-
Ni Roho Ya Aina Gani Unayoonyesha?Mnara wa Mlinzi—2012 | Oktoba 15
-
-
ONYESHA ROHO YA HESHIMA KUTANIKONI
11. (a) Kudumisha roho inayofaa kutatusaidia kuepuka nini? (b) Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Daudi?
11 Tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova amewapa wazee mgawo wa “kulichunga kutaniko la Mungu.” (Mdo. 20:28; 1 Pet. 5:2) Kwa hiyo, tunatambua kwamba ni jambo la hekima kuheshimu mpango wa Mungu, iwe tuna pendeleo la kutumikia tukiwa wazee au la. Kudumisha roho inayofaa kunaweza kutusaidia kuepuka kuhangaikia sana mapendeleo. Mfalme Sauli wa Israeli alipohisi kwamba Daudi alikuwa tishio kwa ufalme wake, Sauli “akawa akimtilia Daudi shaka tangu siku hiyo na kuendelea.” (1 Sam. 18:9) Mfalme huyo alisitawisha roho mbaya na hata alitaka kumuua Daudi. Badala ya kuhangaikia sana mapendeleo au mamlaka kama Sauli, ni vizuri zaidi kuwa kama Daudi. Licha ya matendo yote yasiyo ya haki aliyotendewa, kijana huyo aliendelea kumheshimu yule aliyepewa mamlaka na Mungu.—Soma 1 Samweli 26:23.
12. Ni nini kitakachochangia umoja kutanikoni?
12 Kuwa na maoni yanayotofautiana kunaweza kuwa chanzo cha hasira kutanikoni, hata kati ya waangalizi. Mashauri haya ya Biblia yanaweza kutusaidia katika jambo hilo: “Katika kuonyeshana heshima iweni wa kwanza” na, “Msiwe wenye busara machoni penu wenyewe.” (Rom. 12:10, 16) Badala ya kusisitiza kwamba maoni yetu ndiyo sahihi, tunapaswa kukubali kwamba mara nyingi kuna njia mbalimbali zinazofaa za kushughulikia mambo. Tukijitahidi kuelewa maoni ya wengine, tunaweza kuchangia umoja kutanikoni.—Flp. 4:5.
13. Tunapaswa kuyaonaje maoni yetu, na ni mfano gani katika Biblia unaoonyesha hilo?
13 Je, hilo linamaanisha kwamba ni jambo lisilofaa kutoa maoni yetu ikiwa tunaona jambo fulani ambalo linahitaji kurekebishwa kutanikoni? La hasha. Katika karne ya kwanza, kulikuwa na jambo fulani lililosababisha ubishi mkubwa sana. Akina ndugu “wakapanga Paulo na Barnaba na wengine kati yao wapande kwenda kwa mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu kuhusu bishano hilo.” (Mdo. 15:2) Bila shaka, kila mmoja wa akina ndugu hao alikuwa na maoni yake mwenyewe kuhusu jambo hilo na pia mawazo kuhusu jinsi ambavyo jambo hilo lingeweza kushughulikiwa. Hata hivyo, baada ya kila mmoja kueleza mawazo yake na uamuzi kufanywa kwa mwongozo wa roho takatifu, ndugu hao hawakuendelea kutoa maoni yao. Baada ya barua iliyokuwa na uamuzi huo kuyafikia makutaniko, akina ndugu “walishangilia juu ya kitia-moyo hicho” na “kufanywa imara katika imani.” (Mdo. 15:31; 16:4, 5) Vivyo hivyo leo, baada ya kuwajulisha ndugu wenye madaraka jambo fulani, tunapaswa kuridhika na kuwaachia walishughulikie kupitia sala.
-
-
Ni Roho Ya Aina Gani Unayoonyesha?Mnara wa Mlinzi—2012 | Oktoba 15
-
-
CHANGIA ROHO NZURI KATIKA TENGENEZO LA MUNGU
16, 17. Kuhusu ‘roho tunayoonyesha,’ wewe binafsi umeazimia kufanya nini?
16 Matokeo yanaweza kuwa mazuri sana kila mshiriki wa kutaniko akiazimia kuchangia roho nzuri ya kutaniko. Baada ya kuchunguza mambo haya, huenda tukaamua kwamba sisi binafsi tunaweza kufanya maendeleo katika kuonyesha roho yenye kujenga. Ikiwa ndivyo, hatupaswi kusitasita kuruhusu Neno la Mungu lituchunguze. (Ebr. 4:12) Paulo, ambaye alikuwa mwangalifu sana kuhusu jinsi alivyojiendesha katika makutaniko, alisema hivi: “Sifahamu kitu chochote dhidi yangu mwenyewe. Lakini kwa hilo sionyeshwi kuwa mwadilifu, bali yeye anayenichunguza ni Yehova.”—1 Kor. 4:4.
17 Tunapojitahidi kutenda kulingana na hekima inayotoka juu, badala ya kujiona au kuona pendeleo letu kuwa la maana sana, tutachangia roho nzuri kutanikoni. Tukiwa na roho ya kusamehe na kuwa na maoni mazuri kuwahusu wengine, tutafurahia uhusiano wenye amani pamoja na waamini wenzetu. (Flp. 4:8) Tukifanya mambo hayo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova na Yesu watapendezwa na ‘roho tunayoonyesha.’—Flm. 25.
-