Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ninaweza Kudhibiti Jinsi Gani Hisia Zangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • Kudhibiti Hasira

      Si rahisi kuvumilia uchungu na maumivu yanayotokea unapotendewa isivyofaa. Watu fulani hushindwa kujidhibiti wanapotendewa hivyo. Hata Biblia inasema kwamba kuna watu wenye “mazoea ya kukasirika” na wenye “mifoko ya ghadhabu.” (Methali 22:24; 29:22) Hilo si jambo dogo. Hasira isiyodhibitiwa inaweza kukufanya utende kwa njia ambayo itakufanya ujute baadaye. Kwa hiyo, unaweza kudhibiti hisia zako jinsi gani unapotendewa isivyofaa?

      Kwanza, changanua vizuri hali hiyo, uone ikiwa unaweza kutatua jambo hilo moyoni mwako.a (Zaburi 4:4) Kumbuka kulipa “ubaya kwa ubaya” kutafanya mambo yawe mabaya zaidi. (1 Wathesalonike 5:15) Baada ya kufikiria jambo hilo kwa uzito na kusali, huenda ukaona kwamba unaweza kusahau jambo hilo. Ukiondoa kinyongo moyoni, hutakuwa tena mtumwa wa jambo hilo.—Zaburi 37:8

      Lakini namna gani ikiwa bado una uchungu mwingi? Biblia inasema kuna “wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:7) Je, unaweza kuzungumza na mtu aliyekuumiza? Ikiwa haingefaa kufanya hivyo, unaweza kufaidika kwa kuzungumza na wazazi wako au rafiki mkomavu na kumweleza unavyohisi. Ikiwa mtu fulani anakusumbua kimakusudi, jitahidi kushughulika naye kwa fadhili. Chati iliyo katika ukurasa wa 221 inaweza kukusaidia kufikiria jinsi unavyoweza kushughulikia hali ambazo zimekuwa zikikufanya utende kwa hasira.

      Vyovyote vile, mwombe Yehova akusaidie kuepuka kumwekea kinyongo mtu aliyekuumiza. Kumbuka hili: Ijapokuwa huwezi kubadili lililotokea, unaweza kubadili utakavyoshughulika na hali hiyo. Ukijiacha ulemewe na kinyongo, utakuwa hoi kama samaki aliyenaswa kwenye ndoano. Unamruhusu mtu mwingine aongoze fikira na hisia zako. Ingekuwa afadhali kama wewe mwenyewe ungekuwa kwenye usukani, sivyo?—Waroma 12:19.

  • Ninaweza Kudhibiti Jinsi Gani Hisia Zangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • [Chati/Picha katika ukurasa wa 221]

      Ukurasa wa Mazoezi

      Dhibiti hasira yako

      Malizia chati hii

      Tukio

      Mwanafunzi mwenzangu ananidhihaki

      Itikio la hasira

      Kumtukana

      Itikio bora zaidi

      Kupuuza dhihakaka zake, na kumwonyesha na kumwonyesha kwamba hujakasirika

      Tukio

      Dada yangu “alichukua” viatu vyangu ninavyovipenda sana bila kuniomba

      Itikio la hasira

      Kulipiza kisasi kwa “kuchukua” kitu chake

      Itikio bora zaidi

      ․․․․․

      Tukio

      Dada yangu wananinyima ruhusa

      Itikio la hasira

      ․․․․․

      Itikio bora zaidi

      ․․․․․

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki