-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
22. Ni maswali gani yanayozuka juu ya shambulio la mwisho la mfalme wa kaskazini?
22 Hata hivyo, twajua hatua ambayo mfalme wa kaskazini atachukua hivi karibuni. Akichochewa na ‘habari zitokazo macheo ya jua na kaskazini,’ atapanga vita ili “kuwaondolea mbali watu wengi.” Vita hiyo itapiganwa dhidi ya nani? Nazo ni “habari” gani zinazochochea shambulio hilo?
ASHTUSHWA NA HABARI ZENYE KUSUMBUA
23. (a) Ni tukio gani lenye kutokeza ambalo lazima litukie kabla ya Har–Magedoni? (b) “Wafalme watokao macheo ya jua” ni akina nani?
23 Fikiria jambo ambalo kitabu cha Ufunuo chasema juu ya mwisho wa Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli. Kabla ya “vita ya siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote,” Har–Magedoni, adui huyo mkubwa wa ibada ya kweli “atachomwa kabisa kwa moto.” (Ufunuo 16:14, 16; 18:2-8) Kuharibiwa kwake kuliwakilishwa na kumwagwa kwa bakuli la sita la hasira ya kisasi ya Mungu kwenye mto wa ufananisho wa Eufrati. Mto huo wakauka ili “njia ipate kutayarishwa kwa ajili ya wafalme watokao macheo ya jua.” (Ufunuo 16:12) Wafalme hao ni nani? Si wengine ila Yehova Mungu na Yesu Kristo!—Linganisha Isaya 41:2; 46:10, 11.
24. Ni tendo gani la Yehova ambalo huenda likamsumbua mfalme wa kaskazini?
24 Kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa kwafafanuliwa kinaganaga kwenye kitabu cha Ufunuo, kinachotaarifu hivi: “Pembe kumi ulizoziona [wafalme wanaotawala katika wakati wa mwisho], na hayawani-mwitu [Umoja wa Mataifa], hawa watamchukia kahaba na watamfanya ukiwa na kuwa uchi, na watakula kabisa sehemu zake zenye nyama na watamchoma kabisa kwa moto.” (Ufunuo 17:16) Kwa nini wafalme watamharibu Babiloni Mkubwa? Kwa sababu ‘Mungu atia ndani ya mioyo yao ili watekeleze fikira yake.’ (Ufunuo 17:17) Mfalme wa kaskazini ni mmoja wa watawala hao. Huenda habari asikiazo kutoka “macheo ya jua” zarejezea tendo hilo la Yehova, atiapo ndani ya mioyo ya viongozi wa kibinadamu fikira ya kumwangamiza kahaba huyo mkubwa wa kidini.
-
-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Lakini Mungu tu ndiye atakayeamua habari kamili zitokazo ‘macheo ya jua na kaskazini’ zitakuwa nini, nao wakati utafunua.
-