-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
15. Ni wafalme gani wawili wenye nguvu waliotokana na falme nne za Kigiriki, nao walianzisha ushindani gani?
15 Kwa hiyo, wafalme wawili wenye nguvu—Niketa Seleuko wa Kwanza aliyetawala Siria na Ptolemy wa Kwanza aliyetawala Misri—waliibuka wakiwa wafalme wawili wenye nguvu kutokana na zile falme nne za Kigiriki. Ushindani wa muda mrefu unaofafanuliwa katika Danieli sura ya 11 kati ya “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini,” ulianzishwa na wafalme hao wawili.
-
-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
16. (a) Wale wafalme wawili walikuwa kaskazini na kusini mwa nani? (b) Ni wafalme gani waliokuwa “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini”?
16 Sikiliza! Akifafanua mwanzo wenye kutokeza wa pambano hilo, malaika wa Yehova asema hivi: “Mfalme wa kusini atakuwa hodari, na mmoja wa wakuu wake [wa Aleksanda]; naye [mfalme wa kaskazini] atakuwa hodari kuliko yeye, naye atakuwa na mamlaka; mamlaka yake itakuwa mamlaka kubwa.” (Danieli 11:5) Majina “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini” yarejezea wafalme walio kaskazini na kusini mwa watu wa Danieli, ambao wakati huo walikuwa wamewekwa huru kutokana na utekwa wa Babiloni na walikuwa wamerudi Yuda. “Mfalme wa kusini” wa kwanza alikuwa Ptolemy wa Kwanza wa Misri. Mmojawapo wa majenerali wa Aleksanda aliyemshinda Ptolemy wa Kwanza na kutawala akiwa na “mamlaka kubwa” alikuwa Mfalme wa Siria, Niketa Seleuko wa Kwanza. Akawa “mfalme wa kaskazini.”
-