kutoa salamu ya Nazi na kukataa kuvunja kutokuwamo kwao kwa Kikristo, maelfu walitendwa vibaya kimwili katika Marekani kwa sababu walikataa kusalimu bendera ya Amerika. Wakati wa juma la Novemba 4, 1935, idadi fulani ya watoto wa shule katika Canonsburg, Pennsylvania, walipelekwa kwenye chumba cha kuchemshia maji na kuchapwa viboko kwa kukataa kusalimu bendera. Grace Estep, aliyekuwa mwalimu, aliachishwa wadhifa wake katika shule hiyo kwa sababu iyo hiyo. Mnamo Novemba 6, William na Lillian Gobitas walikataa kusalimu bendera na wakafukuzwa shuleni katika Minersville, Pennsylvania. Baba yao alipeleka mashtaka mahakamani ili watoto wake waruhusiwe kwenda shuleni. Mahakama ya wilaya ya jimbo na mahakama ya mzunguko ya rufani pia ziliamua kesi kwa kuwapendelea Mashahidi wa Yehova. Hata hivyo, katika 1940, huku taifa likikaribia kuingia vitani, Mahakama Kuu ya Marekani, katika Minersville School District v. Gobitis, iliunga mkono sharti la kusalimu bendera kwa shule zote za umma, kwa uamuzi wa 8 kwa 1. Hiyo iliongoza kwenye jeuri ya taifa lote dhidi ya Mashahidi wa Yehova.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kwa sababu watoto wengi wa Mashahidi wa Yehova walifukuzwa shuleni, kwa muda fulani wakati wa miaka ya mwishoni mwa 1930 na mapema miaka ya 1940 ilihitajika kwamba wao waendeshe shule zao wenyewe katika Marekani na Kanada ili kuandaa elimu kwa watoto wao. Hizo ziliitwa Shule za Ufalme.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 672]
Katika sehemu nyingi kulikuwa na uhitaji wa kuanzisha Shule za Ufalme kwa sababu watoto Mashahidi walikuwa wamefukuzwa kutoka shule za umma
-