-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Vifaa vingine vya kurekodia viliwekwa katika magari na mashua, vikuza-sauti vikiwa juu yazo ili sauti iende mbali zaidi. Bert na Vi Horton, katika Australia, waliendesha gari lenye honi kubwa juu yayo iliyoandikwa maneno “Ujumbe wa Ufalme.” Mwaka mmoja walifanya karibu kila barabara katika Melbourne ijae sauti ya kufunuliwa kwa dini bandia kwa njia yenye kuchochea na maelezo yenye kuchangamsha moyo ya baraka za Ufalme wa Mungu. Wakati wa miaka hiyo Claude Goodman alikuwa akipainia katika India. Utumizi wa gari la kuvumisha habari, lenye rekodi katika lugha za wenyeji, kulimwezesha kufikia watu wengi katika mabaraza, bustanini, kando ya barabara—mahali popote ambapo watu wangeweza kupatikana.
Wakati ndugu katika Lebanoni walipoegesha gari la kuvumisha habari kwenye kilima na wakatangaza mihadhara, sauti hiyo ilienda hadi kwenye mabonde. Nyakati nyingi watu walio vijijini wangeogopa kwa sababu hawangeweza kuona chanzo cha sauti huku wakifikiri kwamba Mungu alikuwa akizungumza nao kutoka mbinguni!
Hata hivyo, kulikuwa na nyakati ambapo ndugu waliona wasiwasi. Katika pindi moja, katika Siria, padri wa kijiji aliacha chakula chake mezani, akachukua fimbo yake kubwa ya kutembelea, na kukimbia nje hadi kwenye umati uliokuwa umekusanyika kusikiliza hotuba ya Biblia iliyotolewa kutoka kwa gari la kuvumisha habari. Huku akitikisa fimbo yake kwa hasira na kupiga kelele, aliamuru: “Komeni! Ninawaamuru nyinyi mkome!” Lakini ndugu waling’amua kwamba si kila mtu aliyekubaliana naye; kuna wale waliotaka kusikia. Upesi, baadhi ya watu katika umati walimwinua padri juujuu na kumbeba hadi nyumbani mwake, ambamo walimweka tena kwenye meza ya chakula! Kujapokuwa upinzani wa makasisi, Mashahidi walihakikisha kwamba watu walikuwa na fursa ya kusikiliza.
-
-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 567]
Magari ya kuvumisha habari, nyakati nyingine yakiwa mengi (kama hapa katika Australia), yalitumiwa kutangaza kweli ya Biblia hadharani
-