-
‘Yehova Ameufanya Uso Wake Ung’ae Kuwaelekea’Mnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 15
-
-
Jeremy, ambaye wazazi wake wote ni viziwi, anasema hivi: “Ninakumbuka jinsi baba yangu alivyotumia saa nyingi akisoma na kujaribu kuelewa mafungu machache tu ya makala ya Mnara wa Mlinzi katika chumba chake cha kulala. Kwa ghafula, alitoka katika chumba chake na kusema hivi kwa msisimuko kwa lugha ya ishara: ‘Nimeelewa! Nimeelewa!’ Kisha alianza kunieleza maana ya mafungu aliyosoma. Wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 12 tu. Niliyatazama kwa haraka mafungu hayo na kumwambia hivi kwa lugha ya ishara: ‘Baba, sidhani hiyo ndiyo maana. Yanamaanisha . . .’ Aliniambia kwa ishara niache kumweleza, kisha alirudi katika chumba chake ili kujaribu kuelewa maana ya mafungu hayo. Sitasahau kamwe jinsi alivyoonekana amekata tamaa na jinsi nilivyoguswa moyo nilipomtazama akirudi katika chumba chake cha kulala. Hata hivyo, sasa anaweza kuelewa habari hizo vizuri zaidi kwa sababu ana vichapo vya lugha ya ishara kwenye DVD. Ninafurahi sana kuona uso wake uking’aa anapoeleza jinsi anavyohisi kumhusu Yehova.”
-
-
‘Yehova Ameufanya Uso Wake Ung’ae Kuwaelekea’Mnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 15
-
-
Lorraine, Shahidi aliye kiziwi, anaeleza hivi: “Kujifunza Biblia kumekuwa kama kufumbua fumbo kubwa. Singeweza kuelewa kikamili ujumbe wa Biblia kwa sababu sikuwa na habari kamili. Hata hivyo, kweli za Biblia zilipoanza kupatikana katika lugha ya ishara, mapengo hayo yalijazwa.” George, kiziwi ambaye amekuwa Shahidi kwa miaka 38, anasema hivi: “Hakuna shaka kwamba uwezo wa kuelewa jambo wewe mwenyewe unakusaidia kujiheshimu na kujiamini kwa kadiri fulani. Ninahisi kwamba DVD za lugha ya ishara zimenisaidia sana kukua kiroho.”
-