-
Isikie Sauti Inayotoka NdaniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
Francis S. Collins, mtaalamu wa chembe za urithi ambaye aliongoza jitihada za serikali ya Marekani za kuelewa chembe za urithi za mwanadamu (DNA au ADN), alisema hivi: “Kuwajali wengine bila ubinafsi ni tatizo kubwa kwa mwana-mageuzi. . . . Sifa hiyo haipatani na wazo la kwamba tunachochewa na chembe za urithi zenye ubinafsi.” Pia, alisema: “Watu fulani wanajitolea wenyewe kuwasaidia wale ambao si wa jamii yao na ambao hawana uhusiano wowote nao. . . . Inaonekana kwamba sifa ya kuwajali wengine haiwezi kufafanuliwa na nadharia ya Darwin.”
“Sauti ya Dhamiri”
5. Ni jambo gani ambalo limeonekana mara nyingi kwa watu?
5 Dakt. Collins anaonyesha sababu moja inayotufanya tuwajali wengine: “Sauti ya dhamiri ndiyo inayotuamuru tuwasaidie wengine hata ikiwa hatupati faida yoyote.”a
-
-
Isikie Sauti Inayotoka NdaniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
a Vivyo hivyo, Owen Gingerich, profesa wa utafiti wa elimu ya nyota kwenye Chuo Kikuu cha Harvard, aliandika hivi: “Kwa kweli, huenda kuwajali wengine kukatokeza swali ambalo . . . haliwezi kujibiwa kisayansi kutokana na uchunguzi wa wanyama. Huenda ikawa kwamba jibu linalosadikisha zaidi linatokana na chanzo kingine na linahusiana na sifa za ubinadamu ambazo tumepewa na Mungu, zinazotia ndani dhamiri.”
-