-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Na mbele ya kiti cha ufalme kuna, kana kwamba, ni bahari ya kioo kama fuwele.” (Ufunuo 4:5b, 6a, NW)
-
-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17. Ile “bahari ya kioo kama fuwele” inafananisha nini?
17 Pia Yohana anaona “bahari ya kioo kama fuwele.” Hii ingefananisha nini kwa wale walioalikwa waingie ndani ya kitala cha kimbingu? Paulo alisema juu ya njia ambayo katika hiyo Yesu alitakasa kundi, “akilisafisha kwa mwosho wa maji kwa njia ya neno.” (Waefeso 5:26, NW) Kabla ya kifo chake, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya neno ambalo mimi nimesema kwa nyinyi.” (Yohana 15:3, NW) Kwa sababu hiyo, hii bahari ya kioo kama fuwele lazima iwakilishe Neno la Mungu lenye kusafisha, lililorekodiwa. Wale wa ukuhani wa kifalme ambao wanakuja ndani ya kuwapo kwa Yehova lazima wawe wamekwisha safishwa kikamili kwa Neno lake.
-