-
Uumbaji—Ulitoka Wapi?Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Kwa mfano, Albert Einstein alisadiki kwamba ulimwengu ulikuwa na mwanzo, naye alitamani “kujua jinsi Mungu alivyoumba ulimwengu.” Lakini Einstein hakusema kwamba anaitikadi Mungu aliye mtu halisi; yeye alisema juu ya “hisia ya kidini iliyo katika [ulimwengu wote], ambayo haina fundisho lolote wala haitambui Mungu aliye kama wanadamu.”
-
-
Uumbaji—Ulitoka Wapi?Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Je, wajua kwamba kuitikadi kisababishi kisicho na utu ni kama tu kufuata mafundisho ya kidini ya Mashariki? Watu wengi wa Mashariki huamini kwamba maumbile yalitokea yenyewe tu. Wazo hilo hata linaonyeshwa na herufi za Kichina zinazomaanisha maumbile, ambazo kihalisi zinamaanisha “-enye kutokea -enyewe” au “-enye kuwako bila kuumbwa.” Einstein aliamini kwamba nadharia yake ya hisia ya kidini ya ulimwengu wote iliungwa mkono na Ubudha. Buddha aliamini kwamba si jambo muhimu kama Muumba alishiriki kuumba ulimwengu na binadamu. Vivyo hivyo, dini ya Shinto haiandai ufafanuzi wowote wa jinsi maumbile yalivyotokea, na wafuasi wa dini ya Shinto waamini kwamba miungu ni roho za wafu ambazo huchangamana na maumbile.
-